< Kutoka 12 >

1 Yahweh akasema na Musa na Aruni katika nchi ya Misri. Alisema,
And the Lord spoke unto Moses and Aaron in the land of Egypt, saying,
2 “Kwako wewe, mwezi huu utakuwa mwanzo wa miezi, mwezi wa kwanza wa mwaka kwako.
This month shall be unto you the chief of months: the first shall it be unto you of the months of the year.
3 Liambie kusanyiko la Israeli, 'Siku ya kumi mwezi huu kila mtu lazima achukuwe mwana kondoo au mbuzi mdogo wa kwake, kila familia ifanye hivi, mwana kondoo kwa kila nyumba.
Speak ye unto all the congregation of Israel, saying, On the tenth day of this month they shall take to themselves every man a lamb for every family, a lamb for every house:
4 Kama hiyo nyumba ni ndogo sana kwa mwana kondoo, mwanaume na jirani yake wachukuwe mwana kondoo au nyama ya mbuzi mdogo ambayo itatosha watu. Lazima iwe yatosha kwa kila mtu kula, kwaiyo lazima wachukuwe nyama ya kutosha kulisha wote.
And if the household be too small for a lamb, then shall he take it with his neighbor who is next unto his house, according to the number of the souls; every man according to what he eateth shall ye make a count for the lamb.
5 Mwana kondoo wako au mbuzi wako mdogo lazima asiwe na upungufu, dume mwenye mwaka mmoja. Unaweza kuchukuwa mmoja wa kondoo au mbuzi.
A lamb without blemish, a male of the first year shall ye have; from the sheep, or from the goats may ye take it.
6 Lazima umtunze mpaka siku ya kumi na nne ya huo mwezi. Kisha kusanyiko lote la Israeli lazima liwaue hawa wanyama jioni.
And ye shall have it in keeping until the fourteenth day of the same month; and then the whole assembly of the congregation of Israel shall kill it toward evening.
7 Lazima uchukuwe baadhi ya damu na uweke kwenye sehemu mbili za mihimili ya milango na juu ya fremu za milango ambapo utalia hizo nyama.
And they shall take of the blood, and put it on the two side-posts and on the upper door-post, in the houses, wherein they shall eat it.
8 Lazima ule hizo nyama usiku, baada ya kuchoma kwenye moto. Kula na mkate ulio andaliwa kwa hamira, pamoja na mimea michungu.
And they shall eat the flesh in that night, roasted by the fire, with unleavened bread; together with bitter herbs shall they eat it.
9 Usiile mbichi au imechemshwa kwenye maji. Badala yake, choma kwenye moto na kichwa chake, miguu na sehemu za ndani.
You shall not eat of it raw, nor in any wise sodden with water; but roasted by the fire; its head with its legs, and with its entrails.
10 Usiache ata kidogo kubaki mpaka asubui. Lazima uchome chochote kilicho baki asubui.
And ye shall not let any thing of it remain until morning; and that which remaineth of it until morning ye shall burn with fire.
11 Hivi ndivyo wa paswa kula: ukiwa umefunga mkanda wako, umevaa viatu vyako, na gongo lako mkononi mwako. Lazima ule kwa haraka. Ni Pasaka ya Yahweh.
And thus shall ye eat it, With your loins girded, your shoes on your feet, and your staff in your hand; and ye shall eat it in haste, it is passover unto the Lord.
12 Yahweh anasema hili: Nitaenda katika nchi ya Misri usiku na kushambulia wazaliwa wote wa kwanza wa wanadamu na wanyama katika nchi ya Misri. Nitaleta pigo kwa miungu yote ya Misri. Mimi ni Yahweh.
And I will pass through the land of Egypt in this night, and I will smite every first-born in the land of Egypt, both man and beast; and against all the gods of Egypt will I execute judgments: I am the Lord.
13 Damu itakuwa ishara kwenye nyumba zenu ya kuja kwangu. Nitakapo ona damu, nitapita nitakapo shambulia nchi ya Misri. Ili pigo halitawajia na kuwaharibu.
And the blood shall be to you for a token upon the houses where ye are; and when I see the blood, I will pass over you; and there shall be no plague against you to destroy, when I smite [others] in the land of Egypt.
14 Hii siku itakuwa kumbukumbu kwenu, ambayo lazima muadhimishe kama sherehe ya Yahweh. Itakuwa sheria kwenu pia, kwenye vizazi vyote vya watu wenu, ambayo mwapaswa kuadhimisha leo.
And this day shall be unto you for a memorial; and ye shall celebrate it as a feast unto the Lord; throughout your generations, as an ordinance for ever shall ye celebrate it.
15 Utakula mkate bila hamira wakati wa siku saba. Siku ya kwanza utaondoa hamira kwenye nyumba zenu. Yeyote atakaye kula mkate uliyotiwa chachu kwanzia siku ya kwanza mpaka siku ya saba, huyo mtu lazima akatwe kutoka Israeli.
Seven days shall ye eat unleavened bread; but on the first day ye shall have put away leaven out of your houses; for whosoever eateth leavened bread, that soul shall be cut off from Israel, from the first day until the seventh day.
16 Siku ya kwanza kutakuwa na kusanyiko lililo tengwa kwa ajili yangu, na siku ya saba kutakuwa na kusanyiko kama hilo. Hakuna kazi itakayo fanywa hizi siku, zaidi ya kupika kila mmoja ale. Hiyo ndio kazi pekee itakayo fanywa na wewe.
And on the first day there shall be a holy convocation, and on the seventh day there shall be a holy convocation to you; no manner of work shall be done on them, save what is eaten by every man, that only may be prepared by you.
17 Lazima uadhimishe hii Sherehe ya Mkate Usiotiwa Chachu kwasababu ni siku hii ambayo nitawaleta watu wako, makundi yaliyo na silaha, kwa makundi yaliyo na silaha, kutoka nchi ya Misri. Lazima uadhimishe hii siku kwa vizazi vyote vya watu wako. Hii itakuwa sheria kwako.
And ye shall observe the unleavened bread; for on this selfsame day have I brought forth your armies out of the land of Egypt; therefore shall ye observe this day in your generations as an ordinance for ever.
18 Lazima ule mkate usiotiwa chachu kuanzia jioni ya siku ya kumi na nne ya mwezi wa kwanza wa mwaka, mpaka jioni ya siku ya ishirini na moja ya mwezi.
In the first month, on the fourteenth day of the month, at evening, shall ye eat unleavened bread, until the one and twentieth day of the month at evening.
19 Wakati wa hizi siku, nyumbani mwenu kusipatikane na hamira. Yeyote atakaye kula mkate ulio andaliwa na hamira lazima akatwe kutoka jamii ya Israeli, huyo mtu awe ni mgeni au mtu aliye zaliwa nchini mwenu.
Seven days no leaven shall be found in your houses; for whosoever eateth that which is leavened, even that soul shall be cut off from the congregation of Israel, whether he be a stranger, or one born in the land.
20 Hautakula chochote kilicho andaliwa na hamira. Popote utapo ishi, lazima ule mkate usio na hamira.”'
Nothing that is leavened shall ye eat; in all your habitations shall ye eat unleavened bread.
21 Kisha Musa akawaita viongozi wote wa Israeli na kuwaambia, “Nendeni na mchague mwana kondoo au mbuzi watakao tosha kulisha familia zenu na muue mwana kondoo wa pasaka.
And Moses called for the elders of Israel, and said unto them, Draw out and take for yourselves lambs according to your families, and kill the passover sacrifice.
22 Kisha chukua jani la hisopu na uchovye kwenye damu itakayo kuwa kwenye beseni. Paka damu iliyo kwenye beseni juu ya fremu ya mlango na kwenye mihimili miwili ya mlango. Hakuna ata mmoja atakaye toka nje ya mlango wake mpaka asubui.
And ye shall take a bunch of hyssop, and dip in the blood that is in the basin, and strike the lintel and the two side-posts with the blood that is in the basin; and none of you shall go out frown the door of his house until the morning.
23 Kwa kuwa Yahweh atapita kushambulia Wamisri. Atakapo ona damu juu ya fremu ya mlango na kwenye mihimili miwili ya mlango, atapita mlango wako na ata ruhusu mharibifu kuja nyumbani kwenu kuwashambulia.
And the Lord will pass through to smite the Egyptians; and when he seeth the blood upon the lintel, and on the two side-posts, the Lord will pass over the door, and will not suffer the destroyer to come in unto your houses to smite.
24 Lazima uadhimishe hili tukio. Hili litakuwa daima sheria kwako na kwa uzao wenu.
And ye shall observe this thing, as an ordinance for thee and for thy sons for ever.
25 Utakapo ingia nchi Yahweh atakayo kupa, kama alivyo ahidi kufanya, lazima uadhimishe hili tendo la ibada.
And it shall come to pass, when ye be come into the land which the Lord will give you, according as he hath promised, that ye shall keep this service.
26 Watoto wako watakapo kuuliza, 'Hili tendo la ibada lina maana gani?'
And it shall come to pass, when your children shall say unto you, What mean ye by this service?
27 kisha lazima useme, 'Ni sadaka ya Pasaka ya Yahweh, kwasababu Yahweh kapita nyumba za Waisraeli Misri alipo washambulia Wamisri. Aliweka nyumba zetu huru.”' Kisha watu wakamsujudia Yahweh.
That ye shall say, It is the sacrifice of the passover unto the Lord, who passed over the houses of the children of Israel in Egypt, when he smote the Egyptians, and our houses he spared; and the people bent the head and bowed themselves.
28 Waisraeli wakaenda na kufanya kama Yahweh alivyo waamuru Musa na Aruni.
And the children of Israel went away, and did as the Lord had commanded Moses and Aaron, so did they.
29 Ikawa usiku wa manane kuwa Yahweh akawashambulia wazaliwa wote wa kwanza wa nchi ya Misri, kuanzia mzaliwa wa kwanza wa Farao, aliye keti kiti chake cha enzi, mzaliwa wa kwanza wa mtu aliye gerezani na wazaliwa wote wa kwanza wa mifugo.
And it came to pass at midnight, that the Lord smote every first-born in the land of Egypt, from the first-born of Pharaoh that was to sit on his throne unto the first-born of the captive that was in the dungeon; and all the first-born of cattle.
30 Farao akaamka usiku - yeye, watumishi wake, na Wamisri. Palikuwa na kelele za maombolezo Misri, kwa kuwa hakukuwa na nyumba ambayo hamna mtu hakufa.
And Pharaoh rose up in the night, he, and all his servants, and all the Egyptians; and there was a great cry in Egypt; for there was not a house where there was not some one dead.
31 Farao akamuita Musa na Aruni usiku na kusema, “Inuka, tokeni miongoni mwa watu wangu, nyie pamoja na Waisraeli. Nenda, mmuabudu Yahweh, kama mlivyo sema mnataka kufanya.
And he called for Moses and Aaron by night, and said, Rise up, get you forth from among my people, both ye and the children of Israel; and go, serve the Eternal, as ye have spoken.
32 Chukuweni ng'ombe zenu na kondoo zenu, kama mlivyo sema, na muende, na pia mnibariki.”
Also your flocks and your herds take, as ye have spoken, and be gone; and bless me also.
33 Wamisri walikuwa na haraka ya kuwa ondoa nchini, kwa kuwa walisema, “Sisi ni watu tuliokufa.”
And the Egyptians were urgent upon the people, to make haste to send them away out of the land; for they said, We are all dying.
34 Watu wakachukuwa ngano yao pasipo kuongeza hamira yeyote. Bakuli zao zakukandia ngano zilifungiwa kwenye nguo zao na kwenye mabega yao.
And the people took up their dough before it was yet leavened, their kneading-troughs being bound up in their clothes upon their shoulders.
35 Watu Waisraeli walifanya kama Musa alivyo waambia. Waliwaomba Wamisri vitu vya fedha, vitu vya dhahabu, na nguo.
And the children of Israel had done according to the word of Moses; and they had asked of the Egyptians vessels of silver, and vessels of gold, and garments.
36 Yahweh aliwafanya Wamisri na shauku ya kuwapendeza Waisraeli. Hivyo Wamisri waliwapa chochote walicho waomba. Katika hili, Waisraeli waliwachukulia vingi Wamisri.
And the Lord had given the people favor in the eyes of the Egyptians, so that they gave unto them what they required; and they emptied out Egypt.
37 Waisraeli wakasafiri kutoka Ramesi kwenda Sakothi. Walikuwa na idadi ya wanaume 600, 000 kwa miguu, kuongezea kwa wanawake na watoto.
And the children of Israel journeyed from Ra'meses to Succoth, about six hundred thousand men on foot, beside children.
38 Mchanganyiko wa kundi la wasio Waisraeli pia walienda nao, pamoja na ng'ombe na kondoo, idadi kumbwa ya mifugo.
And a mixed multitude also went up with them; and flocks, and herds, a very large amount of cattle.
39 Walioka mikate na unga wa ngano wenye hamira walio utoa Misri. Ulikuwa hauna hamira kwasababu waliondolewa Misri na hawakuweza chelewa kuandaa chakula.
And they baked of the dough, which they had brought forth out of Egypt, unleavened cakes, for it was not leavened; because they were thrust out of Egypt, and could not tarry, neither had they prepared any provisions for themselves.
40 Waisraeli waliishi Misri kwa miaka 430.
Now the time of the residence of the children of Israel, which they dwelt in Egypt, was four hundred and thirty years.
41 Baada ya miaka 430, siku hiyo hiyo, majeshi yote ya Yahweh yalio jiami waliondoka kutoka nchi ya Misri.
And it came to pass at the end of the four hundred and thirty years, and it happened even on the selfsame day, that all the armies of the Lord went out from the land of Egypt.
42 Huu ulikuwa usiku wakuwa macho, ili Yahweh awatoe kutoka nchi ya Misri. Huu ulikuwa usiku wa Yahweh wa kuadhimishwa na Waisraeli wote na watu wa vizazi vyao vyote.
A night to be observed was this unto the Lord to bring them out from the land of Egypt: this is that night holy to the Lord, to be observed by all the children of Israel in their generations.
43 Yahweh akamwambia Musa na Aruni, “Hii ni sheria ya Pasaka: hakuna mgeni anaye ruhusiwa kuila.
And the Lord said unto Moses and Aaron, This is the ordinance of the passover: No stranger shall eat thereof.
44 Walakini, kila mtumwa wa Misraeli, aliye nunuliwa kwa pesa, anaeza kula baada ya kutahiriwa.
But every man's servant that is bought for money, when thou hast circumcised him, then shall he eat thereof.
45 Wageni na watumishi waajiriwa hawapaswi kula chakula chochote.
A resident foreigner and a hired servant shall not eat thereof.
46 Chakula chapaswa kuliwa ndani ya nyumba moja. Hauruhusiwi kubeba nyama yeyote nje ya nyumba, na hauruhusiwi kuvunja mfumba wowote.
In one house shall it be eaten; thou shalt not carry forth aught of the flesh abroad out of the house; and no bone shall ye break in it.
47 Jamii zote za Israeli za paswa kuadhimisha sherehe.
All the congregation of Israel shall prepare it.
48 Kama mgeni anaishi na wewe na anataka kuadhimisha Pasaka kwa Yahweh, ndugu zake wote wa kiume wapaswa kutahiriwa. Kisha anaeza kuja na kuadhimisha. Atakuwa kama watu walio zaliwa kwenye nchi. Walakini, hakuna mtu asiye tahiriwa anaruhusiwa kula chakula chochote.
And when a stranger sojourneth with thee, and will prepare the passover to the Lord, let his males be circumcised, and then let him come near and prepare it, and he shall be as one that is born in the land; but no uncircumcised person shall eat thereof.
49 Sheria hii hii itahusika kwa mzaliwa wa asili na mgeni anayeishi miongoni mwenu.”
One law shall be to him that is home-born, and unto the stranger that sojourneth among you.
50 Waisraeli wote walifanya kama Yahweh alivyo waamuru Musa na Aruni.
And all the children of Israel did so; as the Lord had commanded Moses and Aaron, so did they.
51 Ikaja kuwa siku hiyo Yahweh akawaleta Israeli kutoka nchi ya Misri kwa makundi yalio jiami.
And it came to pass on the selfsame day, that the Lord did bring forth the children of Israel out of the land of Egypt by their armies.

< Kutoka 12 >