< Esta 4 >

1 Modeka aliposikia kilichokuwa kimepangwa dhidi yao, alirarua mavazi yake na kuvaa maguni na majivu. Akaenda katikati mwa mji na kulia kwa sauti na uchungu mwingi.
Now when Mordecai knew all that was done, Mordecai rent his clothes, and put on sackcloth with ashes, and went out into the midst of the city, and cried with a loud and a bitter cry;
2 Akaenda hadi langoni mwa mfalme; kwa sababu hakuna aliye ruhusiwa kuingia akiwa amevaa magunia.
and he came even before the king's gate; for none might enter within the king's gate clothed with sackcloth.
3 Amri hii ilipofika katika kila jimbo, kulikuwa na kilio kikubwa kwa Wayahudi, na kufunga, kulia na maombolezo. Wengi wao walilala katika magunia na majivu.
And in every province, whithersoever the king's commandment and his decree came, there was great mourning among the Jews, and fasting, and weeping, and wailing; and many lay in sackcloth and ashes.
4 Malkia Esta alipopata habari kutoka kwa wahudumu wake, alipatwa na majonzi. Akatuma watu wampelekee nguo Modekai ili avue magunia na kuvaa nguo nzuri, lakini Modekai hakukubali.
And Esther's maidens and her chamberlains came and told it her; and the queen was exceedingly pained; and she sent raiment to clothe Mordecai; and to take his sackcloth from off him; but he accepted it not.
5 kisha Esta akamwita Hathaki, mmoja wa wasimamizi wa mfalme, ambaye alikuwa amepewa wajibu wa kumuhudumia. Akamwagiza kwenda kwa Modekai ili afahamu kwa nini Modekai ameamua kufanya hivyo.
Then called Esther for Hathach, one of the king's chamberlains, whom he had appointed to attend upon her, and charged him to go to Mordecai, to know what this was, and why it was.
6 Hivyo Hathaki akaenda kwa Modekai katika mji mbele ya lango la mfalme.
So Hathach went forth to Mordecai unto the broad place of the city, which was before the king's gate.
7 Modekai akamweleza Hathaki mambo yote kuhusu maangamizi ya Wayahudi yaliyo pangwa na kiasi cha fedha ambacho Hamani ameahidi kuwapa wahazini wa mfalme, ili kuwaua Wayahudi.
And Mordecai told him of all that had happened unto him, and the exact sum of the money that Haman had promised to pay to the king's treasuries for the Jews, to destroy them.
8 Na kisha akampa nakala ya mbiu ambayo ilitolewa Shushani kwa uangamivu wa Wayahudi. Alifanya hiivyo ili kwamba Hathaki amwambie Esta achukue jukumu la kwenda na kumuomba mfalme na kumsihi kwa niaba ya Wayahudi.
Also he gave him the copy of the writing of the decree that was given out in Shushan to destroy them, to show it unto Esther, and to declare it unto her; and to charge her that she should go in unto the king, to make supplication unto him, and to make request before him, for her people.
9 Hivyo, Hathaki akaenda na kumweleza Esta kile alicho ambiwa na Modekai.
And Hathach came and told Esther the words of Mordecai.
10 Esta akaongea na Hathaki na akamwambia arudi kwa Modekai.
Then Esther spoke unto Hathach, and gave him a message unto Mordecai:
11 Esta akamwambia Hathaki, “Watumishi wote wa mfalme na watu wote katika majimbo yote wanafahamu kuwa mtu yeyote aingiae kwa mfalme bila kibali anapaswa kufa isipokuwa yule ambaye mfalme atamunyoshea fimbo yake ya dhahabu. Ni siku thelathini sasa sijaenda mbele ya mfalme.
'All the king's servants, and the people of the king's provinces, do know, that whosoever, whether man or woman, shall come unto the king into the inner court, who is not called, there is one law for him, that he be put to death, except such to whom the king shall hold out the golden sceptre, that he may live; but I have not been called to come in unto the king these thirty days.'
12 Hathaki akamwambia Modekai maneno aliyoambiwa na Esta.
And they told to Mordecai Esther's words.
13 Modekai akarudisha ujumbe: “usifikiri kwamba wewe utasalimika kuliko Wayahudi wote.
Then Mordecai bade them to return answer unto Esther: 'Think not with thyself that thou shalt escape in the king's house, more than all the Jews.
14 Kama ukikaa kimya kwa wakati huu, Mungu ataleta wokovu kwa njia nyingine, lakini wewe na nyumba ya baba yako mtaangamia. Ni nani ajuaye umekuja katika nafasi hii kwa wakati muafaka kama huu.
For if thou altogether holdest thy peace at this time, then will relief and deliverance arise to the Jews from another place, but thou and thy father's house will perish; and who knoweth whether thou art not come to royal estate for such a time as this?'
15 Kisha Esta akatuma ujumbe kwa Modekai,
Then Esther bade them return answer unto Mordecai:
16 “Nenda, uwakusanyea Wayahudi wote wanaoishi katika mji wa Shushani, na wafunge kwa ajili yangu. Wasile wala kunywa kwa muda wa siku tatu. Mimi na watumishi watumishi wangu wa kike tutafunga kwa siku hizo. Na kisha nitaenda mbele ya mfalme kinyume cha sheria. Na kama nitakufa na nife.
'Go, gather together all the Jews that are present in Shushan, and fast ye for me, and neither eat nor drink three days, night or day; I also and my maidens will fast in like manner; and so will I go in unto the king, which is not according to the law; and if I perish, I perish.'
17 Modekai akaenda na akafanya yote ambayo Esta aliyo mwagiza kufanya.
So Mordecai went his way, and did according to all that Esther had commanded him.

< Esta 4 >