< Kutoka 27 >

1 Nawe fanya madhabahu ya mti wa mshita, urefu wake utakuwa ni dhiraa tano na upana wake dhiraa tano. Hiyo madhabahu itakuwa mraba na kwenda juu kwake kutakuwa dhiraa tatu.
"You shall make the altar of acacia wood, eight feet seven inches long, and eight feet seven inches broad; the altar shall be foursquare: and its height shall be five feet two inches.
2 Nawe fanya pembe nne kama mfano wa pembe za ng'ombe. Hizo pembe zitakuwa za kitu kimoja na madhabahu, nawe utayafunika kwa shaba.
You shall make its horns on its four corners; its horns shall be of one piece with it; and you shall overlay it with bronze.
3 Lazima vyombo vyake vya kuyaondoa majivu yake utavifanya, na majembe yake, na mabakuli yake, na uma zake, na meko yake. Vyombo vyake vyote utavifanya vya shaba.
You shall make its pots to take away its ashes, its shovels, its basins, its flesh hooks, and its fire pans: all its vessels you shall make of bronze.
4 Nawe uifanyie hiyo madhabahu wavu wa shaba. Kisha utie pete nne za shaba katika hizo pembe nne za ule wavu.
You shall make a grating for it of network of bronze: and on the net you shall make four bronze rings in its four corners.
5 Nawe lazima uweke huo wavu chini ya kizingo kiizungukacho madhabahu upande wa chini.
You shall put it under the ledge around the altar beneath, that the net may reach halfway up the altar.
6 Nawe fanya miti kwa ajili ya madhabahu, miti ya mshita, na kuifunika shaba.
You shall make poles for the altar, poles of acacia wood, and overlay them with bronze.
7 Na hiyo miti itatiwa katika viduara, na ile miti itakuwa katika pande mbili za madhabahu, wakati wa kuichukua.
Its poles shall be put into the rings, and the poles shall be on the two sides of the altar, when carrying it.
8 Uifanye ya mbao, yenye mvungu ndani yake kama ulivyooneshwa mlimani.
You shall make it with hollow planks. They shall make it as it has been shown you on the mountain.
9 Nawe ufanye ua wa maskani. Upande wa kusini wa kuelekea kusini kutakuwa na chandarua ya nguo ya kitani nzuri yenye kusokotwa, kwa huo ua, urefu wake upande mmoja utakuwa ni dhiraa mia moja.
"You shall make the court of the tabernacle: for the south side southward there shall be hangings for the court of fine twined linen one hundred seventy-two feet three inches long for one side:
10 Na nguzo zake zitakuwa nguzo ishirini, na vitako vyake ishirini, vitako vyake vitakuwa vya shaba kulabu za zile nguzo na vitanzi vyake vitakuwa vya fedha.
and its pillars shall be thirty-four feet five inches, and their sockets twenty, of bronze; the hooks of the pillars and their fillets shall be of silver.
11 Ni vivyo hivyo upande wa kaskazini, urefu wake hiyo chandarua utakuwa ni dhiraa mia moja, na nguzo zake ishirini, na vitako vyake ishirini vitakuwa vya shaba, kulabu za zile nguzo na vitanzi vyake vitakuwa vya fedha.
Likewise for the north side in length there shall be hangings one hundred seventy-two feet three inches, and its pillars thirty-four feet five inches, and their sockets thirty-four feet five inches, of bronze; the hooks of the pillars, and their fillets, of silver.
12 Na upande wa magharibi, upana wa ua kutakuwa na chandarua ya dhiraa hamsini; nguzo zake kumi, na vitako vyake kumi.
For the breadth of the court on the west side shall be hangings of eighty-six feet one inch; their pillars seventeen feet three inches, and their sockets seventeen feet three inches.
13 Na upana wa ule ua upande wa mashariki kuelekea mashariki utakuwa ni dhiraa hamsini.
The breadth of the court on the east side eastward shall be eighty-six feet one inch.
14 Chandarua upande mmoja wa lango itakuwa dhiraa kumi na tano upana wake. Lazima nguzo zake zitakuwa tatu na vitako vyake vitatu.
The hangings for the one side of the gate shall be twenty-five feet ten inches; their pillars five feet two inches, and their sockets five feet two inches.
15 Upande wa pili ni vivyo hivyo chandarua ya dhiraa kumi na tano; nguzo zake tatu, na vitako vyake vitatu.
For the other side shall be hangings of twenty-five feet ten inches; their pillars five feet two inches, and their sockets five feet two inches.
16 Na kwa lile lango la ua patakuwa na kisitiri cha dhiraa ishirini, kitakuwa cha nguo ya rangi ya buluu, zambarau na nyekundu, na kitani nzuri yenye kusokotwa, kazi ya mshonaji taraza; nguzo zake zitakuwa nne, na vitako vyake vinne.
For the gate of the court shall be a screen of thirty-four feet five inches, of blue, and purple, and scarlet, and fine twined linen, the work of the embroiderer; their pillars six feet eleven inches, and their sockets six feet eleven inches.
17 Nguzo zote za ule ua ziuzungukao pande zote zitakuwa na vitanzi vya fedha; kulabu zake za fedha, na vitako vyake vya shaba.
All the pillars of the court around shall be filleted with silver; their hooks of silver, and their sockets of bronze.
18 Urefu wa huo ua utakuwa dhiraa mia moja, na upana wake utakuwa dhiraa hamsini kotekote, na kwenda juu kwake dhiraa tano; yawe ya nguo ya kitani nzuri, na vitako vyake vitakuwa vya shaba.
The length of the court shall be one hundred seventy-two feet three inches, and the breadth eighty-six feet one inch every where, and the height eight feet seven inches, of fine twined linen, and their sockets of bronze.
19 Vyombo vyote vya maskani vitumiwavyo katika utumishi wake wote, na vigingi vyake vyote, na vigingi vyote vya ule ua, vitakuwa vya shaba.
All the instruments of the tabernacle in all its service, and all its pins, and all the pins of the court, shall be of bronze.
20 awe waamuru wana wa Israeli wakuletee mafuta ya zeituni safi ya kupondwa kwa ajili ya nuru, ili kufanya ile taa kuwaka daima.
"You shall command the children of Israel, that they bring to you pure olive oil beaten for the light, to cause a lamp to burn continually.
21 Ndani ya ile hema ya kukutania, nje ya hilo pazia, lililo mbele ya huo ushuhuda, Haruni na wanawe wataitengeza tangu jioni hadi asubuhi mbele ya BWANA; itakuwa ni amri ya milele katika vizazi vyao vyote kwa ajili ya wana wa Israeli.
In the Tent of Meeting, outside the veil which is before the testimony, Aaron and his sons shall keep it in order from evening to morning before Jehovah: it shall be a statute forever throughout their generations on the behalf of the children of Israel.

< Kutoka 27 >