< Torati 29 >

1 Haya ni maneno ambayo Yahwe alimuamuru Musa kuwaambia watu wa Israeli katika nchi ya Moabu, maneno ambayo yaliongezwa katika agano alilolifanya pamoja nao kule Horebu.
These are the words of the covenant which Jehovah commanded Moses to make with the children of Israel in the land of Moab, besides the covenant which he made with them in Horeb.
2 Musa aliwaita Waisraeli wote na kuwaambia, “Mmeona kila kitu ambacho Yahwe alifanya mbele ya macho yenu katika nchi ya Misri kwa Farao, kwa watumishi wake wote, na kwa nchi yake yote –
Moses called to all Israel, and said to them, You have seen all that Jehovah did before your eyes in the land of Egypt to Pharaoh, and to all his servants, and to all his land;
3 mateso makubwa ambayo macho yenu yaliona, ishara, pamoja na ile miujiza mikubwa.
the great trials which your eyes saw, the signs, and those great wonders:
4 Lakini mpaka leo Yahwe hajawapatia moyo wa kufahamu, macho ya kuona, au masikio ya kusikia.
but Jehovah has not given you a heart to know, and eyes to see, and ears to hear, to this day.
5 Nimewaongoza kwa miaka arobaini jangwani; mavazi yenu hayakuchakaa juu yenu, na ndala zenu hazikuchakaa miguuni mwenu.
I have led you forty years in the wilderness. Your clothes have not worn out on you, and your shoes have not worn out on your feet.
6 Hamkula mkate wowote, na wala hamkunywa divai yoyote au kinywaji chochote chenye ulevi, ili kwamba muweze kujua kuwa mimi ni Yahwe Mungu wenu.
You have not eaten bread, neither have you drunk wine or strong drink; that you may know that I am Jehovah your God.
7 Mlipokuja mahali hapa, Sihoni, mfalme wa Heshboni, na Ogu, mfalme wa Bashani, walikuja dhidi yetu kutupiga, na tukawapiga.
When you came to this place, Sihon the king of Heshbon, and Og the king of Bashan, came out against us to battle, and we struck them:
8 Tulichukua ardhi yao na kuwapa kama urithi Wareubeni, kwa Wagadi, na kwa nusu ya kabila ya Manase.
and we took their land, and gave it for an inheritance to the Reubenites, and to the Gadites, and to the half-tribe of the Manassites.
9 Kwa hiyo shikilia maneno ya agano hili na kuyatenda, ili ufanikiwe katika kila kitu ufanyacho.
Keep therefore the words of this covenant, and do them, that you may prosper in all that you do.
10 Nyie wote, mnasimama leo, mbele ya Yahwe Mungu wenu; machifu wenu, makabila yenu, wazee wenu, na maafisa wenu – wanaume wote wa Israeli,
You stand this day all of you before Jehovah your God; your heads, your tribes, your elders, and your officers, even all the men of Israel,
11 watoto wenu, wake zenu, na wageni ambao wamo miongoni wa kambi yenu, kutoka kwa yule anayekata mbao zenu mpaka kwa yule atekaye maji.
your little ones, your wives, and your foreigner who is in the midst of your camps, from the one who cuts your wood to the one who draws your water;
12 Mpo hapa ili kwamba muingie katika agano la Yahwe Mungu wenu na katika kiapo ambacho Yahwe Mungu wako anafanya na wewe leo,
that you may enter into the covenant of Jehovah your God, and into his oath, which Jehovah your God makes with you this day,
13 ili kwamba awafanye leo kuwa watu wake, na kwamba aweze kuwa Mungu kwa ajili yako, kama alivyonena kwako, na kama alivyoapa kwa mababu zako, kwa Abrahamu, kwa Isaka na kwa Yakobo.
so that he may establish you today as his people, and that he may your God, as he spoke to you and as he swore to your fathers, to Abraham, to Isaac, and to Jacob.
14 Kwa maana ninafanya agano hili na kiapo hiki sio na wewe tu –
Neither with you only do I make this covenant and this oath,
15 pamoja kila mtu aliyesimama hapa pamoja nasi leo mbele ya Yahwe Mungu wetu – bali na wale ambao hawapo pamoja nasi leo pia.
but with him who stands here with us this day before Jehovah our God, and also with him who is not here with us this day
16 Unajua jinsi tulivyoishi katika nchi ya Misri, na jinsi tulivyopenya miongoni mwa mataifa ambao uliwapita.
(for you know how we lived in the land of Egypt, and how we came through the midst of the nations through which you passed;
17 Mmeona sanamu zao zinazokera zilizotengenezwa kwa mbao na mawe, fedha na dhahabu, ambazo zilikuwa miongoni mwenu.
and you have seen their abominations, and their idols, wood and stone, silver and gold, which were among them);
18 Hakikisha hakuna kati yenu mwanamume, mwanamke, ukoo, au kabila ambaye moyo wake unamuacha Yahwe Mungu wetu leo, ili kwenda na kuabudu miungu ya mataifa hayo. Hakikisha hakuna kati yenu mzizi utakaozaa nyongo na pakanga.
lest there should be among you man, or woman, or family, or tribe, whose heart turns away this day from Jehovah our God, to go to serve the gods of those nations; lest there should be among you a root that bears gall and wormwood;
19 Wakati mtu huyo anaposikia maneno ya laana hii, atajifariji moyoni mwake na kusema, “Nitakuwa na amani, ingawa natembea katika ukaidi wa moyo wangu”. Hii itaangamiza ubichi pamoja na ukavu.
and it happen, when he hears the words of this curse, that he bless himself in his heart, saying, "I shall have peace, though I walk in the stubbornness of my heart, to destroy the moist with the dry."
20 Yahwe hatamsamehe, lakini badala yake, hasira ya Yahwe na wivu wake utambanika mtu huyo, na laana zote zilizoandikwa katika kitabu hiki vitakuwa juu yake, na Yahwe ataliondoa jina lake kutoka mbinguni.
God will not be willing to forgive him, but then the anger of Jehovah and his jealousy will burn against that man, and every curse that is written in this book shall rest on him, and Jehovah will blot out his name from under heaven.
21 Yahwe atamuweka kando kwa ajili ya maafa kutoka katika makabila yote ya Israeli, kwa kuzingatia laana zote za agano ambazo zimeandikwa katika kitabu hiki cha sheria.
Jehovah will set him apart to evil out of all the tribes of Israel, according to all the curses of the covenant that is written in this book of the law.
22 Kizazi kifuatacho, watoto wako watakaoinuka baada yako, na mgeni atakayekuja kutoka nchi ya mbali, watazungumza watakapoona mapigo juu ya nchi hii na magonjwa ambayo Yahwe ameyafanya yawe –
The generation to come, your children who shall rise up after you, and the foreigner who shall come from a far land, shall say, when they see the plagues of that land, and the sicknesses with which Jehovah has made it sick;
23 na watakapoona kuwa nchi yote imekuwa salfa na chumvi ichomayo, ambapo hakuna kitu kipandwacho au kuzaa matunda, ambapo hapaoti mmea wowote, kama anguko la Sodoma na Gomora, Adma na Seboimu, ambayo Yahwe aliangamiza katika ghadhabu na hasira yake –
and that the whole land of it is sulfur, salt, and burning, that it is not sown, nor bears, nor any grass grows in it, like the overthrow of Sodom and Gomorrah, Admah and Zeboiim, which Jehovah overthrew in his anger, and in his wrath:
24 watasema kwa pamoja na mataifa mengine, “Kwa nini Yahwe amefanya hili katika nchi hii? Joto ya hasira hii kali inamaanisha nini?”
even all the nations shall say, "Why has Jehovah done thus to this land? What does the heat of this great anger mean?"
25 Kisha watu watasema, “Ni kwa sababu walitelekeza agano la Yahwe, Mungu wa mababu zao, alilofanya nao alipowatoa kutoka Misri,
Then men shall say, "Because they forsook the covenant of Jehovah, the God of their fathers, which he made with them when he brought them forth out of the land of Egypt,
26 na kwa sababu waliondoka na kutumikia miungu mingine na kuzisujudu, miungu ambayo hawakujiua na ambayo hakuwapatia.
and went and served other gods, and worshiped them, gods that they did not know, and that he had not given to them:
27 Kwa hiyo hasira ya Yahwe imewaka dhidi ya nchi hii, ili kuleta juu yake laana zote zilizoandikwa katika kitabu hiki.
therefore the anger of Jehovah was kindled against this land, to bring on it all the curse that is written in this book;
28 Yahwe amewang’oa kutoka nchini kwao kwa hasira, kwa ghadhanu, na kwa ghadhabu kali, na kuwatupa katika nchi nyingine, leo.
and Jehovah rooted them out of their land in anger, and in wrath, and in great indignation, and cast them into another land, as at this day."
29 Mambo ya siri ni ya Yahwe Mungu wetu pekee; lakini mambo yaliyofichuliwa ni ya kwetu milele pamoja na wazawa wetu, ili tufanye maneno yote ya sheria hii.
The secret things belong to Jehovah our God; but the things that are revealed belong to us and to our children forever, that we may do all the words of this law.

< Torati 29 >