< Kutoka 31 >

1 Yahweh akasema na Musa,
Adonai spoke to Moses [Drawn out], saying,
2 “Angalia, nimemwita kwa jina lake Bezaleli mwana wa Uri, mwana wa Huri, wa kabila ya Yuda
“Behold, I have called by name Bezalel the son of Uri, the son of Hur, of the tribe of Judah [Praised]:
3 Nami nimemjaza Bezaleli na roho ya Mungu, katika hekima, na maarifa, na ujuzi, na mambo ya kazi ya kila aina,
and I have filled him with the Spirit of God, in wisdom, and in understanding, and in knowledge, and in all kinds of workmanship,
4 ili abuni kazi za ustadi, kuwa fundi wa dhahabu, na wa fedha, na wa shaba,
to devise skillful works, to work in gold, and in silver, and in bronze,
5 na kukata vito kwa kutiwa mahali, na kuchora miti, na kufanya kazi ya ustadi iwayo yote.
and in cutting of stones for setting, and in carving of wood, to work in all kinds of workmanship.
6 Tena, nimemchagua, awe pamoja naye Oholiabu, mwana wa Ahisamaki, wa kabila ya Dani. Nami nimetia hekima katika mioyo ya wote wenye moyo wa hekima, ili wapate kufanya vyote nilivyokuagiza. Hii ni,
Behold, I myself have appointed with him Oholiab, the son of Ahisamach, of the tribe of Dan [He judged]; and in the heart of all who are wise-hearted I have put wisdom, that they may make all that I have enjoined you:
7 hema ya kukutania na sanduku la ushuhuda, na kiti cha rehema kilicho juu yake, na vyombo vyote vya Hema;
the Tent of Meeting, the ark of the testimony, the mercy seat that is on it, all the furniture of the Tent,
8 na meza, na vyombo vyake, na kinara cha taa safi pamoja na vyombo vyake vyote,
the table and its utensils, the pure menorah ·lamp· with all its utensils, the altar of incense,
9 na madhabahu ya kufukizia uvumba; na madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa na vyombo vyake vyote, na birika na tako lake.
the altar of burnt offering with all its utensils, the basin and its base,
10 Pia mavazi yenye kufumwa kwa uzuri, na mavazi matakatifu ya Haruni kuhani, na mavazi ya wanawe, ili kutumika katika kazi ya ukuhani.
the finely worked garments— the holy garments for Aaron [Light-bringer] the priest— the garments of his sons to minister in the priest’s office,
11 Pia mafuta ya kutiwa, na uvumba wa manukato mazuri, kwa ajili ya mahali patakatifu; sawasawa na yote niliyokuagiza ndivyo watakavyofanya wao.
the anointing oil, and the incense of sweet spices for the holy place: according to all that I have enjoined you they shall do.”
12 akasema na Musa,
Adonai spoke to Moses [Drawn out], saying,
13 “Waambie wana wa Israeli, 'Hakika mtazishika Sabato zangu, kwa kuwa ni ishara kati ya mimi na ninyi katika vizazi vyenu vyote; ili mpate kujua ya kuwa mimi ndimi BWANA niwatakasaye ninyi.
“Speak also to the children of Israel [God prevails], saying, ‘Most certainly you shall keep my Sabbaths: for it is a sign between me and you throughout all your generations; that you may know that I am Yahweh M’Kaddesh [Yahweh our Santifier / He sustains breathing who makes you holy].
14 Basi mtaishika hiyo Sabato; kwa kuwa ni takatifu kwenu; kila mtu atakayeitia unajisi hakika yake atauawa; kwa kuwa kila mtu afanyaye kazi katika siku hiyo, nafsi hiyo itakatiliwa mbali na watu wake.
You shall keep the Sabbath ·To cease· therefore; for it is holy to you. Everyone who profanes it shall surely be put to death; for whoever does any work therein, that soul shall be cut off from among his people.
15 Kazi itafanywa siku sita; lakini siku ya saba ni Sabato ya kustarehe kabisa, takatifu kwa BWANA; kila mtu atakayefanya kazi yo yote katika siku ya Sabato, hakika yake atauawa.
Six days shall work be done, but on the seventh day is a Sabbath ·To cease· of solemn rest, holy to Adonai. Whoever does any work on the Sabbath ·To cease· day shall surely be put to death.
16 Kwa ajili ya hayo wana wa Israeli wataishika Sabato. Kuiangalia sana hiyo Sabato katika vizazi vyao vyote, ni agano la milele.
Therefore the children of Israel [God prevails] shall keep the Sabbath ·To cease·, to observe the Sabbath ·To cease· throughout their generations, for a perpetual covenant ·binding contract between two or more parties·.
17 Ni ishara kati ya mimi na wana wa Israeli milele; kwani kwa siku sita Yahweh alifanya mbingu na nchi, akastarehe kwa siku ya saba na kupumzika.
It is a sign between me and the children of Israel [God prevails] forever; for in six days Adonai made heaven and earth, and on the seventh day he rested, and was refreshed.’”
18 Hapo Mungu alipokuwa amekwisha zungumza na Musa katika mlima wa Sinai, akampa hizo mbao mbili za ushuhuda, mbao mbili za mawe, zilizoandikwa kwa mkono wake.
He gave to Moses [Drawn out], when he finished speaking with him on Mount Sinai [Thorn], the two tablets of the testimony, stone tablets, written with the finger of God.

< Kutoka 31 >