< Kutoka 20 >

1 Mungu alisema maneno yote haya:
God spoke all these words, saying,
2 Ndimi Bwana Mungu wenu, niliyewatoa katika ardhi Misri, nje ya nyumba ya utumwa.
"I am Jehovah your God, who brought you out of the land of Egypt, out of the house of bondage.
3 Msiwe na miungu mingine ila mimi tu.
Do not have other gods before me.
4 Msijitengenezee sanamu za kuchonga kufananisha na kitu chochote kilichopo juu ya mbingu, chini ya ardhi, au ndani ya maji.
"Do not make for yourselves an idol, nor any image of anything that is in the heavens above, or that is in the earth beneath, or that is in the water under the earth:
5 Msipinde na kuabudu sanamu, mimi Yahweh Mungu wenu, ni Mungu mwenye wivu. Nitaadhibu uovu wa mabubu kwa kuleta adhabu juu ya kizazi, cha tatu hadi kizazi cha nne kwa wale wanao nichukia.
you must not bow yourself down to them, nor serve them, for I, Jehovah your God, am a jealous God, visiting the iniquity of the fathers on the children, and upon the children's children, on the third and on the fourth [generation] of those who hate me,
6 Ila nitaweka agano la uaminifu kwa maelfu watakao nipenda na kushika amri zangu.
and showing loving kindness to thousands of those who love me and keep my commandments.
7 Usilitaje bure jina la Yahweh Mungu wako, sitkuwa na hatia kwa yeyote atakaye taja jina langu bure.
"Do not take the name of Jehovah your God in vain, for Jehovah will not hold him guiltless who takes his name in vain.
8 Ikumbuke siku ya Sabato, na kunitengea.
"Remember the Sabbath day, to keep it holy.
9 lazima ufanye kazi zako zote kwa siku sita.
Six days you may labor, and do all your work,
10 Ila siku ya saba ni Sabato kwaajili ya Yahweh Mungu wako. Siku hiyo usifanye kazi yoyote, wewe, au mwana wako, au binti yako, au mtumishi wako wakiume, au mtumishi wako mwanamke, au ng'ombe zako, au mgeni aliye ndani ya malango yako.
but the seventh day is a Sabbath to Jehovah your God. You must not do any work in it, you, nor your son, nor your daughter, your male servant, nor your female servant, nor your livestock, nor your stranger who is within your gates;
11 Kwa siku sita Yahweh aliumba mbingu na nchi, bahari, na vitu vyote vilivyomo, na siku ya saba alipumzika. Kwa hiyo Yahweh aliibariki siku ya Sabato na kuitenga.
for in six days Jehovah made heaven and earth, the sea, and all that is in them, and rested the seventh day; therefore Jehovah blessed the seventh day, and made it holy.
12 Waheshimu baba na mama yako, ili uweze kuishi miaka mingi duniani Yahweh Mungu wako ametoa.
"Honor your father and your mother, that it may be well with you, that your days may be long in the land which Jehovah your God gives you.
13 Usiue.
"Do not commit adultery.
14 Usifanye uasherati (usizini).
"Do not murder.
15 Usiibe kwa mtu yoyote.
"Do not steal.
16 Usishuhudie uongo dhidi ya jirani yako.
"Do not give false testimony against your neighbor.
17 Usitaman nyumba ya jirani yako; usitamani mke wa jirani yako, wala mtumishi wake wakiume, mtumishi wake mwanamke, ng'ombe wake, punda wake, au chochote cha jirani yako.
"Do not covet your neighbor's house. Do not covet your neighbor's wife, nor his male servant, nor his female servant, nor his ox, nor his donkey, nor anything that is your neighbor's."
18 Watu wote waliona radi na umeme, na kusikia sauti ya mbiu, na mlima ukitoa moshi. Watu walipoona hivo, walitetemeka na kusimama mbali.
And all the people saw the thunder and the lightning and the sound of the trumpet and the mountain smoking, and the people were afraid and trembled and kept their distance.
19 Wakamwambia Musa, ongea na sisi, na tutakusikiliza; lakini usiruhusu Mungu kuongea nasi, ama tutakufa.
They said to Moses, "Speak with us yourself, and we will listen; but do not let God speak with us, lest we die."
20 Musa akawaambia watu, “msiogope, Mungu alikuja kuwajaribu ili heshima yake iwe ndani yenu, kwa hiyo msitende dhambi.”
Moses said to the people, "Do not be afraid, for God has come to test you, and that his fear may be before you, that you won't sin."
21 hivyo watu walisimama mbali, na Musa alikaribia giza nene Mungu alipokuwa.
The people stayed at a distance, and Moses drew near to the thick darkness where God was.
22 Yahweh alimwambia Musa, “Ni lazima uwaambie hili Waisraeli: 'Wewe mwenyewe umeona niliongea na wewe kutoka mbinguni.
Jehovah said to Moses, "This is what you shall tell the children of Israel: 'You yourselves have seen that I have talked with you from heaven.
23 Misjitengenezee miungu mingine pamoja nami, miungu ya fedha au miungu ya dhahabu.
You shall most certainly not make alongside of me gods of silver, or gods of gold for yourselves.
24 Tengenezeni madhabahu ya udongo kwa ajili yangu, na lazima mtoe sadaka ya kuteketeza, sadaka ya ushirika, kondoo, na ng'ombe. kila sehemu ntakapotaka jina langu liheshimiwe, nitakuja kwenu na kuwabariki.
You shall make an altar of earth for me, and shall sacrifice on it your burnt offerings and your peace offerings, your sheep and your cattle. In every place where I record my name I will come to you and I will bless you.
25 Kama mtatengeneza madhabahu ya mawe, msijenge na mawe yaiyokatika, na kama mtatumia vyombo vyenu juu yake, mtaweka unajisi.
If you make me an altar of stone, you shall not build it of cut stones; for if you lift up your tool on it, you have polluted it.
26 msije juu ya madhabahu yangu kwa hatua zenu; hii ni ili msioneshe sehemu zenu za siri.”
Neither shall you go up by steps to my altar, that your nakedness may not be exposed to it.'

< Kutoka 20 >