< Kutoka 34 >

1 Yahweh akamwabia Musa, “Kata mbao mbili za mawe kama zile za awali. Nitaandika kwenye hizi mbao za mawe maneno yaliyo kuwa kwenye mbao za mawe za mwanzo, mbao za mawe ulizo zivunja.
Adonai said to Moses [Drawn out], “Chisel two stone tablets like the first: and I will write on the tablets the words that were on the first tablets, which you broke.
2 Kuwa tayari asubui na uje Mlima Sinai, na uje mbele zangu juu ya mlima.
Be ready by the morning, and come up in the morning to Mount Sinai [Thorn], and present yourself there to me on the top of the mountain.
3 Hakuna atakaye kuja nawe. Usiruhusu mtu yeyote aonekana popote kwenye mlima. Hakuna kundi la mifugo wanao ruhusiwa ata kula mbele ya mlima.”
No one shall come up with you or be seen anywhere on the mountain. Do not let the flocks or herds graze in front of that mountain.”
4 Hivyo Musa akakata mbao mbili za mawe kama za mwanzo, na akaamka asubui mapema na kwenda juu ya Mlima Sinai, kama Yahweh alivyo muelekeza. Musa alibeba mbao za mawe mikononi mwake.
He chiseled two tablets of stone like the first; and Moses [Drawn out] rose up early in the morning, and went up to Mount Sinai [Thorn], as Adonai had enjoined him, and took in his hand two stone tablets.
5 Yahweh akaja chini katika wingu na akasima mbele za Musa, na akatamka jina “Yahweh.”
Adonai descended in the cloud, and stood with him there, and proclaimed Adonai’s name.
6 Yahweh akapita kwake na kukiri, “Yahweh, Yahweh, Mungu ni wa rehema na wa neema, sio mwepesi wa hasira, na anadumu katika uwaminifu wa agano na uadilifu,
Adonai passed by before him, and proclaimed, “Yud-Hey-Vav-Hey! Yahweh a merciful and gracious God, slow to anger, and abundant in cheshed ·loving-kindness· and truth,
7 ukishika uaminifu wa agano kwa vizazi maelfu, ukisamehe maasi, makosa, na dhambi. Lakini hamsafishi mwenye hatia. Ataleta adhabu ya dhambi za baba kwa watoto wao na watoto wa watoto wao, kwa kizazi cha tatu na hadi cha nne.”
keeping cheshed ·loving-kindness· for thousands, forgiving iniquity and disobedience and sin; and that will by no means clear the guilty, visiting the iniquity of the fathers on the children, and on the children’s children, on the third and on the fourth generation.”
8 Musa haraka akainamisha kichwa chake kwenye ardhi na kuabudu.
Moses [Drawn out] hurried and bowed his head toward the earth, and worshiped.
9 Kisha akasema, “Kama sasa nimepata upendeleo machoni pako, Bwana wangu, tafadhali nenda pamoja nasi, kwa kuwa hawa watu ni wa korofi. Samehe maasi yetu na dhambi zetu, na utuchukuwe kama urithi wako.”
He said, “If now I have found chen ·grace· in your sight, Lord, please let the Lord go among us; although this is a stiff-necked people; pardon our iniquity and our sin, and take us for your inheritance.”
10 Yahweh akasema, “Ona, ninakaribu kufanya agano. Mbele za watu wako, nitafanya maajabu ambayo hayajawai kufanywa duniani kote wala kwenye taifa lote. Watu wote miongoni mwako wataona matendo yangu, kwa kuwa ni kitu cha hofu ninacho fanya kwako.
He said, “Behold, I make a covenant ·binding contract between two or more parties·: before all your people I will do marvels, such as have not been worked in all the earth, nor in any nation; and all the people among which you are shall see the work of Adonai; for it is an awesome thing that I do with you.
11 Tii amri zangu leo. Ninawaondoa mbele yako Waamori, Wakanani, Wahivi, Wahiti, Waperizi, Wahivi, na Wayebusi.
Observe that which I enjoin you today. Behold, I divorce from before you the Amorite [Descendants of Talkers], the Canaanite [Descendant of Humbled], the Hittite [Descendant of Trembling fear], the Perizzite [Descendant of Belonging to village], the Hivite [Wicked], and the Jebusite [Descendants of Thresher].
12 Kuwa mwanglifu usifanye agano na wakazi wa nchi unayo kwenda, au wata kuwa mtego kwako.
Be careful, lest you make a covenant with the inhabitants of the land where you are going, lest it be for a snare in the middle of you:
13 Badala yake, lazima uvunje madhabahu zao, ponda nguzo zao za mawe, na kukata nguzo zao za Ashera.
but you shall break down their altars, and dash in pieces their pillars, and you shall cut down their Asherah poles;
14 Kwa kuwa wewe haupaswi kumuabudu mungu mwingine, maana Yahweh, ambaye jina lake ni Uwivu, ni Mungu wa uwivu.
for you shall hawa ·bow low, prostrate· to worship no other deity: for Adonai, whose name is Jealous, is a jealous God.
15 Hivyo kuwa mwangalifu usifanye agano na wakazi wa nchi, kwa kuwa wanajifanyia ukahaba kwa miungu yao, na wanatoa dhabihu kwa miungu yao. Kisha mmoja wao ata kukaribisha na wewe utakula baadhi ya dhabihu zake,
“Don’t make a covenant with the inhabitants of the land, lest they play the prostitute after their deities, and sacrifice to their deities, and one call you and you eat of his sacrifice;
16 na kisha utachukuwa baadhi ya mabinti zake kwa wanao, na mabinti wake watafanya ukahaba kwa miungu yao, na watafanya wanao kufanya ukahaba kwa miungu yao.
and you take of their daughters to your sons, and their daughters play the prostitute after their deities, and make your sons play the prostitute after their deities.
17 Usifanye Miungu ya chuma ya kuyayusha.
“You shall make no molten elohim ·deities· for yourselves.
18 Laziam ushike Sherehe ya Mkate Usiotiwachachu. Kama nilivyo kuamuru, lazima ule mkate usio na hamira kwa siku saba kwa muda uliotengwa wa mwezi wa Abibu, maana nikatika mwezi wa Abibu ulitoka Misri.
“You shall keep the festival of Matzah ·Unleavened bread·. Seven days you shall eat matzah ·unleavened bread·, as I enjoined you, at the time appointed in the month Abib; for in the month Abib you came out of Egypt [Abode of slavery].
19 Wazaliwa wote ni mwangu, ata mzaliwa wa kwanza wa kiume wa mifugo, yote ya ng'ombe na kondoo.
“All that opens the womb is mine; and all your livestock that is male, the firstborn of cow and sheep.
20 Lazima umnunue tena mzaliwa kwanza wa punda kwa kondoo, lakini usipo mnunua tena, kisha uivunje shingo yake. Lazima ununue tena wazaliwa wa kwanza wote wa wanao. Hakuna ata mmoja atakye kuja kwangu mikono mitupu.
You shall redeem the firstborn of a donkey with a lamb. If you will not redeem it, then you shall break its neck. You shall redeem all the firstborn of your sons. No one shall appear before me empty.
21 Utafanya kazi kwa siku sita, lakini siku ya saba utapumzika. Ata wakati wakilimo na wa mavuno, lazima upumzike.
“Six days you shall work, but on the seventh day you shall rest: in plowing time and in harvest you shall rest.
22 Lazima uadhimishe Sherehe ya Majuma kwa mazao ya kwanza ya mavuno ya ngano, na lazima uadhimishe Sherehe ya Makusanyo mwisho wa mwaka.
“You shall observe the festival of Shavu'ot ·Weeks· / Pentacost ·Fifty· with the first fruits of wheat harvest, and the festival of in-gathering at the turn of the year.
23 Mara tatu kwa mwaka wanaume wenu wote watajitokeza kwa Bwana Yahweh, Mungu wa Israeli.
Three times in the year all your males shall appear before the Lord Yahweh, Elohim Isra'el [He sustains breathing, God of God prevails].
24 Kwa kuwa nitaondoa mataifa mbele yenu na kutanua mipika. Hakuna atakaye tamani kuwa na ardhi yenu kama yao utakapo toka mbele za Yahweh mara tatu kwa mwaka.
For I will drive out nations before you and enlarge your borders; neither shall any man desire your land when you go up to appear before Adonai, your God, three times in the year.
25 Hautatoa damu ya dhabihu yangu na hamira yeyote, wala nyama yeyote kutoka dhabihu za Sherehe ya Pasaka kubaki hadi asubui.
“You shall not offer the blood of my sacrifice with leavened bread. The sacrifice of the festival of the Pesac ·Passover· shall not be left to the morning.
26 Lazima ulete matunda ya kwanza yalio bora kutoka nyumbani kwako. Usimchemshe mbuzi mtoto katika maziwa ya mama yake.”
“You shall bring the first of the first fruits of your ground to the house of Adonai your God. “You shall not boil a young goat in its mother’s milk fat.”
27 Yahweh akamwabia Musa, “Andika chini haya maneno, kwa kuwa nimejiahidi haya maneno niliyo yasema, na nimefanya agano kwako na Israeli.”
Adonai said to Moses [Drawn out], “Write you these words: for in accordance with these words I have made a covenant with you and with Israel [God prevails].”
28 Musa alikuwa huko na Yahweh kwa siku arobaini na usiku; hakula chakula chochote wala kunywa maji yeyote. Aliandika katika mbao maneno ya agano, Amri kumi.
He was there with Adonai forty days and forty nights; he neither ate bread, nor drank water. He wrote on the tablets the words of the covenant, the Ten Words.
29 Musa alipo shuka chini ya Mlima Sinai na mbao mbili za agano za ushuhuda mikononi mwake, hakujua kuwa ngozi ya kuwa uso wake ulikuwa wa'ngaa akizungumza na Mungu.
When Moses [Drawn out] came down from Mount Sinai [Thorn] with the two tablets of the testimony in Moses [Drawn out]’ hand, when he came down from the mountain, Moses [Drawn out] didn’t know that the skin of his face shone by reason of his speaking with him.
30 Wakati Aruni na Waisraeli walipo muona Musa, ngozi ya uso wake ulikuwa wa ng'aa, na waliogopa kuja karibu yake.
When Aaron [Light-bringer] and all the children of Israel [God prevails] saw Moses [Drawn out], behold, the skin of his face shone; and they were afraid to come near him.
31 Lakini Musa aliwaita, na Aruni na viongozi wa jamii wakaja kwake. Kisha Musa akasema nao.
Moses [Drawn out] called to them, and Aaron [Light-bringer] and all the rulers of the congregation teshuvah ·completely returned· to him; and Moses [Drawn out] spoke to them.
32 Baada ya haya, watu wote wa Israeli wakaja kwa Musa, na akawambia amri zote Yahweh alizo mpa katika Mlima Sinai.
Afterward all the children of Israel [God prevails] came near, and he enjoined to them all that Adonai had spoken with him on Mount Sinai [Thorn].
33 Musa alipo maliza kuzungumza nao, alifunika uso wake kwa kitambaa.
When Moses [Drawn out] was done speaking with them, he put a veil on his face.
34 Wakati Musa alipoenda mbele za Yahweh kusema naye, aliondoa kitambaa, hadi alipo toka. Alipo toka, aliwaambia Waisraeli alicho amriwa kusema.
But when Moses [Drawn out] went in before Adonai to speak with him, he removed the veil, until he came out; and he came out, and spoke to the children of Israel [God prevails] that which he was enjoined.
35 Waisraeli walipo muona Musa ana'ngaa uso, alirudisha kitambaa tena usoni mpaka alipokuwa anaenda kuongea na Yahweh.
The children of Israel [God prevails] saw Moses [Drawn out]’ face, that the skin of Moses [Drawn out]’ face shone: and Moses [Drawn out] put the veil on his face again, until he went in to speak with him.

< Kutoka 34 >