< Kutoka 23 >

1 Haupaswi kutoa taarifa ya uongo kuhusu yeyote. usijiunge na mwanaume muovu kuwa shahidi wa uongo.
“You shall not spread a false report. Don’t join your hand with the wicked to be a malicious witness.
2 Haupaswi kufuata umati kufanya uovu, wala kutoa ushahidi ukiwa na umati ili kupotosha haki.
“You shall not follow a crowd to do evil. You shall not testify in court to side with a multitude to pervert justice.
3 Haupaswi kumpendelea mwanaume maskini kwenye kesi yake.
You shall not favor a poor man in his cause.
4 Ukikutana na ng'ombe wa adui wako au punda wake amepotea, lazima umrudishie.
“If you meet your enemy’s ox or his donkey going astray, you shall surely bring it back to him again.
5 Ukiona punda wa yule anaye kuchukia ameanguka chini na mzigo wake, hauta muacha huyo mtu. Lazima umsaidie na punda wake
If you see the donkey of him who hates you fallen down under his burden, don’t leave him, you shall surely help him with it.
6 Haupaswi kupotosha haki kama yapaswa kwenda kwa watu maskini katika kesi ya mwanaume maskini.
“You shall not deny right judgement to your poor people in their lawsuits.
7 Usijiunge na wengine kufanya shutuma za uongo, na usiue asiye na hatia wala mwenye haki, kwa kuwa sitamuacha muovu.
“Keep far from a false charge, and don’t kill the innocent and righteous: for I will not justify the wicked.
8 Husiwai chukuwa rushwa, kwa kuwa rushwa inawapofusha wanaoona, na kupotosha maneno ya wakweli.
“You shall take no bribe, for a bribe blinds those who have sight and perverts the words of the righteous.
9 Haupaswi kumnyanyasa mgeni, kwa kuwa wewe ulikuwa mgeni katika nchi ya Misri.
“You shall not oppress an alien, for you know the heart of an alien, since you were aliens in the land of Egypt [Abode of slavery].
10 Kwa miaka sita utapanda mbegu kwenye nchi yako na kukusanya mazao yake.
“For six years you shall sow your land, and shall gather in its increase,
11 Lakini katika mwezi wa saba utaacha hakujalimwa, ili kwamba maskini miongoni mwenu wale. Wanacho acha, wanyama wa porini watakula. Utafanya hivyo na mashamba yenu ya mizabibu na ya mizaituni.
but the seventh year you shall let it rest and lie fallow, that the poor of your people may eat; and what they leave the animal of the field shall eat. In the same way, you shall deal with your vineyard and with your olive grove.
12 Wakati wa siku sita utafanya kazi, lakini siku ta saba utapumzika. Fanya hivi ili ng'ombe na punda wako wapumzike, na ili wana wa watumwa wako wa kike na wageni wapumzike na kupata hauweni.
“Six days you shall do your work, and on the seventh day you shall rest, that your ox and your donkey may have rest, and the son of your servant, and the alien may be refreshed.
13 Kuwa makini kwa kila kitu nilicho kwambia. Husitaje majina ya miungu mingine, wala kuruhusu majina yao kusikika kutoka mdomoni mwako.
“Be careful to do all things that I have said to you; and don’t invoke the name of other elohim ·deities· or even let them be sh'ma ·heard obeyed· out of your mouth.
14 Lazima usafiri kusherehekea mara tatu kwa ajili yangu kila mwaka.
“You shall observe a feast to me three times a year.
15 Lazima uadhimishe sherehe ya Mkate usiotiwa Chachu. Kama nilivyo kuamuru, utakula mkate usiotiwa chachu kwa siku saba. Wakati huo, utajitokeza kwangu mwezi wa Abibu, uliowekwa kwa ajili ya kusudi hili. Ni kwa mwezi huu uliyo toka Misri. Lakini usijitokeze kwangu mikono mitupu.
You shall observe the festival of Matzah ·Unleavened bread·. Seven days you shall eat matzah ·unleavened bread·, as I enjoined you, at the time appointed in the month Abib (for in it you came out of Egypt [Abode of slavery]), and no one shall appear before me empty.
16 Lazima uadhimishe Sherehe ya Mavuno, matunda ya kwanza ya kazi yako ulipo panda mbegu shambani. Pia lazima uadhimishe Sherehe ya Ukusanyaji wa mwisho wa mwaka, unapo kusanya mazao yako kutoka shambani.
And the festival of harvest, the first fruits of your labors, which you sow in the field; and the festival of in-gathering, at the end of the year, when you gather in the results of your labors out of the field.
17 Wanaume wote wako lazima wajitokeze kwa Bwana Yahweh mara tatu kila mwaka.
Three times in the year all your males shall appear before the Lord Adonai.
18 Haupaswi kutoa damu iliyo tolewa dhabihu kwangu na mkate uliyotiwa hamira. Mafuta kutoka kwa dhabihu za sherehe zangu hayapaswi kubaki usiku wote mpaka asubui.
“You shall not offer the blood of my sacrifice with leavened bread. The fat of my feast shall not remain all night until the morning.
19 Lazima ulete matunda ya kwanza bora kutoka shambani mwako ndani ya nyumba yangu, nyumba ya Yahweh Mungu wako. Haupaswi kumchemsha mbuzi mtoto akiwa bado ananyonya.
The first of the first fruits of your ground you shall bring into the house of Adonai your God. “You shall not boil a young goat in its mother’s milk fat.
20 Ninaenda kumleta malaika mbele yako kukuongoza njiani, na kukuleta sehemu niliyo iandaa.
“Behold, I send an angel before you, to keep you by the way, and to bring you into the place which I have prepared.
21 Kuwa makini naye na kumtii.
Pay attention to him, and sh'ma ·hear obey· his voice. Don’t provoke him, for he will not pardon your disobedience, for my name is in him.
22 Husimkasirishe, kwa kuwa hatasamehe makosa yako. Jina langu liko kwake. Kama hakika ukimtii sauti yake na kufanya kila ninacho kwambia, kisha nitakuwa adui kwa adui zako na mpinzani kwa wapinzani wako.
But if you sh'ma ·hear obey· sh'ma ·hear obey· his voice, and sh'ma ·hear obey· all that I speak, then I will be an enemy to your enemies, and an adversary to your adversaries.
23 Malaika mwangu ataenda mbele zako na kukuleta kwa Waamori, Wahiti, Waperizi, Wakanani, Wahivi, na Wayebusi. Nitawaharibu.
For my angel shall go before you, and bring you in to the Amorite [Descendants of Talkers], the Hittite [Descendant of Trembling fear], the Perizzite [Descendant of Belonging to village], the Canaanite [Descendant of Humbled], the Hivite [Wicked], and the Jebusite [Descendants of Thresher]; and I will cut them off.
24 Haupaswi kuinamia miungu yao, kuabudu, au kufanya wanavyo fanya. Badala yake, lazima uwapindue kabisa na kuvunja nguzo zao za mawe vipande vipande.
You shall not hawa ·bow low, prostrate· to their deities, nor abad ·serve· them, nor follow their practices, but you shall utterly overthrow them and demolish their pillars.
25 Lazima umuabudu Yahweh Mungu wako, na atabariki mkate wako na maji. Nitaondoa magonjwa miongoni mwenu.
You shall serve Adonai your God, and he will bless your bread and your water, and I will take sickness away from among you.
26 Hakuna mwanamke atakaye kuwa tasa au mimba kuharibika katika nchi yako. Nitawapa maisha marefu.
No one will miscarry or be barren in your land. I will fulfill the number of your days.
27 Nitatuma hofu yangu kwao ambao mnaenda. Nitaua wote mnao kutana nao. Nitafanya maadui zenu wawaogope kwa kugeuza migongo yao kwenu.
I will send my terror before you, and will confuse all the people to whom you come, and I will make all your enemies turn their backs to you.
28 Nitatuma mavu kwenu watakao fukuza Wahivi, Wakanani, na Wahiti mbele zenu.
I will send the hornet before you, which will divorce and drive out the Hivite [Wicked], the Canaanite [Descendant of Humbled], and the Hittite [Descendant of Trembling fear], from before you.
29 Sitawaondoa kwenu kwa mwaka mmoja, au nchi itakuwa imetelekezwa, na wanyama wa porini watakuwa wengi kwenu.
I will not divorce them from before you in one year, lest the land become desolate, and the animals of the field multiply against you.
30 Badala yake, nitawafukuza kidogo kidogo kutoka kwenu mpaka utakapo kuwa umestawi na kurithi nchi.
Little by little I will divorce them from before you, until you have increased and inherit the land.
31 Nitatengeneza mipaka yako kutoka Bahari ya Shamu hadi Bahari ya Wafilisti, na kutoka nyikani hadi Mto Frati. Nitakupa ushindi juu ya wakazi wote wa nchi. Utawaondoa kutoka kwako mwenyewe.
I will set your border from the Sea of Suf [Reed Sea] even to the sea of the Philistines [To roll in dust (As an insult)], and from the wilderness to the River; for I will deliver the inhabitants of the land into your hand, and you shall divorce them from before you.
32 Haupaswi kufanya agano na wao au na miungu yao.
You shall make no covenant ·binding contract between two or more parties· with them, nor with their elohim ·deities·.
33 Hawapaswi kuishi nchini mwako, au watakufanya ufanya dhambi dhidi yangu. Ukiabudu miungu yao, hakika watakuwa mtego kwako.'”
They shall not dwell in your land, lest they make you sin against me, for if you abad ·serve· their deities, it will surely be a snare to you.”

< Kutoka 23 >