< Kutoka 31 >

1 Yahweh akasema na Musa,
Then Yahweh spoke to Moses and said,
2 “Angalia, nimemwita kwa jina lake Bezaleli mwana wa Uri, mwana wa Huri, wa kabila ya Yuda
“See, I have called by name Bezalel son of Uri son of Hur, from the tribe of Judah.
3 Nami nimemjaza Bezaleli na roho ya Mungu, katika hekima, na maarifa, na ujuzi, na mambo ya kazi ya kila aina,
I have filled Bezalel with my Spirit, to give him wisdom, understanding, and knowledge, for all kinds of craftsmanship,
4 ili abuni kazi za ustadi, kuwa fundi wa dhahabu, na wa fedha, na wa shaba,
to make artistic designs and to work in gold, silver, and bronze;
5 na kukata vito kwa kutiwa mahali, na kuchora miti, na kufanya kazi ya ustadi iwayo yote.
also to cut and set stones and to carve wood—to do all kinds of craftsmanship.
6 Tena, nimemchagua, awe pamoja naye Oholiabu, mwana wa Ahisamaki, wa kabila ya Dani. Nami nimetia hekima katika mioyo ya wote wenye moyo wa hekima, ili wapate kufanya vyote nilivyokuagiza. Hii ni,
In addition to him, I have appointed Oholiab son of Ahisamak, from the tribe of Dan. I have put skill into the hearts of all who are wise so that they may make all that I have commanded you. This includes
7 hema ya kukutania na sanduku la ushuhuda, na kiti cha rehema kilicho juu yake, na vyombo vyote vya Hema;
the tent of meeting, the ark of the testimony, the atonement lid on the ark, and all the furniture of the tent—
8 na meza, na vyombo vyake, na kinara cha taa safi pamoja na vyombo vyake vyote,
the table and its utensils, the pure lampstand with all its equipment, the incense altar,
9 na madhabahu ya kufukizia uvumba; na madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa na vyombo vyake vyote, na birika na tako lake.
the altar for burnt offerings with all its equipment, and the large basin with its base.
10 Pia mavazi yenye kufumwa kwa uzuri, na mavazi matakatifu ya Haruni kuhani, na mavazi ya wanawe, ili kutumika katika kazi ya ukuhani.
This also includes the finely-woven garments—the holy garments for Aaron the priest and those of his sons, reserved for me so that they may serve as priests.
11 Pia mafuta ya kutiwa, na uvumba wa manukato mazuri, kwa ajili ya mahali patakatifu; sawasawa na yote niliyokuagiza ndivyo watakavyofanya wao.
This also includes the anointing oil and the sweet incense for the holy place. These craftsmen must make all these things just as I have commanded you.”
12 akasema na Musa,
Then Yahweh spoke to Moses and said,
13 “Waambie wana wa Israeli, 'Hakika mtazishika Sabato zangu, kwa kuwa ni ishara kati ya mimi na ninyi katika vizazi vyenu vyote; ili mpate kujua ya kuwa mimi ndimi BWANA niwatakasaye ninyi.
“Tell the Israelites: 'You must certainly keep Yahweh's Sabbath days, for these will be a sign between him and you throughout your people's generations so that you may know that he is Yahweh, who sets you apart for himself.
14 Basi mtaishika hiyo Sabato; kwa kuwa ni takatifu kwenu; kila mtu atakayeitia unajisi hakika yake atauawa; kwa kuwa kila mtu afanyaye kazi katika siku hiyo, nafsi hiyo itakatiliwa mbali na watu wake.
So you must keep the Sabbath, for it must be treated by you as holy, reserved for him. Everyone who defiles it must surely be put to death. Whoever works on the Sabbath, that person must surely be cut off from his people.
15 Kazi itafanywa siku sita; lakini siku ya saba ni Sabato ya kustarehe kabisa, takatifu kwa BWANA; kila mtu atakayefanya kazi yo yote katika siku ya Sabato, hakika yake atauawa.
Work will be done for six days, but the seventh day is to be a Sabbath of complete rest, holy before Yahweh. Whoever does any work on the Sabbath day must surely be put to death.
16 Kwa ajili ya hayo wana wa Israeli wataishika Sabato. Kuiangalia sana hiyo Sabato katika vizazi vyao vyote, ni agano la milele.
Therefore the Israelites must keep the Sabbath. They must observe it throughout their people's generations as a permanent law.
17 Ni ishara kati ya mimi na wana wa Israeli milele; kwani kwa siku sita Yahweh alifanya mbingu na nchi, akastarehe kwa siku ya saba na kupumzika.
The Sabbath will always be a sign between Yahweh and the Israelites, for in six days Yahweh made heaven and earth, and on the seventh day he rested and was refreshed.'”
18 Hapo Mungu alipokuwa amekwisha zungumza na Musa katika mlima wa Sinai, akampa hizo mbao mbili za ushuhuda, mbao mbili za mawe, zilizoandikwa kwa mkono wake.
When God had finished talking with Moses on Mount Sinai, he gave him two tablets of covenant decrees, made of stone, written on by his own hand.

< Kutoka 31 >