< Kutoka 37 >

1 Bezaleli akafanya Sanduku la mbao za mshita. Mikono miwili na nusu urefu wake, na mkono mmoja na nusu upana wake, na mkono mmoja na nusu kimo chake.
Et Betsaleël fit l’arche de bois de sittim: sa longueur était de deux coudées et demie, et sa largeur d’une coudée et demie, et sa hauteur d’une coudée et demie.
2 Kisha akalifunika kwa dhahabu safi ndani na nje na kulifanyia ukingo wa dhahabu kulizunguka pande zote.
Et il la plaqua d’or pur, dedans et dehors, et lui fit un couronnement d’or tout autour;
3 Kisha akalitengenezea pete nne za dhahabu, za juu ya miguu yake minne, pete mbili upande wake mmoja na pete mbili upande wake mwingine
et il fondit pour elle quatre anneaux d’or, pour ses quatre coins, deux anneaux à l’un de ses côtés, et deux anneaux à l’autre de ses côtés.
4 Kisha akafanya miti ya mshita na kuifunika kwa dhahabu.
Et il fit des barres de bois de sittim, et les plaqua d’or;
5 Halafu akaitia miti hiyo kwenye zile pete zilizo pande za Sanduku ili kulibeba Sanduku.
et il fit entrer les barres dans les anneaux, aux côtés de l’arche, pour porter l’arche.
6 Naye akafanya kifuniko cha dhahabu safi. Mikono miwili na nusu urefu wake, na mkono mmoja na nusu upana wake.
– Et il fit un propitiatoire d’or pur: sa longueur était de deux coudées et demie, et sa largeur d’une coudée et demie.
7 Bezaleli akafanya makerubi wawili wa dhahabu. Kwa kazi ya kufua akawafanya kwenye miisho yote miwili ya kifuniko.
Et il fit deux chérubins d’or; il les fit d’or battu, aux deux bouts du propitiatoire,
8 Kerubi mmoja kwenye mwisho ule, na yule kerubi mwingine kwenye mwisho huu. Aliwafanya makerubi juu ya kifuniko kwenye miisho yote miwili.
un chérubin au bout de deçà, et un chérubin au bout de delà; il fit les chérubins [tirés] du propitiatoire, à ses deux bouts.
9 Nao wakawa makerubi wanaonyoosha mabawa yao mawili kuelekea juu, wakisitiri kifuniko kwa mabawa yao, nazo nyuso zao zilikuwa zikielekeana. Nyuso za makerubi hao zilielekea kifuniko hicho.
Et les chérubins étendaient les ailes en haut, couvrant de leurs ailes le propitiatoire; et leurs faces étaient l’une vis-à-vis de l’autre; les faces des chérubins étaient [tournées] vers le propitiatoire.
10 Bezaleli akafanya meza ya mbao za mshita. Mikono miwili urefu wake, na mkono mmoja upana wake, na mkono mmoja na nusu kimo chake.
Et il fit la table de bois de sittim: sa longueur était de deux coudées, et sa largeur d’une coudée, et sa hauteur d’une coudée et demie;
11 Halafu akaifunika kwa dhahabu safi na kufanya ukingo wa dhahabu kuizunguka pande zote.
et il la plaqua d’or pur, et y fit un couronnement d’or tout autour.
12 Kisha akafanya mzingo wa upana wa kiganja kuizunguka na kufanya ukingo wa dhahabu kwa ajili ya mzingo wake kuizunguka pande zote.
Et il y fit un rebord d’une paume tout autour, et il fit un couronnement d’or à son rebord, tout autour;
13 Tena, akatengeneza pete nne za dhahabu kwa ajili yake na kuziweka pete hizo kwenye zile pembe nne zilizokuwa kwa ajili ya ile miguu minne.
et il lui fondit quatre anneaux d’or, et il mit les anneaux aux quatre coins qui étaient à ses quatre pieds.
14 Pete hizo zilikuwa karibu na ule mzingo, ili kutegemeza ile miti ya kuibeba meza hiyo.
Les anneaux étaient près du rebord, pour recevoir les barres, pour porter la table;
15 Halafu akafanya ile miti ya mshita na kuifunika kwa dhahabu ili kuibeba ile meza.
et il fit les barres de bois de sittim, et les plaqua d’or, pour porter la table.
16 Baada ya hilo akafanya kutokana na dhahabu safi vile vyombo vilivyo juu ya meza, sahani zake na vikombe vyake na mabakuli yake na mitungi yake iliyotumiwa kumimina matoleo ya kinywaji.
Et il fit d’or pur les ustensiles qui étaient sur la table, ses plats, et ses coupes, et ses vases, et les gobelets avec lesquels on fait les libations.
17 Kisha akafanya kinara cha taa cha dhahabu safi. Kwa kazi ya kufua akakifanya kinara cha taa. Pande zake na matawi yake, vikombe vyake, mafundo yake na maua yake vikatokea kwake.
Et il fit le chandelier d’or pur; il fit le chandelier [d’or] battu; son pied, et sa tige, ses calices, ses pommes, et ses fleurs, étaient [tirés] de lui;
18 Na matawi sita yalikuwa yakitoka kwenye pande zake, matawi matatu ya kinara cha taa kutoka kwenye upande wake mmoja na matawi mengine matatu ya kinara cha taa kutoka kwenye ule upande wake mwingine.
et six branches sortaient de ses côtés, trois branches du chandelier d’un côté, et trois branches du chandelier de l’autre côté.
19 Vikombe vitatu vyenye umbo la maua ya mlozi vilikuwa kwenye kikundi kimoja cha matawi, vifundo na maua yakifuatana; na vikombe vitatu vyenye umbo la maua ya mlozi vilikuwa kwenye kile kikundi kingine cha matawi, vifundo na maua yakifuatana. Hivyo ndivyo ilivyokuwa kwa yale matawi sita yaliyokuwa yakitoka katika kile kinara cha taa.
Il y avait, sur une branche, trois calices en forme de fleur d’amandier, une pomme et une fleur, et, sur une [autre] branche, trois calices en forme de fleur d’amandier, une pomme et une fleur; ainsi pour les six branches sortant du chandelier.
20 Na kwenye kile kinara cha taa kulikuwa na vikombe vinne vyenye umbo la maua ya mlozi, vifundo vyake na maua yake yakifuatana.
Et il y avait au chandelier quatre calices en forme de fleur d’amandier, ses pommes et ses fleurs;
21 Na kile kifundo chini ya matawi mawili kilitoka kwake, na kifundo kilicho chini ya yale matawi mengine mawili kilitoka kwake, na kifundo kingine kilicho chini ya matawi mengine mawili zaidi kilitoka kwake, kwa ajili ya matawi sita yanayotoka katika kinara.
et une pomme sous deux branches [sortant] de lui, et une pomme sous deux branches [sortant] de lui, et une pomme sous deux branches [sortant] de lui, pour les six branches qui sortaient de lui;
22 Vifundo vyake na matawi yake vilitoka kwake, vyote vilikuwa kitu kimoja cha kazi ya kufua, cha dhahabu safi.
leurs pommes et leurs branches étaient [tirées] de lui, le tout battu, d’une pièce, d’or pur.
23 Kisha akafanya taa zake saba na mikasi ya tambi zake na vyetezo vyake kutokana na dhahabu safi.
– Et il fit ses sept lampes, et ses mouchettes, et ses vases à cendre, d’or pur:
24 Alikifanya kwa talanta ya dhahabu safi, hicho pamoja na vyombo vyake vyote.
il le fit, avec tous ses ustensiles, d’un talent d’or pur.
25 Sasa akafanya madhabahu ya uvumba kutokana na mbao za mshita. Mkono mmoja urefu wake na mkono mmoja upana wake, ikiwa mraba, na mikono miwili kimo chake. Pembe zake zilitoka kwake.
Et il fit l’autel de l’encens, de bois de sittim: sa longueur était d’une coudée, et sa largeur d’une coudée; il était carré; et sa hauteur était de deux coudées; ses cornes étaient [tirées] de lui.
26 Kisha akaifunika kwa dhahabu safi, upande wake wa juu na pande zake za kando kuizunguka na pembe zake, naye akafanya ukingo wa dhahabu kuizunguka pande zote.
Et il le plaqua d’or pur, le dessus et ses parois, tout autour, et ses cornes. Et il lui fit un couronnement d’or tout autour.
27 Naye akaifanyia pete mbili za dhahabu chini ya ukingo wake kwenye pande zake mbili, kwenye pande zake mbili zinazoelekeana, za kutegemeza ile miti ya kuibeba.
Et il lui fit deux anneaux d’or au-dessous de son couronnement, sur ses deux côtés, à ses deux coins, pour recevoir les barres, pour le porter par elles.
28 Kisha akafanya ile miti ya mshita na kuifunika kwa dhahabu.
Et il fit les barres de bois de sittim, et les plaqua d’or.
29 Tena akafanya yale mafuta yanayotumiwa kutia mafuta na ule uvumba safi uliotiwa manukato, kazi ya mtengenezaji wa marhamu.
Et il fit l’huile sainte de l’onction et le pur encens des drogues odoriférantes, d’ouvrage de parfumeur.

< Kutoka 37 >