< Torati 32 >

1 Tega sikio, enyi mbingu, na niruhusu kuzungumza.
Słuchajcie, niebiosa, a będę mówić; niech i ziemia słucha słów moich ust.
2 Acha dunia isikie maneno ya kinywa changu. Acha mafundisho yangu yamwagike chini kama mvua, acha usemi wangu udondoke kama umande, kama mvua tulivu juu ya majani laini, na kama mvua za manyunyu juu ya mimea.
Moja nauka będzie kropić jak deszcz, moja mowa będzie ściekać jak rosa, jak drobny deszcz na zioła, jak krople na trawę.
3 Kwa maana nitatangaza jina la Yahwe, na kumpatia ukuu Mungu wetu.
Będę bowiem głosił imię PANA. Uznajcie wielkość naszego Boga.
4 Mwamba, kazi yake ni kamili; kwa maana njia zake ni za haki. Yeye ni Mungu mwaminifu, hana udhalimu. Yeye ni wa haki na mwadilifu.
On jest Skałą, a jego dzieło [jest] doskonałe, bo wszystkie jego drogi są sprawiedliwe. Jest Bogiem prawdziwym i bez nieprawości, sprawiedliwym i prawym.
5 Wamefanya yaliyo maovu dhidi yake. Wao sio watoto wake. Ni aibu kwao. Wao ni kizazi kiovu na kilichopindika.
Zepsuli się, ich skaza nie [jest skazą] jego dzieci; pokolenie złe i przewrotne.
6 Je! Unamzawadia Yahwe kwa njia hii, enyi watu wapumbavu na msiojitambua? Je! yeye si baba yenu, yule ambaye aliwaumba? Aliwaumba na kuwaimarisha.
Tak to odpłacasz PANU, ludu głupi i niemądry? Czy nie jest on twoim ojcem, który cię nabył dla siebie? Czy nie on cię uczynił i utwierdził?
7 Kumbukeni siku zile za zamani, tafakari juu ya miaka mingi ya nyuma. Muulize baba yako naye atakuonyesha, wazee wako nao watakuambia.
Wspomnij dni dawne, rozważ lata wielu pokoleń. Zapytaj swego ojca, a oznajmi ci; swoich starszych, a powiedzą ci.
8 Pale ambapo Aliye Juu alipowapatia mataifa urithi wao – alipowagawa wanadamu wote, na kuweka mipaka ya watu, na alipoimarisha idadi ya miungu yao.
Gdy Najwyższy rozdzielał dziedzictwa narodom, a oddzielał synów Adama, wyznaczył granice narodom według liczby synów Izraela.
9 Kwa maana fungu la Yahwe ni watu wake; Yakobo ni mgao wa urithi wake.
Działem PANA [jest] bowiem jego lud, Jakub jest jego wydzielonym dziedzictwem.
10 Alimpata katika nchi ya jangwa, na katika jangwa kame na livumalo upepo; alimkinga na kumtunza, alimlinda kama mboni ya jicho lake.
Znalazł go na pustynnej ziemi i na wielkim, strasznym pustkowiu. Obwodził go, uczył, strzegł jak źrenicy swego oka.
11 Kama tai akichungaye kiota chake na kupiga piga mabawa juu ya makinda yake, Yahwe alitandaza mabawa yake na kuwachukua, na kuwabeba kwenye mapapatio yake.
Jak orzeł pobudza swoje młode, trzepocze [skrzydłami] nad swymi orlętami, rozpościera swoje skrzydła, bierze je i nosi je na skrzydłach;
12 Yahwe pekee alimuongoza, hapakuwa na mungu mgeni pamoja naye.
Tak PAN sam prowadził go i nie było z nim żadnego obcego boga.
13 Alimfanya aendeshe katika maeneo ya juu ya nchi, na alimlisha matunda ya mbugani; alimrutubisha kwa asali kutoka kwenye jiwe, na mafuta kutoka kwenye mwamba mgumu sana.
Wzniósł go po wysokich miejscach ziemi, aby żywił się plonami pól, i pozwolił mu ssać miód ze skały i oliwę ze skalnego krzemienia;
14 Alikula siagi kutoka katika kundi na kunywa maziwa kutoka katika kundi la mifugo, pamoja na mafuta ya wanakondoo, kondoo dume wa Bashani na mbuzi, pamoja na ngano safi kabisa – nawe ulikunywa divai itokayo povu iliyotengenezwa kwa juisi ya mizabibu.
Masło od krów i mleko od owiec wraz z tłuszczem jagniąt, barany odchowane w Baszanie, kozły razem z tłuszczem ziaren pszenicy, a piłeś z wybornej krwi winogron.
15 Lakini Yeshuruni akakua kwa unene na kupiga mateke – ulikua kwa unene, ulikua mnene sana, na ulikuwa umekula ujazo wako – alimuacha Mungu aliyemuumba, na kukataa Mwamba wa wokovu wake.
Lecz Jeszurun utył i wierzgał – otyłeś, obrosłeś w tłuszcz, zgrubiałeś; opuściłeś Boga, który cię uczynił, i lekceważyłeś Skałę swego zbawienia.
16 Walimfanya Yahwe apatwe wivu kwa miungu yao ya ajabu; kwa maudhi yao walimkasirisha.
Pobudzili go do zazdrości obcymi [bogami], rozdrażnili go obrzydliwościami.
17 Walitoa dhabihu kwa mapepo, ambayo sio Mungu – miungu ambayo hawajaijua, miungu ambayo imejitokeza hivi karibuni, miungu ambayo mababu zenu hawakuogopa.
Składali ofiary demonom, a nie Bogu; nowym bogom, których nie znali, świeżo przybyłym, których się nie bali wasi ojcowie.
18 Umetelekeza Mwamba, ambao ulikuwa baba yako, na ukasahau Mungu aliyekuzaa.
O Skale, która cię spłodziła, zapomniałeś, i zapomniałeś Boga, swego Stwórcę.
19 Yahwe aliliona hili na kuwakataa, kwa sababu watoto wake wa kiume na mabinti zake walimchokoza.
Gdy PAN to zobaczył, wzgardził nimi z powodu rozdrażnienia swoich synów i córek.
20 “Nitaficha uso wangu kwao”, alisema, “nami nitaona mwisho wao utakuaje; maana wao ni kazazi kaidi, watoto ambao sio waaminifu.
I powiedział: Zakryję przed nimi swoje oblicze, zobaczę, jaki będzie ich koniec. Są bowiem pokoleniem przewrotnym, synami, w których nie ma wiary.
21 Wamenifanya kuwa na wivu kwa kile ambacho sio mungu na kunikasirisha kwa mambo yao yasiyo na maana. Nitawafanya waone wivu kwa wale ambao sio taifa; nitawakasirisha kwa taifa pumbavu.
Oni mnie pobudzili do zazdrości tym, [co] nie jest Bogiem; rozdrażnili mnie swymi marnościami. Ja też pobudzę ich do zazdrości tymi, [którzy] nie są ludem, rozdrażnię ich przez głupi naród.
22 Kwa maana moto kuwashwa kwa hasira yangu na inawaka hadi chini mwa Sheoli; inameza ulimwengu na mavuno yake; inawasha moto misingi ya milima. (Sheol h7585)
Zapłonął bowiem ogień mojego gniewu i spłonie aż do głębin piekła, i pożre ziemię i jej plony, i wypali posady gór. (Sheol h7585)
23 Nitarundia maafa juu yao; nitafyatua mishale yangu yote kwao;
Zgromadzę na nich nieszczęścia, zużyję na nich moje strzały.
24 Watapotea kwa njaa na kumezwa kwa joto liwakalo na uharibifu mchungu; nitatuma kwao meno ya wanyama wa mwituni, pamoja na sumu ya vitu vitambaao mavumbini.
[Będą] wyczerpani z głodu i strawieni gorączką i gorzką zarazą. Wyślę na nich też zęby bestii, z jadem gadów ziemskich.
25 Nje panga litawatwaa, na ndani ya vyumba hofu kuu itafanya hivyo. Wote mwanamume kijana na bikra nitawaangamiza, mchanga anyonyaye, na mwanamume mwenye mvi.
Na zewnątrz osieroci ich miecz, a w domach – strach, tak młodzieńca, jak i dziewicę, niemowlę i sędziwego.
26 Nilisema nitawasambaza mbali, kwamba nitafanya kumbukumbu yao kukoma miongoni mwa wanadamu.
Powiedziałem: Rozproszę ich po kątach, wymażę pamięć o nich wśród ludzi;
27 Isingekuwa kwamba naogopa uchokozi wa adui, na kwamba adui zake wangehukumu kimakosa, na kwamba wangesema, “Mkono wetu umeinuliwa,” ningefanya haya yote.
Gdybym się nie obawiał pychy wroga, by ich wrogowie nie powstali i nie powiedzieli: Nasza wielka ręka, a nie PAN, uczyniła to wszystko.
28 Kwa maana Israeli ni taifa linalopungukiwa na hekima, na hakuna ufahamu ndani mwao.
Ten naród bowiem jest pozbawiony rady i nie ma rozumu.
29 Ah laiti wangekuwa na hekima, wangeelewa hili, na kuzingatia ujio wa hatima yao!
Oby byli mądrzy, zrozumieliby to i zważaliby na swój koniec.
30 Inawezekanaje mmoja kufukuza maelfu, na wawili kuweka makumi elfu mbioni, isipokuwa Mwamba wao hajawauza, na Yahwe hajawaachilia kwao?
Jakże mógłby jeden gonić tysiąc i dwóch zmusić do ucieczki dziesięć tysięcy, gdyby ich Skała nie zaprzedała ich i PAN ich nie wydał?
31 Kwa maana mwamba wa maadui zetu si kama Mwamba wetu, kama vile maadui zetu wanavyokiri.
Bo ich skała nie jest jak nasza Skała, nasi wrogowie [sami] są sędziami.
32 Kwa maana mzabibu wao unatoka kwenye mzabibu wa Sodoma, na kwenye mashamba ya Gomorra; na zabibu zake ni zabibu za sumu; vishada vyao ni vichungu.
Ich winorośl bowiem pochodzi z winorośli Sodomy i z pól Gomory, ich grona to grona trujące, ich kiście są gorzkie.
33 Mvinyo yao ni sumu ya nyoka na sumu katili ya nyoka.
Ich wino jest jadem smoków, okrutną trucizną żmij.
34 Huu mpango haujafichwa kwangu kwa siri, na kufungwa kabisa katika hazina zangu?
Czy to nie jest u mnie ukryte, zapieczętowane w moich skarbcach?
35 Kisasi ni changu kutoa, na fidia, katika muda mguu wao utakapotereza; kwa maana siku ya maafa kwao ipo karibu, na vitu vitakavyokuja juu yao vitaharakisha kutendeka.
Do mnie należy zemsta i odpłata; ich noga poślizgnie się w [wyznaczonym] czasie. Bliski bowiem jest dzień ich klęski, a ich przyszłość spieszy się do nich.
36 Kwa maana Yahwe atatoa haki kwa watu wake, na atawahurumia watumishi wake. Atahakikisha kuwa nguvu yao imetoweka, na hakuna atakayesalia, iwe watumwa au watu huru.
PAN bowiem będzie sądzić swój lud, zlituje się nad swymi sługami, gdy zobaczy, że ich siła ustała i że nie ma ani niewolnika, ani wolnego.
37 Kisha atasema, “wako wapi miungu yao, mwamba ambao wamekimbilia? –
I powie: Gdzie są ich bogowie? [Ta] skała, w której pokładali ufność?
38 miungu iliyokula sadaka zao nene na kunywa mvinyo wa sadaka zao za kinywaji? Na wainuke na kukusaidia; na wawe ulinzi kwako.
Ci, co jadali tłuszcz ich ofiar i pili wino ich ofiar z płynów? Niech wstaną i wam pomogą, niech będą waszym schronieniem.
39 Tazama sasa mimi, hata mimi, ni Mungu, na kwamba hakuna mungu tofauti yangu; ninaua, na ninaleta uhai; ninajeruhi, na ninaponya, na hakuna mtu atakayekuokoa kutoka kwa uwezo wangu.
Spójrzcie teraz, że to ja, tylko ja jestem, a nie ma innych bogów oprócz mnie. Ja zabijam i ożywiam, ja ranię i ja leczę, i nikt nie wyrwie z mojej ręki.
40 Kwa maana ninainua mikono yangu mbinguni na kusema, “Niishivyo milele, nitatenda.
Podnoszę bowiem swą rękę ku niebu i mówię: Ja żyję na wieki.
41 Nitakapong’oa panga langu lingaaro, na mkono wangu utakapoanza kuleta haki, nitalipiza kisasi juu ya maadui zangu, na kuwalipa wale wote wanichukiao.
Jeśli zaostrzę swój błyszczący miecz i moja ręka chwyci sąd, dokonam zemsty na swoich wrogach i odpłacę tym, którzy mnie nienawidzą.
42 Nitafanya mishale yangu kulewa na damu, na panga langu litameza nyama kwa damu ya waliouawa na mateka, na kutoka kwa vichwa vya viongozi wa adui.”
Krwią upoję moje strzały, mój miecz naje się mięsa, krwią zabitych i pojmanych, jak tylko zacznę mścić się nad wrogami.
43 Furahi, enyi mataifa, na watu wa Mungu, kwa maana atalipiza kisasi damu ya watumishi wake; atalipiza kisasi juu ya maadui zake, naye atafanya upatanisho kwa ajili ya nchi yake, kwa watu wake.
Weselcie się, narody, z jego ludem, gdyż on pomści krew swoich sług i odpłaci zemstą swoim wrogom, a będzie łaskawy dla swej ziemi i swego ludu.
44 Musa alikuja na kunena maneno yote ya wimbo huu masikioni mwa watu, yeye na Yoshua mwana wa Nuni.
Przyszedł więc Mojżesz i powiedział wszystkie słowa tej pieśni do uszu tego ludu, on i Ozeasz, syn Nuna.
45 Kisha Musa alimaliza kunena maneno haya yote kwa Israeli yote.
A [gdy] Mojżesz skończył mówić wszystkie te słowa do całego Izraela;
46 Aliwaambia, “Imarisheni akili yenu kwa haya maneno ambayo nimewashuhudia kwenu leo, ili kwamba muwaamuru watoto wenu kuyashika, maneno yote ya sheria hii.
Powiedział do nich: Weźcie sobie do serca wszystkie te słowa, które wam dzisiaj oświadczam, byście przykazywali je waszym dzieciom, by pilnowały wypełnienia wszystkich słów tego prawa;
47 Kwa maana hili si jambo dogo kwako, kwa sababu ni uzima wako, na kupitia jambo hili utarefusha siku zako katika nchi ambayo unakwenda juu ya Yordani kumiliki.”
Nie jest to bowiem dla was słowem pustym, gdyż jest waszym życiem. I dzięki niemu przedłużycie swoje dni na ziemi, do której się przeprawiacie przez Jordan, aby ją posiąść.
48 Yahwe alizungumza na Musa katika siku hiyo hiyo na kusema,
I tego samego dnia PAN powiedział do Mojżesza:
49 “Nenda katika usawa huu wa milima wa Abarimu, juu ya mlima wa Nebo, ambao upo katika nchi ya Moabu, mkabala na Yeriko. Utatazama nchi ya Kanani, ambayo ninawapatia watu wa Israeli kama miliki yao.
Wstąp na tę górę Abarim, na górę Nebo, która jest w ziemi Moabu naprzeciw Jerycha, i spójrz na ziemię Kanaan, którą daję synom Izraela w posiadanie.
50 Utakufa katika mlima utakaopanda, na utakusanywa kwa watu wako, kama Haruni Muisraeli mwenzako alivyokufa juu ya mlima wa Hori na kukusanywa kwa watu wake. Hii
I umrzesz na tej górze, na którą wstąpisz, i zostaniesz przyłączony do swego ludu, tak jak umarł twój brat Aaron na górze Hor i został przyłączony do swego ludu;
51 itatendeka kwa sababu haukuwa mwaminifu kwangu miongoni mwa watu wa Israeli katika maji ya Meriba kule Kadeshi, katika jangwa la Zini; kwa sababu haukunitendea utukufu na heshima miongoni mwa watu wa Israeli.
Za to, że wystąpiliście przeciwko mnie pośród synów Izraela przy wodach Meriba w Kadesz, na pustyni Syn, i nie poświęciliście mnie pośród synów Izraela.
52 Kwa maana utaona nchi mbele yako, lakini hautakwenda kule, katika nchi ninayowapatia watu wa Israeli.”
Przed sobą zobaczysz ziemię, lecz nie wejdziesz do tej ziemi, którą daję synom Izraela.

< Torati 32 >