< Esta 6 >

1 Usiku ule mfalme hakupata usingizi. Akaagiza vitabu vya kumbukumbu vya matukio ya ufalme wake viletwe na visomwe mbele zake. Vitabu visomwa kwa sauti mbele ya mfalme.
On that night, the king couldn't sleep. He commanded the book of records of the chronicles to be brought, and they were read to the king.
2 Ikakutwa kuwa Modekai alikuwa ametoa taarifa kuhusu Bighana na Tereshi, walinzi walio linda lango, waliokuwa wamepanga kumuangamiza Mfalme Ahusiero.
It was found written that Mordecai had told of Bigthana and Teresh, two of the king's eunuchs, who were doorkeepers, who had tried to lay hands on the King Achashyerosh.
3 Kisha mfalme akauliza, Modekai alifanyiwa nini cha heshima kwa kwa taarifa aliyoitoa? Ndipo watumishi wa mfalme wakamwambia, “Hakufanyiwa kitu chochote.”
The king said, "What honor and dignity has been bestowed on Mordecai for this?" Then the king's servants who attended him said, "Nothing has been done for him."
4 Kisha mfalme akauliza, “Ni nani aliye ndani ya ua.” Na Hamani alikuwa ameingia katika ua wa mfalme ili amwombe mfalme atoe kibali ili Modekai atundikwe kwenye mti aliouandaa.
The king said, "Who is in the court?" Now Haman had come into the outer court of the king's house, to speak to the king about hanging Mordecai on the gallows that he had prepared for him.
5 Watumishi wakamjibu, “Hamani amesimama katika ua ya mfalme.” Mfalme akasema, “Mwambieni aingie ndani.”
The king's servants said to him, "Look, Haman stands in the court." The king said, "Let him come in."
6 Mara tu Hamani alipoingia, mfalme akamuuliza, afanyiewe nini mtu yule ambaye mfalme anampenda na kumheshimu?” Hamani akafikiri moyoni mwake, “Ni nani ambaye mfalme ampenda na kumuheshimu zaidi yangu?
So Haman came in. The king said to him, "What shall be done to the man whom the king delights to honor?" Now Haman said in his heart, "Who would the king delight to honor more than myself?"
7 Hamani amjibu mfame, Kwa mtu yule ambaye mfalme ampenda na kumuheshimu,
Haman said to the king, "For the man whom the king delights to honor,
8 avikwe nguo za kifalme, mavazi ambayo mfalme amekwisha yavaa na farasi ambaye ametumiwa na mfalme na ambaye ana taji ya kifalme kichwani mwake.
let royal clothing be brought which the king uses to wear, and the horse that the king rides on, and on the head of which a crown royal is set.
9 Nguo hizo na farasi apewe msimamizi bora kuliko wote. Na wamvike yule ambaye mfalme ampenda na kumuheshimu, na wampandishe juu ya farasi na kumpitisha katika mitaa yote ya mji. Na watangaze mbele yake, “Hivi ndivyo alivyofanyiwa mtu yule ambaye mfalme ampenda na kumuheshimu!”
And let the clothing and the horse be delivered to the hand of one of the king's most noble officials, and let him clothe the man whom the king delights to honor with them, and have him ride on horseback through the city square, and proclaim before him, 'Thus shall it be done to the man whom the king delights to honor.'"
10 Kisha mfalme akamwambia, Hamani “fanya hima, mvike Modekai nguo na umpandishe kwenye farasi, na lisipungue hata jambo moja katika hayo uliyo yasema.”
Then the king said to Haman, "Hurry and take the clothing and the horse, as you have said, and do this for Mordecai the Jew, who sits at the King's Gate. Let nothing fail of all that you have spoken."
11 Kisha Hamani akachukua mavazi na farasi. Akamvika Modekai na akampandisha kwenye farasi na kumpitisha katika mitaa yote ya mji. Akatangaza mbele zake, “Hii imefanyika kwa mtu ambaye mfalme anampenda na kumuheshimu!”
Then Haman took the clothing and the horse, and arrayed Mordecai, and had him ride through the city square, and proclaimed before him, "Thus shall it be done to the man whom the king delights to honor."
12 Baada ya hayo Modekai alirudi kwenye lango la mfalme. Huku Hamani akarudi kwa haraka nyumbani kwake, huku akiomboleza, na akiwa ameinamisha kichwa chake.
Mordecai came back to the King's Gate, but Haman hurried to his house, mourning and having his head covered.
13 Akawaeleza rafiki zake pamoja na Zereshi mkewe. Kisha rafiki zake wenye hekima pamoja na Zereshi mkewe. Kama Modekai, ambaye umeanza kuanguka mbele zake ni wa uzao wa Wayahudi, hautamshinda, bali utandelea kuanguka mbele zake.”
Haman recounted to Zeresh his wife and all his friends everything that had happened to him. Then his wise men and Zeresh his wife said to him, "If Mordecai, before whom you have begun to fall, is of Jewish descent, you will not prevail against him, but you will surely fall before him."
14 Walipokuwa wakiendelea na maongezi, wasimamizi wa mfalme wakamjia Hamani ili aende kwenye karamu aliyoiandaa Esta.
While they were yet talking with him, the king's eunuchs came, and hurried to bring Haman to the banquet that Esther had prepared.

< Esta 6 >