< Torati 22 >

1 Hautakiwi kumtazama ng’ombe au kondoo wa Muisraeli mwenzako akikosea njia na ukajificha kwao; hakika unapaswa kuwarejesha kwake.
اگر گاو یا گوسفند برادر خود را گم شده بینی، از او رومگردان. آن را البته نزدبرادر خود برگردان.۱
2 Iwapo Muisraeli mwenzako hayupo karibu nawe, au kama haumfahamu, basi unapaswa kumleta mnyama huyo nyumbani kwako, na lazima uwe naye mpaka pale mwenyewe atakapomtafuta, na kisha lazima umrejeshee mwenyewe.
و اگر برادرت نزدیک تونباشد یا او را نشناسی، آن را به خانه خود بیاور ونزد تو بماند، تا برادرت آن را طلب نماید، آنگاه آن را به او رد نما.۲
3 Unapaswa kufanya vivyo hivyo kwa punda wake; unapaswa kufanya vivyo hivyo na vazi lake; unapaswa kufanya vivyo hivyo kwa kila kitu alichopoteza Muisraeli mwenzako, kitu chochote alichopoteza na ukakipata; hautakiwi kujificha.
و به الاغ او چنین کن و به لباسش چنین عمل نما و به هر چیز گمشده برادرت که از او گم شود و یافته باشی چنین عمل نما، نمی توانی از او روگردانی.۳
4 Haupaswi kumwona punda wa Muisraeli mwenzako au ng’ombe wake kaanguka chini barabarani na kujificha dhidi yao; hakika unapaswa kumsaidia kumwinua tena.
اگر الاغ یا گاو برادرت را در راه افتاده بینی، از آن رومگردان، البته آن را با او برخیزان.۴
5 Mwanamke hatakiwi kuvaa kinachokusudiwa kwa mwanamume, vilevile mwanamume hapaswi kuvaa mavazi ya mwanamke; kwa maana yeyote afanyaye vitu hivi ni chukizo kwa Yahwe Mungu wako.
متاع مرد بر زن نباشد، و مرد لباس زن رانپوشد، زیرا هر‌که این کار را کند مکروه یهوه خدای توست.۵
6 Iwapo kiota cha ndege kikaonekana barabarani mbele yako, kwenye mti wowote au juu ya ardhi, kikiwa na makinda ya ndege au mayai ndani mwake, na mama yao akiwa juu yao au juu ya mayai, haupaswi kumchukua mama pamoja na makinda au mayai yake.
اگر اتفاق آشیانه مرغی در راه به نظر تو آید، خواه بر درخت یا بر زمین، و در آن بچه‌ها یاتخمها باشد، و مادر بر بچه‌ها یا تخمها نشسته، مادر را با بچه‌ها مگیر.۶
7 Hakika unapaswa kumuacha mama aende zake, ila makinda yake unaweza kuyachukua. Tii amri hii ili uenende vyema, na siku zako ziweze kurefushwa.
مادر را البته رها کن وبچه‌ها را برای خود بگیر، تا برای تو نیکو شود وعمر دراز کنی.۷
8 Ujengapo nyumba mpya, basi unapaswa kujenga kitalu kwa ajili ya paa yako ili usilete damu juu ya nyumba yako mtu akianguka kutoka pale.
چون خانه نو بنا کنی، بر پشت بام خوددیواری بساز، مبادا کسی از آن بیفتد و خون برخانه خود بیاوری.۸
9 Haupaswi kupanda shamba lako la mizabibu kwa mbegu mbili, ili kwamba mavuno yote yasichukuliwe na sehemu takatifu, mbegu uliyoipanda pamoja na matunda ya mzabibu.
در تاکستان خود دو قسم تخم مکار، مباداتمامی آن، یعنی هم تخمی که کاشته‌ای و هم محصول تاکستان، وقف شود.۹
10 Haupaswi kulimia ng’ombe na punda kwa pamoja.
گاو و الاغ را با هم جفت کرده، شیار منما.۱۰
11 Haupaswi kuvaa kitambaa kilichotengenezwa kwa sufu na kitani kwa pamoja.
پارچه مختلط از پشم و کتان با هم مپوش.۱۱
12 Unapaswa kutengeneza pindo katika pembe nne za nguo unayoivaa.
بر چهار گوشه رخت خود که خود را به آن می‌پوشانی، رشته‌ها بساز.۱۲
13 Iwapo mwanamume kachukua mke, kisha kalala naye, na baadae kumchukia,
اگر کسی برای خود زنی گیرد و چون بدودرآید، او را مکروه دارد.۱۳
14 na kisha kumtuhumu kwa vitu vya aibu na kumharibia sifa yake kwa kusema, “Nilimchukua huyu mwanamke, lakini nilipomkaribia sikukuta ushahidi waubikra kwake”.
و اسباب حرف بدونسبت داده، از او اسم بد شهرت دهد و گوید این زن را گرفتم و چون به او نزدیکی نمودم، او را باکره نیافتم.۱۴
15 Kisha baba na mama mzazi wa binti wanatakiwa kupeleka ushahidi wa ubikra wake kwa wazee mlangoni mwa mji.
آنگاه پدر یا مادر آن دختر علامت بکارت دختر برداشته، نزد مشایخ شهر نزددروازه بیاورند.۱۵
16 Baba wa binti anapaswa kuwaambia wazee, “nilimpatia binti yangu kwa mwanamume huyu awe mkewe, naye anamchukia.
و پدر دختر به مشایخ بگوید: «دختر خود را به این مرد به زنی داده‌ام، و از اوکراهت دارد،۱۶
17 Tazama, amemtuhumu na vitu vya aibu na kusema, “Sikukuta ushahidi wa ubikra kwa binti yako”. Lakini ushahidi huu hapa wa ubikra wa binti yangu”. Kisha watatandaza shuka mbele ya wazee wa mji.
و اینک اسباب حرف بدو نسبت داده، می‌گوید دختر تو را باکره نیافتم، و علامت بکارت دختر من این است.» پس جامه را پیش مشایخ شهر بگسترانند.۱۷
18 Wazee wa mji wanapaswa kumchukua mwanamume huyo na kumuadhibu;
پس مشایخ آن شهرآن مرد را گرفته، تنبیه کنند.۱۸
19 nao wanapaswa kumtoza faini ya shekeli mia moja ya fedha, na kumpatia baba wa binti, kwa sababu mwanamume kasababisha sifa mbaya kwa bikra wa Israeli. Binti huyu anapaswa kuwa mke wake; mwanamume huyu hatakiwi kumfukuza katika siku zake zote.
و او را صد مثقال نقره جریمه نموده، به پدر دختر بدهند چونکه برباکره اسرائیل بدنامی آورده است. و او زن وی خواهد بود و در تمامی عمرش نمی تواند او رارها کند.۱۹
20 Ila kama jambo hili ni la kweli, kwamba ushahidi wa bikra ya binti haukupatikana,
لیکن اگر این سخن راست باشد، و علامت بکارت آن دختر پیدا نشود،۲۰
21 basi wanapaswa kumpeleka binti mlangoni kwa baba yake, na kisha wanamume wa mji wake wanatakiwa kumpiga kwa mawe hadi afe, kwa sababu amefanya jambo la aibu katika Israeli, kwa kutenda kama kahaba chini ya nyumba ya baba yake, nanyi mtakuwa mmeondoa uovu miongoni mwenu.
آنگاه دختر را نزددر خانه پدرش بیرون آورند، و اهل شهرش او رابا سنگ سنگسار نمایند تا بمیرد، چونکه در خانه پدر خود زنا کرده، در اسرائیل قباحتی نموده است. پس بدی را از میان خود دور کرده‌ای.۲۱
22 Iwapo mwanamume kakutwa analala na mwanamke ambaye ni mke wa mtu, basi wote wanapaswa kufa, mwanamume aliyelala na mwanamke pamoja na mwanamke mwenyewe; nanyi mtakuwa mmeondoa uovu miongoni mwenu.
اگر مردی یافت شود که با زن شوهرداری همبستر شده باشد، پس هر دو یعنی مردی که بازن خوابیده است و زن، کشته شوند. پس بدی رااز اسرائیل دور کرده‌ای.۲۲
23 Iwapo kuna msichana bikra, ambaye amechumbiwa na mwanamume, kisha mwanamume mwingine kamkuta mjini na kulala naye,
اگر دختر باکره‌ای به مردی نامزد شود ودیگری او را در شهر یافته، با او همبستر شود،۲۳
24 wachukueni wote wawili malangoni mwa mji, na kuwapiga mawe. Unapaswa kumpiga msichana mawe, kwa sababu hakupaza sauti kuomba msaada, ingawa alikuwa ndani ya mji. Unapaswa kumpiga mwanamume mawe, kwa sababu amemwingilia mke wa jirani yake; nanyi mtakuwa mmeondoa uovu miongoni mwenu
پس هر دو ایشان را نزد دروازه شهر بیرون آورده، ایشان را با سنگها سنگسار کنند تا بمیرند؛ اما دختر را چونکه در شهر بود و فریاد نکرد، ومرد را چونکه زن همسایه خود را ذلیل ساخت، پس بدی را از میان خود دور کرده‌ای.۲۴
25 Lakini kama mwanamume amemkuta msichana aliyechumbiwa shambani, na kama akamkamata na kulala naye, basi mwanamume pekee aliyelala naye ndiye lazima afe.
اما اگر آن مرد دختری نامزد را در صحرایابد و آن مرد به او زور آورده، با او بخوابد، پس آن مرد که با او خوابیده، تنها کشته شود.۲۵
26 Lakini kwake msichana msifanye chochote; hakuna dhambi inayostahili kifo kwake msichana. Kwa maana suala hili ni kama mwanamume amshambuliapo jirani yake na kumuua.
و اما بادختر هیچ مکن زیرا بر دختر، گناه مستلزم موت نیست، بلکه این مثل آن است که کسی بر همسایه خود برخاسته، او را بکشد.۲۶
27 Kwa maana alimkuta shambani; msichana huyu aliyechumbiwa alipaza sauti, lakini hapakuwa na mtu wa kumuokoa.
چونکه او را درصحرا یافت و دختر نامزد فریاد برآورد و برایش رهاننده‌ای نبود.۲۷
28 Iwapo mwanamume amemkuta msichana ambaye ni bikra lakini hajachumbiwa, na kama akamkamata na kulala naye, na kama wakagundulika,
و اگر مردی دختر باکره‌ای را که نامزدنباشد بیابد و او را گرفته، با او همبستر شود وگرفتار شوند،۲۸
29 basi mwanamume aliyelala naye lazima atoe shekeli hamsini za fedha kwa baba wa msichana, naye lazima awe mke wake, kwa sababu amemdhalilisha. Hatakiwi kumfukuza katika siku zake zote.
آنکه آن مرد که با او خوابیده است پنجاه مثقال نقره به پدر دختر بدهد و آن دختر زن او باشد، چونکه او را ذلیل ساخته است و در تمامی عمرش نمی تواند او را رها کند.۲۹
30 Mwanamume hapaswi kumchukua mke wa baba yake kama wake; hatakiwi kuchukua haki za ndoa za baba yake.
هیچ‌کس زن پدر خود را نگیرد و دامن پدرخود را منکشف نسازد.۳۰

< Torati 22 >