< Kutoka 11 >

1 Kisha Yahweh akamwambia Musa, “Bado kuna pigo moja nitalo lileta kwa Farao na Misri. Baada ya hilo, atakuacha uondoke hapa. Atakapo kuachia uende, ata kuondoa kabisa.
Then Yahweh said to Moses, “There is still one more plague that I will bring on Pharaoh and Egypt. After that, he will let you go from here. When he finally lets you go, he will drive you away completely.
2 Waelekeze watu kwamba kila mwanaume na mwanamke amuulizie jirani yake vitu vya fedha na vitu vya dhahabu.”
Instruct the people that every man and woman is to ask of his or her neighbor for articles of silver and articles of gold.”
3 Sasa Yahweh aliwafanya Wamisri kuwa na shauku ya kuwapendeza Waisraeli. Aidha, Musa alikuwa wakuvutia sana machoni pa watumishi wa Farao na watu wa Misri.
Now Yahweh had made the Egyptians eager to please the Israelites. Moreover, the man Moses was very impressive in the sight of Pharaoh's servants and the people of Egypt.
4 Musa akasema, “Yahweh asema hivi: 'Wakati wa usiku wa manane nitaenda Misri yote.
Moses said, “Yahweh says this: 'About midnight I will go throughout Egypt.
5 Wazaliwa wa kwanza wote wa nchi ya Misri watakufa, kuanzia mzaliwa wa kwanza wa Farao, anaye keti kiti chake cha enzi, mpaka mzaliwa wa kwanza wa misichana mtumwa anaye saga mbegu, na kwa wazaliwa wa kwanza wa mifugo.
All the firstborn in the land of Egypt will die, from the firstborn of Pharaoh, who sits on his throne, to the firstborn of the slave girl who is behind the handmill grinding it, and to all the firstborn of the cattle.
6 Kisha kutakuwa na kilio kikubwa nchi yote ya Misri, kama ambacho hakijawai wala hakitatokea tena.
Then there will be a great wailing throughout all the land of Egypt, such as has never been nor ever will be again.
7 Lakini ata mbwa hata bweka kwa watu wa Israeli, dhidi ya mtu au mnyama. Kwa hili utajuwa kuwa nina watendea Wamisri na Waisraeli tofauti.'
But not even a dog will bark against any of the people of Israel, against either man or beast. In this way you will know that I am treating the Egyptians and the Israelites differently.'
8 Watumishi wote hawa wako, Farao, watakuja chini yangu na kunisujudu mimi. Watasema, 'Nenda, wewe na watu wote wanao kufuata!' Baada ya hapo nitaondoka.” Kisha akaondoka mbele ya Farao kwa hasira kubwa.
All these servants of yours, Pharaoh, will come down to me and bow down to me. They will say, 'Go, you and all the people who follow you!' After that I will go out.” Then he went out from Pharaoh in great anger.
9 Yahweh akamwambia Musa, Farao hatakusikiliza. Hii ni ili nifanye mambo ya ajabu katika nchi ya Misri.”
Yahweh said to Moses, “Pharaoh will not listen to you. This is so that I will do many amazing things in the land of Egypt.”
10 Musa na Aruni wakafanya mambo haya ya kushangaza mbele za Farao. Lakini Yahweh aliufanya moyo wa Farao mgumu, na Farao hakuwaacha watu wa Israeli kuondoka katika nchi yake.
Moses and Aaron did all these wonders before Pharaoh. But Yahweh hardened Pharaoh's heart, and Pharaoh did not let the people of Israel go out of his land.

< Kutoka 11 >