< Kutoka 14 >

1 Yahweh akasema na Musa na kumwambia,
The Lord told Moses,
2 “Waambie Waisraeli wageuke na kueka kambi mbele ya Pi Hahirothi, katikati ya Migdoli na bahari, mbele ya Baali Zefoni. Wapaswa kueka kambi pembenni ya Pi Hahirothi.
“Tell the Israelites to turn back and set up camp near Pi-hahiroth, between Migdol and the sea. You are to camp beside the sea, opposite Baal-zephon.
3 Farao atasema kuhusu Waisraeli, 'Wanaangaika kwenye nchi. Nyikani imewafunika.'
Pharaoh will conclude about the Israelites: ‘They're wandering about the country in confusion—the desert has blocked them from leaving.’
4 Nitaufanya moyo wa Farao mgumu, na yeye ata wakimbiza. Nitapata utukufu kwasababu ya Farao na jeshi lake lote. Wamisri watajua mimi ni Yahweh.” Kisha Waisraeli wakaeka kambi kama walivyo elekezwa.
I will give Pharaoh a stubborn attitude so that he will chase after them to get them back. But I will gain respect through what happens to Pharaoh and all his army, and the Egyptians will know that I am the Lord.” So the Israelites did as they were instructed.
5 Mfalme wa Misri alipo ambiwa Waisraeli wametoroka, nia ya Farao na watumishi wake ikageuka dhidi ya watu. Wakasema, “Tumefanya nini kwa kuwaacha Waisraeli waende huru na wasitutumikie?”
When the king of Egypt found out that the Israelites had left in a hurry, Pharaoh and his officials changed their minds about what had happened and said, “What have we done? We have let all these Israelite slaves go!”
6 Kisha Farao akachukuwa magari yake ya farasi na jeshi lake.
So Pharaoh had his chariot made ready and set out with his army.
7 Alichukuwa magari ya farasi mia sita imara na magari yote ya farasi ya Misri, pamoja na maafisa wa hayo magari.
He took 600 of his best chariots along with all the other chariots of Egypt, each with their officer-in-charge.
8 Yahweh akafanya mgumu moyo wa Farao, mfalme wa Misri, na mfalme akawafukuzia Waisraeli. Sasa Waisraeli waliondoka kwa shangwe.
The Lord gave Pharaoh, king of Egypt, a stubborn attitude so he chased after the Israelites, who were leaving with their fists raised in triumph.
9 Lakini Wamisri wali wafukuzia, pamoja na farasi na magari ya farasi, wapanda farasi, na jeshi lake. Walikuta Waisraeli wameeka kambi pembezoni mwa bahari kati ya Pi Hahirothi na Baali Zefoni.
The Egyptians set out in pursuit—all Pharaoh's horses and chariots, horsemen and soldiers. They caught up with the Israelites while they were camped beside the sea near Pi-hahiroth, opposite Baal-zephon.
10 Farao alipo karibia, Waisraeli walitaza juu na kushangaa. Wamisri walikuwa wakija kwao, na waliogopa. Waisraeli walimlilia Yahweh.
The Israelites looked back and saw Pharaoh and the Egyptian army approaching. They were absolutely terrified and cried out to the Lord for help.
11 Walimwambia Musa, “Ni kwasababu hakukuwa na makaburi Misri, hadi umetuleta tufe huku nyikani? Kwanini umetutendea hivi, kwa kututoa Misri?
They complained to Moses, “Were there no graves in Egypt that you had to bring us out here in the desert to die? What have you done to us by making us leave Egypt?
12 Hili si ndilo tulilo kwambia Misri? Tulikwambia, 'Utuache, ili tuwafanyie Wamisri kazi.' Ingekuwa bora kwetu sisi kuwafanyia kazi kuliko kufa nyikani.”
Didn't we tell you back in Egypt, ‘Leave us alone so that we can go on being slaves to the Egyptians’? It would have been better for us to be Egyptian slaves than to die here in the desert!”
13 Musa akawaambia watu, “Msiogope. Simameni imara na muone wokovu Yahweh atakao uleta kwenu leo. Kwa maana hamtawaona tena Wamisri mnao waona leo.
But Moses said to the people, “Do not be afraid. Stand where you are and you will see how the Lord will save you today. The Egyptians you see right now, you will never see again!
14 Yahweh ata wapigania, na ninyi mtasima imara.”
The Lord is going to fight for you—you don't need to do anything.”
15 Kisha Yahweh akamwambia Musa, “Kwanini wewe, Musa, unaendelea kuniita mimi? Waambie Waisraeli waendelee mbele.
The Lord told Moses, “Why are you crying out to me for help? Tell the Israelites to move forward.
16 Nyanyua gongo lako juu, nyoosha mkono wako kuelekea baharini na uigawanye sehemu mbili, ili watu wa Israeli wapite baharini kwenye nchi kavu.
You are to pick up your walking stick and hold it out in your hand over the sea. Divide it so the Israelites can walk through the sea on dry ground.
17 Jitahadharishe kuwa nitafanya mioyo ya Wamisri kuwa migumu ili wawafuate. Nitapata utukufu kwasababu ya Farao na jeshi lake lote, magari yake ya farasi, na wapanda farasi.
I will give Egyptians a stubborn, hard-hearted attitude so that they will chase in after them. Then I will gain respect through what happens to Pharaoh and all his army, chariots, and horsemen.
18 Kisha Wamisri watajua kuwa mimi ni Yahweh nitakapo pata utukufu kwasababu ya Farao, magari yake ya farasi, na wapanda farasi wake.”
The Egyptians will know that I am the Lord when I gain respect through Pharaoh, his chariots, and his horsemen.”
19 Malaika wa Mungu, aliyeenda mbele ya Waisraeli, aliama na kwenda nyuma yao. Nguzo ya wingu ili sogea mbele yao na kwenda kusimama nyumba yao.
The angel of God, who had been leading the Israelites, moved behind them. The pillar of cloud also moved from in front of them and stood behind them,
20 Wingu lilikuja katikati ya kambi ya Misri na kambi ya Israeli. Lilikuwa wingu jeusi kwa Wamisri, lakini liliangaza usiku kwa ajili ya Waisraeli, hivyo upande mmoja haukuweza kuja karibu ya mwingine usiku wote.
so that it was positioned between the Egyptian and Israelite camps. Though the cloud was in darkness on one side, but it lit up the night on the other. No one from either camp went near the other during the night.
21 Musa akanyoosha mkono wake kuelekea bahari. Yahweh akasogeza bahari nyuma kwa upepo mkali wa mashariki usiku huo wote na kufanya bahari nchi kavu. Kwa namna hii maji yaligawanyika.
Then Moses held out his hand over the sea, and all through the night the Lord forced the sea back with a strong east wind, and turned the bottom of the sea into dry land. So the water was divided,
22 Waisraeli walienda katikati ya bahari kwa nchi kavu. Maji yaliunda ukuta mkono wao wa kulia na mkono wao wa kushoto.
and the Israelites walked through the sea on dry ground, with walls of water to their right and left.
23 Wamisri waka wafukuzia. Wali wafuata hadi katikati ya bahari - farasi wote wa Farao, magari ya farasi, na wapanda farasi.
The Egyptians chased after them—all Pharaoh's horses, chariots, and horsemen. They followed the Israelites into the sea.
24 Lakini masaa ya mapema ya asubui, Yahweh alitazama chini jeshi la Wamisri kupitia nguzo ya moto na wingu. Alisababisha hofu miongoni mwa Wamisri.
But at the end of the night the Lord looked down on the Egyptian army from the pillar of fire and cloud, and he threw them into a panic.
25 Magari yao ya farasi yalikuwa yana kwama matairi, na wapanda farasi waliendesha kwa ugumu. Hivyo Wamisri walisema, “Acha tuwakimbie Waisraeli, kwa kuwa Yahweh anawapigania dhidi yetu.”
He made their chariot wheels get stuck so it was hard for them to drive. The Egyptians shouted out, “Retreat! We must run from the Israelites because the Lord is fighting for them against us!”
26 Yahweh akamwambia Musa, “Nyoosha mkono kuelekea bahari ili maji yawarudie Wamisri, magari yao ya farasi, na wapanda farasi wao.”
Then the Lord told Moses, “Hold out your hand over the sea, so that the water will pour back over the Egyptians and their chariots and horsemen.”
27 Hivyo Musa akanyoosha mkono wake kuelekea bahari, na ikarudi kwenye hali yake ya kawaida palipo pambazuka. Wamisri walikimbilia ndani ya bahari, na Yahweh akawaingiza Wamisri katikati ndani yake.
So Moses held out his hand over the sea, and at dawn the sea returned to normal. As the Egyptians retreated, the Lord swept them into the sea.
28 Maji yakarudi na kufunika magari ya farasi ya Farao, wapanda farasi, na jeshi lake lote lililo fuata magari ya farasi kwenye bahari. Hakuna aliyepona.
The water poured back and covered the chariots and horsemen—the whole of Pharaoh's army that had chased after the Israelites into the sea. Not a single one of them survived.
29 Walakini, Waisraeli walitembea kwenye nchi kavu katikati ya bahari. Maji yalikuwa ukuta kwao mkono wa kulia na mkono wa kushoto.
But the Israelites had walked through the sea on dry ground, with walls of water to their right and left.
30 Hivyo Yahweh akaokoa Israeli hiyo siku kutoka mkono wa Wamisri, na Israeli ikaona maiti za Wamisri ufukweni.
The Lord saved the Israelites from the threat of the Egyptians—the Israelites saw the Egyptians lying dead on the shore.
31 Israeli ilipoona nguvu kubwa Yahweh aliyo itumia dhidi ya Wamisri, watu walimsifu Yahweh, na kumwamini Yahweh na mtumishi wake Musa.
When the Israelites saw the great power that the Lord had used against the Egyptians, they were in awe of the Lord, and they trusted in him and in his servant Moses.

< Kutoka 14 >