< Kutoka 38 >

1 Naye akafanya madhabahu ya toleo la kuteketezwa kwa mbao za mshita. Mikono mitano urefu wake, na mikono mitano upana wake, ilikuwa mraba, na mikono mitatu kimo chake.
و مذبح قربانی سوختنی را از چوب شطیم ساخت. طولش پنج ذراع، وعرضش پنج ذراع مربع، و بلندیش سه ذراع.۱
2 Halafu akafanya pembe zake kwenye zile ncha zake nne. Pembe zake zilitoka kwake. Kisha akaifunika kwa shaba.
وشاخهایش را بر چهار گوشه‌اش ساخت. شاخهایش از همان بود و آن را از برنج پوشانید.۲
3 Baada ya hilo akavifanya vyombo vyote vya madhabahu, yale makopo na zile sepetu na yale mabakuli, zile nyuma na vile vyetezo. Vyombo vyake vyote alivifanya kwa shaba.
و همه اسباب مذبح را ساخت، یعنی: دیگها وخاک اندازها و کاسه‌ها و چنگالها و مجمرها وهمه ظروفش را از برنج ساخت.۳
4 Tena akaifanyia madhabahu kiunzi cha fito, mtandao wa shaba, chini ya ukingo wake, chini kuelekea katikati yake.
و برای مذبح، آتش دانی مشبک از برنج ساخت، که زیرحاشیه‌اش بطرف پایین تا نصفش برسد.۴
5 Halafu akatengeneza pete nne kwenye ile miisho minne karibu na kile kiunzi cha shaba, ili kuitegemeza ile miti.
و چهارحلقه برای چهار سر آتش دان برنجین ریخت، تاخانه های عصاها باشد.۵
6 Bezaleli akafanya miti ya mshita na kuifunika kwa shaba.
و عصاها را از چوب شطیم ساخته، آنها را به برنج بپوشانید.۶
7 Kisha akaitia ile miti kwenye zile pete zilizo pande za madhabahu ili kuibeba. Akaifanya kuwa sanduku la mbao lenye uwazi.
و عصاهارا در حلقه‌ها بر دو طرف مذبح گذرانید، برای برداشتنش به آنها، و مذبح را از چوبها مجوف ساخت.۷
8 Kisha akafanya beseni ya shaba na kinara chake cha shaba. Kwa kutumia vioo vya watumishi wanawake ambao walifanya utumishi uliopangwa kwenye mwingilio wa hema la mkutano.
و حوض را از برنج ساخت، و پایه‌اش را از برنج از آینه های زنانی که نزد دروازه خیمه اجتماع برای خدمت جمع می‌شدند.۸
9 Naye akafanya ule ua. Upande unaokabili Negebu, kuelekea kusini, mapazia ya ua yalikuwa ya kitani bora kilichosokotwa, kwa mikono mia moja.
و صحن را ساخت که برای طرف جنوبی به سمت یمانی. پرده های صحن از کتان نازک تابیده شده صد ذراعی بود.۹
10 Nguzo zake ishirini na vikalio vyake ishirini vilikuwa vya shaba. Misumari ya nguzo na viungo vyake vilikuwa vya fedha
ستونهای آنها بیست بود، و پایه های آنها بیست بود، از برنج و قلابهای آنهاو پشت بندهای آنها از نقره.۱۰
11 Pia, kwa ajili ya upande wa kaskazini kulikuwa na mikono mia. Nguzo zake ishirini na vikalio vyake ishirini vilikuwa vya shaba. Misumari ya nguzo na viungo vyake vilikuwa vya fedha.
و برای طرف شمالی صد ذراعی بود، و ستونهای آنها بیست ازبرنج، و قلابهای ستونها و پشت بندهای آنها ازنقره بود.۱۱
12 Lakini kwa ajili ya upande wa magharibi mapazia yalikuwa mikono hamsini. Nguzo zake zilikuwa kumi na vikalio vyake kumi. Misumari ya nguzo na viungo vyake vilikuwa vya fedha.
و برای طرف غربی، پرده های پنجاه ذراعی بود، و ستونهای آنها ده و پایه های آنها ده، و قلابها و پشت بندهای ستونها از نقره بود.۱۲
13 Na kwa ajili ya upande wa mashariki kulikuwa na mikono hamsini.
وبرای طرف شرقی به سمت طلوع، پنجاه ذراعی بود.۱۳
14 Mapazia yalikuwa mikono kumi na mitano kwa upande mmoja. Nguzo zake zilikuwa tatu na vikalio vyake vitatu.
و پرده های یک طرف دروازه پانزده ذراعی بود، ستونهای آنها سه و پایه های آنها سه.۱۴
15 Na kwa ajili ya upande ule mwingine, huu na ule, wa lango la ua, mapazia yalikuwa mikono kumi na mitano. Nguzo zake zilikuwa tatu na vikalio vyake vitatu.
و برای طرف دیگر دروازه صحن از این طرف واز آن طرف پرده‌ها پانزده ذراعی بود، ستونهای آنها سه و پایه های آنها سه.۱۵
16 Mapazia yote ya ua kuzunguka pande zote yalikuwa ya kitani bora kilichosokotwa.
همه پرده های صحن به هر طرف از کتان نازک تابیده شده بود.۱۶
17 Navyo vikalio vya nguzo vilikuwa vya shaba. Vibanio vya vikalio na viungo vyake vilikuwa vya fedha navyo vilifunikwa kwa shaba sehemu ya juu, na kulikuwa na viungo vya shaba kwa ajili ya nguzo zote za ua.
و پایه های ستونها از برنج بود، و قلابها وپشت بندهای ستونها از نقره، و پوشش سرهای آنها از نقره، و جمیع ستونهای صحن به پشت بندهای نقره پیوسته شده بود.۱۷
18 Nacho kisitiri cha lango la ua kilikuwa na mikono ishirini urefu. Cha uzi wa bluu na sufu iliyotiwa rangi ya zambarau na kitambaa chenye rangi nyekundu ya kochinili na kitani bora kilichosokotwa, na urefu wake ulikuwa mikono ishirini, nacho kimo kotekote kilikuwa mikono mitano sawasawa na mapazia ya ua.
و پرده دروازه صحن از صنعت طراز از لاجورد و ارغوان و قرمز و کتان نازک تابیده شده بود. طولش بیست ذراع، و بلندیش به عرض پنج ذراع موافق پرده های صحن.۱۸
19 Na nguzo zake nne na vikalio vyake vinne vilikuwa vya shaba. Misumari yake ilikuwa ya fedha na utando wa vichwa vyake na viungo vyake ulikuwa wa fedha.
و ستونهای آنها چهار، وپایه های برنجین آنها چهار، و قلابهای آنها ازنقره، و پوشش سرهای آنها و پشت بندهای آنهااز نقره بود.۱۹
20 Na misumari yote ya hema kwa ajili ya maskani na kwa ajili ya ua kuzunguka pande zote ilikuwa ya shaba
و همه میخهای مسکن و صحن، به هر طرف از برنج بود.۲۰
21 Hivi ndivyo vitu vilivyohesabiwa vya maskani, maskani ya Ushuhuda, vilivyohesabiwa kwa amri ya Musa, kuwa utumishi wa Walawi chini ya uongozi wa Ithamari mwana wa Aruni kuhani.
این است حساب مسکن، یعنی مسکن شهادت، چنانکه حسب فرمان موسی به خدمت لاویان، به توسط ایتاماربن هارون کاهن حساب آن گرفته شد.۲۱
22 Naye Bezaleli mwana wa Uri mwana wa Huru wa kabila la Yuda alifanya yote ambayo Yahweh alikuwa amemwamuru Musa.
و بصلئیل بن اوری بن حور از سبطیهودا، آنچه را که خداوند به موسی‌امر فرموده بود بساخت.۲۲
23 Na pamoja naye alikuwa Oholiabu mwana wa Ahisamaki wa kabila la Dani, fundi na mtarizi na mfumaji wa uzi wa bluu na sufu iliyotiwa rangi ya zambarau na kitambaa chenye rangi nyekundu ya kochinili na kitani bora.
و با وی اهولیاب بن اخیسامک ازسبط دان بود، نقاش و مخترع و طراز در لاجورد وارغوان و قرمز و کتان نازک.۲۳
24 Dhahabu yote iliyotumiwa kwa ajili ya kazi katika kazi yote ya mahali patakatifu ikawa jumla ya dhahabu ya toleo la kutikisa, talanta ishirini na tisa na shekeli 730 kulingana na shekeli ya mahali patakatifu.
و تمام طلایی که در کار صرف شد، یعنی در همه کار قدس، ازطلای هدایا بیست و نه وزنه و هفتصد و سی مثقال موافق مثقال قدس بود.۲۴
25 Nayo fedha ya wale walioandikishwa kati ya kusanyiko ilikuwa talanta mia moja na shekeli 1, 775 kulingana na shekeli ya mahali patakatifu,
و نقره شمرده شدگان جماعت صد وزنه و هزار و هفتصد وهفتاد و پنج مثقال بود، موافق مثقال قدس.۲۵
26 ile nusu shekeli kwa ajili ya mtu mmoja ilikuwa nusu shekeli kulingana na shekeli ya mahali patakatifu, Kwa kila mtu aliyekuwa akipita kuingia upande wa wale waliokuwa wameandikishwa kuanzia miaka ishirini na zaidi, jumla ya watu 603, 550.
یک درهم یعنی نیم مثقال موافق مثقال قدس، برای هر نفری از آنانی که به سوی شمرده شدگان گذشتند، از بیست ساله و بالاتر، که ششصد و سه هزار وپانصد و پنجاه نفر بودند.۲۶
27 Na talanta mia moja za fedha zilitumiwa kutengeneza vikalio vya mahali patakatifu na vikalio vya lile pazia. Vikalio mia moja vilitoshana na talanta mia moja, talanta moja kwa kikalio kimoja.
و اما آن صد وزنه نقره برای ریختن پایه های قدس و پایه های پرده بود. صد پایه از صد وزنه یعنی یک وزنه برای یک پایه.۲۷
28 Na kutokana na zile shekeli 1, 775 alifanyiza vibanio vya nguzo na kuvifunika sehemu yake ya juu na kuviunganisha pamoja.
و از آن هزار و هفتصد و هفتاد و پنج مثقال قلابها برای ستونها ساخت، و سرهای آنهارا پوشانید، و پشت بندها برای آنها ساخت.۲۸
29 Nayo shaba ya toleo la kutikisa ilikuwa talanta sabini na shekeli 2, 400.
وبرنج هدایا هفتاد وزنه و دو هزار و چهارصد مثقال بود.۲۹
30 Naye akaitumia kufanya vile vikalio vya mwingilio wa hema la mkutano na ile madhabahu ya shaba na kile kiunzi chake cha shaba, na vyombo vyote vya madhabahu,
و از آن پایه های دروازه خیمه اجتماع، ومذبح برنجین، و شبکه برنجین آن و همه اسباب مذبح را ساخت.۳۰
31 na vile vikalio vya ua kuzunguka pande zote, na vile vikalio vya lango la ua, na misumari yote ya maskani na misumari yote ya ua kuzunguka pande zote.
و پایه های صحن را به هرطرف، و پایه های دروازه صحن و همه میخهای مسکن و همه میخهای گرداگرد صحن را.۳۱

< Kutoka 38 >