< Torati 29 >

1 Haya ni maneno ambayo Yahwe alimuamuru Musa kuwaambia watu wa Israeli katika nchi ya Moabu, maneno ambayo yaliongezwa katika agano alilolifanya pamoja nao kule Horebu.
These ben the wordis of boond of pees, which the Lord comaundide to Moyses, that he schulde smyte with the sones of Israel in the lond of Moab, outakun that bond of pees, which he couenauntide with hem in Oreb.
2 Musa aliwaita Waisraeli wote na kuwaambia, “Mmeona kila kitu ambacho Yahwe alifanya mbele ya macho yenu katika nchi ya Misri kwa Farao, kwa watumishi wake wote, na kwa nchi yake yote –
And Moises clepid al Israel, and seide to hem, Ye sien alle thingis whiche the Lord dide bifor you in the lond of Egipt, to Farao and alle hise seruauntis, and to al his lond;
3 mateso makubwa ambayo macho yenu yaliona, ishara, pamoja na ile miujiza mikubwa.
the greet temptaciouns whiche thin iyen sien, `tho signes, and grete wondris.
4 Lakini mpaka leo Yahwe hajawapatia moyo wa kufahamu, macho ya kuona, au masikio ya kusikia.
And the Lord yaf not to you an herte vndurstondynge, and iyen seynge, and eeris that moun here, til in to present dai.
5 Nimewaongoza kwa miaka arobaini jangwani; mavazi yenu hayakuchakaa juu yenu, na ndala zenu hazikuchakaa miguuni mwenu.
He ledde you bi fourti yeer thoruy deseert; youre clothis weren not brokun, nether the schoon of youre feet weren waastid bi eldnesse;
6 Hamkula mkate wowote, na wala hamkunywa divai yoyote au kinywaji chochote chenye ulevi, ili kwamba muweze kujua kuwa mimi ni Yahwe Mungu wenu.
ye eetun not breed, ye drunken not wyn and sidur, that ye schulden wite that he is youre Lord God.
7 Mlipokuja mahali hapa, Sihoni, mfalme wa Heshboni, na Ogu, mfalme wa Bashani, walikuja dhidi yetu kutupiga, na tukawapiga.
And ye camen to this place; and Seon, the kyng of Esebon yede out, and Og, the kyng of Basan, and camen to us to batel. And we han smyte hem,
8 Tulichukua ardhi yao na kuwapa kama urithi Wareubeni, kwa Wagadi, na kwa nusu ya kabila ya Manase.
and we token awey the lond `of hem, and we yauen `the lond to possessioun, to Ruben, and to Gad, and to the half lynage of Manasses.
9 Kwa hiyo shikilia maneno ya agano hili na kuyatenda, ili ufanikiwe katika kila kitu ufanyacho.
Therfor kepe ye the wordis of this couenaunt, and fille ye tho, that ye vndirstonde all thingis whiche ye schulen do.
10 Nyie wote, mnasimama leo, mbele ya Yahwe Mungu wenu; machifu wenu, makabila yenu, wazee wenu, na maafisa wenu – wanaume wote wa Israeli,
Alle ye stonden to day bifor youre Lord God, youre princes, and lynagis, and the grettere men in birthe, and techeris, al the puple of Israel,
11 watoto wenu, wake zenu, na wageni ambao wamo miongoni wa kambi yenu, kutoka kwa yule anayekata mbao zenu mpaka kwa yule atekaye maji.
fre children, and youre wyues, and comelyngis that dwellen with thee in castels, outakun the heweris of stonus, and outakun hem that beren watris;
12 Mpo hapa ili kwamba muingie katika agano la Yahwe Mungu wenu na katika kiapo ambacho Yahwe Mungu wako anafanya na wewe leo,
that thou go in the boond of pees of thi Lord God, and in the ooth which thi Lord God smytith with thee,
13 ili kwamba awafanye leo kuwa watu wake, na kwamba aweze kuwa Mungu kwa ajili yako, kama alivyonena kwako, na kama alivyoapa kwa mababu zako, kwa Abrahamu, kwa Isaka na kwa Yakobo.
that he reise thee in to a puple to hym silf, and that he be thi Lord God, as he spak to thee, and as he swoor to thi fadris, to Abraham, Ysaac, and Jacob.
14 Kwa maana ninafanya agano hili na kiapo hiki sio na wewe tu –
And not to you aloone Y smyte this loond of pees, and conferme these othis,
15 pamoja kila mtu aliyesimama hapa pamoja nasi leo mbele ya Yahwe Mungu wetu – bali na wale ambao hawapo pamoja nasi leo pia.
but to alle men, present and absent.
16 Unajua jinsi tulivyoishi katika nchi ya Misri, na jinsi tulivyopenya miongoni mwa mataifa ambao uliwapita.
For ye witen hou we dwelliden in the lond of Egipt, and how we passiden bi the myddis of naciouns; whiche ye passiden,
17 Mmeona sanamu zao zinazokera zilizotengenezwa kwa mbao na mawe, fedha na dhahabu, ambazo zilikuwa miongoni mwenu.
and siyen abhomynaciouns and filthis, that is, idols `of hem, tre and stoon, siluer and gold, whiche thei worschipiden.
18 Hakikisha hakuna kati yenu mwanamume, mwanamke, ukoo, au kabila ambaye moyo wake unamuacha Yahwe Mungu wetu leo, ili kwenda na kuabudu miungu ya mataifa hayo. Hakikisha hakuna kati yenu mzizi utakaozaa nyongo na pakanga.
Lest perauenture among you be man ether womman, meyne ether lynage, whos herte is turned away to dai fro youre Lord God, that he go, and serue the goddis of tho folkis; and a roote buriounnynge galle and bitternesse be among you;
19 Wakati mtu huyo anaposikia maneno ya laana hii, atajifariji moyoni mwake na kusema, “Nitakuwa na amani, ingawa natembea katika ukaidi wa moyo wangu”. Hii itaangamiza ubichi pamoja na ukavu.
and whanne he hath herd the wordis of this ooth, he blesse hym silf in his herte, and seie, Pees schal be to me, and Y schal go in the schrewidnesse of myn herte; and lest the drunkun take the thirsti,
20 Yahwe hatamsamehe, lakini badala yake, hasira ya Yahwe na wivu wake utambanika mtu huyo, na laana zote zilizoandikwa katika kitabu hiki vitakuwa juu yake, na Yahwe ataliondoa jina lake kutoka mbinguni.
and the Lord forgyue not to hym, but thanne ful greetli his strong veniaunce be feers, and the feruour ayens that man, and alle the cursis that ben writun in this book `sitte on hym; and `the Lord do away his name vndur heuene,
21 Yahwe atamuweka kando kwa ajili ya maafa kutoka katika makabila yote ya Israeli, kwa kuzingatia laana zote za agano ambazo zimeandikwa katika kitabu hiki cha sheria.
and waaste hym in to perdicioun fro alle the lynagis of Israel, bi the cursis that ben conteyned in the book of this lawe and of boond of pees.
22 Kizazi kifuatacho, watoto wako watakaoinuka baada yako, na mgeni atakayekuja kutoka nchi ya mbali, watazungumza watakapoona mapigo juu ya nchi hii na magonjwa ambayo Yahwe ameyafanya yawe –
And the generacioun suynge schal seie, and the sones that schulen be borun aftirward, and pilgrimys that schulen come fro fer, seynge the veniauncis of that lond, and the sikenessis bi whiche the Lord turmentide that lond,
23 na watakapoona kuwa nchi yote imekuwa salfa na chumvi ichomayo, ambapo hakuna kitu kipandwacho au kuzaa matunda, ambapo hapaoti mmea wowote, kama anguko la Sodoma na Gomora, Adma na Seboimu, ambayo Yahwe aliangamiza katika ghadhabu na hasira yake –
brennynge `that lond with brymston and heete of the sunne, so that it be no more sowun, nether bringe forth ony grene thing, in to ensaumple of destriyng of Sodom and of Gommorre, of Adama and of Seboym, whiche the Lord destriede in his ire and stronge veniaunce.
24 watasema kwa pamoja na mataifa mengine, “Kwa nini Yahwe amefanya hili katika nchi hii? Joto ya hasira hii kali inamaanisha nini?”
And alle folkis schulen seie, Whi dide the Lord so to this lond? What is the greet ire of his stronge veniaunce?
25 Kisha watu watasema, “Ni kwa sababu walitelekeza agano la Yahwe, Mungu wa mababu zao, alilofanya nao alipowatoa kutoka Misri,
and thei schulen answere, For thei forsoken the couenaunt of the Lord, whiche he couenauntide with her fadris, whanne he ledde hem out of the lond of Egipt,
26 na kwa sababu waliondoka na kutumikia miungu mingine na kuzisujudu, miungu ambayo hawakujiua na ambayo hakuwapatia.
and thei serueden alien goddis, and worschipiden hem, whiche thei knewen not, and to whiche thei weren not youun;
27 Kwa hiyo hasira ya Yahwe imewaka dhidi ya nchi hii, ili kuleta juu yake laana zote zilizoandikwa katika kitabu hiki.
therfor the strong veniaunce of the Lord was wrooth ayens this lond, that he brouyte yn on it alle the cursis that ben writun in this book;
28 Yahwe amewang’oa kutoka nchini kwao kwa hasira, kwa ghadhanu, na kwa ghadhabu kali, na kuwatupa katika nchi nyingine, leo.
and he castide hem out of her lond, in ire and strong veniaunce, and in gretteste indignacioun; and he castide forth in to an alien lond, as it is preued to dai.
29 Mambo ya siri ni ya Yahwe Mungu wetu pekee; lakini mambo yaliyofichuliwa ni ya kwetu milele pamoja na wazawa wetu, ili tufanye maneno yote ya sheria hii.
Thingis ben hid of oure Lord God, `that is, in his biforknowing, whiche thingis ben schewid to us, and to oure sones with outen ende, that we do alle the wordis of this lawe.

< Torati 29 >