< Torati 23 >

1 Mwanamume aliyejeruhiwa kwa kupondwa au kukatwa haruhusiwi kuingia katika kusanyiko la Yahwe.
He that is crushed or maimed in his privy parts shall not enter into the assembly of the LORD.
2 Mwana haramu haruhusiwi kuwa miongoni mwa kusanyiko la Yahwe; kutoka hadi kizazi cha kumi cha uzao wake, hakuna kati yao anatakiwa kuwa kwenye kusanyiko la Yahwe.
A bastard shall not enter into the assembly of the LORD; even to the tenth generation shall none of his enter into the assembly of the LORD.
3 Muamori au Mmoabu haruhusiwi kuwa miongoni mwa kusanyiko la Yahwe; kutoka hadi kizazi cha kumi cha uzao wake, hakuna kati yao anatakiwa kuwa kwenye kusanyiko la Yahwe.
An Ammonite or a Moabite shall not enter into the assembly of the LORD; even to the tenth generation shall none of them enter into the assembly of the LORD for ever;
4 Hii ni kwa sababu hawakukutana nanyi kwa mkate na maji barabarani mlipokuwa mmetoka nje ya Misri, na kwa sababu walimkodisha Balaamu mwana wa Beoro kutoka Pethoro kule Aramu Naharaimu, awalaani.
because they met you not with bread and with water in the way, when ye came forth out of Egypt; and because they hired against thee Balaam the son of Beor from Pethor of Aram-naharaim, to curse thee.
5 Lakini Yahwe Mungu wako hakumsikiliza Balaamu; badala yake, Yahwe Mungu wako aligeuza laana kuwa baraka kwenu, kwa sababu Yahwe Mungu wako aliwapenda.
Nevertheless the LORD thy God would not hearken unto Balaam; but the LORD thy God turned the curse into a blessing unto thee, because the LORD thy God loved thee.
6 Hamtakiwi kutafuta amani au mafanikio yao, katika siku zenu zote.
Thou shalt not seek their peace nor their prosperity all thy days for ever.
7 Hutakiwi kumchukia Muedomi, kwa maana ni kaka yako; hutakiwi kumchukia Mmisri, kwa maana ulikuwa mgeni katika nchi yake.
Thou shalt not abhor an Edomite, for he is thy brother; thou shalt not abhor an Egyptian, because thou wast a stranger in his land.
8 Wazawa wa kizazi cha tatu wanaozaliwa kwao wanaweza kuwa katika kusanyiko la Yahwe.
The children of the third generation that are born unto them may enter into the assembly of the LORD.
9 Utakapotembea kijeshi dhidi ya maadui zako, basi unapaswa kujitenga na kila aina ya uovu.
When thou goest forth in camp against thine enemies, then thou shalt keep thee from every evil thing.
10 Iwapo miongoni mwenu kuna mwanamume ambaye sio msafi kwa sababu ya jambo lililofanyika kwake usiku, basi anatakiwa atoke nje ya kambi ya jeshi; hatakiwi kurudi kambini.
If there be among you any man, that is not clean by reason of that which chanceth him by night, then shall he go abroad out of the camp, he shall not come within the camp.
11 Jioni ikifika, anatakiwa ajiogeshe kwa maji; na jua likizama atarudi ndani kambini.
But it shall be, when evening cometh on, he shall bathe himself in water; and when the sun is down, he may come within the camp.
12 Pia unatakiwa kuwa na eneo nje ya kambi ambayo utakwenda;
Thou shalt have a place also without the camp, whither thou shalt go forth abroad.
13 na utakuwa na kitu katika zana zako cha kuchimbia; utakapochuchumaa kujisaidia, unapaswa kuchimbia nacho na kisha kurudishia udongo na kufunika kile kilichotoka kwako.
And thou shalt have a paddle among thy weapons; and it shall be, when thou sittest down abroad, thou shalt dig therewith, and shalt turn back and cover that which cometh from thee.
14 Kwa maana Yahwe Mungu wako anatembea miongoni mwa kambi yenu kuwapa ushindi na kuwapa maadui zenu mkononi mwenu. Kwa hiyo kambi yenu lazima iwe takatifu, ili kwamba asione kitu chochote kichafu miongoni mwenu na kuwaacha.
For the LORD thy God walketh in the midst of thy camp, to deliver thee, and to give up thine enemies before thee; therefore shall thy camp be holy; that He see no unseemly thing in thee, and turn away from thee.
15 Hutakiwi kumrudishia bwana mtumwa aliyetoroka kwake.
Thou shalt not deliver unto his master a bondman that is escaped from his master unto thee;
16 Mruhusu aishi pamoja nawe, katika mji wowote atakaochagua. Usimuonee.
he shall dwell with thee, in the midst of thee, in the place which he shall choose within one of thy gates, where it liketh him best; thou shalt not wrong him.
17 Hapatakiwi kuwa na kahaba wa kidhehebu miongoni mwa mabinti wa Israeli, na wala hapatakiwi kuwa na kahaba wa kidhehebu miongoni mwa wana wa kiume wa Israeli.
There shall be no harlot of the daughters of Israel, neither shall there be a sodomite of the sons of Israel.
18 Hautakiwi kuleta mshahara wa kahaba au mshahara wa mbwa katika nyumba ya Yahwe Mungu wako kwa kiapo chochote; kwa maana vyote hivi na machukizo mbele ya Yahwe Mungu wako.
Thou shalt not bring the hire of a harlot, or the price of a dog, into the house of the LORD thy God for any vow; for even both these are an abomination unto the LORD thy God.
19 Hutakiwi kumkopesha Muisraeli mwenzako kwa riba – riba ya fedha, riba ya chakula, au riba ya kitu chochote kinachokopeshwa kwa riba.
Thou shalt not lend upon interest to thy brother: interest of money, interest of victuals, interest of any thing that is lent upon interest.
20 Kwa mgeni unaweza kukopesha kwa riba; lakini kwa Muisraeli mwenzako haupaswi kukopesha kwa riba, ili kwamba Yahwe Mungu wako aweze kukubariki katika kila jambo uwekalo mkono wako, katika nchi ambayo mnaenda kumiliki.
Unto a foreigner thou mayest lend upon interest; but unto thy brother thou shalt not lend upon interest; that the LORD thy God may bless thee in all that thou puttest thy hand unto, in the land whither thou goest in to possess it.
21 Unapofanya kiapo kwa Yahwe Mungu wako, haupaswi kukawia kuikamilsha, kwa maana Yahwe Mungu wako hakika atadai kiapo hicho; itakuwa dhambi kako usipokamilisha.
When thou shalt vow a vow unto the LORD thy God, thou shalt not be slack to pay it; for the LORD thy God will surely require it of thee; and it will be sin in thee.
22 Lakini iwapo utajizuia kutoa kiapo, haitakuwa dhambi kwako.
But if thou shalt forbear to vow, it shall be no sin in thee.
23 Kile ambacho kimetoka kinywani mwako unapaswa kukifuata na kukitekeleza; kulingana na kiapo ulichotamka kwa Yahwe Mungu wako, chochote ulichotamka kwa hiari kwa kinywa chako.
That which is gone out of thy lips thou shalt observe and do; according as thou hast vowed freely unto the LORD thy God, even that which thou hast promised with thy mouth.
24 Utakapokwenda katika shamba la mizabibu la jirani yako, unatakiwa kula mizabibu idadi yoyote unayotaka, lakini hautakiwi kuhifadhi yoyote katika kikapu chako.
When thou comest into thy neighbour's vineyard, then thou mayest eat grapes until thou have enough at thine own pleasure; but thou shalt not put any in thy vessel.
25 Utakapokwenda katika shamba la zao lililoiva la jirani yako, unaweza kuvuna kichwa cha mavuno kwa mkono wako, lakini haupaswi kutumia mundu kuvuna zao lililoiva la jirani yako.
When thou comest into thy neighbour's standing corn, then thou mayest pluck ears with thy hand; but thou shalt not move a sickle unto thy neighbour's standing corn.

< Torati 23 >