< Torati 19 >

1 Wakati Yahwe Mungu wenu anayafutilia mbali mataifa, yale ambayo Yahwe Mungu wenu anawapa nchi yao, na wakati mnakuja kwao na kuishi katika miji yao na nyumba,
When Yahweh your God cuts off the nations, those whose land Yahweh your God is giving you, and when you come after them and live in their cities and houses,
2 mnapaswa kuchagua miji mitatu kwa ajili yenu katikati mwa nchi yenu ambayo Yahwe Mungu anawapa kuimiliki.
you must select three cities for yourself in the middle of your land that Yahweh your God is giving you to possess.
3 Mnapaswa kujenga barabara na kugawa mipaka ya nchi yenu katika maeneo matatu, nchi ambayo Yahwe Mungu wenu anafanya kuimiliki, ili kwamba kila mmoja anayeua mtu mwingine apate kukimbia hapo.
You must build a road and divide the borders of your land into three parts, the land that Yahweh your God is causing you to inherit, so that everyone who kills another person may flee there.
4 Hii ni sheria kwa ajili ya mtu anayeua mwingine na anayekimbilia huko kuishi: yeyote auae jirani yake bila kujua, na hapo awali hakumchukia-
This is the law for the one who kills another and who flees there to live—anyone who kills his neighbor unintentionally, and did not previously hate him.
5 kama wakati mtu aingiapo katika msitu pamoja na jirani yake kukata kuni, na mkono wake ukata mti chini kwa shoka, na kichwa uteleza kutoka kwenye mpini na kumpiga jirani yake mpaka akafa- basi mtu huyu anapaswa kukimbilia katika moja ya miji hii na kuishi.
For example, if a man goes into the forest with his neighbor to cut wood, and his chops with the ax to cut down a tree, and the ax head slips off of the handle and strikes his neighbor and kills him—then that man must flee to one of these cities and save his life.
6 Vinginevyo damu ya mlipiza kisasi atamfuata yeye aliyetoa uhai, na kwa hasira kali anampita kwa sababu ilikuwa safari ndefu. Na anampiga na kumuua, ijapokuwa mtu huyo akustahili kufa; na hata akustahili adhabu ya kifo kwa sababu hakumchukia jirani yake kabla hili halijatokea.
Otherwise the avenger of blood might go after the one who took a life, and in the heat of his anger overtake him, if the distance is too great, strike him and kill him, even though that man did not deserve to die, since he had not hated his neighbor in the past.
7 Basi sasa ninakuamuru kuchagua miji mitatu kwa ajili yako.
Therefore I command you to select three cities for yourself.
8 Kama Yahwe Mungu wenu apanua mipaka yenu, kama alivyoapa kwa mababu zenu kufanya, na kuwapa nchi yote ambayo amewaahadia kuwapa mababu zenu;
If Yahweh your God enlarges your borders, as he has sworn to your ancestors to do, and gives you all the land that he promised to give to your ancestors;
9 kama mnazishika amri hizi zote kuzifanya, ambazo ninakuamuru leo- amri za kumpenda Yahwe Mungu wenu na daima kutembea katika njia zake, basi mnapaswa kuongeza miji mitatu zaidi kwa ajili yenu, isipokuwa ile mitatu.
if you keep all these commandments to do them, which I am commanding you today—commandments to love Yahweh your God and to always walk in his ways, then you must add three more cities for yourself, besides these three.
10 Fanya hivi ili kwamba damu isiyo na hatia isimwangwe katikati ya nchi ambayo Yahwe Mungu wenu anawapa kwa ajili ya urithi, ili kwamba pasiwepo hatia ya damu kwenu.
Do this so that innocent blood is not shed in the midst of the land that Yahweh your God is giving you for as an inheritance, so that no bloodguilt may be on you.
11 Lakini kama yeyote anamchukia jirani yake, uongo unamsubiri, uinuka dhidi yake, na majeraha ya kufa kwake ili kwamba anakufa, na kama basi anakimbia katika moja ya miji hii-
But if anyone hates his neighbor, lies in wait for him, rises up against him, and mortally wounds him so that he dies, and if he then flees into one of these cities—
12 basi wazee wa mji wake wanapaswa kumtoa na kumrudisha toka huko, na kumkabizi katika mkono wa ndugu mhusika, ili kwamba amuue.
then the elders of his city must send and bring him back from there, and turn him over into the hand of the responsible relative, so that he may die.
13 Jicho lako halipaswi kumuonea huruma; badala yake; unapaswa kuondoa hatia ya damu kutoka Israel, ili kwamba iwe vizuri kwako.
Your eye must not pity him; instead, you must eradicate the bloodguilt from Israel, that it may go well with you.
14 Haupaswi kuondoa alama ya jirani yako ambayo wameweka katika eneo muda mrefu, katika urithi wako ambao utarithi, katika nchi ambayo Yahwe Mungu wako anakupa kumiliki.
You must not remove your neighbor's landmark that they set in place a long time ago, in your inheritance that you will inherit, in the land that Yahweh your God is giving you to possess.
15 Shahidi moja peke hapaswi kuinuka dhidi ya mtu kwa ajili ya uovu wowote, au kwa ajili ya dhambi yoyote, katika jambo lolote ambalo amefanya dhambi; kwa kinywa cha mashahidi wawili, au kwa kinywa cha mashahidi watatu, kunapaswa jambo lolote lilithibitishwe.
One sole witness must not rise up against a man for any iniquity, or for any sin, in any matter that he sins; at the mouth of two witnesses, or at the mouth of three witnesses, must any matter be confirmed.
16 Kama ushuhuda wa mtu asiye na haki anainua dhidi ya mtu yeyote kushuhudia dhidi yake kwa mambo mabaya.
Suppose that an unrighteous witness rises up against any man to testify against him of wrongdoing.
17 Basi watu wote wawili, mmoja kati ya yule utata upo, anapaswa kusimama mbele ya Yahwe, mbele ya makuhani na waamuzi ambao wanatumika siku hizo.
Then both men, the ones between whom the controversy exists, must stand before Yahweh, before the priests and the judges who serve in those days.
18 Waamuzi wanapaswa kuchunguza kwa uangalifu; ona, kama ushahidi ni ushahidi wa uongo na umeshuhudiwa kwa uongo dhidi ya ndugu yake,
The judges must make diligent inquiries; see, if the witness is a false witness and has testified falsely against his brother,
19 basi unapaswa kufanya kwake, kama alivyokusudia kufanya kwa ndugu yake, na utaondoa uovu kutoka miongoni mwenu.
then must you do to him, as he had wished to do to his brother; and you will remove the evil from among you.
20 Basi wale wanaobaki watasikia na kuogopa, na kuanzia hapo na kuendelea hawatafanya tena aina ya ouvu miongoni mwao.
Then those who remain will hear and fear, and will from then on commit no longer any such evil among you.
21 Macho yako hapaswi kuona huruma; maisha yatalipa kwa maisha, jicho kwa jicho, jino kwa jino, mkono kwa mkono, mguu kwa mguu.
Your eyes must not pity; life will pay for life, eye for eye, tooth for tooth, hand for hand, foot for foot.

< Torati 19 >