< Mhubiri 8 >

1 Ni mtu gani mwenye hekima? Ambaye anafahamu matukio yana maana gani katika maisha? Hekima ndani ya mtu husababisha uso wake kung'ara, na ugumu wa uso wake hubadilika.
Who is a wise man? Who knows what the events in life mean? Wisdom in a man causes his face to shine, and the hardness of his face is changed.
2 Ninakushauri kuitii amri ya mfalme kwa sababu ya kiapo cha Mungu cha kumlinda yeye.
I advise you to obey the king's command because of God's oath to protect him.
3 Usiharakishe kuondoka mbele ya uwepo wake, na usisimame kuunga mkono jambo lisilofaa, kwa kuwa mfalme anafanya chochote anacho tamani.
Do not hurry out of his presence, and do not stand in support of something wrong, for the king does whatever he desires.
4 Neno la mfalme hutawala, kwa hiyo ni nani atakaye mwambia, 'Unafanya nini?
The king's word rules, so who will say to him, “What are you doing?”
5 Yeyote ashikaye amri za mfalme hukwepa madhara. Moyo wa mwenye hekima hutambua mwelekeo muafaka na muda wa kuenda.
Whoever keeps the king's commands avoids harm. A wise man's heart recognizes the proper course and time of action.
6 Kwa kuwa kila jambo lina jibu sahihi, na wakati wa kujibu, kwa sababu taabu ya mtu ni kubwa.
For every matter there is a correct response and a time to respond, because the troubles of man are great.
7 Hakuna anaye fahamu kinacho fuata. Ni nani awezaye kumwambia nini kinacho kuja?
No one knows what is coming next. Who can tell him what is coming?
8 Hakuna mwenye uwezo juu ya roho aizuie roho; wala hana mamlaka juu ya siku ya kufa; wala hakuna kuruhusiwa katika vita vile; wala uovu hautamwokoa yule aliyeuzoea.
No one is ruler over his breath so as to stop the breath, and no one has power over the day of his death. No one is discharged from the army during a battle, and wickedness will not rescue those who are its slaves.
9 Mambo hayo yote nimeyaona, nikatia moyo wangu katika kila kazi iliyofanyika chini ya jua. Kuna wakati ambapo mtu mmoja anayo mamlaka juu ya mwenziwe kwa hasira yake.
I have realized all this; I have applied my heart to every kind of work that is done under the sun. There is a time when a person oppresses another person to that person's hurt.
10 Hivyo niliwaona wabaya wakizikwa hadharani. Waliondolewa mahali patakatifu na kuzikwa mahali waliposifiwa na watu katika mji walipokuwa wamefanya matendo maovu. Hii nayo haifai.
So I saw the wicked buried publicly. They were taken from the holy area and buried and were praised by people in the city where they had done their wicked deeds. This also is uselessness.
11 Wakati hukumu dhidi ya tendo ovu haihukumiwi haraka, hushawishi mioyo ya wanadamu kutenda ubaya.
When a sentence against an evil crime is not executed quickly, it entices the hearts of human beings to do evil.
12 Hata kama mwenye dhambi afanye uovu mara mia moja na bado aishi kwa muda mrefu, bado ninafahamu itakuwa vyema kwa wale wanao muheshimu Mungu, wanaouheshimu uwepo wake walio nao.
Even though a sinner does evil a hundred times and still lives a long time, yet I know that it will be better for those who respect God, for those who stand before him and show him respect.
13 Lakini haitakuwa vyema kwa mtu mwovu; mkewe hatacheleweshwa. Siku zake kama kizuri kitowekacho upesi, kwa sababu hamuheshimu Mungu.
But it will not go well for a wicked man; his life will not be prolonged. His days are like a fleeting shadow because he does not honor God.
14 Kuna mvuke mwingine usio faa, jambo jingine linaofanyika juu ya dunia. Mambo hutokea kwa watu wenye haki kama yatokeavyo kwa watu waovu, na mambo hutokea kwa wenye haki kama yatokeavyo kwa waovu. Ninasema hili pia ni mvuke usiofaa.
There is another useless vapor—something else that is done on the earth. Things happen to righteous people as they happen to wicked people, and things happen to wicked people as they happen to righteous people. I say that this also is useless vapor.
15 Kwa hiyo nikapendekeza furaha, kwa sababu mtu hana jambo bora chini ya jua zaidi ya kula na kunywa na kuwa na furaha. furaha ndiyo itamfuata katika kazi zake kwa siku zote za maisha yake ambayo Mungu amempa chini ya jua.
So I recommend happiness, because a man has no better thing under the sun than to eat and drink and to be happy. It is happiness that will accompany him in his labor for all the days of his life that God has given him under the sun.
16 Nikauweka moyo wangu kufamu hekima na kufahamu kazi inayofanyika juu ya nchi, kazi ambayo inafanyika mara nyingi pasipo kufumba macho usiku au mchana.
When I applied my heart to know wisdom and to understand the work that is done on the earth, work often done without sleep for the eyes at night or in the day,
17 Kisha nika tafakari matendo yote ya Mungu, na kwamba mtu hawezi kuelewa kazi inayofanyika chini ya jua. Bila kujali mtu anafanya kupata majibu, hatayapata. Ingawa mwenye hekima anaweza kuamini anajua, kitu kweli hajui.
then I considered all of God's deeds, and that man cannot understand the work that is done under the sun. No matter how much a man labors to find the answers, he will not find them. Even though a wise man might believe he knows, he really does not.

< Mhubiri 8 >