< Kutoka 19 >

1 Katika mwezi wa tatu baada ya watu wa Israeli kutoka Misri, siku hiyo, walikwenda nyikani ya Sinai.
In the third month after the children of Israel were gone forth out of the land of Egypt, the same day came they into the wilderness of Sinai.
2 Walipo ondoka Refidimu na kuja nyikani ya Sinai, walieka kambi mbele ya mlima.
And when they were departed from Rephidim, and were come to the wilderness of Sinai, they encamped in the wilderness; and there Israel encamped before the mount.
3 Musa akaenda juu kwa Mungu. Yahweh alimuita kutoka mlimani na kusema, “Lazima uiambie nyumba ya Yakobo, watu wa Israeli:
And Moses went up unto God, and the LORD called unto him out of the mountain, saying: 'Thus shalt thou say to the house of Jacob, and tell the children of Israel:
4 Uliona nilicho fanya kwa Wamisri, jinsi nilivyo kubeba kwa mabawa ya tai na kukuleta kwangu.
Ye have seen what I did unto the Egyptians, and how I bore you on eagles' wings, and brought you unto Myself.
5 Kisha sasa, ukinisikiliza kwa utii sauti yangu na kushika agano langu, kisha utakuwa mali yangu ya pekee miongoni mwa watu wote, kwa kuwa dunia yote ni yangu.
Now therefore, if ye will hearken unto My voice indeed, and keep My covenant, then ye shall be Mine own treasure from among all peoples; for all the earth is Mine;
6 Utakuwa ufalme wa kikuhani na taifa takatifu langu. Haya ni maneno wapaswa kuwaambia Waisraeli.
and ye shall be unto Me a kingdom of priests, and a holy nation. These are the words which thou shalt speak unto the children of Israel.'
7 Hivyo Musa akaja na kuwaita wazee wa watu. Aliweke mbele yao maneno yote haya Yahweh aliyo muamuru.
And Moses came and called for the elders of the people, and set before them all these words which the LORD commanded him.
8 Watu wote walijibu pamoja na kusema, “Tutafanya yote Yahweh aliyo tuambia.” Kisha musa akaja kutoa taarifa ya maneno watu kwa Yahweh.
And all the people answered together, and said: 'All that the LORD hath spoken we will do.' And Moses reported the words of the people unto the LORD.
9 Yahweh akamwambia Musa, “Nitakuja kwako kwa wingu nene ili watu wasikie ninapo sema na wewe na wakuamini milele.” Kisha Musa kamwambia Yahweh maneno ya Yahweh.
And the LORD said unto Moses: 'Lo, I come unto thee in a thick cloud, that the people may hear when I speak with thee, and may also believe thee for ever.' And Moses told the words of the people unto the LORD.
10 Yahweh akamwambia Musa, “Nenda kwa watu. Leo na kesho lazima uwatenge, na kuwafanya waoshe mavazi yao.
And the LORD said unto Moses: 'Go unto the people, and sanctify them to-day and to-morrow, and let them wash their garments,
11 Kuwa tayari kwa siku ya tatu, kwa kuwa siku ya tatu Yahweh atashuka chini ya Mlima Sayuni.
and be ready against the third day; for the third day the LORD will come down in the sight of all the people upon mount Sinai.
12 Lazima uweke mipaka kote kuzunguka mlima kwa ajili ya watu. Uwaambie, 'Kuweni waangalifu msiende juu ya mlima au kushika mipaka yake. Yeyote atakaye shika mlima ata uawa.'
And thou shalt set bounds unto the people round about, saying: Take heed to yourselves, that ye go not up into the mount, or touch the border of it; whosoever toucheth the mount shall be surely put to death;
13 Hakuna mkono wa mtu yeyote kumshika mtu huyu. Badala yake, lazima apigwe mawe au kuchomwa mshale. Iwe ni mtu au mnyama, lazima auawe. Tarumbeta itakapo pigwa muda mrefu, wanaweza kuja chini ya mguu wa mlima.”
no hand shall touch him, but he shall surely be stoned, or shot through; whether it be beast or man, it shall not live; when the ram's horn soundeth long, they shall come up to the mount.'
14 Kisha Musa akashuka mlimani kwenda kwa watu. Aliwatenga watu kwa ajili ya Yahweh na wakaosha mavazi yao.
And Moses went down from the mount unto the people, and sanctified the people; and they washed their garments.
15 Aliwaambia watu, “Kuweni tayari siku ya tatu; msiwakaribie wake zenu.”
And he said unto the people: 'Be ready against the third day; come not near a woman.'
16 Siku ya tatu, ilipo fika asubui, kulikuwa na ngurumo na radi na wingu nene kwenye mlima, na sauti kubwa ya tarumbeta. Watu wote kambini waliogopa.
And it came to pass on the third day, when it was morning, that there were thunders and lightnings and a thick cloud upon the mount, and the voice of a horn exceeding loud; and all the people that were in the camp trembled.
17 Musa akaleta watu kutoka kambini kukutana na Mungu, na wakasimama miguuni mwa mlima.
And Moses brought forth the people out of the camp to meet God; and they stood at the nether part of the mount.
18 Mlima Sina ulijwa kabisa na moshi kwasababu Yahweh alishuka na moto na moshi. Moshi ulipanda juu kama moshi wa tanuru, na mlima wote ulitikisika kwa vurugu.
Now mount Sinai was altogether on smoke, because the LORD descended upon it in fire; and the smoke thereof ascended as the smoke of a furnace, and the whole mount quaked greatly.
19 Sauti ya tarumbeta ilipo ongezeka na zaidi, Musa akazungumza, na Mungu kamjibu kwa sauti.
And when the voice of the horn waxed louder and louder, Moses spoke, and God answered him by a voice.
20 Yahweh akashuka chini ya Mlima Sinai, juu ya mlima, na akamuita Musa kuja juu. Kisha Musa akapanda juu.
And the LORD came down upon mount Sinai, to the top of the mount; and the LORD called Moses to the top of the mount; and Moses went up.
21 Yahweh akamwabia Musa, “Shuka chini na uwaonye watu wasipite kuniangalia, au wengi wao wataangamia.
And the LORD said unto Moses: 'Go down, charge the people, lest they break through unto the LORD to gaze, and many of them perish.
22 Acha pia mukuhani wanao kuja karibu yangu wakitenge - wajiandae kwa ujio - ili nisiwashambulie.”
And let the priests also, that come near to the LORD, sanctify themselves, lest the LORD break forth upon them.'
23 Musa akamwabia Yahweh, “Watu hawawezi kuja juu ya mlima, kwa kuwa umetuamuru: 'Eka mipaka kuzunguka mlima na utenge kwa ajili ya Yahweh.'”
And Moses said unto the LORD: 'The people cannot come up to mount Sinai; for thou didst charge us, saying: Set bounds about the mount, and sanctify it.'
24 Yahweh akamwambia, Nenda, shuka chini ya mlima, na umelete Aruni na wewe, lakini usiache makuhani na watu kupita vizuizi na kuja kwangu, au nitawashambulia.”
And the LORD said unto him: 'Go, get thee down, and thou shalt come up, thou, and Aaron with thee; but let not the priests and the people break through to come up unto the LORD, lest He break forth upon them.'
25 Hivyo Musa akaenda chini kwa watu na kusema nao.
So Moses went down unto the people, and told them.

< Kutoka 19 >