< Kutoka 36 >

1 Hivyo Bezaleli na Oholiabu na kila mtu mwenye ustadi ambaye Yahweh aliye mpa ustadi na uwezo kujua jinsi ya kufanya kazi katika ujenzi wa sehemu takatifu wafanye kazi kadiri ya yote Yahweh aliyo amuru.”
Bezaleel, Oholiab y todo artesano hábil, a quienes Yavé dotó de capacidad y entendimiento para hacer toda obra para el servicio del Santuario, hicieron según todo lo que Yavé ordenó.
2 Musa akamuita Bezaleli, Oholiabu, na kila mtu mwenye ujuzi ambaye Yahweh kampa ujuzi, na ambaye moyoni mwake ulichochewa kuja na kufanya kazi.
Moisés llamó a Bezaleel, a Oholiab y a todo artesano hábil en cuyo corazón Yavé puso sabiduría, a todo aquel cuyo corazón lo impulsó a ir a la obra para hacerla.
3 Walipokea kutoka kwa Musa sadaka zote ambazo Waisraeli walizo leta kwa ujenzi ya sehemu takatifu. Watu walikuwa bado wanaleta sadaka za hiari kila asubui kwa Musa.
En la presencia de Moisés tomaron toda la contribución que los hijos de Israel llevaron para la obra del servicio del Santuario a fin de realizarla. Ellos llevaban contribución voluntaria cada mañana.
4 Hivyo watu wote walikuwa na ujuzi walikuwa wakifanya kazi sehemu takatifu walikuja kutoka kwenye kazi walikuwa wakifanya.
Tanto así que todos los maestros que hacían toda la obra del Santuario, cada uno en la obra que hacía,
5 Wachonga mawe walimwabia Musa, “Watu wanaleta zaidi sana ya yanayo itajika kufanya kazi Yahweh aliyo tuamuru.”
fueron a Moisés y dijeron: El pueblo trae mucho más de lo que es necesario para el servicio de la obra que Yavé ordenó que se haga.
6 Hivyo Musa akaamuru mtu yeyote asilete tena kwa ujenzi wa sehemu takatifu. Kisha watu wakaacha kuleta hivi vitu.
Entonces Moisés dio orden, y pregonaron por el campamento: ¡Nadie, hombre o mujer, haga algo más como contribución para el Santuario! Y así se impidió al pueblo llevar más,
7 Walikuwa na zaidi ya vitu vya ujenzi.
pues el material que tenían era suficiente y aun más que suficiente para hacer toda la obra.
8 Hivyo wachonga mawe miongoni mwao wakajenga lile hema la kuabudia kwa mapazia kumi yaliyo jengwa kitamba kizuri na buluu, zambarau, na sufu nyekundu kwa aina ya kerubi. Hii ni kazi ya Bezaleli, mjenzi mwenye ujuzi sana.
Todos los hábiles artesanos, entre los que hacían la obra, hicieron el Tabernáculo de diez cortinas de cordoncillo de lino fino, y [tela] azul, púrpura y carmesí. Las hicieron con querubines, como obra de hábil artífice.
9 Urefu wa kila pazia ulikuwa mikono ishirini na nane, nao upana wa kila kitambaa ulikuwa mikono minne. Vitambaa vyote hivyo vilikuwa na kipimo kimoja.
La longitud de cada cortina era de 12,6 metros, y la anchura de 1,8 metros. Todas las cortinas tenían una misma medida.
10 Bezaleli akaunganisha vitambaa vitano pamoja, na vile vitambaa vingine vitano akaviunganisha pamoja.
Él unió cinco cortinas la una con la otra, y de igual manera las otras cinco.
11 Kisha akafanya vitanzi vya uzi wa bluu kwenye upindo wa kitambaa kilicho mahali pa kuungania. Akafanya vivyo hivyo kwenye upindo wa kitambaa cha nje kabisa kilicho mahali pale pengine pa kuungania.
Hizo unas presillas de azul en la unión del borde de la cortina del extremo. Lo mismo hizo en el otro extremo de la segunda.
12 Akafanya vitanzi hamsini kwenye kitambaa kimoja, akafanya vitanzi hamsini kwenye mwisho wa kitambaa kilichokuwa mahali pale pengine pa kuungania, vitanzi hivyo vikiwa vinaelekeana.
Hizo 50 presillas en una cortina y 50 en la segunda cortina que estaba en la unión. Las presillas se correspondían unas con otras.
13 Mwishowe akafanya kulabu hamsini za dhahabu na kuviunganisha vitambaa hivyo pamoja kwa kulabu hizo, hivi kwamba hiyo ikawa maskani moja.
Hizo también 50 broches de oro. Con los broches unió las cortinas la una con la otra, y así el Tabernáculo fue una unidad.
14 Bezaleli akafanya vitambaa vya mahema vya manyoya ya mbuzi kwa ajili ya hema lililo juu ya maskani. Vitambaa kumi na moja ndivyo alivyofanyiza.
Hizo también 11 cortinas de pelo de cabra para formar una tienda sobre el Tabernáculo.
15 Urefu wa kila kitambaa ulikuwa mikono thelathini, nao upana wa kila kitambaa ulikuwa mikono minne. Vitambaa hivyo kumi na moja vilikuwa na kipimo kimoja.
La longitud de cada cortina era de 13,5 metros, y la anchura de 1,8 metros. Las 11 cortinas tenían una misma medida.
16 Kisha akaunganisha vitambaa vitano pamoja na vile vitambaa vingine sita pamoja.
Unió cinco cortinas por una parte y seis por la otra.
17 Kisha akafanya vitanzi hamsini kwenye upindo wa kitambaa cha nje kabisa kilicho mahali pa kuungania, naye akafanya vitanzi hamsini kwenye upindo wa kile kitambaa kingine kilichoungana nacho.
Hizo 50 presillas en el borde de una cortina en la unión, y otras 50 en el borde de la segunda serie.
18 Bezaleli akafanya kulabu hamsini za shaba kwa ajili ya kuliunganisha hilo hema pamoja liwe kipande kimoja.
Luego hizo 50 broches de bronce para unir la Tienda de modo que fuera una unidad.
19 Naye akafanya kifuniko cha hema kutokana na ngozi za kondoo dume zilizotiwa rangi nyekundu na kifuniko kutokana na ngozi za sili, upande wa juu.
Para el Tabernáculo hizo una cubierta de pieles de carnero teñidas de rojo, y otra cubierta de pieles de tejones por encima.
20 Bezaleli akafanya viunzi vya mbao vya hema ya kukutani kutokana na mbao za mshita.
Además hizo para el Tabernáculo los tablones de madera de acacia que serían colocados de manera vertical.
21 Urefu wa kiunzi ulikuwa mikono kumi, nao upana wa kila kiunzi ulikuwa mkono mmoja na nusu.
La longitud de cada tablón era de 4,5 metros, y la anchura, de 67,5 centímetros.
22 Kila kiunzi kilikuwa na ndimi mbili zilizounganishwa. Hivyo ndivyo alivyofanya viunzi vyote vya maskani.
Cada tablón tenía dos espigas para ser unidos el uno con el otro. Así hizo con todos los tablones del Tabernáculo.
23 Basi akafanya viunzi vya maskani, viunzi ishirini kwa ajili ya upande kuelekea kusini.
Hizo, pues, los tablones para el Tabernáculo: 20 tablones para el lado sur.
24 Bezaleli akafanya vikalio arobaini vya fedha viwe chini ya vile viunzi ishirini, vikalio viwili chini ya kiunzi kimoja pamoja na ndimi zake mbili na vikalio vingine viwili chini ya kiunzi kingine pamoja na ndimi zake mbili.
Hizo 40 basas de plata para poner debajo de los 20 tablones: dos basas debajo de un tablón para ponerlas en sus dos espigas, y dos basas debajo del otro.
25 Na kwa ajili ya ule upande mwingine wa maskani, upande wa kaskazini, akafanya viunzi ishirini
Para el lado norte del Tabernáculo hizo 20 tablones
26 na vikalio vyake arobaini vya fedha. Vikalio viwili chini ya kiunzi kimoja na vikalio viwili chini ya kiunzi kingine
y 40 basas de plata: dos basas debajo de un tablón y dos basas debajo del otro.
27 Na kwa ajili ya zile pande za nyuma za maskani kuelekea magharibi akafanya viunzi sita.
Para el lado posterior del Tabernáculo, al occidente, hizo seis tablones.
28 Naye akafanya viunzi viwili vya pembeni ya maskani kwenye pande zake mbili za nyuma
Para las esquinas del Tabernáculo en los dos extremos hizo dos tablones,
29 Hizi zilikuwa pacha upande wa chini, lakini juu ya kila moja kwenye pete ya kwanza. Hivyo ndivyo alivyoifanya yote miwili, ile miimo ya pembeni.
los cuales eran acoplados por abajo y acoplados por arriba con un aro. Así hizo los dos para las dos esquinas.
30 Basi vikajumlika kuwa viunzi vinane na vikalio vyake kumi na sita vya fedha, vikalio viwili kando ya vikalio viwili chini ya kila kiunzi.
Así que eran ocho tablones, y sus basas de plata eran 16: dos basas debajo de cada tablón.
31 Bezaleli akafanya miti ya mshita, mitano kwa ajili ya viunzi vya upande mmoja wa maskani,
También hizo los travesaños de madera de acacia: cinco para los tablones de un lado del Tabernáculo,
32 na miti mitano kwa ajili ya viunzi vya upande ule mwingine wa maskani na miti mitano kwa ajili ya viunzi vya maskani kwa ajili ya zile pande mbili za nyuma za magharibi.
cinco travesaños para el otro lado, y cinco travesaños para los tablones de la parte posterior del Tabernáculo, al occidente.
33 Kisha akafanya mti wa katikati upitie katikati ya vile viunzi toka mwisho mmoja mpaka ule mwingine.
Hizo el travesaño del centro para que pasara por la mitad de los tablones de un extremo al otro.
34 Naye akavifunika vile viunzi kwa dhahabu, akafanyiza pete zake za dhahabu ziwe vitegemezo kwa ajili ya ile miti, akaifunika ile miti kwa dhahabu.
Recubrió de oro los tablones y los travesaños. También hizo las argollas de oro por las cuales pasarían las varas.
35 Bezaleli akafanya pazia, la uzi wa bluu na sufu iliyotiwa rangi ya zambarau na kitambaa cha rangi nyekundu ya kochinili na kitani bora kilichosokotwa, kalitia makerubi kwa kazi ya mjenzi.
Hizo la cortina de azul, púrpura y carmesí y cordoncillo de lino fino. La hizo con querubines, obra de hábil artífice.
36 Kisha akalifanyia nguzo nne za mshita na kuzifunika kwa dhahabu, vibanio vyake vikiwa vya dhahabu, na kutengeneza vikalio vinne vya fedha kwa ajili yake.
Para la cortina hizo cuatro columnas de acacia recubiertas de oro, con sus capiteles de oro. Fundió para ellas cuatro basas de plata.
37 Naye akafanya kisitiri kwa ajili ya mwingilio wa hema kutokana na uzi wa bluu na sufu iliyotiwa rangi ya zambarau na kitambaa chenye rangi nyekundu ya kochinili na kitani bora kilichosokotwa, kazi ya mfumaji.
Hizo también la cortina para la entrada al Tabernáculo de azul, púrpura y carmesí, y cordoncillo de lino fino, obra de bordador.
38 Pia akafanya na nguzo zake tano na vibanio vyake. Naye akavifunika vilele vyake na viungo vyake kwa dhahabu, lakini vile vikalio vyake vitano vilikuwa vya shaba.
[Colocó] también las cinco columnas con sus capiteles, y cubrió sus capiteles y sus molduras de oro. Pero sus cinco basas eran de bronce.

< Kutoka 36 >