< Torati 29 >

1 Haya ni maneno ambayo Yahwe alimuamuru Musa kuwaambia watu wa Israeli katika nchi ya Moabu, maneno ambayo yaliongezwa katika agano alilolifanya pamoja nao kule Horebu.
These [are] [the] words of the covenant which he commanded Yahweh Moses to make with [the] people of Israel in [the] land of Moab besides the covenant which he had made with them at Horeb.
2 Musa aliwaita Waisraeli wote na kuwaambia, “Mmeona kila kitu ambacho Yahwe alifanya mbele ya macho yenu katika nchi ya Misri kwa Farao, kwa watumishi wake wote, na kwa nchi yake yote –
And he summoned Moses all Israel and he said to them you you have seen all that he did Yahweh to eyes your in [the] land of Egypt to Pharaoh and to all servants his and to all land his.
3 mateso makubwa ambayo macho yenu yaliona, ishara, pamoja na ile miujiza mikubwa.
The trials great which they saw eyes your the signs and the wonders great those.
4 Lakini mpaka leo Yahwe hajawapatia moyo wa kufahamu, macho ya kuona, au masikio ya kusikia.
And not he has given Yahweh to you a heart to know and eyes to see and ears to hear until the day this.
5 Nimewaongoza kwa miaka arobaini jangwani; mavazi yenu hayakuchakaa juu yenu, na ndala zenu hazikuchakaa miguuni mwenu.
And I led you forty year[s] in the wilderness not they wore out clothes your from on you and sandal your not it wore out from on foot your.
6 Hamkula mkate wowote, na wala hamkunywa divai yoyote au kinywaji chochote chenye ulevi, ili kwamba muweze kujua kuwa mimi ni Yahwe Mungu wenu.
Bread not you ate and wine and strong drink not you drank so that you may know that I [am] Yahweh God your.
7 Mlipokuja mahali hapa, Sihoni, mfalme wa Heshboni, na Ogu, mfalme wa Bashani, walikuja dhidi yetu kutupiga, na tukawapiga.
And you came to the place this and he came out Sihon [the] king of Heshbon and Og [the] king of Bashan to meet us for battle and we defeated them.
8 Tulichukua ardhi yao na kuwapa kama urithi Wareubeni, kwa Wagadi, na kwa nusu ya kabila ya Manase.
And we took land their and we gave it for an inheritance to the Reubenite[s] and to the Gadite[s] and to [the] half of [the] tribe of the Manassite[s].
9 Kwa hiyo shikilia maneno ya agano hili na kuyatenda, ili ufanikiwe katika kila kitu ufanyacho.
And you will keep [the] words of the covenant this and you will do them so that you may cause to prosper all that you will do!
10 Nyie wote, mnasimama leo, mbele ya Yahwe Mungu wenu; machifu wenu, makabila yenu, wazee wenu, na maafisa wenu – wanaume wote wa Israeli,
You [are] standing this day all of you before Yahweh God your chiefs your tribes your elders your and officials your every man of Israel.
11 watoto wenu, wake zenu, na wageni ambao wamo miongoni wa kambi yenu, kutoka kwa yule anayekata mbao zenu mpaka kwa yule atekaye maji.
Little one[s] your wives your and sojourner your who [is] in [the] midst of camps your from [the] cutter of wood your unto [the] drawer of water your.
12 Mpo hapa ili kwamba muingie katika agano la Yahwe Mungu wenu na katika kiapo ambacho Yahwe Mungu wako anafanya na wewe leo,
To pass on you in [the] covenant of Yahweh God your and in oath his which Yahweh God your [is] making with you this day.
13 ili kwamba awafanye leo kuwa watu wake, na kwamba aweze kuwa Mungu kwa ajili yako, kama alivyonena kwako, na kama alivyoapa kwa mababu zako, kwa Abrahamu, kwa Isaka na kwa Yakobo.
So as to establish you this day - of him to a people and he he will become for you God just as he spoke to you and just as he swore to ancestors your to Abraham to Isaac and to Jacob.
14 Kwa maana ninafanya agano hili na kiapo hiki sio na wewe tu –
And not with you to alone you I [am] making the covenant this and the oath this.
15 pamoja kila mtu aliyesimama hapa pamoja nasi leo mbele ya Yahwe Mungu wetu – bali na wale ambao hawapo pamoja nasi leo pia.
For with [the one] who there he here with us [is] standing this day before Yahweh God our and with [the one] who there not he here [is] with us this day.
16 Unajua jinsi tulivyoishi katika nchi ya Misri, na jinsi tulivyopenya miongoni mwa mataifa ambao uliwapita.
For you you know this: we dwelt in [the] land of Egypt and this: we passed in [the] midst of the nations which you passed through.
17 Mmeona sanamu zao zinazokera zilizotengenezwa kwa mbao na mawe, fedha na dhahabu, ambazo zilikuwa miongoni mwenu.
And you saw detestable things their and idols their wood and stone silver and gold which [were] with them.
18 Hakikisha hakuna kati yenu mwanamume, mwanamke, ukoo, au kabila ambaye moyo wake unamuacha Yahwe Mungu wetu leo, ili kwenda na kuabudu miungu ya mataifa hayo. Hakikisha hakuna kati yenu mzizi utakaozaa nyongo na pakanga.
Lest there [be] among you a man or a woman or a clan or a tribe who heart his [is] turning away this day from with Yahweh God our to go to serve [the] gods of the nations those lest there [be] among you a root bearing fruit poison and wormwood.
19 Wakati mtu huyo anaposikia maneno ya laana hii, atajifariji moyoni mwake na kusema, “Nitakuwa na amani, ingawa natembea katika ukaidi wa moyo wangu”. Hii itaangamiza ubichi pamoja na ukavu.
And it will be when hears he [the] words of the oath this and he will bless himself in heart his saying peace it will belong to me for in [the] stubbornness of heart my I walk so as to sweep away the watered [ground] with the thirsty [ground].
20 Yahwe hatamsamehe, lakini badala yake, hasira ya Yahwe na wivu wake utambanika mtu huyo, na laana zote zilizoandikwa katika kitabu hiki vitakuwa juu yake, na Yahwe ataliondoa jina lake kutoka mbinguni.
Not he will be willing Yahweh to forgive him for then it will smoke [the] anger of Yahweh and jealousy his on the man that and it will lie down on him every oath that is written in the book this and he will wipe out Yahweh name his from under the heavens.
21 Yahwe atamuweka kando kwa ajili ya maafa kutoka katika makabila yote ya Israeli, kwa kuzingatia laana zote za agano ambazo zimeandikwa katika kitabu hiki cha sheria.
And he will separate him Yahweh for harm from all [the] tribes of Israel according to all [the] oaths of the covenant that is written in [the] book of the law this.
22 Kizazi kifuatacho, watoto wako watakaoinuka baada yako, na mgeni atakayekuja kutoka nchi ya mbali, watazungumza watakapoona mapigo juu ya nchi hii na magonjwa ambayo Yahwe ameyafanya yawe –
And it will say the generation later children your who they will arise from after you and the foreigner who he will come from a land distant and they will see [the] plagues of the land that and diseases its which he has made sick Yahweh it.
23 na watakapoona kuwa nchi yote imekuwa salfa na chumvi ichomayo, ambapo hakuna kitu kipandwacho au kuzaa matunda, ambapo hapaoti mmea wowote, kama anguko la Sodoma na Gomora, Adma na Seboimu, ambayo Yahwe aliangamiza katika ghadhabu na hasira yake –
[is] sulfur And salt a burning waste all land its not it is sown and not it causes to grow and not it comes up in it any vegetation like [the] overthrow of Sodom and Gomorrah Admah (and Zeboiim *Qk) which he overthrew Yahweh in anger his and in rage his.
24 watasema kwa pamoja na mataifa mengine, “Kwa nini Yahwe amefanya hili katika nchi hii? Joto ya hasira hii kali inamaanisha nini?”
And they will say all the nations concerning what? has he done Yahweh thus to the land this why? [is] [the] heat of the anger great this.
25 Kisha watu watasema, “Ni kwa sababu walitelekeza agano la Yahwe, Mungu wa mababu zao, alilofanya nao alipowatoa kutoka Misri,
And people will say on that they forsook [the] covenant of Yahweh [the] God of ancestors their which he made with them when brought out he them from [the] land of Egypt.
26 na kwa sababu waliondoka na kutumikia miungu mingine na kuzisujudu, miungu ambayo hawakujiua na ambayo hakuwapatia.
And they went and they served gods other and they bowed down to them gods which not they had known them and not he had assigned to them.
27 Kwa hiyo hasira ya Yahwe imewaka dhidi ya nchi hii, ili kuleta juu yake laana zote zilizoandikwa katika kitabu hiki.
And it burned [the] anger of Yahweh on the land that to bring on it every curse that is written in the book this.
28 Yahwe amewang’oa kutoka nchini kwao kwa hasira, kwa ghadhanu, na kwa ghadhabu kali, na kuwatupa katika nchi nyingine, leo.
And he plucked up them Yahweh from on land their in anger and in rage and in wrath great and he threw out them to a land another as the day this.
29 Mambo ya siri ni ya Yahwe Mungu wetu pekee; lakini mambo yaliyofichuliwa ni ya kwetu milele pamoja na wazawa wetu, ili tufanye maneno yote ya sheria hii.
The hidden [things] [belong] to Yahweh God our and the revealed [things] [belong] to us and to descendants our until perpetuity to do all [the] words of the law this.

< Torati 29 >