< Kutoka 29 >

1 Sasa Hivi ndivyo wapaswa kufanya kuwatenga ili wanitumikie kama makuhani. Chukuwa mtoto wa ng'ombe dume na kondoo bila lawama,
“This is the thing that you shall do to them to make them holy, to minister to me in the priest’s office: take one young bull and two rams without defect,
2 mkate bila hamira, na keki bila hamira iliyo changanywa na mafuta. Pia chukuwa maandazi bila hamira yalio pakwa mafuta. Fanya maandazi kwa unga mzuri wa ngano.
matzah ·unleavened bread·, unleavened cakes mixed with oil, and unleavened wafers anointed with oil: you shall make them of fine wheat flour.
3 Lazima uweke kwenye ndoo moja, leta kwenye ndoo, na kuleta pamoja na ng'ombe dume na wana kondoo wawili.
You shall put them into one basket, and bring them in the basket, with the bull and the two rams.
4 Lazima nawe umlete Aruni na wana wake wawili katika lango la kuingilia hema la kukutania. Lazima uwasafishe Aruni na wana wake kwenye maji.
You shall bring Aaron [Light-bringer] and his sons to the door of the Tent of Meeting, and shall wash them with water.
5 Kisha twaa hayo mavazi na kumvika Haruni; itie kanzu, na joho ya naivera, na naivera, na kifuko cha kifuani, na kumkaza kwa huo mshipi wa naivera uliosukwa kwa ustadi.
You shall take the garments, and put on Aaron [Light-bringer] the coat, the robe of the ephod, the ephod, and the breastplate, and clothe him with the skillfully woven band of the ephod;
6 Nawe mvike kile kilemba kichwani, na ile taji takatifu utaitia katika kile kilemba.
and you shall set the turban on his head, and put the holy crown on the turban.
7 Ndipo utakapotwaa hayo mafuta ya kutiwa, na kummiminia kichwani mwake, na kumtia mafuta.
Then you shall take the anointing oil, and pour it on his head, and anoint him.
8 Kisha walete hao wanawe na kuwavika kanzu.
You shall bring his sons, and put coats on them.
9 Nawe uwakaze mishipi, Aruni na wanawe, na kuwavika kofia. Nao watakuwa na huo ukuhani kwa amri ya milele. Nawe utawaweka Haruni na wanawe kwa kazi takatifu.
You shall clothe them with belts, Aaron [Light-bringer] and his sons, and bind headbands on them: and they shall have the priesthood by a perpetual regulation: and you shall consecrate Aaron [Light-bringer] and his sons.
10 Kisha utamleta huyo ng’ombe mbele ya hema ya kukutania; na Haruni na wanawe wataweka mikono yao juu ya kichwa cha huyo ng’ombe.
“You shall bring the bull before the Tent of Meeting: and Aaron [Light-bringer] and his sons shall lay their hands on the head of the bull.
11 Kisha utamchinja huyo ng’ombe mbele ya Yahweh pa hema ya kukutania. BWANA,
You shall kill the bull before Adonai, at the door of the Tent of Meeting.
12 Kisha twaa baadhi ya damu ya ng’ombe, uitie katika pembe za madhabahu kwa kidole chako; na kuimimina damu yote chini ya madhabahu.
You shall take of the blood of the bull, and put it on the horns of the altar with your finger; and you shall pour out all the blood at the base of the altar.
13 Kisha chukuwa mafuta yote yafunikayo matumbo, na kitambi kilicho katika ini, na figo mbili, na mafuta yaliyo juu yake, uyateketeze yote juu ya madhabahu.
You shall take all the fat that covers the innards, the cover of the liver, the two kidneys, and the fat that is on them, and burn them on the altar.
14 Lakini nyama yake huyo ng’ombe, na ngozi yake, na mavi yake, utayachoma kwa moto nje ya marago; ni sadaka kwa ajili ya dhambi.
But the meat of the bull, and its skin, and its dung, you shall burn with fire outside of the camp: it is a sin offering.
15 Pia mtwae kondoo mume mmoja; na Aruni na wanawe wataweka mikono yao juu ya kichwa chake huyo kondoo mume.
“You shall also take the one ram; and Aaron [Light-bringer] and his sons shall lay their hands on the head of the ram.
16 Kisha utamchinja huyo kondoo mume, na kuitwaa damu yake, na kuinyunyiza katika madhabahu kuizunguka kando-kando.
You shall kill the ram, and you shall take its blood, and sprinkle it around on the altar.
17 Kisha utamkata-kata kondoo vipande vyake, na kuyaosha matumbo yake na miguu yake, na kuiweka pamoja na vipande vyake na kichwa chake,
You shall cut the ram into its pieces, and wash its innards, and its legs, and put them with its pieces, and with its head.
18 nawe mteketeze kondoo mzima juu ya madhabahu. Ni sadaka ya kuteketezwa kwa ajili yaYahweh; ni harufu nzuri, sadaka iliyosongezwa kwa Yahweh kwa njia ya moto.
You shall burn the whole ram on the altar: it is a burnt offering to Adonai; it is a pleasant aroma, an offering made by fire to Adonai.
19 Kisha mtwae huyo kondoo mwingine; na Aruni na wanawe wataweka mikono yao juu ya kichwa chake huyo kondoo.
“You shall take the other ram; and Aaron [Light-bringer] and his sons shall lay their hands on the head of the ram.
20 Kisha utamchinja kondoo, na kuitwaa damu yake, na kuitia katika ncha ya sikio la Aruni la upande wa kuume, na katika ncha za masikio ya kuume ya wanawe, na katika vyanda vya gumba vya mikono yao ya kuume, na katika vidole vikuu vya miguu yao ya kuume, na kuinyunyiza hiyo damu katika madhabahu kuizunguka kando-kando.
Then you shall kill the ram, and take some of its blood, and put it on the tip of the right ear of Aaron [Light-bringer], and on the tip of the right ear of his sons, and on the thumb of their right hand, and on the big toe of their right foot, and sprinkle the blood around on the altar.
21 Kisha twaa katika hiyo damu iliyo juu ya madhabahu, na katika hayo mafuta ya kutiwa, na kumnyunyizia Aruni, juu ya mavazi yake, na wanawe, na mavazi yao pia, pamoja naye; naye atatakaswa, na mavazi yake, na wanawe, na mavazi ya wanawe, pamoja naye.
You shall take of the blood that is on the altar, and of the anointing oil, and sprinkle it on Aaron [Light-bringer], and on his garments, and on his sons, and on the garments of his sons with him: and he shall be made holy, and his garments, and his sons, and his sons’ garments with him.
22 Tena yatwae mafuta ya huyo kondoo mume, na mkia wake wa mafuta, na mafuta yafunikayo matumbo, na kitambi kilicho katika ini, na figo mbili, na mafuta yaliyo katika hizo figo, na paja la kuume; kwani ni kondoo ambaye ni wa kuwekwa kwa kazi takatifu.
Also you shall take some of the ram’s fat, the fat tail, the fat that covers the innards, the cover of the liver, the two kidneys, the fat that is on them, and the right thigh (for it is a ram of consecration),
23 Utwae na mkate mmoja wa unga, na mkate mmoja ulioandaliwa kwa mafuta, na kaki moja katika kile kikapu cha mikate isiyotiwa chachu, kilichowekwa mbele ya Yahweh.
and one loaf of bread, one cake of oiled bread, and one wafer out of the basket of matzah ·unleavened bread· that is before Adonai.
24 Nawe utavitia hivi vyote katika mikono ya Aruni, na katika mikono ya wanawe; nawe utavitikisa-tikisa viwe sadaka ya kutikiswa mbele za Yahweh.
You shall put all of this in Aaron [Light-bringer]’s hands, and in his sons’ hands, and shall wave them for a wave offering before Adonai.
25 Kisha uvitwae vile vitu mikononi mwao, na kuviteketeza juu ya madhabahu, juu ya ile sadaka ya kuteketezwa, viwe harufu nzuri mbele yangu; ni sadaka iliyotengenezwa kwangu kwa njia ya moto.
You shall take them from their hands, and burn them on the altar on the burnt offering, for a pleasant aroma before Adonai: it is an offering made by fire to Adonai.
26 Kisha twaa kidari cha huyo kondoo wa kuwekwa kwake Haruni kwa kazi takatifu, na kukitikisa-tikisa kiwe sadaka ya kutikiswa mbele za Yahwe nacho kitakuwa ni sehemu yako.
“You shall take the breast of ram of consecration for Aaron [Light-bringer], and wave it for a wave offering before Adonai: and it shall be your portion.
27 Nawe kitakase kile kidari cha ile sadaka ya kutikiswa, na lile paja la sadaka ya kuinuliwa, lililotikiswa, na lililoinuliwa juu, vya yule kondoo wa kuwekwa kwa kazi takatifu, huyo aliyekuwa kwa ajili ya Aruni na wanawe.
You shall sanctify the breast of the wave offering, and the thigh of the wave offering, which is waved, and which is heaved up, of the ram of consecration, even of that which is for Aaron [Light-bringer], and of that which is for his sons:
28 Navyo vitakuwa vya Haruni na wanawe posho ya lazima sikuzote itokayo kwa hao wana wa Israeli; kwa kuwa ni sadaka ya kuinuliwa; nayo itakuwa ni sadaka ya kuinuliwa itokayo kwa hao wana wa Israeli katika dhabihu zao za sadaka za amani, ni sadaka yao ya kuinuliwa kwa ajili ya Yahweh.
and it shall be for Aaron [Light-bringer] and his sons as their chok ·portion· forever from the children of Israel [God prevails]; for it is a wave offering: and it shall be a wave offering from the children of Israel [God prevails] of the sacrifices of their peace offerings, even their wave offering to Adonai.
29 Na hayo mavazi matakatifu ya Aruni yatakuwa ya wanawe baada yake, wayavae watakapotiwa mafuta, na watakapowekwa kwa kazi takatifu.
“The holy garments of Aaron [Light-bringer] shall be for his sons after him, to be anointed in them, and to be consecrated in them.
30 Huyo mwanawe atakayekuwa kuhani badala yake atayavaa muda wa siku saba, hapo atakapoingia ndani ya hiyo hema ya kukutania, ili atumike ndani ya mahali patakatifu.
Seven days shall the son who is priest in his place put them on, when he comes into the Tent of Meeting to minister in the holy place.
31 Nawe twaa huyo kondoo mume aliyekuwa wa kuwekwa kwa kazi takatifu, na kuitokosa nyama yake katika mahali patakatifu.
“You shall take the ram of consecration, and boil its meat in a holy place.
32 Na Aruni na wanawe wataila ile nyama ya kondoo, na mikate iliyo katika kile kikapu, hapo mbele ya mlango wa hema ya kukutania.
Aaron [Light-bringer] and his sons shall eat the meat of the ram, and the bread that is in the basket, at the door of the Tent of Meeting.
33 Nao watakula vile vitu ambavyo upatanisho ulifanywa kwa hivyo, ili kuwaweka kwa kazi takatifu na kuwatakasa; lakini mgeni asivile, maana, ni vitu vitakatifu.
They shall eat those things with which atonement was made, to consecrate and sanctify them: but a stranger shall not eat of it, because they are holy.
34 Na kwamba kitu cho chote cha ile nyama, iliyo kwa ajili ya kuweka kwa kazi takatifu, au cho chote cha hiyo mikate, kikisalia hata asubuhi, ndipo utavichoma kwa moto hivyo vilivyosalia; havitaliwa, maana, ni vitu vitakatifu
If anything of the meat of the consecration, or of the bread, remains to the morning, then you shall burn the remainder with fire: it shall not be eaten, because it is holy.
35 Ni hivyo utakavyowatendea Aruni na wanawe kama nilivyo kuagiza. Utawaweka kwa kazi takatifu siku saba.
“You shall do so to Aaron [Light-bringer], and to his sons, according to all that I have enjoined you. You shall consecrate them seven days.
36 Kila siku utamtoa ng’ombe wa sadaka ya dhambi kwa ajili ya upatanisho; nawe utaisafisha hiyo madhabahu, hapo utakapofanya upatanisho kwa ajili ya hiyo madhabahu; nawe utaitia mafuta, ili kuitakasa.
Every day you shall offer the bull of sin offering for atonement: and you shall cleanse the altar, when you make atonement for it; and you shall anoint it, to sanctify it.
37 Utafanya upatanisho kwa ajili ya hiyo madhabahu muda wa siku saba, na kuitakasa; ndipo madhabahu itakapokuwa takatifu sana; kila kitu kiigusacho madhabahu kitakuwa kitakatifu.
Seven days you shall make atonement for the altar, and sanctify it: and the altar shall be most holy; whatever touches the altar shall be holy.
38 Lazima utoe kwenye madhabahu wana-kondoo wa mwaka mmoja wawili siku baada ya siku
“Now this is that which you shall offer on the altar: two lambs a year old day by day continually.
39 daima. Mwana-kondoo mmoja utamchinja asubuhi; na mwana-kondoo wa pili utamchinja jioni
The one lamb you shall offer in the morning; and the other lamb you shall offer at evening:
40 Pamoja na mwana-kondoo mmoja utatoa vibaba vitatu vya unga mzuri uliochanganyika na mafuta yenye kupondwa, kiasi cha kibaba na robo kibaba; na divai kiasi cha kibaba na robo kibaba, iwe sadaka ya kinywaji.
and with the one lamb a tenth part of an ephah [an omer 2.3 q; 2.2 L] of fine flour mixed with the fourth part of a hin [2.6 qt; 1.2 L] of beaten oil, and the fourth part of a hin [2.6 qt; 1.2 L] of wine for a drink offering.
41 Na huyo mwana-kondoo wa pili utamchinja wakati wa jioni. Nawe utamfanyia vivyo kama ile sadaka ya unga ya asubuhi, na kama ile sadaka yake ya kinywaji. Hii itatoa harufu nzuri, ni dhabihu ya kusongezwa kwangu kwa njia ya moto.
The other lamb you shall offer at evening, and shall do to it according to the meal offering of the morning, and according to its drink offering, for a pleasant aroma, an offering made by fire to Adonai.
42 Itakuwa ni sadaka ya kuteketezwa milele katika vizazi vyenu vyote mlangoni pa ile hema ya kukutania mbele ya Yahweh, hapo nitakapokutana nanyi, ili niseme na wewe hapo.
It shall be a continual burnt offering throughout all your generations at the door of the Tent of Meeting before Adonai, where I will meet with you, to speak there to you.
43 Nami nitakutana na wana wa Israeli hapo; na hiyo hema itafanywa takatifu na utukufu wangu. Nami nitaitakasa hiyo hema ya kukutania, na hiyo madhabahu.
There I will meet with the children of Israel [God prevails]; and the place shall be sanctified by my glory.
44 Pia Aruni na wanawe nitawatakasa, ili wanitumikie katika kazi ya ukuhani.
I will sanctify the Tent of Meeting and the altar: Aaron [Light-bringer] also and his sons I will sanctify, to minister to me in the priest’s office.
45 Na mimi nitakaa kati ya wana wa Israeli, nami nitakuwa Mungu wao.
I will dwell among the children of Israel [God prevails], and will be their God.
46 Nao watanijua kuwa mimi ndimi Yahweh, Mungu wao, niliyewaleta watoke katika nchi ya Misri, nipate kukaa kati yao. Ni mimi Yahweh, Mungu wao.
They shall know that I am Adonai their God, who brought them out of the land of Egypt [Abode of slavery], that I might dwell among them: I am Adonai their God.

< Kutoka 29 >