< Kutoka 38 >

1 Naye akafanya madhabahu ya toleo la kuteketezwa kwa mbao za mshita. Mikono mitano urefu wake, na mikono mitano upana wake, ilikuwa mraba, na mikono mitatu kimo chake.
Hizo el altar del holocausto cuadrado con madera de acacia, de 2,25 metros de largo y de ancho y 1,35 metros de alto.
2 Halafu akafanya pembe zake kwenye zile ncha zake nne. Pembe zake zilitoka kwake. Kisha akaifunika kwa shaba.
Le hizo sus cuernos en las cuatro esquinas de una misma pieza, y lo recubrió de bronce.
3 Baada ya hilo akavifanya vyombo vyote vya madhabahu, yale makopo na zile sepetu na yale mabakuli, zile nyuma na vile vyetezo. Vyombo vyake vyote alivifanya kwa shaba.
También hizo de bronce todos los utensilios del altar: calderos, palas, tazones, tenedores y sartenes.
4 Tena akaifanyia madhabahu kiunzi cha fito, mtandao wa shaba, chini ya ukingo wake, chini kuelekea katikati yake.
Además hizo para el altar un enrejado de bronce en forma de red el cual puso debajo de su borde hasta la mitad.
5 Halafu akatengeneza pete nne kwenye ile miisho minne karibu na kile kiunzi cha shaba, ili kuitegemeza ile miti.
Fundió cuatro argollas para las cuatro esquinas del enrejado de bronce, como sujetadores para las varas.
6 Bezaleli akafanya miti ya mshita na kuifunika kwa shaba.
Hizo las varas de madera de acacia y las revistió de bronce.
7 Kisha akaitia ile miti kwenye zile pete zilizo pande za madhabahu ili kuibeba. Akaifanya kuwa sanduku la mbao lenye uwazi.
Luego introdujo las varas por las argollas en los lados del altar para transportarlo con ellas. Lo hizo hueco, de tablas.
8 Kisha akafanya beseni ya shaba na kinara chake cha shaba. Kwa kutumia vioo vya watumishi wanawake ambao walifanya utumishi uliopangwa kwenye mwingilio wa hema la mkutano.
Hizo la fuente y su fuste de bronce con los espejos de las mujeres que velaban a la puerta del Tabernáculo de Reunión.
9 Naye akafanya ule ua. Upande unaokabili Negebu, kuelekea kusini, mapazia ya ua yalikuwa ya kitani bora kilichosokotwa, kwa mikono mia moja.
También hizo el patio. Las cortinas de cordoncillo de lino fino por el lado sur tenían 45 metros.
10 Nguzo zake ishirini na vikalio vyake ishirini vilikuwa vya shaba. Misumari ya nguzo na viungo vyake vilikuwa vya fedha
Sus 20 columnas y sus 20 basas eran de bronce, pero los capiteles de las columnas y sus molduras, de plata.
11 Pia, kwa ajili ya upande wa kaskazini kulikuwa na mikono mia. Nguzo zake ishirini na vikalio vyake ishirini vilikuwa vya shaba. Misumari ya nguzo na viungo vyake vilikuwa vya fedha.
Por el lado norte también eran de 45 metros. Sus 20 columnas y sus 20 basas eran de bronce, pero los capiteles de las columnas y sus molduras, de plata.
12 Lakini kwa ajili ya upande wa magharibi mapazia yalikuwa mikono hamsini. Nguzo zake zilikuwa kumi na vikalio vyake kumi. Misumari ya nguzo na viungo vyake vilikuwa vya fedha.
Por el lado del occidente las cortinas eran de 22,5 metros, con sus diez columnas y sus diez basas. Los capiteles de sus columnas y sus molduras eran de plata.
13 Na kwa ajili ya upande wa mashariki kulikuwa na mikono hamsini.
Por el lado del oriente eran de 22,5 metros.
14 Mapazia yalikuwa mikono kumi na mitano kwa upande mmoja. Nguzo zake zilikuwa tatu na vikalio vyake vitatu.
Las cortinas por un lado de la entrada eran de 6,75 metros, con sus tres columnas y sus tres basas.
15 Na kwa ajili ya upande ule mwingine, huu na ule, wa lango la ua, mapazia yalikuwa mikono kumi na mitano. Nguzo zake zilikuwa tatu na vikalio vyake vitatu.
Por el otro lado de la entrada, a ambos lados de la entrada al patio, las cortinas eran de 6,75 metros, con sus tres columnas y sus tres basas.
16 Mapazia yote ya ua kuzunguka pande zote yalikuwa ya kitani bora kilichosokotwa.
Todas las cortinas alrededor del patio eran de cordoncillo de lino fino.
17 Navyo vikalio vya nguzo vilikuwa vya shaba. Vibanio vya vikalio na viungo vyake vilikuwa vya fedha navyo vilifunikwa kwa shaba sehemu ya juu, na kulikuwa na viungo vya shaba kwa ajili ya nguzo zote za ua.
Las basas de las columnas eran de bronce. Pero los capiteles de sus columnas y sus molduras, y el revestimiento de sus capiteles eran de plata. Todas las columnas del patio tenían molduras de plata.
18 Nacho kisitiri cha lango la ua kilikuwa na mikono ishirini urefu. Cha uzi wa bluu na sufu iliyotiwa rangi ya zambarau na kitambaa chenye rangi nyekundu ya kochinili na kitani bora kilichosokotwa, na urefu wake ulikuwa mikono ishirini, nacho kimo kotekote kilikuwa mikono mitano sawasawa na mapazia ya ua.
La cortina de la entrada al patio era obra de bordador en material de azul, púrpura y carmesí y cordoncillo de lino fino. La longitud era de nueve metros y la anchura de 2,25 metros, lo mismo que las cortinas del patio.
19 Na nguzo zake nne na vikalio vyake vinne vilikuwa vya shaba. Misumari yake ilikuwa ya fedha na utando wa vichwa vyake na viungo vyake ulikuwa wa fedha.
Sus columnas y sus basas de bronce eran cuatro. Pero sus capiteles y sus molduras eran de plata.
20 Na misumari yote ya hema kwa ajili ya maskani na kwa ajili ya ua kuzunguka pande zote ilikuwa ya shaba
Todas las estacas del Tabernáculo y del patio alrededor eran de bronce.
21 Hivi ndivyo vitu vilivyohesabiwa vya maskani, maskani ya Ushuhuda, vilivyohesabiwa kwa amri ya Musa, kuwa utumishi wa Walawi chini ya uongozi wa Ithamari mwana wa Aruni kuhani.
Estas son las cuentas del Tabernáculo del Testimonio registradas conforme al mandato de Moisés por medio de los levitas bajo la dirección de Itamar, hijo del sacerdote Aarón.
22 Naye Bezaleli mwana wa Uri mwana wa Huru wa kabila la Yuda alifanya yote ambayo Yahweh alikuwa amemwamuru Musa.
Bezaleel, hijo de Uri, hijo de Hur, de la tribu de Judá, hizo todo lo que Yavé ordenó a Moisés.
23 Na pamoja naye alikuwa Oholiabu mwana wa Ahisamaki wa kabila la Dani, fundi na mtarizi na mfumaji wa uzi wa bluu na sufu iliyotiwa rangi ya zambarau na kitambaa chenye rangi nyekundu ya kochinili na kitani bora.
Y con él estaba Oholiab, hijo de Ahisamac, de la tribu de Dan, artífice, diseñador y bordador en [tela] azul, púrpura y carmesí y cordoncillo de lino fino.
24 Dhahabu yote iliyotumiwa kwa ajili ya kazi katika kazi yote ya mahali patakatifu ikawa jumla ya dhahabu ya toleo la kutikisa, talanta ishirini na tisa na shekeli 730 kulingana na shekeli ya mahali patakatifu.
Todo el oro empleado para el trabajo, en toda la obra del Santuario, el oro de la ofrenda mecida, fue de 965 kilogramos.
25 Nayo fedha ya wale walioandikishwa kati ya kusanyiko ilikuwa talanta mia moja na shekeli 1, 775 kulingana na shekeli ya mahali patakatifu,
La plata de los censados de la congregación ascendió a 3,32 toneladas.
26 ile nusu shekeli kwa ajili ya mtu mmoja ilikuwa nusu shekeli kulingana na shekeli ya mahali patakatifu, Kwa kila mtu aliyekuwa akipita kuingia upande wa wale waliokuwa wameandikishwa kuanzia miaka ishirini na zaidi, jumla ya watu 603, 550.
[Esto representaba] 5,5 gramos de plata por cada uno de los empadronados mayores de 20 años, los cuales fueron 603.550.
27 Na talanta mia moja za fedha zilitumiwa kutengeneza vikalio vya mahali patakatifu na vikalio vya lile pazia. Vikalio mia moja vilitoshana na talanta mia moja, talanta moja kwa kikalio kimoja.
Se emplearon 3,3 toneladas de plata para fundir las basas del Santuario y las basas del velo. Para 100 basas [emplearon] 3,3 toneladas, 33 kilogramos por basa.
28 Na kutokana na zile shekeli 1, 775 alifanyiza vibanio vya nguzo na kuvifunika sehemu yake ya juu na kuviunganisha pamoja.
Con 19,5 kilogramos hizo los capiteles de las columnas y las molduras.
29 Nayo shaba ya toleo la kutikisa ilikuwa talanta sabini na shekeli 2, 400.
El bronce de la ofrenda mecida ascendió a 2,3 toneladas.
30 Naye akaitumia kufanya vile vikalio vya mwingilio wa hema la mkutano na ile madhabahu ya shaba na kile kiunzi chake cha shaba, na vyombo vyote vya madhabahu,
Con él hizo las basas de la puerta del Tabernáculo de Reunión, el altar de bronce y su rejilla de bronce, todos los utensilios del altar,
31 na vile vikalio vya ua kuzunguka pande zote, na vile vikalio vya lango la ua, na misumari yote ya maskani na misumari yote ya ua kuzunguka pande zote.
las basas del patio que lo rodeaba, las basas de la entrada al patio, todas las estacas del Tabernáculo y todas las estacas del patio que lo rodeaba.

< Kutoka 38 >