< Torati 25 >

1 Iwapo kutakuwa na malumbano kati ya wanaume na wakaenda mahakamani, na waamuzi wakawahukumu, basi watamwachilia mtakatifu na kumhukumu muovu.
If there is a controversy between men, and they come to judgment, and the judges judge them; then they shall justify the upright, and condemn the wicked.
2 Iwapo mwanamume mwenye hatia anastahili kupigwa, basi muamuzi atamfanya alale chini na kupigwa mbele zake kwa idadi iliyoamriwa kulingana na kosa lake.
It shall be, if the wicked man is worthy to be beaten, that the judge shall cause him to lie down, and to be beaten before his face, according to his wickedness, by number.
3 Muamuzi anaweza kumpatia mapigo arobaini, lakini hapaswi kuvuka idadi hiyo; kwa maana akivuka idadi hiyo na kumpiga kwa mapigo mengi zaidi, basi Muisraeli mwenzako atakuwa kaaibishwa mbele ya macho yenu.
He may sentence him to no more than forty stripes. He shall not give more; lest, if he should give more, and beat him more than that many stripes, then your brother will be degraded in your sight.
4 Haupaswi kumfunga punda wako pua na mdomo anapokuwa akilima shamba lako.
You shall not muzzle the ox when he treads out the grain.
5 Iwapo kaka wanaishi pamoja na mmoja wao akafariki bila kuwa na mwana, basi mke wa marehemu hatakiwi kuolewa na mtu nje ya familia. Badala yake, kaka yake mumewe anapaswa kulala naye na kumchukua kuwa mke wake na kutekeleza wajibu wa kaka wa mume kwake.
If brothers dwell together, and one of them dies, and has no son, the wife of the dead shall not be married outside to a stranger. Her husband’s brother shall go in to her, and take her as his wife, and perform the duty of a husband’s brother to her.
6 Hii ni kwamba mtoto wa kwanza atakayezaliwa arithi chini ya jina la kaka yake mwanamume aliyefariki, ili jina lake lisiangamie ndani ya Israeli.
It shall be that the firstborn whom she bears shall succeed in the name of his brother who is dead, that his name not be blotted out of Israel [God prevails].
7 Lakini kama mwanamume hataki kumchukua mke wa kaka yake awe wake, basi mke wa kaka yake anapaswa kwenda malangoni mpaka kwa wazee na kusema, “Kaka wa mume wangu amekataa kuwajibika kwa niaba ya jina la kaka yake humu Israeli; hataki kufanya wajibu wa kaka wa mume kwangu”.
If the man does not want to take his brother’s wife, then his brother’s wife shall go up to the gate to the elders, and say, “My husband’s brother refuses to raise up to his brother a name in Israel [God prevails]. He will not perform the duty of a husband’s brother to me.”
8 Kisha wazee wa mji wake wanapaswa kumuita na kuzungumza naye. Lakini tuseme atasisitiza na kusema, “Sitaki kumchukua”.
Then the elders of his city shall call him, and speak to him: and if he stands and says, “I don’t want to take her;”
9 Basi mke wa kaka yake anatakiwa kuja kwake mbele ya wazee, kumvua ndara zake miguuni mwake, na kumtemea usoni. Anapaswa kumjibu na kusema, “Hivi ndivyo kinachofanyika kwa mwanamume asiyetaka kujenga nyumba ya kaka yake”.
then his brother’s wife shall come to him in the presence of the elders, and loose his shoe from off his foot, and spit in his face. She shall answer and say, “So shall it be done to the man who does not build up his brother’s house.”
10 Jina lake Israeli litaitwa, “Nyumba ya mtu aliyevuliwa ndara zake”.
His name shall be called in Israel [God prevails], “The house of him who had his shoe removed.”
11 Iwapo wanamume wamepigana wao kwa wao, na mke wa mmoja wao kaja kumkomboa mumewe dhidi ya yule aliyempiga, naye akanyosha mkono wake na kumshika sehemu za siri,
When men strive against each other, and the wife of one draws near to deliver her husband out of the hand of him who strikes him, and puts out her hand, and takes him by his private parts,
12 basi unapaswa kuukata mkono yake; jicho lako halipaswi kuwa na huruma.
then you shall cut off her hand. Your eye shall have no pity.
13 Haupaswi kuwa na mizani ya uzito tofauti katika mfuko wako, mkubwa na mdogo.
You shall not have in your bag diverse weights, one heavy and one light.
14 Hautakiwi kuwa na vipimo tofauti ndani ya nyumba yako, vikubwa na vidogo.
You shall not have in your house diverse measures, one large and one small.
15 Unatakiwa kuwa na uzito kamili na wa haki; unatakiwa kuwa na vipimo kamili na vya haki, ili siku zako ziwe ndefu katika nchi ambayo Yahwe Mungu wako anakupatia.
You shall have a perfect and just weight. You shall have a perfect and just measure, that your days may be long in the land which Adonai your God gives you.
16 Kwa maana wote wanaofanya vitu hivi, wote wanaovunja haki, ni chukizo kwa Yahwe Mungu wako.
For all who do such things, all who deal dishonestly, are an abomination to Adonai your God.
17 Kumbuka ni jambo gani Amaleki alichofanya kwako barabarani ulipokuwa ukitoka Misri,
Remember what Amalek did to you by the way as you came out of Egypt [Abode of slavery];
18 jinsi alivyokutana na wewe barabarani na kuwashambulia kati yenu kwa nyuma, wale waliokuwa wamelegea nyuma, mlipokuwa dhaifu na kuchoka, hakumheshimu Mungu.
how he met you by the way, and struck the rearmost of you, all who were feeble behind you, when you were faint and weary; and he didn’t fear God.
19 Kwa hiyo, Yahwe Mungu wako atakapowapa pumziko kutoka kwa maadui zako kila sehemu, katika nchi ambayo Yahwe Mungu wako anawapatia kumiliki kama urithi, hautakiwi kusahau kuwa unapaswa kufuta kumbukumbu ya Waamaleki chini ya mbingu.
Therefore it shall be, when Adonai your God has given you rest from all your enemies all around, in the land which Adonai your God gives you for an inheritance to possess it, that you shall blot out the memory of Amalek [Man who licks up] from under the sky. You shall not forget.

< Torati 25 >