< Torati 7 >

1 Wakati Yahwe Mungu wenu atuleta katika nchi ambayo mnaenda kuimiliki na kuwaondoa mataifa mengi mbele zenu- Mhiti, Mgirgashi na Mwamori, na Mkanaani, na Mperizi, Mhivi, Myebusi- mataifa saba makubwa na yenye nguvu kuliko wewe.
When the LORD thy God shall bring thee into the land whither thou goest to possess it, and shall cast out many nations before thee, the Hittite, and the Girgashite, and the Amorite, and the Canaanite, and the Perizzite, and the Hivite, and the Jebusite, seven nations greater and mightier than thou;
2 Na wakati Yahwe Mungu wenu awapa ninyi ushindi juu yao pindi mnakutana nao katika vita, mtawashambulia, basi mnapaswa kuwateketeza kabisa. Hamtafanya agano nao, wala kuonesha huruma kwao.
and when the LORD thy God shall deliver them up before thee, and thou shalt smite them; then thou shalt utterly destroy them; thou shalt make no covenant with them, nor show mercy unto them;
3 Wala hamtapanga ndoa zozote pamoja nao, hamtawatoa binti zenu kwa vijana wao, na hamtawachukua binti zao kwa vijana wenu.
neither shalt thou make marriages with them: thy daughter thou shalt not give unto his son, nor his daughter shalt thou take unto thy son.
4 Kwa kuwa watawabadilisha vijana wenu kutonifuata mimi, ili kwamba waweze kuabudu miungu yao. Kwa hiyo hasira ya Yahwe itawashwa dhidi yenu na atawaangamiza haraka.
For he will turn away thy son from following Me, that they may serve other gods; so will the anger of the LORD be kindled against you, and He will destroy thee quickly.
5 Hivi ndivyo mtakavyo washughulikia nao; mtavunja madhabahu zao, vunja nguzo zao za mawe katika vipande, kata chini ncha za Asherahi, na kuzichoma sanamu za kutupwa.
But thus shall ye deal with them: ye shall break down their altars, and dash in pieces their pillars, and hew down their Asherim, and burn their graven images with fire.
6 Kwa kuwa wewe ni taifa uliyetengwa kwa Yahwe Mungu wako. Amekuchagua wewe kuwa watu kwa ajili yake kumiliki, zaidi ya watu wengine wote ambao wako katika uso wa dunia.
For thou art a holy people unto the LORD thy God: the LORD thy God hath chosen thee to be His own treasure, out of all peoples that are upon the face of the earth.
7 Yahwe hakuweka upendo wake juu yenu au kuwachagua kwa sababu mlikuwa zaidi katika idadi kuliko watu wowote, kwa kuwa mlikuwa wachache kuliko watu wote-
The LORD did not set His love upon you, nor choose you, because ye were more in number than any people — for ye were the fewest of all peoples —
8 Lakini kwa sababu anawapenda ninyi, anataka kushika kiapo alichoapa kwa baba zenu. Huyu ni Yahwe aliyewatoa kwa mkono wa uweza na kuwakomboa kutoka nyumba ya utumwa, kutoka mkono wa Farao, mfalme wa Misri.
but because the LORD loved you, and because He would keep the oath which He swore unto your fathers, hath the LORD brought you out with a mighty hand, and redeemed you out of the house of bondage, from the hand of Pharaoh king of Egypt.
9 Kwa hiyo tambua ya kuwa Yahwe Mungu wako-ni Mungu, Mungu mwaminifu, anayetunza maagano na uaminifu kwa vizazi elfu kwa wale wanaompenda na kuyashika maagizo yake,
Know therefore that the LORD thy God, He is God; the faithful God, who keepeth covenant and mercy with them that love Him and keep His commandments to a thousand generations;
10 lakini huwalipa wale wanaomchukia kwa sura zao, kuwaangamiza, hatakuwa na huruma kwa yeyote anayemchukia; atamlipa kwa uso wake.
and repayeth them that hate Him to their face, to destroy them; He will not be slack to him that hateth Him, He will repay him to his face.
11 Kwa hiyo utashika maagizo, amri, na sheria ninazokuamuru leo, ili kwamba uzifanye.
Thou shalt therefore keep the commandment, and the statutes, and the ordinances, which I command thee this day, to do them.
12 Kama mtasikiliza maagizo haya, kuyashika na kuyafanya, itakuwa Yahwe Mungu wenu atawashika pamoja na agano na uaminifu ambao aliapa kwa baba zenu.
And it shall come to pass, because ye hearken to these ordinances, and keep, and do them, that the LORD thy God shall keep with thee the covenant and the mercy which He swore unto thy fathers,
13 Atawapenda, atawabariki, na kuwazidisha, pia atabariki tunda la miili yenu na tunda la ardhi yenu, nafaka zenu, divai mpya, mafuta yenu, atazidisha mifugo na kundi lako la mifugo michanga, katika nchi ambayo aliapa kwa baba zenu kuwapa.
and He will love thee, and bless thee, and multiply thee; He will also bless the fruit of thy body and the fruit of thy land, thy corn and thy wine and thine oil, the increase of thy kine and the young of thy flock, in the land which He swore unto thy fathers to give thee.
14 Mtabarikiwa zaidi kuliko watu wengine wote; hapatakuwa na mwanaume asiyekuwa na mtoto au mwanamke tasa miongoni mwenu au miongoni mwa mifugo.
Thou shalt be blessed above all peoples; there shall not be male or female barren among you, or among your cattle.
15 Yahwe atawaondolea magonjwa yote; hakuna magonjwa mabaya ya Misri ambayo mnayajua yatawekwa juu yenu, Lakini atayaweka kwa wote wanaowachukia ninyi.
And the LORD will take away from thee all sickness; and He will put none of the evil diseases of Egypt, which thou knowest, upon thee, but will lay them upon all them that hate thee.
16 Mtayaondoa makundi ya watu wote ambayo Yahwe Mungu wenu awapa ushindi, na jicho lenu halitawaonea huruma. Na hamtaabudu miungu yao, kwa kuwa huo utakuwa mtego kwenu.
And thou shalt consume all the peoples that the LORD thy God shall deliver unto thee; thine eye shall not pity them; neither shalt thou serve their gods; for that will be a snare unto thee.
17 Kama mtasema kwenye mioyo, Haya mataifa ni mengi zaidi kuliko mimi; nitawezaje kuwafukuza?
If thou shalt say in thy heart: 'These nations are more than I; how can I dispossess them?'
18 Usiwaogope; utakumbuka akilini Yahwe nini Mungu wenu alifanya kwa Farao na Misri yote?
thou shalt not be afraid of them; thou shalt well remember what the LORD thy God did unto Pharaoh, and unto all Egypt:
19 Mateso makuu ambayo macho yenu yaliona, ishara, maajabu, mkono wa uweza, mkono ulionyoshwa ambao Yahwe Mungu wenu alivyowatoa. Yahwe Mungu wenu atafanya kile kile kwa watu wote ambao mnawaogopa.
the great trials which thine eyes saw, and the signs, and the wonders, and the mighty hand, and the outstretched arm, whereby the LORD thy God brought thee out; so shall the LORD thy God do unto all the peoples of whom thou art afraid.
20 Zaidi ya yote, Yahwe Mungu wenu atatuma nyigu miongoni mwao, mpaka wale waliobaki na wale wanaojificha wenyewe mbele yenu waangamizwa mbele ya uwepo wenu.
Moreover the LORD thy God will send the hornet among them, until they that are left, and they that hide themselves, perish from before thee.
21 Hamtatishikeni nao, kwa kuwa Yahwe Mungu wenu yuko miongoni mwenu, Mungu mkuu na wa kuogofya.
Thou shalt not be affrighted at them; for the LORD thy God is in the midst of thee, a God great and awful.
22 Yahwe Mungu wenu atayaondoa mataifa mbele zenu kidogo kidogo. Hamtayashinda yote kwa wakati mmoja, au wanyama wa mwitu watakuwa wengi karibu yenu.
And the LORD thy God will cast out those nations before thee by little and little; thou mayest not consume them quickly, lest the beasts of the field increase upon thee.
23 Lakini Yahwe Mungu wenu atawapa ninyi ushindi dhidi yao wakati mkutanapo vitani; atawachanganya kwa kiasi kikubwa mpaka wameangamizwa.
But the LORD thy God shall deliver them up before thee, and shall discomfit them with a great discomfiture, until they be destroyed.
24 Atawaweka wafalme wao chini ya utawala wenu, na mtafanya jina lao kuangamia toka chini ya mbingu. Hakuna atakayeweza kusimama mbele yenu, mpaka muwaangamize.
And He shall deliver their kings into thy hand, and thou shalt make their name to perish from under heaven; there shall no man be able to stand against thee, until thou have destroyed them.
25 Utazichoma sanamu za kuchonga za miungu yao- usitamani madini ya fedha au dhahabu yanayofunika na kuichukua kwa ajili yenu, kwa sababu mkifanya, mtanaswa nayo-kwa kuwa ni chukizo kwa Yahwe Mungu wenu.
The graven images of their gods shall ye burn with fire; thou shalt not covet the silver or the gold that is on them, nor take it unto thee, lest thou be snared therein; for it is an abomination to the LORD thy God.
26 Hamtaleta chukizo lolote ndani ya nyumba zenu na kuanza kuiabudu. Mtachukizwa kabisa na kuchukia kwa kuwa imetengwa kwa ajili ya uharibifu.
And thou shalt not bring an abomination into thy house, and be accursed like unto it; thou shalt utterly detest it, and thou shalt utterly abhor it; for it is a devoted thing.

< Torati 7 >