< Kutoka 12 >

1 Yahweh akasema na Musa na Aruni katika nchi ya Misri. Alisema,
Then spake Yahweh, unto Moses and unto Aaron, in the land of Egypt saying—
2 “Kwako wewe, mwezi huu utakuwa mwanzo wa miezi, mwezi wa kwanza wa mwaka kwako.
This month, is, to you, a beginning of months, —the first, it is, to you, of the months of the year.
3 Liambie kusanyiko la Israeli, 'Siku ya kumi mwezi huu kila mtu lazima achukuwe mwana kondoo au mbuzi mdogo wa kwake, kila familia ifanye hivi, mwana kondoo kwa kila nyumba.
Speak ye unto all the assembly of Israel, saying, On the tenth of this month, then let them take to them, each man a lamb for his ancestral household, a lamb for a household.
4 Kama hiyo nyumba ni ndogo sana kwa mwana kondoo, mwanaume na jirani yake wachukuwe mwana kondoo au nyama ya mbuzi mdogo ambayo itatosha watu. Lazima iwe yatosha kwa kila mtu kula, kwaiyo lazima wachukuwe nyama ya kutosha kulisha wote.
But if the household be too small for a lamb, then shall he and his neighbour that is near unto his house take one, according to the number of souls, —each man according to his eating, shall ye number for the lamb.
5 Mwana kondoo wako au mbuzi wako mdogo lazima asiwe na upungufu, dume mwenye mwaka mmoja. Unaweza kuchukuwa mmoja wa kondoo au mbuzi.
A lamb without defect a male a year old, shall yours be, —from the sheep or from the goats, shall ye take it.
6 Lazima umtunze mpaka siku ya kumi na nne ya huo mwezi. Kisha kusanyiko lote la Israeli lazima liwaue hawa wanyama jioni.
So shall it be yours, to keep, until the fourteenth day of this month, —then shall all the convocation of the assembly of Israel slay it between the two evenings.
7 Lazima uchukuwe baadhi ya damu na uweke kwenye sehemu mbili za mihimili ya milango na juu ya fremu za milango ambapo utalia hizo nyama.
And they shall take of the blood, and put upon the two door-posts and upon the upper-beam, —upon the houses wherein they are to eat it.
8 Lazima ule hizo nyama usiku, baada ya kuchoma kwenye moto. Kula na mkate ulio andaliwa kwa hamira, pamoja na mimea michungu.
Then shall they eat the flesh, in the same night, —roast with fire, and with unleavened cakes, with bitter herbs, shall they eat it.
9 Usiile mbichi au imechemshwa kwenye maji. Badala yake, choma kwenye moto na kichwa chake, miguu na sehemu za ndani.
Do not eat of it underdone, nor cooked by boiling in water, —but roast with fire, its head with its legs, and with its inward parts.
10 Usiache ata kidogo kubaki mpaka asubui. Lazima uchome chochote kilicho baki asubui.
And ye shall let nothing thereof remain until morning, —but that which is left remaining until morning, in the fire shall ye consume.
11 Hivi ndivyo wa paswa kula: ukiwa umefunga mkanda wako, umevaa viatu vyako, na gongo lako mkononi mwako. Lazima ule kwa haraka. Ni Pasaka ya Yahweh.
And, thus, shall ye eat it, —your loins, girded, your sandals, on your feet, and, your staff, in your hand, —so shall ye eat it in haste, it is Yahweh’s, passing over.
12 Yahweh anasema hili: Nitaenda katika nchi ya Misri usiku na kushambulia wazaliwa wote wa kwanza wa wanadamu na wanyama katika nchi ya Misri. Nitaleta pigo kwa miungu yote ya Misri. Mimi ni Yahweh.
I will pass along, therefore, throughout the land of Egypt this night, and will smite every firstborn in the land of Egypt, from man even to beast, —and against all the gods of Egypt, will I execute judgments—I, Yahweh.
13 Damu itakuwa ishara kwenye nyumba zenu ya kuja kwangu. Nitakapo ona damu, nitapita nitakapo shambulia nchi ya Misri. Ili pigo halitawajia na kuwaharibu.
Then shall the blood serve you for a sign, on the houses wherein ye are, then will I behold the blood, and will pass over you, —and there shall be among you no plague to destroy, when I smite the land of Egypt.
14 Hii siku itakuwa kumbukumbu kwenu, ambayo lazima muadhimishe kama sherehe ya Yahweh. Itakuwa sheria kwenu pia, kwenye vizazi vyote vya watu wenu, ambayo mwapaswa kuadhimisha leo.
So shall this day serve you for a memorial, and ye shall celebrate it, as a festival to Yahweh, —to your generations—as an age-abiding statute, shall ye celebrate it.
15 Utakula mkate bila hamira wakati wa siku saba. Siku ya kwanza utaondoa hamira kwenye nyumba zenu. Yeyote atakaye kula mkate uliyotiwa chachu kwanzia siku ya kwanza mpaka siku ya saba, huyo mtu lazima akatwe kutoka Israeli.
Seven days, unleavened cakes, shall ye eat, surely, on the first day, shall ye put away leaven, out of your houses, —for whosoever eateth what is leavened, then shall that soul be cut off out of Israel, from the first day, unto the seventh day.
16 Siku ya kwanza kutakuwa na kusanyiko lililo tengwa kwa ajili yangu, na siku ya saba kutakuwa na kusanyiko kama hilo. Hakuna kazi itakayo fanywa hizi siku, zaidi ya kupika kila mmoja ale. Hiyo ndio kazi pekee itakayo fanywa na wewe.
Both on the first day, a holy convocation, and on the seventh day—a holy convocation, shall there be to you, —no work, shall be done therein, save only what must be eaten by every soul, that alone, shall be done by you.
17 Lazima uadhimishe hii Sherehe ya Mkate Usiotiwa Chachu kwasababu ni siku hii ambayo nitawaleta watu wako, makundi yaliyo na silaha, kwa makundi yaliyo na silaha, kutoka nchi ya Misri. Lazima uadhimishe hii siku kwa vizazi vyote vya watu wako. Hii itakuwa sheria kwako.
So then ye shall observe the unleavened cakes, because on this self-same day, brought I forth your hosts out of the land of Egypt, —so then ye shall observe this day to your generations, as a statute age-abiding,
18 Lazima ule mkate usiotiwa chachu kuanzia jioni ya siku ya kumi na nne ya mwezi wa kwanza wa mwaka, mpaka jioni ya siku ya ishirini na moja ya mwezi.
In the first month, on the fourteenth day of the month in the evening, shall ye eat unleavened cakes, —until the one-and-twentieth day of the month in the evening,
19 Wakati wa hizi siku, nyumbani mwenu kusipatikane na hamira. Yeyote atakaye kula mkate ulio andaliwa na hamira lazima akatwe kutoka jamii ya Israeli, huyo mtu awe ni mgeni au mtu aliye zaliwa nchini mwenu.
For seven days, leaven, shall not be found in your houses, —for, whosoever eateth what is leavened, then shall that soul be cut off out of the assembly of Israel, whether sojourner or native of the land.
20 Hautakula chochote kilicho andaliwa na hamira. Popote utapo ishi, lazima ule mkate usio na hamira.”'
Nothing leavened, shall ye eat, —in all your dwellings, shall ye eat unleavened cakes.
21 Kisha Musa akawaita viongozi wote wa Israeli na kuwaambia, “Nendeni na mchague mwana kondoo au mbuzi watakao tosha kulisha familia zenu na muue mwana kondoo wa pasaka.
So then Moses called for all the elders of Israel, and said unto them, —Proceed and take for yourselves one of the flock according to your families, and slay the passover.
22 Kisha chukua jani la hisopu na uchovye kwenye damu itakayo kuwa kwenye beseni. Paka damu iliyo kwenye beseni juu ya fremu ya mlango na kwenye mihimili miwili ya mlango. Hakuna ata mmoja atakaye toka nje ya mlango wake mpaka asubui.
Then shall ye take a bunch of hyssop, and dip it in the blood which is in the basin, and strike the upper beam and the two door-posts, with the blood which is in the basin, —and, ye, shall not go forth any man out of the entrance of his house, until morning,
23 Kwa kuwa Yahweh atapita kushambulia Wamisri. Atakapo ona damu juu ya fremu ya mlango na kwenye mihimili miwili ya mlango, atapita mlango wako na ata ruhusu mharibifu kuja nyumbani kwenu kuwashambulia.
And Yahweh will pass along to plague the Egyptians, and when he beholdeth the blood upon the upper beam and upon the two door-posts, then will Yahweh pass over the entrance, and not suffer the destroyer to enter into your houses to inflict on you the plague.
24 Lazima uadhimishe hili tukio. Hili litakuwa daima sheria kwako na kwa uzao wenu.
And ye shall observe this thing, —for a statute to thee and to thy sons unto times age-abiding.
25 Utakapo ingia nchi Yahweh atakayo kupa, kama alivyo ahidi kufanya, lazima uadhimishe hili tendo la ibada.
And so it shall come to pass when ye shall enter into the land which Yahweh will give you as he hath spoken, —and ye shall observe this service;
26 Watoto wako watakapo kuuliza, 'Hili tendo la ibada lina maana gani?'
and it shall come to pass that your sons shall say unto you, —What is this your service?
27 kisha lazima useme, 'Ni sadaka ya Pasaka ya Yahweh, kwasababu Yahweh kapita nyumba za Waisraeli Misri alipo washambulia Wamisri. Aliweka nyumba zetu huru.”' Kisha watu wakamsujudia Yahweh.
Then shall ye say—A passover sacrifice, it is to Yahweh, who passed-over the houses of the sons of Israel, in Egypt, when he plagued the Egyptians but our houses, he delivered. Then did the people bend their heads and bow themselves down.
28 Waisraeli wakaenda na kufanya kama Yahweh alivyo waamuru Musa na Aruni.
And the sons of Israel went their way and did, —as Yahweh had commanded Moses and Aaron, so, did they.
29 Ikawa usiku wa manane kuwa Yahweh akawashambulia wazaliwa wote wa kwanza wa nchi ya Misri, kuanzia mzaliwa wa kwanza wa Farao, aliye keti kiti chake cha enzi, mzaliwa wa kwanza wa mtu aliye gerezani na wazaliwa wote wa kwanza wa mifugo.
And it came to pass, at midnight, that Yahweh, smote every firstborn in the land of Egypt, from the firstborn of Pharaoh who sat upon his throne, unto the firstborn of the captive who was in the pit of his prison, —and every firstborn of beasts.
30 Farao akaamka usiku - yeye, watumishi wake, na Wamisri. Palikuwa na kelele za maombolezo Misri, kwa kuwa hakukuwa na nyumba ambayo hamna mtu hakufa.
Then rose up Pharaoh by night, he, and all his servants, and all the Egyptians, and there arose a great outcry throughout Egypt, —for there was not a house, where there was not one dead.
31 Farao akamuita Musa na Aruni usiku na kusema, “Inuka, tokeni miongoni mwa watu wangu, nyie pamoja na Waisraeli. Nenda, mmuabudu Yahweh, kama mlivyo sema mnataka kufanya.
So he called for Moses and for Aaron by night and said—Rise ye, go forth out of the midst of my people, both ye and the sons of Israel, —and go serve Yahweh according to your word;
32 Chukuweni ng'ombe zenu na kondoo zenu, kama mlivyo sema, na muende, na pia mnibariki.”
also, your flocks and your herds, take ye, as ye spake and go your way, —so shall ye bless, even me.
33 Wamisri walikuwa na haraka ya kuwa ondoa nchini, kwa kuwa walisema, “Sisi ni watu tuliokufa.”
And the Egyptians became urgent with the people, to send them in haste out of the land, —for they said—We all, are dying.
34 Watu wakachukuwa ngano yao pasipo kuongeza hamira yeyote. Bakuli zao zakukandia ngano zilifungiwa kwenye nguo zao na kwenye mabega yao.
So the people took up their dough, ere yet it was leavened, —with their kneading-bowls, bound up in their mantles on their shoulders,
35 Watu Waisraeli walifanya kama Musa alivyo waambia. Waliwaomba Wamisri vitu vya fedha, vitu vya dhahabu, na nguo.
And the sons of Israel, did according to the word of Moses, —and asked of the Egyptians, articles of silver and articles of gold and mantles.
36 Yahweh aliwafanya Wamisri na shauku ya kuwapendeza Waisraeli. Hivyo Wamisri waliwapa chochote walicho waomba. Katika hili, Waisraeli waliwachukulia vingi Wamisri.
And Yahweh, gave the people favour in the eyes of the Egyptians and they gave them gladly, —so they spoiled the Egyptians.
37 Waisraeli wakasafiri kutoka Ramesi kwenda Sakothi. Walikuwa na idadi ya wanaume 600, 000 kwa miguu, kuongezea kwa wanawake na watoto.
Then did the sons of Israel break up from Rameses, towards Succoth, —about six hundred thousand foot of men grown, besides little ones.
38 Mchanganyiko wa kundi la wasio Waisraeli pia walienda nao, pamoja na ng'ombe na kondoo, idadi kumbwa ya mifugo.
Moreover also, a mixed multitude, came up with them, —flocks also, and herds, exceeding much cattle,
39 Walioka mikate na unga wa ngano wenye hamira walio utoa Misri. Ulikuwa hauna hamira kwasababu waliondolewa Misri na hawakuweza chelewa kuandaa chakula.
Then baked they the dough which they had brought out of Egypt—into round unleavened cakes for it had not been leavened, —for they had been driven out of Egypt and could not tarry, and indeed no provisions, had they made ready for themselves.
40 Waisraeli waliishi Misri kwa miaka 430.
Now, the time during which the sons of Israel dwelt in Egypt, was four hundred and thirty years.
41 Baada ya miaka 430, siku hiyo hiyo, majeshi yote ya Yahweh yalio jiami waliondoka kutoka nchi ya Misri.
And it came to pass at the end of four hundred and thirty years, yea it came to pass, on this self-same day, that all the hosts of Yahweh had come forth out of the land of Egypt.
42 Huu ulikuwa usiku wakuwa macho, ili Yahweh awatoe kutoka nchi ya Misri. Huu ulikuwa usiku wa Yahweh wa kuadhimishwa na Waisraeli wote na watu wa vizazi vyao vyote.
A night of solemn observances, it is unto Yahweh, for bringing them forth out of the land of Egypt, —this same night, pertaineth to Yahweh, for solemn observances by all the sons of Israel to their generations.
43 Yahweh akamwambia Musa na Aruni, “Hii ni sheria ya Pasaka: hakuna mgeni anaye ruhusiwa kuila.
And Yahweh said unto Moses and Aaron: This, is the statute of the passover, —No stranger, shall eat thereof;
44 Walakini, kila mtumwa wa Misraeli, aliye nunuliwa kwa pesa, anaeza kula baada ya kutahiriwa.
but, every man’s servant bought with silver, —when thou hast circumcised him, then, shall he eat thereof:
45 Wageni na watumishi waajiriwa hawapaswi kula chakula chochote.
An alien or a hireling, shall not eat thereof.
46 Chakula chapaswa kuliwa ndani ya nyumba moja. Hauruhusiwi kubeba nyama yeyote nje ya nyumba, na hauruhusiwi kuvunja mfumba wowote.
In one house, shall it be eaten, thou shalt not take forth out of the house any of the flesh outside; and a, bone thereof, shalt thou not break.
47 Jamii zote za Israeli za paswa kuadhimisha sherehe.
All the assembly of Israel, shall keep it.
48 Kama mgeni anaishi na wewe na anataka kuadhimisha Pasaka kwa Yahweh, ndugu zake wote wa kiume wapaswa kutahiriwa. Kisha anaeza kuja na kuadhimisha. Atakuwa kama watu walio zaliwa kwenye nchi. Walakini, hakuna mtu asiye tahiriwa anaruhusiwa kula chakula chochote.
And when there may sojourn with thee a sojourner who may wish to keep a passover to Yahweh, there must be circumcised to him every male and then, may he draw near to keep it, so shall he be as a native of the land, —but no uncircumcised male, shall eat thereof.
49 Sheria hii hii itahusika kwa mzaliwa wa asili na mgeni anayeishi miongoni mwenu.”
One law, shall there be for the native, and for the sojourner that sojourneth in your midst.
50 Waisraeli wote walifanya kama Yahweh alivyo waamuru Musa na Aruni.
Thus did all the sons of Israel, —as Yahweh had commanded Moses and Aaron, so, did they.
51 Ikaja kuwa siku hiyo Yahweh akawaleta Israeli kutoka nchi ya Misri kwa makundi yalio jiami.
And it came to pass, on this self-same day, that Yahweh brought forth the sons of Israel out of the land of Egypt, by their hosts.

< Kutoka 12 >