< Kutoka 2 >

1 Sasa mwanamme wa kabila la Lawi alimuoa mwanamke Mlawi.
A man of the house of Levi [United with] went and took a daughter of Levi [United with] as his wife.
2 Yule mwanamke akapata mimba na kuzaa mtoto wa kiume. Alipoona ya kuwa alikuwa mtoto mwenye afaya, alimficha kwa miezi mitatu.
The woman conceived, and bore a son, upon seeing what a fine child he was, she hid him three months.
3 Lakini alipokuwa hawezi kuendelea kumficha tena, alichukua kikapu cha manyasi akakipaka sifa na lami. Akamtia mtoto ndani yake na kukiweka juu ya maji katika majani kando ya mto.
When she could no longer hide him, she took a papyrus basket for him, and coated it with tar and with pitch. She put the child in it, and laid it in the reeds by the river’s bank.
4 Dada yake akasimama kwa mbali ili ajue yatakayompata.
His sister stood far off, to see what would be done to him.
5 Binti Farao akashuka kuoga mtoni wakati vijakazi wake wakitembea kando ya mto. Naye akaona kile kikapu katika majani na akamtuma kijakazi wake kwenda kukileta.
Pharaoh’s daughter came down to bathe at the river. Her maidens walked along by the riverside. She saw the basket among the reeds, and sent her servant to get it.
6 Alipokifungua, aliomwona mtoto. Tazama, mtoto alikuwa analia. Alimhurumia na kusema, “Bila shaka huyu ni mmoja wapo wa watoto wa Waebrania.”
She opened it, and saw the child, and behold, the baby cried. She had compassion on him, and said, “This is one of the Hebrews’ children.”
7 Basi dada wa yule mtoto akamwambia binti Farao, “Je naweza kwenda kukutafutia mwanamke wa Kiebrania aje akulele mtoto kwa ajili yako?”
Then his sister said to Pharaoh’s daughter, “Should I go and call a nurse for you from the Hebrew women, that she may nurse the child for you?”
8 Binti Farao akamwambia, “Nenda.” Hivyo yule binti akaenda na kumwita mama yake yule mtoto.
Pharaoh’s daughter said to her, “Go.” The maiden went and called the child’s mother.
9 Binti Farao akamwambia mama yake yule mtoto, “Mchukue mtoto huyu ukaninyonyeshee, nami nitakupa posho.” Hivyo yule mwanamke akamchukua mtoto na kumnyonyesha.
Pharaoh’s daughter said to her, “Take this child away, and nurse him for me, and I will give you your wages.” The woman took the child, and nursed it.
10 Mtoto alipokuwa mkubwa, akamleta kwa binti Farao, na akawa mtoto wake. Akamwita jina lake Musa akisema, “Kwa sababu nilimtoa katika maji.”
The child grew, and she brought him to Pharaoh’s daughter, and he became her son. She named him Moses [Drawn out], and said, “Because I drew him out of the water.”
11 Musa alipokuwa mtu mzima, alienda kwa watu wake na kuona kazi ngumu walizokuwa wanafanya. Alimuona Mmisri akimpiga Mwebrania, mmoja wa watu wa jamii yake.
In those days, when Moses [Drawn out] had grown up, he went out to his brothers, and looked at their burdens. He saw an Egyptian [person from Abode of slavery] striking a Hebrew [Immigrant], one of his brothers.
12 Aliangalia huku na kule, na alipoona ya kuwa hakuna mtu, alimuua yule mmisri na kuuficha mwili wake katika mchanga.
He looked this way and that way, and when he saw that there was no one, he killed the Egyptian [person from Abode of slavery], and hid him in the sand.
13 Alienda tena siku iliyofuata, na tazama, Waebrania wawili walikuwa wanapigana. Alimwambia yule aliyekuwa na makosa, “Kwa nini unampigia mwenzako?”
He went out the second day, and behold, two men of the Hebrews [Immigrants] were fighting with each other. He said to him who did the wrong, “Why do you strike your fellow?”
14 Lakini yule mtu alisema, “Ni nani aliyekuweka wewe kuwa kiongozi na mwamuzi juu yetu? Unataka kuniua na mimi kama ulivyomuua yule mmisri?” Ndipo Musa akaogopa na kusema, “Hakika niliyoyafanya yamejulikana.”
He said, “Who made you a prince and a judge over us? Do you plan to kill me, as you killed the Egyptian [person from Abode of slavery]?” Moses [Drawn out] was afraid, and said, “Surely this thing is known.”
15 Farao aliposikia habari hizi, alijaribu kumuua Musa. Lakini Musa alikimbia na kwenda kuishi katika nchi ya Wamidiani. Kule alikaa chini kando ya mto.
Now when Pharaoh sh'ma ·heard obeyed· this thing, he sought to kill Moses [Drawn out]. But Moses [Drawn out] fled from the face of Pharaoh, and lived in the land of Midian [Strife], and he sat down by a well.
16 Wakati huo kuhani wa Midiani alikuwa na mabinti saba. Walikuja mtoni kuchota maji na kujaza vyombo vyao ili wawanyweshe mifuko ya baba yao.
Now the priest of Midian [Strife] had seven daughters. They came and drew water, and filled the troughs to water their father’s flock.
17 Wachungaji walikuja na kutaka kuwafukuza, lakini Musa alienda kuwasaidia. Kisha akawanywesha mifugo wao.
The shepherds came and divorced them away; but Moses [Drawn out] stood up and helped them, and watered their flock.
18 Wale mabinti walipoenda kwa Reueli baba yao, aliwauliza, “Kwa nini mmerudi nyumbani mapema hivi leo?”
When they came to Reuel, their father, he said, “How is it that you have returned so early today?”
19 Wakamwambia, “Mmisri mmoja alituokoa dhidi ya wachungaji. Pia alichota maji na kuwanywesha mifugo wetu.”
They said, “An Egyptian [person from Abode of slavery] delivered us out of the hand of the shepherds, and moreover he drew water for us, and watered the flock.”
20 Kisha akawauliza binti zake, “Yu wapi sasa? Kwa nini mlimwacha? Mwiteni ili apate kula chakula pamoja nasi.”
He said to his daughters, “Where is he? Why is it that you have left the man? Call him, that he may eat bread.”
21 Musa akakubali kukaa na yule mtu ambaye pia alimpa binti yake Zipora ili amuoe.
Moses [Drawn out] was content to dwell with the man. He gave Moses [Drawn out] Zipporah, his daughter.
22 Alizaa mtoto wa kiume, na Musa akamwita jina lake Geshomu; akisema; “Nimekuwa mkazi katika nchi ya ugeni.”
She bore a son, and he named him Gershom, for he said, “I have lived as a foreigner in a foreign land.”
23 Muda mrefu baadaye, mfalme wa Misri akafa. Waisraeli walilalamika kwa sababu ya kazi za utumwa. Walilia kutafuta msaada, na maombi yao yakamfikia Mungu kwa sababu ya mateso yao.
In the course of those many days, the king of Egypt [Abode of slavery] died, and the children of Israel [God prevails] sighed because of the bondage, and they cried, and their cry came up to God because of the bondage.
24 Mungu aliposikia malalamiko yao, Mungu alikumbuka agano lake na Abrahamu, na Isaka, na Yakobo.
God sh'ma ·heard obeyed· their groaning, and God remembered his covenant ·binding contract between two or more parties· with Abraham [Father of a multitude], with Isaac [Laughter], and with Jacob [Supplanter].
25 Mungu aliwaona Waisraeli na akaielewa hali yao.
God saw the children of Israel [God prevails], and God was concerned about them.

< Kutoka 2 >