< Torati 4 >

1 Sasa, Israeli, sikiliza sheria na amri ambayo niko karibu kukufundisha, kuzifanya, ili kwamba uweze kuishi na kuingia ndani na kumiliki nchi ambayo Yahwe, Mungu wa baba zako, anakupa.
And now O Israel listen to the statutes and to the judgments which I [am] about to teach you to observe so that you may live and you will go and you will take possession of the land which Yahweh [the] God of ancestors your [is] about to give to you.
2 Hautaongeza maneno ambayo nakuamuru, wala hautayapunguza, ili kwamba uweze kushika amri ya Yahwe Mungu wako ambazo naenda kukuamuru.
Not you must add to the word which I [am] about to command you and not you must diminish from it to keep [the] commandments of Yahweh God your which I [am] about to command you.
3 Macho yako yamekwisha ona nini Yahwe alifanya kwa sababu ya Baal Peor, kwa kuwa watu wote waliomfuata Baali Peor, Yahwe Mungu wenu amekwisha kuwaangamiza kutoka miongoni mwenu.
Own eyes your [are] the [ones which] saw [that] which he did Yahweh at Baal Peor for every person who he walked after Baal Peor he destroyed him Yahweh God your from midst your.
4 Lakini walioambatana na Yahwe Mungu wenu wako hai leo, kila moja wenu.
And you who were clinging on Yahweh God your [are] alive all of you this day.
5 Tazama, nimewafundisha sheria na amri, kama Yahwe Mungu wangu alivyoniamuru mimi, ila kwamba mfanye hivyo katikati mwa nchi ambayo mnaiendea ili kusudi muimiliki.
See - I have taught you statutes and judgments just as he commanded me Yahweh God my to do thus in [the] midst of the land where you [are] about to go there towards to take possession of it.
6 Kwa hiyo washikilieni na kuwafanya, kwa kuwa hii ni hekima yenu na uelewa wenu mbele ya macho ya watu watakaosikia amri hizi zote na kusema, “Hakika taifa hili kubwa lina watu wa hekima na uelewa.'
And you will take care and you will observe [them] for that [will be] wisdom your and understanding your to [the] eyes of the peoples which they will hear! all the statutes these and they will say certainly [is] a people wise and understanding the nation great this.
7 Kuna taifa gani jingine la vile liko hapo lina mungu karibu nao, kama Yahwe Mungu wetu tunapomwita wakati wowote?
For who? [is] a nation great which [belongs] to it a god near to it like Yahweh God our in all calling we to him.
8 Kuna taifa kubwa gani jingine liko hapo ambalo lina sheria na amri ili kwamba haki pamoja na sheria ambayo ninaweka mbele yenu leo?
And who? [is] a nation great which [belongs] to it statutes and judgments righteous like all the law this which I [am] setting before you this day.
9 Zingatia peke na kuwa makini kujilinda, ili usisahau mambo ambayo macho yako yameona, ili kwamba yasiuwache moyo wako kwa siku zote za maisha yako. Badala yake, yafanye yajulikane kwa watoto wako na wana watoto wako.
Only take heed to yourself and guard self your exceedingly lest you should forget the things which they have seen eyes your and lest they should depart from heart your all [the] days of life your and you will make known them to children your and to [the] children of children your.
10 Kuhusu siku ile uliyosimama mbele ya Yahwe Mungu wako katika Horeb, wakati Yahwe alisema nami, 'Nikusanyie watu, na nitawafanya wasikia maneno yangu, ili kwamba waweze kujifunza kuniogopa mimi siku zote ambazo wanazoishi duniani, na kwamba waweze kuwafundisha watoto wao.
[the] day When you stood before Yahweh God your at Horeb when said Yahweh to me assemble to me the people so I may make hear them words my that they will learn! to fear me all the days which they [will be] alive on the land and children their they will teach!
11 Mlikuja karibu na kusimama katika wayo wa mlima. Mlima uliwaka moto kwenye moyo wa mbinguni, pamoja na giza, mawingu na giza jembamba.
And you drew near! and you stood! under the mountain and the mountain [was] burning with fire to [the] heart of the heavens darkness cloud and thick darkness.
12 Yahwe alizungumza katikati ya moto, ulisikia suati pamoja na maneno yake, lakini hakuona umbo, ila ulisikia sauti peke.
And he spoke Yahweh to you from [the] middle of the fire a sound of words you [were] hearing and a form not you [were] seeing except a voice.
13 Alitangaza kwenu agano lake ambalo aliwaamuru ninyi kulifanya, amri kumi. Aliziandika kwenye vibao viwili vya mawe.
And he declared to you covenant his which he commanded you to observe [the] ten the words and he inscribed them on two tablets of stone.
14 Yahwe aliniamuru mimi kwa wakati huo kuwafundisha sheria na amri, ili kwamba muweze kuzifanya katika nchi mnaoivuka kwenda kuimiliki.
And me he commanded Yahweh at the time that to teach you statutes and judgments to observe you them in the land where you [are] about to pass over there towards to take possession of it.
15 Basi iweni waangalifu ninyi wenyewe - kwa kuwa mliona hakuna namna ya umbo siku hiyo ambapo Yahweh alizungumza nanyi huko Horeb kutoka katikati mwa moto,
And you will take heed exceedingly to selves your for not you saw any form on [the] day [when] he spoke Yahweh to you at Horeb from [the] middle of the fire.
16 ili kwamba usiharibike na kuchonga umbo katika sura ya kiumbe chochote, umbo la mwanaume au mtu wa kike,
Lest you should act corruptly! and you will make for yourselves an image of a form of any figure a likeness of a male or a female.
17 au sura ya mnyama aliye katika nchi, au sura ya ndege yoyote wa mabawa arukae katika anga, au
A likeness of any animal which [is] on the earth a likeness of any bird of wing which it flies in the heavens.
18 sura ya kitu chochote kitambaacho katika ardhi, au sura ya samaki yoyote katika maji chini ya ardhi.
A likeness of any creeping [thing] on the ground a likeness of any fish which [is] in the waters from under to the earth.
19 Hautainua macho yako juu mbinguni na kutazama jua, mwezi, au nyota - jeshi lote la mbinguni- ukusogezwa na kuviabudu na kuvisujudia- vile vyote ambavyo Yahwe Mungu wenu amewapa hisa watu wote walio chini ya anga lote.
And lest you should lift up eyes your the heavens towards and you will see the sun and the moon and the stars all [the] host of the heavens and you will be drawn aside and you will bow down to them and you will serve them which he has assigned Yahweh God your them to all the peoples under all the heavens.
20 Lakini Yahwe amewatoa ninyi na kuwaleta nje ya tanuru la chuma, nje ya Misri, kuwa kwake watu wa urithi wake, kama mlivyo leo.
And you he took Yahweh and he brought out you from [the] furnace of iron from Egypt to become for him a people of inheritance as the day this.
21 Yahwe alinikasirikia mimi kwa sababu yenu; aliapa kwamba nisiende ng'ambo ya Yordani, na kwamba nisiende kwenye nchi nzuri, nchi ambayo Yahwe Mungu wenu anawapa ninyi kama urithi.
And Yahweh he was angry with me on words your and he swore to not to pass over I the Jordan and to not to go into the land good which Yahweh God your [is] about to give to you an inheritance.
22 Badala yake, ninapaswa kufa katika nchi hii, sipaswi kwenda ng'ambo ya Yordani, lakini mtaenda ng'ambo na kuimiliki nchi nzuri
For I [am] about to die in the land this not I [am] about to pass over the Jordan and you [are] about to pass over and you will take possession of the land good this.
23 Zingatia ninyi wenyewe, ili kwamba msisahau agano la Yahwe Mungu wenu, alilolifanya pamoja nanyi, na kujichongea mfano wa sanamu katika uombo la kitu chochote ambacho Yahwe Mungu wenu amewakataza kufanya.
Take heed to yourselves lest you should forget [the] covenant of Yahweh God your which he has made with you and you will make for yourselves an image a form of anything which he commanded you Yahweh God your.
24 Kwa kuwa Yahwe Mungu wenu ni moto ulao, Mungu wa wivu.
For Yahweh God your [is] a fire consuming he a God jealous.
25 Wakati mnapozaa watoto na wana watoto, na wakati mtakapo kuwa katika nchi kwa muda mrefu, na kama mtaharibikiwa ninyi na kuchonga umbo la umbo lolote, na kufanya uovu machoni pa Yahwe Mungu wenu, kumchoche katika hasira-
For you will father children and children of children and you will grow old in the land and you will act corruptly and you will make an image of a form of anything and you will do the evil in [the] eyes of Yahweh God your to provoke to anger him.
26 Nitaita nchi na mbingu kushuhudia dhidi yenu leo kwa kuwa mapema kabisa mtaangamia kutoka katika nchi ambayo mnaiendea huko ng'ambo ya Yordani kuimiliki, hamtazidisha siku zenu ndani yake, lakini mtaangamizwa kabisa.
I call as witnesses against you this day the heavens and the earth that certainly you will perish! quickly from on the land where you [are] about to pass over the Jordan there towards to take possession of it not you will prolong! days on it for utterly you will be destroyed!
27 Yahwe atawatawanyisha ninyi miongoni mwa watu, na mtabaki wachache ki-idadi miongoni mwa mataifa, ambapo Yahwe atawaongoza mbali.
And he will scatter Yahweh you among the peoples and you will be left men of number among the nations where he will drive away Yahweh you there towards.
28 Huko mtatumikia miungu mingine, kazi ya mikono ya watu, mbao na mawe, ambayo wala haioni, kusikia, wala kunusa.
And you will serve there gods [the] work of [the] hands of a human wood and stone which not they see! and not they hear! and not they eat! and not they smell!
29 Lakini kuanzia hapo mtamtafuta Yahwe Mungu wenu, na mtampata, wakati mtakapomtafuta kwa moyo wenu wote na roho zenu zote.
And you will seek from there Yahweh God your and you will find [him] for you will seek him with all heart your and with all being your.
30 Wakati mnakuwa katika dhiki, na wakati haya yote yatakuwa yamekuja kwenu, katika siku za badae mtamrudia Yahwe Mungu wenu na kusikia sauti yake.
When it is distress to you and they will come upon you all the things these at [the] end of the days and you will return to Yahweh God your and you will listen to voice his.
31 Kwa kuwa Yahwe Mungu wenu ni Mungu wa rehema; hatawaangusha wala kuwaangamiza ninyi, wala kusahau agano la baba zenu ambalo aliapa kwao.
For [is] a God compassionate Yahweh God your not he will abandon you and not he will destroy you and not he will forget [the] covenant of ancestors your which he swore to them.
32 Kwa ajili ya kuuliza sasa kuhusu siku zilizopita ambazo zilikuwa mbele yenu: tangu siku ile ambayo Mungu alimuumba mtu katika nchi, kutoka pande moja ya mbingu hadi nyingine, uliza kama kumekuwepo chochote kama hiki kikubwa, au chochote kama hicho imewahi kusikiwa?
That ask please to days former which they were before you from the day when he created God - humankind on the earth and to from [the] end of the heavens and to [the] end of the heavens ¿ has it happened like the thing great this or ¿ has it been heard like it.
33 Ilishawahi kutokea watu kusikia sauti ya Mungu kuongea katikati ya moto, kama mlivyosikia, na kuishi?
¿ Has it heard a people [the] voice of a god speaking from [the] middle of the fire just as you have heard you and has it lived?
34 Au Mungu ameshawahi kujaribu kwenda na kujichukulia kwa ajili yake taifa kutoka miongoni mwa taifa, kwa majaribu, ishara na maajabu na kwa vita, na mkono wa nguvu, na mkono ulionyoshwa, na magaidi wakuu, vile vyovyote ambavyo Yahwe Mungu wenu alifanya kwa ajili yenu Misri mbele ya macho yenu?
Or - ¿ has it attempted a god to come to take for itself a nation from [the] midst of a nation by trials by signs and by wonders and by battle and by a hand strong and by an arm outstretched and by terrors great like all that he did for you Yahweh God your in Egypt to eyes your.
35 Kwenu haya yalioneshwa, ili muweze kujua kuwa Yahwe ni Mungu, na kwamba hakuna mwingine zaidi yake.
You you were shown to know that Yahweh he [is] God there not [is] still more from to alone him.
36 Toka mbinguni alifanya msikie sauti yake, ili kwamba aweze kuwaelekeza, juu ya nchi aliwafanya muone moto wake mkuu, mlisikia maneno yake toka katikati ya moto.
From the heavens he caused to hear you voice his to discipline you and on the earth he showed you fire his great and words his you heard from [the] middle of the fire.
37 Kwa sababu aliwapenda baba zenu, alichagua wazao wao baada yao, na kuwatoa ninyi Misri kwa uwepo wake, kwa nguvu yake kubwa,
And because that he loved ancestors your and he chose offspring his after him and he brought out you by own presence his by power his great from Egypt.
38 ili kusudi awatowe kutoka mbele ya mataifa makubwa na yenye nguvu kuliko ninyi, kuwaleta ndani, kuwapa ninyi nchi yao kama urithi, hivi leo.
To dispossess nations great and mighty more than you from before you to bring in you to give to you land their an inheritance as the day this.
39 Tambua hivi leo, weka kwenye moyo wako, Yahwe ni Mungu juu ya mbingu na chini ya dunia, hakuna mwingine yeyote.
And you will know this day and you will bring back to heart your that Yahweh he [is] God in the heavens above and on the earth beneath there not [is] still more.
40 Mtazishika sheria zake na amri zake ambazo nawaamuru leo, ili kwamba iweze kuwa vizuri kwenu na watoto wenu baada yenu, na kwamba muweze kuongeza siku zenu katika nchi ambayo Yahwe Mungu wenu amewapa milele.”
And you will keep statutes his and commandments his which I [am] commanding you this day that it will go well for you and for children your after you and so that you may prolong days on the land which Yahweh God your [is] about to give to you all the days.
41 Kisha Musa alichagua miji mitatu mashariki mwa Yordani,
Then he set apart Moses three cities on [the] other side of the Jordan [the] rising of towards [the] sun.
42 ili kwamba yoyote aweze kukimbia kati ya moja yao kama imemuua mtu mwingine kwa ajili, pasipo kuwa adui hapo awali. Kwa kukimbilia kwenye moja ya miji hii, atakuwa amenusurika.
To flee there towards a killer who he will kill neighbor his with no knowledge and he not [was] hating him from yesterday [the] third day and he will flee to one of the cities these and he will live.
43 Walikuwa: Bezeri katika jangwa, nchi tambarare, kwa Warubenites; Ramothi huko Gileadi, kwa Gadites; na Golani huko Bashani, kwa Manassites.
Bezer in the wilderness in [the] land of the plain for the Reubenite[s] and Ramoth in Gilead for the Gadite[s] and Golan in Bashan for the Manassite[s].
44 Hii ni sheria ambayo Musa aliweka mbele ya watu wa Israeli,
And this [is] the law which he set Moses before [the] people of Israel.
45 hizi ni amri za agano, sheria, na amri zingine alizungumza na watu wa Israeli wakati walipotoka Misri,
These [are] the testimonies and the statutes and the judgments which he spoke Moses to [the] people of Israel when came out they from Egypt.
46 pindi walikuwa Mashariki mwa Yordani, katika bonde mkabala wa Beth Peori, katika nchi ya Sihoni, mfalme wa Amorites, aliyewahi kuishi Heshbon, ambaye Musa na watu wa Israeli waliwahi kumshinda wakati walipotoka Misri.
On [the] other side of the Jordan in the valley opposite to Beth Peor in [the] land of Sihon [the] king of the Amorite[s] who [was] dwelling in Heshbon whom he struck down Moses and [the] people of Israel when came out they from Egypt.
47 Walichukua nchi yake kama urithi, na nchi ya Ogi mfalme wa Bashani- hawa, wafalme wawili wa Amorites, waliokuwa ng'ambo ya pili ya Yordani kuelekea Mashariki.
And they took possession of land his and [the] land of - Og [the] king of Bashan [the] two [the] kings of the Amorite[s] who [was] on [the] other side of the Jordan [the] rising of [the] sun.
48 Himaya hii ilienda kutoka Aroer, katika ukingo wa bonde la Arnon, kwa mlima wa Sion (mlima Hermon),
From Aroer which [is] on [the] edge of [the] wadi of Arnon and to [the] mountain of Siyon that [is] Hermon.
49 na ilijumuisha tambarare zote za bonde la mto Yordani, Mashariki mwa ng'ambo ya pili ya Yordani, kuelekea bahari ya Arabah, kuelekea miteremko ya mlima Pisgah.
And all the Arabah [the] other side of the Jordan east-wards and to [the] sea of the Arabah under [the] slopes of Pisgah.

< Torati 4 >