< Torati 5 >

1 Musa aliwaita Israeli yote na akasema nao, “Sikiliza, Israeli, kwa amri na sheria ambazo nitasema katika masikio yenu leo, muweze kujifunza na kuzishika.
Moses called to all Israel and said to them, “Listen, Israel, to the statutes and the decrees that I will speak in your ears today, that you may learn them and keep them.
2 Yahwe Mungu wetu alifanya agano nasi huko Horeb.
Yahweh our God made a covenant with us at Horeb.
3 Yahwe hakufanya agano hili pamoja na mababu zetu, lakini na sisi, sisi wote tu hai hapa leo.
Yahweh did not make this covenant with our ancestors, but with us, all of us alive here today.
4 Yahwe alizungumza nawe uso kwa uso kwenye mlima toka katikati mwa moto
Yahweh spoke with you face to face on the mount out of the middle of the fire
5 (Nilisimama kati ya Yahwe na wewe kwa wakati huo, kukufunulia wewe neno lake, kwa kuwa ulikuwa umeogopa kwa sababu ya moto, na haukwenda juu ya mlima), Yahwe alisema,
(I stood between Yahweh and you at that time, to reveal to you his word; for you were afraid because of the fire, and you did not go up the mountain). Yahweh said,
6 'Mimi ni Yahweh Mungu wako, niliyekutoa katika nchi ya Misri, kutoka nyumba ya utumwa.
'I am Yahweh your God, who brought you out of the land of Egypt, out of the house of slavery.
7 Hautakuwa na miungu mingine mbele yangu.
You will have no other gods before me.
8 Hautajifanyia mwenyewe sanamu ya kuchonga wala mfano wa kitu chochote kilicho juu mbinguni, au kilicho chini ya dunia, au kilicho chini ya maji.
You will not make for yourself a carved figure nor any likeness of anything that is in heaven above, or that is in the earth beneath, or that is in the water below.
9 Hautavisujudia au kuvitumikia, kwa kuwa Mimi, Yahwe Mungu wako, ni Mungu wa wivu, Nawaadhibu uovu wa mababu kwa kuleta adhabu juu ya watoto, kwa kizazi cha tatu na cha nne cha wale wanichukiao,
You will not bow down to them or serve them, for I, Yahweh your God, am a jealous God. I punish the ancestors' wickedness by bringing punishment on the children, to the third and fourth generation of those who hate me,
10 na kuonesha agano la uaminifu kwa maelfu, kwa wale wanaonipenda na kushika amri zangu.
and showing covenant faithfulness to thousands, to those who love me and keep my commandments.
11 Hautalichukua jina la Yahwe Mungu wako bure, kwa kuwa Yahwe hatamshikilia kuwa ana hatia yeye alichukuae jina bure.
You will not take the name of Yahweh your God in vain, for Yahweh will not hold him guiltless that takes his name in vain.
12 Zingantia siku ya Sabato kwa kuiweka takatifu, kama Yahwe Mungu wako alivyokuamuru.
Observe the Sabbath day to keep it holy, as Yahweh your God commanded you.
13 Kwa siku sita utafanya kazi na fanya kazi zako zote,
For six days you will labor and do all your work;
14 lakini siku ya saba ni Sabato kwa Yahwe Mungu wako. Kwa siku hiyo hautafanya kazi yoyote- si wewe, wala mwana wako, wala binti yako, wala mjakazi wako wa kiume, wala maksai wako, wala punda wako, wala mifugo wako, wala mgeni yeyote aliye katika malango yako. Hii ni kwamba mjakazi wako wa kiume na mjakazi wako wa kike wapate kumpuzika pamoja na wewe.
but the seventh day is a Sabbath to Yahweh your God. On it you will not do any work—not you, nor your son, nor your daughter, nor your male servant, nor your female servant, nor your ox, nor your donkey, nor any of your cattle, nor any foreigner who is within your gates. This is so that your male servant and your female servant may rest as well as you.
15 Utakumbuka katika akili yako kwamba ulikuo mtumwa katika nchi ya Misri, na Yahwe Mungu wako alikutoa kutoka huko kwa mkono wa uweza na mkono ulionyoshwa. Kwa hiyo Yahwe Mungu wako amekuamuru kuitunza siku ya Sabato.
You will call to mind that you were a servant in the land of Egypt, and Yahweh your God brought you out from there by a mighty hand and by an outstretched arm. Therefore Yahweh your God has commanded you to keep the Sabbath day.
16 Mheshimu baba yako na mama yako, kama Yahwe Mungu wako alivyokuamuru kufanya, ili kwamba uweze kuishi muda mrefu katika nchi ambayo Yahwe Mungu wako akupa, ili kwamba iende kwa uzuri kwako.
Honor your father and your mother, as Yahweh your God has commanded you to do, that you may live a long time in the land that Yahweh your God gives you, and so that it may go well with you.
17 Hautaua,
You will not murder.
18 hautazini,
You will not commit adultery.
19 hautaiba,
You will not steal.
20 hautashuhudia uongo dhidi ya ndugu yako.
You will not give false witness against your neighbor.
21 Hautamtamani mke wa jirani yako, hautatamani nyumba ya jirani yako, shamba lake, au mjakazi wake wa kiume, au mjakazi wake wa kike, maksai au punda wako, au chochote ambacho ni mali ya jirani yako.
You will not covet your neighbor's wife, you will not covet your neighbor's house, his field, or his male servant, or his female servant, his ox, or his donkey, or anything that belongs to your neighbor.'
22 Haya maneno Yahwe alisema kwa sauti kubwa kwa kusanyiko lako lote kwenye mlima toka katikati mwa moto, mawingu, giza zito, hakuongeza maneno yoyote zaidi. Na aliandika chini kwenye mbao mbili za mawe na akanipa mimi.
These words Yahweh spoke in a loud voice to all your assembly on the mountain out of the middle of the fire, of the cloud, and of the thick darkness; he did not add any more words. He wrote them down on two tablets of stone and gave them to me.
23 Ilipokaribia, pindi uliposikia sauti toka katikati mwa giza, wakati mlima unawaka moto, kuwa mlikuja karibu nami, wazee wako wote, na wakuu wa makibila yako.
It came about, when you heard the voice out of the middle of the darkness, while the mountain was burning, that you came near to me—all your elders and the heads of your tribes.
24 Ulisema, Tazama, Yahwe Mungu wetu ametuonesha utukufu wake na ukuu wake, na tumeisikia sauti yake toka katikati mwa moto, tumeona leo kwamba wakati Mungu azungumza na watu, wanaweza kuishi.
You said, 'Look, Yahweh our God has shown us his glory and his greatness, and we have heard his voice out of the middle of the fire; we have seen today that when God speaks with people, they can live.
25 Lakini kwanini tufe? Kwa kuwa mto huu mkuu utatutoshereza sisi; kama tutasikia sauti ya Yahwe Mungu wetu tena, tutakufa.
But why should we die? For this great fire will consume us; if we hear the voice of Yahweh our God any longer, we will die.
26 Kwa kuwa badala yetu kuna miongoni mwetu wa mwili ambao wamesikia sauti ya Mungu aliye hai akizungumza toka katikati mwa moto na kuishi, kama tulivyofanya?
For who besides us is there among all flesh who has heard the voice of the living God speak out of the middle of the fire and lived, as we have done?
27 Kwenu ninyi, mnapaswa kwenda na kusikiliza kila kitu ambacho Yahwe Mungu wetu asema; rudia kwetu kila kitu ambacho Yahwe Mungu wetu asema kwenu; tutamsikiliza na kumtii.'
As for you, you should go and listen to everything that Yahweh our God says; repeat to us everything that Yahweh our God says to you; we will listen to it and obey it.'
28 Yahweh alisikia maneno yenu pindi mlipozungumza nami. Alisema na mimi, “Nimekwisha sikia maneno ya watu hawa, kile wanasema kwako. Kile walichosema kilikuwa kizuri.
Yahweh heard your words when you spoke to me. He said to me, 'I have heard the words of this people, what they said to you. What they said was good.
29 Oh, kulikuwa na moyo wa namba hiyo ndani yao, kwamba wataniheshimu na daima kushika amri zangu zote, ili iweze kuwa vizuri kwao na pamoja na watoto wao milele!
Oh, that there were such a heart in them, that they would honor me and always keep all my commandments, that it might go well with them and with their children forever!
30 Nenda useme nao, “Rudini kwenye mahema.”
Go say to them, “Return to your tents.”
31 Lakini kwenu, simama karibu nami, na nitakuambia amri zote, sheria, na maagizo ambayo mtawafundisha, ili kwamba waweze kuyashika katika nchi ambayo nitawapa kumiliki.'
But as for you, stand here by me, and I will tell you all the commandments, the statutes, and the decrees that you will teach them, so that they may keep them in the land that I will give them to possess.'
32 Utashika, kwa hiyo, kile Yahwe Mungu wenu amewaamuru; hamtageukia mkono wa kulia au kushoto.
You will keep, therefore, what Yahweh your God has commanded you; you will not turn aside to the right hand or to the left.
33 Mtatembea katika njia zote ambazo Yahwe Mungu wenu, amewaamuru ili kusudi muweze kuishi, na ili kwamba iweze kwenda vizuri kwenu, na kwamba muweze kuongeza siku zenu katika nchi ambayo mtaimiliki.
You will walk in all the ways that Yahweh your God has commanded you, so that you may live, and so that it may go well with you, and that you may prolong your days in the land that you will possess.

< Torati 5 >