< Kutoka 36 >

1 Hivyo Bezaleli na Oholiabu na kila mtu mwenye ustadi ambaye Yahweh aliye mpa ustadi na uwezo kujua jinsi ya kufanya kazi katika ujenzi wa sehemu takatifu wafanye kazi kadiri ya yote Yahweh aliyo amuru.”
And Bezaleel, and Aholiab, and every wise-hearted man, in whom Jehovah hath given wisdom and understanding to know to do every work of the service of the sanctuary, have done according to all that Jehovah commanded.
2 Musa akamuita Bezaleli, Oholiabu, na kila mtu mwenye ujuzi ambaye Yahweh kampa ujuzi, na ambaye moyoni mwake ulichochewa kuja na kufanya kazi.
And Moses calleth unto Bezaleel, and unto Aholiab, and unto every wise-hearted man in whose heart Jehovah hath given wisdom, every one whom his heart lifted up, to come near unto the work to do it.
3 Walipokea kutoka kwa Musa sadaka zote ambazo Waisraeli walizo leta kwa ujenzi ya sehemu takatifu. Watu walikuwa bado wanaleta sadaka za hiari kila asubui kwa Musa.
And they take from before Moses all the heave-offering which the sons of Israel have brought in for the work of the service of the sanctuary to do it; and still they have brought in unto him a willing-offering morning by morning.
4 Hivyo watu wote walikuwa na ujuzi walikuwa wakifanya kazi sehemu takatifu walikuja kutoka kwenye kazi walikuwa wakifanya.
And all the wise men, who are doing all the work of the sanctuary, come each from his work which they are doing,
5 Wachonga mawe walimwabia Musa, “Watu wanaleta zaidi sana ya yanayo itajika kufanya kazi Yahweh aliyo tuamuru.”
and speak unto Moses, saying, 'The people are multiplying to bring in more than sufficient for the service of the work which Jehovah commanded to make.'
6 Hivyo Musa akaamuru mtu yeyote asilete tena kwa ujenzi wa sehemu takatifu. Kisha watu wakaacha kuleta hivi vitu.
And Moses commandeth, and they cause a voice to pass over through the camp, saying, 'Let not man or woman make any more work for the heave-offering of the sanctuary;' and the people are restrained from bringing,
7 Walikuwa na zaidi ya vitu vya ujenzi.
and the work hath been sufficient for them, for all the work, to do it, and to leave.
8 Hivyo wachonga mawe miongoni mwao wakajenga lile hema la kuabudia kwa mapazia kumi yaliyo jengwa kitamba kizuri na buluu, zambarau, na sufu nyekundu kwa aina ya kerubi. Hii ni kazi ya Bezaleli, mjenzi mwenye ujuzi sana.
And all the wise-hearted ones among the doers of the work make the tabernacle; ten curtains of twined linen, and blue, and purple, and scarlet, [with] cherubs, work of a designer, he hath made them.
9 Urefu wa kila pazia ulikuwa mikono ishirini na nane, nao upana wa kila kitambaa ulikuwa mikono minne. Vitambaa vyote hivyo vilikuwa na kipimo kimoja.
The length of the one curtain [is] eight and twenty by the cubit, and the breadth of the one curtain four by the cubit; one measure [is] to all the curtains.
10 Bezaleli akaunganisha vitambaa vitano pamoja, na vile vitambaa vingine vitano akaviunganisha pamoja.
And he joineth the five curtains one unto another, and the [other] five curtains he hath joined one unto another;
11 Kisha akafanya vitanzi vya uzi wa bluu kwenye upindo wa kitambaa kilicho mahali pa kuungania. Akafanya vivyo hivyo kwenye upindo wa kitambaa cha nje kabisa kilicho mahali pale pengine pa kuungania.
and he maketh loops of blue on the edge of the one curtain, at the end, in the joining; so he hath made in the edge of the outmost curtain, in the joining of the second;
12 Akafanya vitanzi hamsini kwenye kitambaa kimoja, akafanya vitanzi hamsini kwenye mwisho wa kitambaa kilichokuwa mahali pale pengine pa kuungania, vitanzi hivyo vikiwa vinaelekeana.
fifty loops he hath made in the one curtain, and fifty loops hath he made in the end of the curtain which [is] in the joining of the second; the loops are taking hold one on another.
13 Mwishowe akafanya kulabu hamsini za dhahabu na kuviunganisha vitambaa hivyo pamoja kwa kulabu hizo, hivi kwamba hiyo ikawa maskani moja.
And he maketh fifty hooks of gold, and joineth the curtains one unto another by the hooks, and the tabernacle is one.
14 Bezaleli akafanya vitambaa vya mahema vya manyoya ya mbuzi kwa ajili ya hema lililo juu ya maskani. Vitambaa kumi na moja ndivyo alivyofanyiza.
And he maketh curtains of goats' [hair] for a tent over the tabernacle; eleven curtains he hath made them;
15 Urefu wa kila kitambaa ulikuwa mikono thelathini, nao upana wa kila kitambaa ulikuwa mikono minne. Vitambaa hivyo kumi na moja vilikuwa na kipimo kimoja.
the length of the one curtain [is] thirty by the cubit, and the breadth of the one curtain [is] four cubits; one measure [is] to the eleven curtains;
16 Kisha akaunganisha vitambaa vitano pamoja na vile vitambaa vingine sita pamoja.
and he joineth the five curtains apart, and the six curtains apart.
17 Kisha akafanya vitanzi hamsini kwenye upindo wa kitambaa cha nje kabisa kilicho mahali pa kuungania, naye akafanya vitanzi hamsini kwenye upindo wa kile kitambaa kingine kilichoungana nacho.
And he maketh fifty loops on the outer edge of the curtain, in the joining; and fifty loops he hath made on the edge of the curtain which is joining the second;
18 Bezaleli akafanya kulabu hamsini za shaba kwa ajili ya kuliunganisha hilo hema pamoja liwe kipande kimoja.
and he maketh fifty hooks of brass to join the tent — to be one;
19 Naye akafanya kifuniko cha hema kutokana na ngozi za kondoo dume zilizotiwa rangi nyekundu na kifuniko kutokana na ngozi za sili, upande wa juu.
and he maketh a covering for the tent of rams' skins made red, and a covering of badgers' skins above.
20 Bezaleli akafanya viunzi vya mbao vya hema ya kukutani kutokana na mbao za mshita.
And he maketh the boards for the tabernacle of shittim wood, standing up;
21 Urefu wa kiunzi ulikuwa mikono kumi, nao upana wa kila kiunzi ulikuwa mkono mmoja na nusu.
ten cubits [is] the length of the [one] board, and a cubit and a half the breadth of the [one] board;
22 Kila kiunzi kilikuwa na ndimi mbili zilizounganishwa. Hivyo ndivyo alivyofanya viunzi vyote vya maskani.
two handles [are] to the one board, joined one unto another; so he hath made for all the boards of the tabernacle.
23 Basi akafanya viunzi vya maskani, viunzi ishirini kwa ajili ya upande kuelekea kusini.
And he maketh the boards for the tabernacle; twenty boards for the south side southward;
24 Bezaleli akafanya vikalio arobaini vya fedha viwe chini ya vile viunzi ishirini, vikalio viwili chini ya kiunzi kimoja pamoja na ndimi zake mbili na vikalio vingine viwili chini ya kiunzi kingine pamoja na ndimi zake mbili.
and forty sockets of silver he hath made under the twenty boards, two sockets under the one board for its two handles, and two sockets under the other board for its two handles.
25 Na kwa ajili ya ule upande mwingine wa maskani, upande wa kaskazini, akafanya viunzi ishirini
And for the second side of the tabernacle, for the north side, he hath made twenty boards,
26 na vikalio vyake arobaini vya fedha. Vikalio viwili chini ya kiunzi kimoja na vikalio viwili chini ya kiunzi kingine
and their forty sockets of silver, two sockets under the one board, and two sockets under the other board;
27 Na kwa ajili ya zile pande za nyuma za maskani kuelekea magharibi akafanya viunzi sita.
and for the sides of the tabernacle, westward, hath he made six boards;
28 Naye akafanya viunzi viwili vya pembeni ya maskani kwenye pande zake mbili za nyuma
and two boards hath he made for the corners of the tabernacle, in the two sides;
29 Hizi zilikuwa pacha upande wa chini, lakini juu ya kila moja kwenye pete ya kwanza. Hivyo ndivyo alivyoifanya yote miwili, ile miimo ya pembeni.
and they have been twins below, and together they are twins at its head, at the one ring; so he hath done to both of them at the two corners;
30 Basi vikajumlika kuwa viunzi vinane na vikalio vyake kumi na sita vya fedha, vikalio viwili kando ya vikalio viwili chini ya kila kiunzi.
and there have been eight boards; and their sockets of silver [are] sixteen sockets, two sockets under the one board.
31 Bezaleli akafanya miti ya mshita, mitano kwa ajili ya viunzi vya upande mmoja wa maskani,
And he maketh bars of shittim wood, five for the boards of the one side of the tabernacle,
32 na miti mitano kwa ajili ya viunzi vya upande ule mwingine wa maskani na miti mitano kwa ajili ya viunzi vya maskani kwa ajili ya zile pande mbili za nyuma za magharibi.
and five bars for the boards of the second side of the tabernacle, and five bars for the boards of the tabernacle, for the sides westward;
33 Kisha akafanya mti wa katikati upitie katikati ya vile viunzi toka mwisho mmoja mpaka ule mwingine.
and he maketh the middle bar to enter into the midst of the boards from end to end;
34 Naye akavifunika vile viunzi kwa dhahabu, akafanyiza pete zake za dhahabu ziwe vitegemezo kwa ajili ya ile miti, akaifunika ile miti kwa dhahabu.
and the boards he hath overlaid with gold, and their rings he hath made of gold, places for bars, and he overlayeth the bars with gold.
35 Bezaleli akafanya pazia, la uzi wa bluu na sufu iliyotiwa rangi ya zambarau na kitambaa cha rangi nyekundu ya kochinili na kitani bora kilichosokotwa, kalitia makerubi kwa kazi ya mjenzi.
And he maketh the vail of blue, and purple, and scarlet, and twined linen, work of a designer he hath made it, [with] cherubs;
36 Kisha akalifanyia nguzo nne za mshita na kuzifunika kwa dhahabu, vibanio vyake vikiwa vya dhahabu, na kutengeneza vikalio vinne vya fedha kwa ajili yake.
and he maketh for it four pillars of shittim [wood], and overlayeth them with gold; their pegs [are] of gold; and he casteth for them four sockets of silver.
37 Naye akafanya kisitiri kwa ajili ya mwingilio wa hema kutokana na uzi wa bluu na sufu iliyotiwa rangi ya zambarau na kitambaa chenye rangi nyekundu ya kochinili na kitani bora kilichosokotwa, kazi ya mfumaji.
And he maketh a covering for the opening of the tent, of blue, and purple, and scarlet, and twined linen, work of an embroiderer,
38 Pia akafanya na nguzo zake tano na vibanio vyake. Naye akavifunika vilele vyake na viungo vyake kwa dhahabu, lakini vile vikalio vyake vitano vilikuwa vya shaba.
also its five pillars, and their pegs; and he overlaid their tops and their fillets [with] gold, and their five sockets [are] brass.

< Kutoka 36 >