< Kutoka 35 >

1 Musa akawakusanya jamii yote ya Waisraeli na kuwaambia, “Haya ndio mambo Yahweh aliyo waamuru mfanye.
Moses assembled all the congregation of the children of Israel, and said to them, "These are the words which Jehovah has commanded, that you should do them.
2 Kwa siku sita kazi ya weza fanywa, lakini kwako, siku ya saba lazima iwe siku takatifu, siku ya Sabato ya mapumziko, takatifu kwa Yahweh. Yeyote atakaye fanya kazi hiyo siku lazima auawe.
'Six days shall work be done, but on the seventh day there shall be a holy day for you, a Sabbath of solemn rest to Jehovah: whoever does any work in it shall be put to death.
3 Haupaswi kuwasha moto kwenye nyumba zenu siku ya Sabato.”
You shall kindle no fire throughout your habitations on the Sabbath day.'"
4 Musa akasema na jamii yote ya Waisraeli, kwa kusema, “Hichi ndicho kitu Yahweh alicho amuru.
Moses spoke to all the congregation of the children of Israel, saying, "This is the thing which Jehovah commanded, saying,
5 Chukuwa sadaka kwa ajili ya Yahweh, wote wenye moyo mkunjufu. Leta sadaka kwa Yahweh - dhahabu, fedha, shaba,
'Take from among you an offering to Jehovah. Whoever is of a willing heart, let him bring it, Jehovah's offering: gold, silver, bronze,
6 buluu, zambarau, sufu nyekundu na kitambaa kizuri; nywele za mbuzi;
blue, purple, scarlet, fine linen, goats' hair,
7 ngozi za kondoo zilizotiwa rangi nyekundu na ngozi za pomboo; na mbao za mshita;
rams' skins dyed red, sea cow hides, acacia wood,
8 mafuta ya taa kwa pahali patakatifu, viungo vya manukato kwa hayo mafuta ya kutiwa,
oil for the light, spices for the anointing oil and for the sweet incense,
9 kwa uvumba mzuri na vito vya shohamu na vito vya kutiwa kwa hiyo naivera, na kwa hicho kifuko cha kifuani.
onyx stones, and stones to be set for the ephod and for the breastplate.
10 Kila mwanaume mwenye ustadi kati yenu aje na afanye kila kitu ambacho Yahweh aliyaamuru —
"'Let every wise-hearted man among you come, and make all that Jehovah has commanded:
11 hema la kuabudia, na kifuniko chake, na vifungo vyake, na mbao zake, nguzo, na sakafu;
the tabernacle, its outer covering, its roof, its clasps, its boards, its bars, its pillars, and its sockets;
12 pia sanduku na nguzo zake, kiti cha rehema, na pazia la kusitiri.
the ark, and its poles, the mercy seat, the curtain to screen it;
13 Walileta meza na miguu yake, vyombo vyake vyote, na mkate wa wonyesho;
the table with its poles and all its vessels, and the show bread;
14 kinara cha taa, vyombo vyake, taa, na mafuta ya zile taa;
the lampstand also for the light, with its vessels, its lamps, and the oil for the light;
15 ile madhabahu ya uvumba na nguzo zake, mafuta ya upako na uvumba ulitiwa maukato; kishikizo cha mwingilio wa hema ya kuabudia;
and the altar of incense with its poles, the anointing oil, the sweet incense, the screen for the door, at the door of the tabernacle;
16 madhabahu ya sadaka ya kuteketeza na kitunzi cha shaba na nguzo na vyombo; na ile beseni kubwa na sakafu yake.
the altar of burnt offering, with its grating of bronze, its poles, and all its vessels, the basin and its base;
17 Walileta vishikizo kwa ajili ya nyuani na nguzo zake na sakafu yake, na pazia kwa ajili mwingilio wa nyauni;
the hangings of the court, its pillars, their sockets, and the screen for the gate of the court;
18 na ile misumari ya hema la kuabudia na nyuani, pamoja na kamba zake.
the pins of the tabernacle, the pins of the court, and their cords;
19 Walileta mavazi yaliyofumwa kutumikia sehemu takatifu, mavazi takatifu ya Aruni kuhani na wanae, kwa wao kutumika kama makuhani.”
the finely worked garments, for ministering in the holy place, the holy garments for Aaron the priest, and the garments of his sons, to minister in the priest's office.'"
20 Kisha makabila yote ya Israeli yakaondoka na kwenda kutoka uweponi mwa Musa.
All the congregation of the children of Israel departed from the presence of Moses.
21 Kila mtu moyo wake ulimchochea na aliye andaliwa na roho yake alikuja na kuleta sadaka kwa Yahweh kwa matengenezo ya hema ya kuabudia, kwa vitu vyote kwajili ya huduma ndani yake, na kwa vazi takatifu.
They came, everyone whose heart stirred him up, and everyone whom his spirit made willing, and brought Jehovah's offering, for the work of the Tent of Meeting, and for all of its service, and for the holy garments.
22 Walikuja, wote wanaume kwa wanawake, wote waliokuwa na moyo wa utayari. Walileta madini, hereni, pete, na vitu vya thamani, vitu vyote tofauti vyenye madini ya dhahabu. Waliwasilisha sadaka za dhahabu kama sadaka ya kupunga kwa Yahweh.
They came, both men and women, as many as were willing-hearted, and brought brooches, earrings, signet rings, and armlets, all jewels of gold; even every man who offered an offering of gold to Jehovah.
23 Kila mmoja alikuwa na sufu ya buluu, dhambarau, au nyekundu, nguo nzuri, singa za mbuzi, ngozi za kondoo zilizobadili kuwa nyekundu, na ngozi ya pomboo walivileta.
Everyone, with whom was found blue, purple, scarlet, fine linen, goats' hair, rams' skins dyed red, and sea cow hides, brought them.
24 kila mmoja alitengeneza sadaka ya fedha au shaba walizileta kama sadaka kwa Yahweh, na kila mmoja aliyekuwa na mti wa mshita kwa matumizi ya kazi aliuleta.
Everyone who did offer an offering of silver and bronze brought Jehovah's offering; and everyone, with whom was found acacia wood for any work of the service, brought it.
25 kila mwanamke mwenye ustadi walisokota sufu kwa mikono yao na walileta sufu walizosokota za buluu, dhambarau, au sufu nyekundu, au nguo nzuri.
All the women who were wise-hearted spun with their hands, and brought that which they had spun, the blue, the purple, the scarlet, and the fine linen.
26 Wanawake wote wenye mioyo iliyochochewa na walio na ustadi walisokota singa za mbuzi.
All the women whose heart stirred them up in wisdom spun the goats' hair.
27 Viongozi walileta mawe ya shohamu na mawe mengine kwaajili ya kuwekwa kwenye hiyo naivera na hicho kifuko cha kifuani;
And the leaders brought the onyx stones, and the stones to be set, for the ephod and for the breastplate;
28 walileta viungo na mafuta kwaajili ya taa, kwa mafuta ya upako, na kwa uvumba wa manukato.
and the spice, and the oil for the light, for the anointing oil, and for the sweet incense.
29 Waisraeli walileta sadaka ya hiyari kwa Yahweh; kila mwanaume na mwanamke ambao mioyo yao ilikuwa tayari walileta vifaa kwaajili kazi zote ambazo Yahweh aliamuru kupitia Musa zifanyike.
The children of Israel brought a freewill offering to Jehovah; every man and woman, whose heart made them willing to bring for all the work, which Jehovah had commanded to be made by Moses.
30 Musa alisema kwa waisraeli, “Tazama, Yahweh ameita kwa jina juu ya Bezaleli mwana wa Uri mwana wa Huri, kutoka kabila la Yuda.
Moses said to the children of Israel, "Look, God has called by name Bezalel the son of Uri, the son of Hur, of the tribe of Judah.
31 Aliijaza Bezaleli kwa Roho yake, kumpa hekima, uwelewa, na maarifa, kwa aina zote za ujenzi,
He has filled him with the Spirit of God, in wisdom, in understanding, in knowledge, and in all manner of workmanship;
32 kufanya sanaa ya ubunifu na kufanya kazi za dhahabu, shaba, na shaba;
and to make skillful works, to work in gold, in silver, in bronze,
33 pia kukata na kupanga mawe na mbao iliochongwa- kufanya kazi za aina zote kwa ubunifu na ujenzi.
in cutting of stones for setting, and in carving of wood, to work in all kinds of skillful workmanship.
34 Aliiweka kufundisha ndani ya moyo wake, yeye pamoja na Oholiabu mwana wa Ahisamaki, kutoka kabila la Dani.
He has put in his heart that he may teach, both he, and Oholiab, the son of Ahisamach, of the tribe of Dan.
35 Aliwajaza kwa ustadi wa kufanya kazi za aina zote, kufanya kazi ya kama kuchora mawe, kama mwerevu, kama mtia taraza katika nyuzi za rangu ya buluu, dhambarau, na nyekundu na nguo nzuri, na kama washonaji. Walikuwa wachonga mawe wa kazi zote, na walikuwa wabunifu wa sanaa.
He has filled them with wisdom of heart, to work all manner of workmanship, of the engraver, of the skillful workman, and of the embroiderer, in blue, in purple, in scarlet, and in fine linen, and of the weaver, even of those who do any workmanship, and of those who make skillful works.

< Kutoka 35 >