< Kutoka 31 >

1 Yahweh akasema na Musa,
And the LORD spoke unto Moses, saying:
2 “Angalia, nimemwita kwa jina lake Bezaleli mwana wa Uri, mwana wa Huri, wa kabila ya Yuda
'See, I have called by name Bezalel the son of Uri, the son of Hur, of the tribe of Judah;
3 Nami nimemjaza Bezaleli na roho ya Mungu, katika hekima, na maarifa, na ujuzi, na mambo ya kazi ya kila aina,
and I have filled him with the spirit of God, in wisdom, and in understanding, and in knowledge, and in all manner of workmanship,
4 ili abuni kazi za ustadi, kuwa fundi wa dhahabu, na wa fedha, na wa shaba,
to devise skilful works, to work in gold, and in silver, and in brass,
5 na kukata vito kwa kutiwa mahali, na kuchora miti, na kufanya kazi ya ustadi iwayo yote.
and in cutting of stones for setting, and in carving of wood, to work in all manner of workmanship.
6 Tena, nimemchagua, awe pamoja naye Oholiabu, mwana wa Ahisamaki, wa kabila ya Dani. Nami nimetia hekima katika mioyo ya wote wenye moyo wa hekima, ili wapate kufanya vyote nilivyokuagiza. Hii ni,
And I, behold, I have appointed with him Oholiab, the son of Ahisamach, of the tribe of Dan; and in the hearts of all that are wise-hearted I have put wisdom, that they may make all that I have commanded thee:
7 hema ya kukutania na sanduku la ushuhuda, na kiti cha rehema kilicho juu yake, na vyombo vyote vya Hema;
the tent of meeting, and the ark of the testimony, and the ark-cover that is thereupon, and all the furniture of the Tent;
8 na meza, na vyombo vyake, na kinara cha taa safi pamoja na vyombo vyake vyote,
and the table and its vessels, and the pure candlestick with all its vessels, and the altar of incense;
9 na madhabahu ya kufukizia uvumba; na madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa na vyombo vyake vyote, na birika na tako lake.
and the altar of burnt-offering with all its vessels, and the laver and its base;
10 Pia mavazi yenye kufumwa kwa uzuri, na mavazi matakatifu ya Haruni kuhani, na mavazi ya wanawe, ili kutumika katika kazi ya ukuhani.
and the plaited garments, and the holy garments for Aaron the priest, and the garments of his sons, to minister in the priest's office;
11 Pia mafuta ya kutiwa, na uvumba wa manukato mazuri, kwa ajili ya mahali patakatifu; sawasawa na yote niliyokuagiza ndivyo watakavyofanya wao.
and the anointing oil, and the incense of sweet spices for the holy place; according to all that I have commanded thee shall they do.'
12 akasema na Musa,
And the LORD spoke unto Moses, saying:
13 “Waambie wana wa Israeli, 'Hakika mtazishika Sabato zangu, kwa kuwa ni ishara kati ya mimi na ninyi katika vizazi vyenu vyote; ili mpate kujua ya kuwa mimi ndimi BWANA niwatakasaye ninyi.
'Speak thou also unto the children of Israel, saying: Verily ye shall keep My sabbaths, for it is a sign between Me and you throughout your generations, that ye may know that I am the LORD who sanctify you.
14 Basi mtaishika hiyo Sabato; kwa kuwa ni takatifu kwenu; kila mtu atakayeitia unajisi hakika yake atauawa; kwa kuwa kila mtu afanyaye kazi katika siku hiyo, nafsi hiyo itakatiliwa mbali na watu wake.
Ye shall keep the sabbath therefore, for it is holy unto you; every one that profaneth it shall surely be put to death; for whosoever doeth any work therein, that soul shall be cut off from among his people.
15 Kazi itafanywa siku sita; lakini siku ya saba ni Sabato ya kustarehe kabisa, takatifu kwa BWANA; kila mtu atakayefanya kazi yo yote katika siku ya Sabato, hakika yake atauawa.
Six days shall work be done; but on the seventh day is a sabbath of solemn rest, holy to the LORD; whosoever doeth any work in the sabbath day, he shall surely be put to death.
16 Kwa ajili ya hayo wana wa Israeli wataishika Sabato. Kuiangalia sana hiyo Sabato katika vizazi vyao vyote, ni agano la milele.
Wherefore the children of Israel shall keep the sabbath, to observe the sabbath throughout their generations, for a perpetual covenant.
17 Ni ishara kati ya mimi na wana wa Israeli milele; kwani kwa siku sita Yahweh alifanya mbingu na nchi, akastarehe kwa siku ya saba na kupumzika.
It is a sign between Me and the children of Israel for ever; for in six days the LORD made heaven and earth, and on the seventh day He ceased from work and rested.'
18 Hapo Mungu alipokuwa amekwisha zungumza na Musa katika mlima wa Sinai, akampa hizo mbao mbili za ushuhuda, mbao mbili za mawe, zilizoandikwa kwa mkono wake.
And He gave unto Moses, when He had made an end of speaking with him upon mount Sinai, the two tables of the testimony, tables of stone, written with the finger of God.

< Kutoka 31 >