< Kutoka 4 >

1 Musa akajibu, “Lakini itakuwaje wasiponiamini mimi au wasiponisikiliza na kusema, 'Yahwe hajakutokea wewe?”
Moses [Drawn out] answered, “But, behold, they will not believe me, nor sh'ma ·hear obey· to my voice; for they will say, ‘Adonai has not appeared to you.’”
2 Yahwe akamwambia, “Hicho ni nini mkononi mwako?” Musa aksema, “Ni fimbo.”
Adonai said to him, “What is that in your hand?” He said, “A rod.”
3 Yahwe akasema, “Itupe chini.” Musa akaitupa chini ile fimbo, nayo ikageuka na kuwa nyoka. Musa akarudi nyumba.
He said, “Throw it on the ground.” He threw it on the ground, and it became a snake; and Moses [Drawn out] ran away from it.
4 Yahwe akamwambia Musa, “Mchukue kwa kumshikia mkia wake.” Hivyo alimchukua yule nyoka. Mara ikaggeuka na kuwa fimbo mkononi mwake tena.
Adonai said to Moses [Drawn out], “Stretch out your hand, and take it by the tail.” He stretched out his hand, and took hold of it, and it became a rod in his hand.
5 “Hii ni ili wapate kuamini ya kuwa Yahwe, Mungu wa baba zao, Mungu wa wa Abrahamu, Mungu wa Isaka, na Mungu wa Yakobo amekutokea wewe.”
“That they may believe that Adonai, the God of their fathers, the God of Abraham [Father of a multitude], the God of Isaac [Laughter], and the God of Jacob [Supplanter], has appeared to you.”
6 Yahwe pia alimwambia, “Sasaingiza mkono wako ndani ya vazi lako.” Hivyo Musa akaingiza mkono wake ndani ya vazi lake. Na alipoutoa nje, tazama, mkono wake ulikuwa na ukoma, mweupe kama theluji.
Adonai said furthermore to him, “Now put your hand inside your cloak.” He put his hand inside his cloak, and when he took it out, behold, his hand was leprous, as white as snow.
7 Yahwe akasema, “Ingiza mkono wako ndani ya vazi lako tena.” Hivyo akaingiza mkono wake ndani ya vazi lake, na alipoutoa nje aliona ukiwa mzima tena kama ulivyo mwili wake wote.
He said, “Put your hand inside your cloak again.” He put his hand inside his cloak again, and when he took it out of his cloak, behold, it had turned again as his other flesh.
8 Yahwe akasema, “Kama hawatakuamini wewe - kama hawatazingatia ishara yanggu ya kwanza ya nguvu zangu au kuziamini, basi wataamini ishara ya pili.
“It will happen, if they will not believe you or sh'ma ·hear obey· the voice of the first sign, that they will believe the voice of the latter sign.
9 Na ikiwa hawataamini hata ishara hizi zote mbili za nguvu zangu, au wasipokusikiliza wewe, basi chota maji kutoka katika mto na uyamwage katika nchi kavu. Maji utakayoyamwaga yatakuwa damu katika nchi kavu.”
It will happen, if they will not believe even these two signs or sh'ma ·hear obey· your voice, that you shall take of the water of the river, and pour it on the dry land. The water which you take out of the river will become blood on the dry land.”
10 Ndipo Musa akamwambia Yahwe, “Bwana, mimi ni mzuri wa kuongea, si hapo kwanza au hata baada ya kuwa umeongea na mtumishi wako. Mimi ni mdhaifu wa kuongea na nina kigugumizi.”
Moses [Drawn out] said to Adonai, “O Lord, I am not eloquent, neither before now, nor since you have spoken to your servant; for I am slow of speech, and of a slow tongue.”
11 Yahwe akamwambia, “Ni nani anayeumba mdomo wa mwanadamu? Ni nani amfanyaye mwanadamu kuwa bubu au aone au kipofu? Je si mimi Yahwe?
Adonai said to him, “Who made man’s mouth? Or who makes one mute, or deaf, or seeing, or blind? Is not it I, Adonai?
12 Sasa nenda, nami nitauongoza mdomo wako na nitakufundisha cha kusema.”
Now therefore go, and I will be with your mouth, and teach you what you shall speak.”
13 Lakini Musa akasema, “Bwana, tafadhali mtume mtu mwingine, yeyote unayependa kumtuma.”
He said, “Oh, Lord, please send someone else.”
14 Kisha Yahwe akamkasirikia Musa. Akasema, “Vipi kuhusu Aroni kaka yako yule Mlawi? Najua ya kuwa anaweza kuongea vizuri. Hata hivyo, anakuja kukutana na wewe, na atakapokuona moyo wake utajawa na furaha.
Adonai’s anger burned against Moses [Drawn out], and he said, “What about Aaron [Light-bringer], your brother, the Levite [Descendant of United with]? I know that he can speak well. Also, behold, he comes out to meet you. When he sees you, he will be glad in his heart.
15 Wewe utaongea naye na utaweka maneno ya kusema kinywani mwake. Nami nitakiongoza kinywa chako na kinywa chake pia, nami nitaonesha ninyi nyote yawapasayo kutenda.
You shall speak to him, and put the words in his mouth. I will be with your mouth, and with his mouth, and will teach you what you shall do.
16 Yeye ataongea na watu kwa niaba yako. Yeye atakuwa msemaji wako, na wewe utakuwa kama Mungu kwake.
He will be your spokesman to the people; and it will happen, that he will be to you a mouth, and you will be to him as God.
17 Utachukua hii fimbo pamoja nawe mkononi mwako. Kwa fimbo hii utafanya ishara.”
You shall take this rod in your hand, with which you shall do the signs.”
18 Hivyo Musa alirudi kwa Yethro - baba mkwe wake na kumwambia, “Niruhusu nipate kurudi kwa ndugu zangu walioko Misri ili niweze kuona kama bado wako hai.” Yethro akwambia Musa, “Nenda kwa amani.”
Moses [Drawn out] went and returned to Jethro [Abundance] his father-in-law, and said to him, “Please let me go and return to my brothers who are in Egypt [Abode of slavery], and see whether they are still alive.” Jethro [Abundance] said to Moses [Drawn out], “Go in peace.”
19 Yahwe akamwambia Musa kule Midiani, “Nenda, rudi Misri, kwa kuwa watu wote waliotaka kukuua wameshakufa.”
Adonai said to Moses [Drawn out] in Midian [Strife], “Go, return into Egypt [Abode of slavery]; for all the men who sought your life are dead.”
20 Musa akamchukua mke wake na watoto wake wa kiume na kuwapandisha kwenye punda. Akarudi mpaka nchi ya Misri, naye alichukua fimbo ya Mungu pamoja naye mkononi mwake.
Moses [Drawn out] took his wife and his sons, and set them on a donkey, and he returned to the land of Egypt [Abode of slavery]. Moses [Drawn out] took God’s rod in his hand.
21 Yahwe akamwambia Musa, “Utakaporudi Misri, jitahidi kufanya ishara zote nilizokupa kufanya mbele ya Farao. Lakini nitaufanya moyo wake kuwa mgumu, naye hawatawaacha watu waende.
Adonai said to Moses [Drawn out], “When you go back into Egypt [Abode of slavery], see that you do before Pharaoh all the wonders which I have put in your hand, but I will harden his heart and he will not let the people go.
22 Lazima umwambie Farao, 'Hivi ndivyo asemavyo Yahwe: Israeli ni mtoto wangu, mzaliwa wa kwanza wangu,
You shall tell Pharaoh, ‘Adonai says, Israel [God prevails] is my son, my firstborn,
23 nami nakuamuru, “Mwache mwanangu aende ili apate kuniabudu mimi.” Lakini kwa kuwa umekataa kumwachia, hakika nitamuua mtoto wako wa kiume, mzaliwa wa kwanza wako.”'
and I have said to you, “Let my son go, that he may abad ·serve· me;” and you have refused to let him go. Behold, I will kill your son, your firstborn.’”
24 Sasa wakiwa njiani, wakati wa usiku walipopumzika, Yahwe alikutana na Musa na kutaka kumuua.
On the way at a lodging place, Adonai met Moses [Drawn out] and wanted to kill him.
25 Kisha Zipora akachukua kisu kikali na kukata govi la mtoto wake wa kiume na kuligusisha miguuni pake. Kisha akasema, “Hakika wewe ni bwana harusi wangu kwa njia ya damu.”
Then Zipporah took a flint, and cut off the foreskin of her son, and cast it at his feet; and she said, “Surely you are a bridegroom of blood to me.”
26 Hivyo Yahwe akamwachia. Akasema, “Wewe ni bwana harusi wa damu” kwa sababu ya kutahiriwa.
So he let him alone. Then she said, “You are a bridegroom of blood,” because of the circumcision.
27 Yahwe akamwambia Aroni, “Nenda nyikani ukutane na Musa.” Aroni akaenda na kukutana naye katika mlima wa Mungu, na kumbusu.
Adonai said to Aaron [Light-bringer], “Go into the wilderness to meet Moses [Drawn out].” He went, and met him on God’s mountain, and kissed him.
28 Musa akwambia Aroni maneno yote ya Yahwe ambayo alimtuma kusema na kwa habari za ishara zote za nguvu za Yahwe ambazo alimwagiza kutenda.
Moses [Drawn out] told Aaron [Light-bringer] all Adonai’s words with which he had sent him, and all the signs with which he had enjoined him.
29 Kisha Musa na Aroni wakaenda na kuwakusanya wazee wote wa Israeli.
Moses [Drawn out] and Aaron [Light-bringer] went and gathered together all the elders of the children of Israel [God prevails].
30 Aroni akawaambia maneno yote ambayo Yahwe alimwambia Musa. Pia alionesha ishara na miujiza ya nguvu za Yahwe mbele ya watu.
Aaron [Light-bringer] spoke all the words which Adonai had spoken to Moses [Drawn out], and did the signs in the sight of the people.
31 Watu waliamini. Waliposikia ya kuwa Yahwe aliwaona Waisraeli na ya kwamba aliyaona mateso yao, waliinamisha vichwa vyao na kumwabudu.
The people believed, and when they sh'ma ·heard obeyed· that Adonai had visited the children of Israel [God prevails], and that he had seen their affliction, then they hawa ·bowed low, prostrated· their heads and worshiped.

< Kutoka 4 >