< Torati 33 >

1 Hii ni baraka ambayo Musa mtu wa Mungu aliwabariki watu wa Israeli kabla ya kifo chake.
And this is the blessing, wherewith Moses the man of God blessed the children of Israel before his death.
2 Alisema: Yahwe alikuja kutoka Sinai na akainuka kutoka Seiri juu yao. Aling'ara kutoka mlima wa Paramu, na akaja na elfu kumi ya watakatifu. Katika mkono wake wa kuume radi zilimulika.
And he said, The LORD came from Sinai, And rose from Seir unto them; He shined forth from mount Paran, And he came from the ten thousands of holy ones: At his right hand was a fiery law unto them.
3 Kweli, anawapenda watu; watakatifu wake wote wapo mikononi mwako, na walimsujudu mguuni mwake; walipokea maneno yako.
Yea, he loveth the peoples; All his saints are in thy hand: And they sat down at thy feet; [Every one] shall receive of thy words.
4 Musa alituamuru sheria, urithi kwa kusanyiko la Yakobo.
Moses commanded us a law, An inheritance for the assembly of Jacob.
5 Kisha pakawa na mfalme Yeshurumu, pale ambapo wakuu wa watu walipokusanyika, makabila yote ya Israeli pamoja.
And he was king in Jeshurun, When the heads of the people were gathered, All the tribes of Israel together.
6 Acha Rubeni aishi na asife, lakini wanaume wake wawe wachache.
Let Reuben live, and not die; Yet let his men be few.
7 Hii ni baraka ya Yuda. Musa akasema: Sikiliza sauti ya Yuda, Yahwe, na umlete kwa watu wake tena. Mpiganie; kuwa msaada dhidi ya maadui wake.
And this is [the blessing] of Judah: and he said, Hear, LORD, the voice of Judah, And bring him in unto his people: With his hands he contended for himself; And thou shalt be an help against his adversaries.
8 Kuhusu Lawi, Musa akasema: Thumimu yako na Urimu yako ni ya mtakatifu wako, yule uliyemjaribu kule Masa, ambaye ulishindana naye katika maji ya Meriba.
And of Levi he said, Thy Thummim and thy Urim are with thy godly one, Whom thou didst prove at Massah, With whom thou didst strive at the waters of Meribah;
9 Mtu aliyesema juu ya baba na mama yake, “Sijawaona.” Wala hakuwatambua kaka zake, wala hakuzingatia juu ya watoto wake wenyewe. Kwa maana alilinda neno lako na kushika agano lako.
Who said of his father, and of his mother, I have not seen him; Neither did he acknowledge his brethren, Nor knew he his own children: For they have observed thy word, And keep thy covenant.
10 Anafundisha Yakobo maagizo yako na Israeli sheria yako. Ataweka ubani mbele yako na sadaka kamili ya kuteketezwa juu ya dhabahu lako.
They shall teach Jacob thy judgments, And Israel thy law: They shall put incense before thee, And whole burnt offering upon thine altar.
11 Bariki mali zake, Yahwe, na kubali kazi ya mikono yake. Vunja viuno vya wale wanaoinuka dhidi yake, na wale watu wanaomchukia, ili wasiinuke tena.
Bless, LORD, his substance, And accept the work of his hands: Smite through the loins of them that rise up against him, And of them that hate him, that they rise not again.
12 Kuhusu Benyamini, Musa akasema: Yule anayependwa na Yahwe anaishi kwa usalama kando yake; Yahwe anamkinga siku nzima, naye huishi katikati ya mikono ya Yahwe.
Of Benjamin he said, The beloved of the LORD shall dwell in safety by him; He covereth him all the day long, And he dwelleth between his shoulders.
13 Kuhusu Yusufu, Musa akasema: Nchi yake na ibarikiwe na Yahwe na vitu vya thamani vya mbinguni, na umande, na kina kilalacho chini.
And of Joseph he said, Blessed of the LORD be his land; For the precious things of heaven, for the dew, And for the deep that coucheth beneath,
14 Nchi yake na ibarikiwe na vitu vya thamani mavuno ya jua, na vitu vya thamani mazao ya miezi,
And for the precious things of the fruits of the sun, And for the precious things of the growth of the moons,
15 kwa vitu vizuri vya milima ya zamani, na kwa vitu vya thamani vya milima ya milele.
And for the chief things of the ancient mountains, And for the precious things of the everlasting hills,
16 Nchi yake ibarikiwe na vitu vya thamani vya ardhi na wingi wake, na kwa mapenzi mema ya yule aliyekuwa kichakani. Baraka na ifike juu ya kichwa cha Yusufu, na juu ya kichwa cha yule aliyekuwa mwana wa mfalme kwa kaka zake.
And for the precious things of the earth and the fulness thereof, And the good will of him that dwelt in the bush: Let [the blessing] come upon the head of Joseph, And upon the crown of the head of him that was separate from his brethren.
17 Mzawa wa kwanza wa ng’ombe, katika utukufu wake, na pembe zake ni pembe za ng’ombe mwitu. Kwa hawa atawasukuma watu, wote, hadi mwisho wa ulimwengu. Hawa ni maelfu makumi ya Efraimu; hawa ni maelfu wa Manase.
The firstling of his bullock, majesty is his; And his horns are the horns of the wild-ox: With them he shall push the peoples all of them, [even] the ends of the earth: And they are the ten thousands of Ephraim, And they are the thousands of Manasseh.
18 Kuhusu Zabuloni, Musa alisema: Furahi, Zabuloni, katika kutoka kwako, na wewe, Isakari, katika mahema yako.
And of Zebulun he said, Rejoice, Zebulun, in thy going out; And, Issachar, in thy tents.
19 Watawaita watu hadi milimani. Huko watatoa sadaka za utakatifu. Maana watanyonya wingi wa bahari, na mchanga wa ufukweni.
They shall call the peoples unto the mountain; There shall they offer sacrifices of righteousness: For they shall suck the abundance of the seas, And the hidden treasures of the sand.
20 Kuhusu Gadi, Musa alisema: Abarikiwe yule amkuzaye Gadi. Ataishi pale kama simba jike, naye atanyakua mkono au kichwa.
And of Gad he said, Blessed be he that enlargeth Gad: He dwelleth as a lioness, And teareth the arm, yea, the crown of the head.
21 Alitoa sehemu nzuri kwake mwenyewe, maana kulikuwa na fungu la ardhi la kiongozi lililohifadhiwa. Alikuja na vichwa vya watu. Alitekeleza haki ya Yahwe na maagizo yake pamoja na Israeli.
And he provided the first part for himself, For there was the lawgiver’s portion reserved; And he came [with] the heads of the people, He executed the justice of the LORD, And his judgments with Israel.
22 Kuhusu Dani, Musa alisema: Dani ni mwana wa simba arukaye kutoka Bashani.
And of Dan he said, Dan is a lion’s whelp, That leapeth forth from Bashan.
23 Kuhusu Naftali, Musa alisema: Naftali, aliyeridhika na fadhila, na kujaa kwa baraka za Yahwe, miliki nchi iliyopo magharibi na kusini.
And of Naphtali he said, O Naphtali, satisfied with favour, And full with the blessing of the LORD: Possess thou the west and the south.
24 Kuhusu Asheri, Musa alisema: Abarakiwe Asheri Zaidi ya watoto wengine wa kiume; naye akubalike kwa kaka zake, na achovye mguu wake ndani ya mafuta ya zeituni.
And of Asher he said, Blessed be Asher with children; Let him be acceptable unto his brethren, And let him dip his foot in oil.
25 Vyuma vya mji wako na viwe chuma na shaba; kama vile siku zako zitakavyokuwa, ndivyo usalama wako utakavyokuwa.
Thy bars shall be iron and brass; And as thy days, so shall thy strength be.
26 Hakuna aliye kama Mungu, Yeshurumu – aliyekamili, anayeendesha katika mbingu kukusaidia, na katika utukufu wake juu ya mawingu.
There is none like unto God, O Jeshurun, Who rideth upon the heaven for thy help, And in his excellency on the skies.
27 Mungu wa milele ni kimbilio, na chini yake kuna mikono ya milele. Husukuma adui mbele yako, naye alisema, “Angamiza!”
The eternal God is [thy] dwelling place, And underneath are the everlasting arms: And he thrust out the enemy from before thee, And said, Destroy.
28 Israeli waliishi katika usalama. Wana wa Yakobo walikuwa salama katika nchi ya nafaka na divai mpya; hakika, mbingu na idondoshe umande juu yake.
And Israel dwelleth in safety, The fountain of Jacob alone, In a land of corn and wine; Yea, his heavens drop down dew.
29 Baraka zako ni nyingi, Israeli! Nani kama wewe, watu waliokombolewa na Yahwe, ngao ya msaada wako, na upanga wa utukufu wako? Maadui zako watakuja kwako kwa kutetemeka; utakanyanga sehemu zao zilizoinuka.
Happy art thou, O Israel: Who is like unto thee, a people saved by the LORD, The shield of thy help, And that is the sword of thy excellency! And thine enemies shall submit themselves unto thee; And thou shalt tread upon their high places.

< Torati 33 >