< Torati 33 >

1 Hii ni baraka ambayo Musa mtu wa Mungu aliwabariki watu wa Israeli kabla ya kifo chake.
And this [is] the blessing which he blessed Moses [the] man of God [the] people of Israel before death his.
2 Alisema: Yahwe alikuja kutoka Sinai na akainuka kutoka Seiri juu yao. Aling'ara kutoka mlima wa Paramu, na akaja na elfu kumi ya watakatifu. Katika mkono wake wa kuume radi zilimulika.
And he said Yahweh from Sinai he came and he dawned from Seir to them he shone forth from [the] mountain of Paran and he came from ten thousands of holy one[s] from right [hand] his (fire of law *QK) for them.
3 Kweli, anawapenda watu; watakatifu wake wote wapo mikononi mwako, na walimsujudu mguuni mwake; walipokea maneno yako.
Also [he is] loving peoples all holy [ones] his [are] in hand your and they they were led to foot your he will take from words your.
4 Musa alituamuru sheria, urithi kwa kusanyiko la Yakobo.
A law he commanded to us Moses a possession [the] assembly of Jacob.
5 Kisha pakawa na mfalme Yeshurumu, pale ambapo wakuu wa watu walipokusanyika, makabila yote ya Israeli pamoja.
And he was in Jeshurun king when gathered themselves [the] chiefs of [the] people together [the] tribes of Israel.
6 Acha Rubeni aishi na asife, lakini wanaume wake wawe wachache.
Let him live Reuben and may not he die and let it be men his number.
7 Hii ni baraka ya Yuda. Musa akasema: Sikiliza sauti ya Yuda, Yahwe, na umlete kwa watu wake tena. Mpiganie; kuwa msaada dhidi ya maadui wake.
And this of Judah and he said hear O Yahweh [the] voice of Judah and to people his you will bring him own hands his he contended for himself and a help from foes his you will be.
8 Kuhusu Lawi, Musa akasema: Thumimu yako na Urimu yako ni ya mtakatifu wako, yule uliyemjaribu kule Masa, ambaye ulishindana naye katika maji ya Meriba.
And of Levi he said Thummim your and Urim your [belong] to a man faithful [one] your whom you put to [the] test him at Massah you contended with him at [the] waters of Meribah.
9 Mtu aliyesema juu ya baba na mama yake, “Sijawaona.” Wala hakuwatambua kaka zake, wala hakuzingatia juu ya watoto wake wenyewe. Kwa maana alilinda neno lako na kushika agano lako.
Who said of father his and of mother his not I saw him and brothers his not he recognized and (children his *QK) not he acknowledged that they kept word your and covenant your they observed.
10 Anafundisha Yakobo maagizo yako na Israeli sheria yako. Ataweka ubani mbele yako na sadaka kamili ya kuteketezwa juu ya dhabahu lako.
They will teach judgments your to Jacob and law your to Israel they will put incense in nose your and [the] whole offering on altar your.
11 Bariki mali zake, Yahwe, na kubali kazi ya mikono yake. Vunja viuno vya wale wanaoinuka dhidi yake, na wale watu wanaomchukia, ili wasiinuke tena.
Bless O Yahweh wealth his and [the] work of hands his you will be pleased with shatter loins [those who] rise against him and [those who] hate him from they will rise!
12 Kuhusu Benyamini, Musa akasema: Yule anayependwa na Yahwe anaishi kwa usalama kando yake; Yahwe anamkinga siku nzima, naye huishi katikati ya mikono ya Yahwe.
Of Benjamin he said [the] beloved [one] of Yahweh he dwells to security on him [who] covers over him all the day and between shoulders his he dwells.
13 Kuhusu Yusufu, Musa akasema: Nchi yake na ibarikiwe na Yahwe na vitu vya thamani vya mbinguni, na umande, na kina kilalacho chini.
And of Joseph he said [be] blessed of Yahweh land his from [the] excellent gift of heaven from [the] dew and from [the] deep [which] lies beneath.
14 Nchi yake na ibarikiwe na vitu vya thamani mavuno ya jua, na vitu vya thamani mazao ya miezi,
And from [the] excellent gift of [the] produce of [the] sun and from [the] excellent gift of [the] yield of [the] months.
15 kwa vitu vizuri vya milima ya zamani, na kwa vitu vya thamani vya milima ya milele.
And from [the] top of [the] mountains of ancient time and from [the] excellent gift of [the] hills of antiquity.
16 Nchi yake ibarikiwe na vitu vya thamani vya ardhi na wingi wake, na kwa mapenzi mema ya yule aliyekuwa kichakani. Baraka na ifike juu ya kichwa cha Yusufu, na juu ya kichwa cha yule aliyekuwa mwana wa mfalme kwa kaka zake.
And from [the] excellent gift of [the] earth and what fills it and [the] favor of [the one who] dwelt [the] bush may it come! to [the] head of Joseph and to [the] scalp of [the] consecrated one of brothers his.
17 Mzawa wa kwanza wa ng’ombe, katika utukufu wake, na pembe zake ni pembe za ng’ombe mwitu. Kwa hawa atawasukuma watu, wote, hadi mwisho wa ulimwengu. Hawa ni maelfu makumi ya Efraimu; hawa ni maelfu wa Manase.
[the] firstborn of Ox his splendor [belongs] to him and [are the] horns of a wild ox horns his with them peoples he will gore together [the] ends of [the] earth and they [are] [the] ten thousands of Ephraim and they [are] [the] thousands of Manasseh.
18 Kuhusu Zabuloni, Musa alisema: Furahi, Zabuloni, katika kutoka kwako, na wewe, Isakari, katika mahema yako.
And of Zebulun he said rejoice O Zebulun when going out you and Issachar in tents your.
19 Watawaita watu hadi milimani. Huko watatoa sadaka za utakatifu. Maana watanyonya wingi wa bahari, na mchanga wa ufukweni.
Peoples a mountain they will summon there they will sacrifice sacrifices of righteousness for [the] abundance of [the] seas they will suck and hidden [things] of hidden [things] of sand.
20 Kuhusu Gadi, Musa alisema: Abarikiwe yule amkuzaye Gadi. Ataishi pale kama simba jike, naye atanyakua mkono au kichwa.
And of Gad he said [be] blessed [one who] enlarges Gad like a lion he dwells and he tears an arm also a scalp.
21 Alitoa sehemu nzuri kwake mwenyewe, maana kulikuwa na fungu la ardhi la kiongozi lililohifadhiwa. Alikuja na vichwa vya watu. Alitekeleza haki ya Yahwe na maagizo yake pamoja na Israeli.
And he saw [the] choicest for himself for there [the] portion of a commander [was] reserved and he came [the] chiefs of [the] people [the] righteousness of Yahweh he executed and judgments his with Israel.
22 Kuhusu Dani, Musa alisema: Dani ni mwana wa simba arukaye kutoka Bashani.
And of Dan he said Dan [is] a cub of a lion he leaps forth from Bashan.
23 Kuhusu Naftali, Musa alisema: Naftali, aliyeridhika na fadhila, na kujaa kwa baraka za Yahwe, miliki nchi iliyopo magharibi na kusini.
And of Naphtali he said Naphtali [is] satisfied of favor and full [the] blessing of Yahweh [the] west and [the] south take possession of!
24 Kuhusu Asheri, Musa alisema: Abarakiwe Asheri Zaidi ya watoto wengine wa kiume; naye akubalike kwa kaka zake, na achovye mguu wake ndani ya mafuta ya zeituni.
And of Asher he said [be] blessed more than [the] sons Asher may he be [the] favored [one] of brothers his and [one who] dips in oil foot his.
25 Vyuma vya mji wako na viwe chuma na shaba; kama vile siku zako zitakavyokuwa, ndivyo usalama wako utakavyokuwa.
[will be] iron And bronze bolts your and [will be] like days your strength your.
26 Hakuna aliye kama Mungu, Yeshurumu – aliyekamili, anayeendesha katika mbingu kukusaidia, na katika utukufu wake juu ya mawingu.
There not [is] like God O Jeshurun [who] rides heaven for help your and in majesty his clouds.
27 Mungu wa milele ni kimbilio, na chini yake kuna mikono ya milele. Husukuma adui mbele yako, naye alisema, “Angamiza!”
[is] a hiding place [the] God of Ancient time and [are] beneath arms of antiquity and he has driven out from before you [the] enemy and he has said destroy.
28 Israeli waliishi katika usalama. Wana wa Yakobo walikuwa salama katika nchi ya nafaka na divai mpya; hakika, mbingu na idondoshe umande juu yake.
And it has dwelt Israel security alone [the] spring of Jacob to a land of grain and new wine also heavens his they drop dew.
29 Baraka zako ni nyingi, Israeli! Nani kama wewe, watu waliokombolewa na Yahwe, ngao ya msaada wako, na upanga wa utukufu wako? Maadui zako watakuja kwako kwa kutetemeka; utakanyanga sehemu zao zilizoinuka.
How blessed [are]! you O Israel who? [is] like you a people [which] it has been saved by Yahweh [the] shield of help your and who [is] [the] sword of eminence your so they may cringe enemies your to you and you on high places their you will tread.

< Torati 33 >