< Esta 2 >

1 Baada ya mambo haya na baada ya hasira ya mfalme Ahusiero kutulia, alifikiri kuhusu Malkia Vashiti na alichokuwa amekifanya na tangazo alilokuwa ameamuru litolewe ya Vashiti kupoteza sifa za kuwa malkia.
After these things, when the anger of King Ahasuerus subsided, he thought about Vashti and what she had done. He also thought about the decree that he had made against her.
2 Kisha vijana waliomtumikia mfalme wakasema, mfalme atafutiwemabikira warembo.
Then the king's young men who served him said, “Let a search be made on the king's behalf for beautiful young virgins.
3 Mfalme na achague wasimamizi katika majimbo yote ya ufalme wake, ili wawakusanye mabikira warembo wote harem katika ikulu ya Susa. Mabikira hawa wawe chini ya usimamizi wa Hegai, msimamizi, ambaye ni mkuu wa wanawake, na wapewe vipodozi vyao vyote.
Let the king appoint officers in all the provinces of his kingdom, to gather together all the beautiful young virgins to the harem in the fortress in Susa. Let them be put under the care of Hegai, the king's official, who is in charge of the women, and let him give them their cosmetics.
4 Na binti yule atakaye mfurahisha mfalme ndiye atakaye kuwa Malkia badala ya Vashiti.” Mfalme alupenda ushauri na akafanya kama alivoshauriwa,
Let the young girl who pleases the king become queen in the place of Vashti.” This advice pleased the king, and he did so.
5 Katika mji wa Shushani alikuwepo Myahudi aliyeitwa Modekai mwana wa Jaira mwana wa Shimei mwana wa Kishi, aliye kuwa wa kabila la Benjamini.
There was a certain Jew in the fortress of Susa whose name was Mordecai son of Jair son of Shimei son of Kish, who was a Benjamite.
6 Yeye ni miongoni mwa Wayahudi waliochukuliwa pamoja na Yekonia, mfalme wa Yuda kutoka Yerusalemu na kupelekwa uhamishoni na mfalme Nebukadreza.
He had been taken away from Jerusalem with the exiles along with those taken with Jehoiachin, king of Judah, whom Nebuchadnezzar king of Babylonia carried away.
7 Modekai alikuwa akimlea, Hadasa, yaani Esta, binti wa mjomba wake kwa sababu hakuwa na wazaai wake wote wawili. Modekai alimchukuwa kama binti yake. Esta alikuwa na umbo zuri na uso wa kupendeza.
He was caring for Hadassah, that is, Esther, his uncle's daughter, because she had neither father nor mother. The young woman had a beautiful figure and was lovely in appearance. Mordecai took her as his own daughter.
8 Wasichana wengi waliletwa ikulu Shushani, baada ya tangazo na amri ya mfalme kutolewa. Waliwekwa chini ya usimamizi wa Hegai. Esta naye alikuwa ni miongoni mwa wasichana walioletwa na kuwekwa chini ya usimamizi wa Hegai, mwangalizi wa wanawake.
When the king's order and decree were proclaimed, many young women were brought to the fortress of Susa. They were put under Hegai's care. Esther also was taken into the king's palace and put under the care of Hegai, the overseer of the women.
9 Esta alimfurahisha, na akapata kibali mbele ya Hegai. Akampa vipodozi na sehemu ya chakula. Akampa wahudumu wa kike saba kutoka katika ikulu ya mfalme, na akampeleka na wahudumu wa kike katika sehemu bora katika nyumba ya wanawake.
The young girl pleased him, and she found favor with him. Immediately he provided her with cosmetics and her portion of food. He assigned to her seven servant girls from the king's palace, and he moved her and the servant girls to the best place in the house of the women.
10 Esta hakuwa amemweleza mtu yeyote kuhusu jamaa zake kwa sababu Modekai alikuwa amemzuia.
Esther had not told anyone who her people or relatives were, for Mordecai had instructed her not to tell.
11 kila siku Modekai alienda na kurudi mbele nje ya ua wa nyumba ya wanawake, ili kwamba asikie kuhusu mambo ya Esta na atakachofanyiwa.
Every day Mordecai walked back and forth in front of the courtyard outside the house of the women, to learn about Esther's welfare, and about what would be done with her.
12 Zamu ilipofika ya kila msichana kwenda kwa mfalme Ahusero kwa kufuata maelekezo kwa wanawake, kila msichana alitakiwa kumaliza miezi kumi na miwili ya urembo, miezi sita ya mafuta ya manemane na miezi sita ya vipodozi.
When the turn came for each girl to go to King Ahasuerus—complying with the regulations for the women, each girl had to complete twelve months of beauty treatments, six months with oil of myrrh, and six with perfumes and cosmetics—
13 wakati msichana alipoenda kwa mfalme, alipewa chochote alichotamani kutoka katika nyumba ya wanawake ili aende nacho katika nyuma ya mfalme.
when a young woman went to the king, whatever she desired was given to her from the house of the women, for her to take to the palace.
14 Msichana alipaswa kwenda wakati wa usiku na kurudi katika nyumba ya wanawake, na kwa msimamizi Shaashigazi, msimamizi wa mfalme, ambaye alikuwa mwenye kuwalinda masulia. Msichana hakuruhusiwa kwenda tena kwa mfalme isipokuwa amemfurahiha mfalme na mfalme akaamuru arudi tena.
In the evening she would go in, and in the morning she would return to the second house of the women, and to the custody of Shaashgaz, the king's official, who was in charge of the concubines. She would not return to the king again unless he had taken great pleasure in her and called for her again.
15 Zamu ya Esta ilipotimia( mwana wa Abihaili, mjomba wa Modekai alikuw amemchukua kama kama binti yake) kwenda mbele ya mfalme, hakutaka kitu chochote isipokuwa vile ambavyo Hegai, msimamizi wa wanawake alimtaka avichukue.
Now when the time came for Esther (daughter of Abihail, the uncle of Mordecai, who had taken her as his own daughter) to go in to the king, she did not ask for anything but what Hegai the king's official, who was in charge of the women, suggested. Now Esther received the favor of all who saw her.
16 Esta akapata kibali mbele ya kila aliyemwona. Esta akapelekwa kwa Mfalme Ahusiero katika makazi ya kifalme mwezi wa kumi, ambao ni mwezi wa Tabeti, katika mwaka wa saba wa utawala wake.
Esther was taken to King Ahasuerus into the royal residence on the tenth month, which is the month of Tebeth, in the seventh year of his reign.
17 Mfalme alimpenda Esta zaidi kuliko wanawake wengine, na alipata kibali kuliko na wema mbele zake zaidi kuliko mabikira wengine na hivyo mfalme akamvika taji ya kimalkia badala ya Vashiti.
The king loved Esther more than all the other women and she received acceptance and favor before him, more than all the other virgins. So he set the royal crown on her head and made her queen instead of Vashti.
18 mfalme akawafanyia karamu kubwa wasimamizi na wahudumu wake wote, karamu ya Esta na akawapa unafuu wa kodi katika majimbo. Pia akawapa zawadi kwa ukarimu.
The king gave a great feast for all his officials and his servants, “Esther's feast,” and he granted relief from taxation to the provinces. He also gave gifts with royal generosity.
19 Modekai alikuwa ameketi katika lango la mfalme wakati mabikira walipokuwa wamekusanyika kwa mara ya pili.
Now when the virgins had been gathered together a second time, Mordecai was sitting at the king's gate.
20 Esta alifuata ushauri Modekai ya kutomwambia mtu yeyote kuhusu jamaa zake. aliendelea kufuata ushauri wa Modekai kama alivyofanya alipokuwa mdogo.
Esther had not yet told anyone about her relatives or her people, as Mordecai had instructed her. She continued to follow Mordecai's advice, as she had done when she was raised by him.
21 katika siku hizo ambazo Modekai alikuwa ameketi getini kwa mfalme, Bighani na Tereshi, wasimamizi wa mfalme walio linda lando, walikasirika na wakatafuta kumuua mfalme Ahusiero.
In those days, while Mordecai was sitting at the king's gate, two of the king's officials, Bigthana and Teresh, who guarded the doorway, became angry and sought to do harm to King Ahasuerus.
22 Jambo lilipowekwa wazi kwa Modekai, alimtaarifu Malkia Esta na Esta akamweleza kile achoelezwa na Modekai.
When the matter was revealed to Mordecai, he told Queen Esther, and Esther spoke to the king in the name of Mordecai.
23 Habari hii ilipepelelezwa na kuonekana kuwa kweli na wanaume wawili walinyongwa juu ya mti. Na habari hii ikaandikwa katika kitabu cha taarifa mbele ya mfalme.
The report was investigated and confirmed, and both the men were hanged from a gallows. This account was written in the book of the chronicles in the presence of the king.

< Esta 2 >