< Waefeso 3 >

1 Kwa sababu ya hii mimi, Paulo, ni mfungwa wa Yesu Kristo kwa ajili yenu Mataifa.
For this cause, I Paul, the prisoner of Christ Jesus for you the nations,
2 Na amini ya kwamba mmesikia juu ya kazi ya neema ya Mungu aliyo nipa kwa ajili yenu.
if, indeed, you heard of the dispensation of the grace of God that was given to me in regard to you,
3 Nawaandikieni kutokana na jinsi ufunuo ulivyo funuliwa kwangu. Huu ni ukweli uliyofichika ambao niliandika kwa kifupi kwenye barua nyingine.
that by revelation He made known to me the secret, according as I wrote before in few [words]—
4 Usomapo kuhusu haya, utaweza kutambua busara yangu katika ukweli huu uliofichika kuhusu Kristo.
in regard to which you are able, reading [it], to understand my knowledge in the secret of the Christ,
5 Kwa vizazi vingine ukweli huu haukufanywa utambulike kwa wana wa watu. Ila kwa sasa umewekwa wazi kwa Roho kwa Mitume waliotengwa na Manabii.
which in other generations was not made known to the sons of men, as it was now revealed to His holy apostles and prophets in the Spirit—
6 Ukweli huu uliofichika ni kwamba watu wa Mataifa ni washiriki wenzetu na wajumbe wenzetu wa mwili. Niwashiriki pamoja na ahadi ya Kristo Yesu kupitia injili.
that the nations are fellow-heirs, and of the same body, and partakers of His promise in the Christ, through the good news,
7 Na kwa hili nimefanyika mtumishi kwa zawadi ya neema ya Mungu iliyotolewa kwangu kupitia utendaji wa nguvu yake.
of which I became a servant, according to the gift of the grace of God that was given to me, according to the working of His power;
8 Mungu alitoa zawadi hii kwangu, japo kuwa mimi ni mtu mdogo wa wote katika wale waliotengwa kwa ajili ya Mungu. Zawadi hii ni kwamba inanipasa kuwatangazia mataifa injili yenye utajiri usiochunguzika wa Kristo.
to me—the less than the least of all the holy ones—was given this grace, among the nations to proclaim good news—the untraceable riches of the Christ,
9 inanipasa kuwaangazia watu wote juu ya nini ni mpango wa Mungu wa siri. Huu ni mpango ambao ulikuwa umefichwa kwa miaka mingi iliyopita, na Mungu ambaye aliviumba vitu vyote. (aiōn g165)
and to cause all to see what [is] the fellowship of the secret that has been hid from the ages in God, who created all things by Jesus Christ, (aiōn g165)
10 Hii ilikuwa kwamba, kupitia Kanisa, watawala na mamlaka katika sehemu za mbingu wapate kujua pande nyingi za asili ya hekima ya Mungu.
that there might be made known now to the principalities and the authorities in the heavenly [places], through the Assembly, the manifold wisdom of God,
11 Haya yangetokea kupitia mpango wa milele ambao aliukamilisha ndani ya Kristo Yesu Bwana wetu. (aiōn g165)
according to a purpose of the ages, which He made in Christ Jesus our Lord, (aiōn g165)
12 Kwa kuwa katika Kristo tuna ujasiri na uwezo wa kuingia kwa ujasiri kwa sababu ya imani yetu kwake.
in whom we have the freedom and the access in confidence through the faith of Him,
13 Kwa hiyo nawaomba msikate tamaa kwasababu ya mateso yangu kwa ajili yenu. Haya ni utukufu wenu.
for this reason, I ask [you] not to faint in my tribulations for you, which is your glory.
14 Kwa sababu hii napiga magoti kwa Baba.
For this cause I bow my knees to the Father of our Lord Jesus Christ,
15 ambaye kwa yeye kila familia mbinguni na juu ya nchi imeitwa jina.
of whom the whole family in the heavens and on earth is named,
16 Ninaomba kwamba apate kuwanemesha, kutokana na utajiri wa utukufu wake, awafanye imara kwa nguvu kupitia Roho wake, ambaye yu ndani yenu.
that He may give to you, according to the riches of His glory, to be strengthened through His Spirit with might, in regard to the inner man,
17 Ninaomba kwamba Kristo aishi ndani ya mioyo yenu kupitia imani.
that the Christ may dwell through the faith in your hearts, having been rooted and founded in love,
18 Ninaomba kwamba muwe na shina na msingi wa upendo wake. Muwe katika pendo lake ili muweze kuelewa, pamoja na wote waaminio, jinsi upana, na urefu na kimo na kina cha upendo wa Kristo.
that you may be in strength to comprehend, with all the holy ones, what [is] the breadth, and length, and depth, and height,
19 Ninaomba Kwamba mjue ukuu wa upendo wa Kristo, ambao unazidi ufahamu. Mfanye haya ili mjazwe na ukamilifu wote wa Mungu.
to know also the love of the Christ that is exceeding the knowledge, that you may be filled—to all the fullness of God;
20 Na sasa kwake yeye awezaye kufanya kila jambo, zaidi ya yote tuyaombayo au tuyawazayo, kupitia nguvu yake itendayo kazi ndani yetu,
and to Him who is able to do exceedingly [and] abundantly above all things that we ask or think, according to the power that is working in us,
21 kwake yeye kuwe utukufu ndani ya kanisa na katika Kristo Yesu kwa vizazi vyote milele na milele. Amina. (aiōn g165)
to Him [is] the glory in the Assembly in Christ Jesus, to all the generations of the age of the ages. Amen. (aiōn g165)

< Waefeso 3 >