< Torati 18 >

1 Makuhani, ambao ni Walawi, na makabila yote ya Lawi, hayatakuwa na mgao wala urithi pamoja na Israel; wanapaswa kula dhabihu ya Yahwe iliyotengenezwa kwa moto kama urithi wao.
Not it will belong to the priests the Levites all [the] tribe of Levi a portion and an inheritance with Israel [the] fire offerings of Yahweh and inheritance his they will eat!
2 Hawatakuwa na urithi miongoni mwa ndugu zao; Yahwe ni urithi wao, kama alivyosema nao.
And an inheritance not it will belong to him in [the] midst countrymen his Yahweh he [is] inheritance his just as he spoke to him.
3 Hii ni sababu ya makuhani kutoka kwa watu, kutoka kwa wale wanaotoa dhabihu, kama itakuwa ng'ombe au kondoo: wanapaswa kutoa kwa kuhani bega, mashavu mawili, na sehemu za ndani.
And this it will be [the] right of the priests from with the people from with [those who] sacrifice the sacrifice whether ox or sheep and he will give to the priest the arm and the two cheeks and the stomach.
4 Mazao ya kwanza ya nafaka zako, mvinyo wako mpya, na mafuta yako, na manyoya ya kwanza ya kondoo zako, unapaswa umpe.
[the] first of Grain your new wine your and fresh oil your and [the] first of [the] fleece of sheep your you will give to him.
5 Kwa kuwa Yahwe Mungu wako amemchagua kutoka kwenye makabila yote yako kusimama kutumika kwa jina la Yahwe, yeye na wana wake milele.
For him he has chosen Yahweh God your from all tribes your to stand to serve in [the] name of Yahweh he and descendants his all the days.
6 Kama Mlawi anatoka kati ya miji yenu nje ya Israel yote kutoka ambapo anaishi, na utamani kwa moyo wake wote kuja katika eneo Yahwe atachagua,
And if he will come Levite from one of gates your from all Israel where he [was] sojourning there and he will come in all [the] desire of self his to the place which he will choose Yahweh.
7 basi anapaswa kutumika kwa jina la Yahwe Mungu wake kama ndugu zake wote Walawi wanafanya, wanaosimama mbele ya Yahwe.
And he will serve in [the] name of Yahweh God his like all relatives his the Levites who stand there before Yahweh.
8 Wanapaswa kuwa na mgao wa kufanana wa kula, badala ya kile kinachokuja kutokana na mauzo ya urithi wa familia yake.
A portion like a portion they will eat besides sales his on the fathers.
9 Wakati mmekuja katika nchi ambayo Yahwe Mungu wenu anawapa, mnapaswa kujifunza kuangalia machukizo ya mataifa.
If you [have] gone into the land which Yahweh God your [is] about to give to you not you will learn to do according to [the] abominations of the nations those.
10 Pasipatikana miongoni mwenu mmoja anayemweka kijana wake au binti yake kwenye moto, yeyote anatumia uganga, yeyote anatabiri, au mchawi, mchawi yeyote,
Not he will be found among you [one who] makes pass son his and daughter his in the fire [one who] divines divinations a soothsayer and an augurer and a sorcerer.
11 yeyote aongeae na wafu, au yeyote aongeae na roho.
And [one who] casts a spell and [one who] consults a necromancer and a familiar spirit and [one who] enquires to the dead.
12 Kwa yeyote afanyae mambo haya ni chukizo kwa Yahwe; ni kwa sababu ya machukizo haya ambayo Yahwe Mungu wenu anawaondosha mbele zenu.
That [is] [the] abomination of Yahweh every [one who] does these [things] and on account of the abominations these Yahweh God your [is] about to dispossess them from before you.
13 Mnapaswa kuwa wakamilifu mbele ya Yahwe Mungu wenu.
Blameless you will be with Yahweh God your.
14 Kwa mataifa haya ambayo mtayafukuza kusikiliza wale wafanyao uchawi na uganga; lakini kwenu, Yahwe Mungu wenu amewakataza ninyi kufanya hivyo.
For - the nations these which you [are] about to dispossess them to soothsayers and to diviners they listen and you not thus he has permitted to you Yahweh God your.
15 Yahwe Mungu wenu atainua kwa ajili yenu nabii kutoka miongoni mwenu, mmoja wa ndugu zenu, kama mimi. Mnapaswa kumsikiliza.
A prophet from midst your one of countrymen your like me he will raise up for you Yahweh God your to him you will listen!
16 Hiki ndicho mlichouliza kutoka kwa Yahwe Mungu wenu huko Horebu katika siku ya kusanyiko, kusema, “Acha tusisikie tena sauti ya Yahwe Mungu wetu, wala kuona moto mkuu tena, wala tutakufa.”
According to all that you asked from with Yahweh God your at Horeb on [the] day of the assembly saying not me repeat to hear [the] voice of Yahweh God my and the fire great this not let me see again and not I will die.
17 Yahwe alisema nami, “Kile walichosema ni kizuri.
And he said Yahweh to me they have done well [that] which they have spoken.
18 Nitamwinua nabii kwa ajili yao kutoka miongoni mwa ndugu zao, kama wewe. Nitaweka maneno yangu katika kinywa chake, na ataongea nao yote niliyowakuamuru.
A prophet I will raise up for them from [the] midst of countrymen their like you and I will put words my in mouth his and he will speak to them all that I will command him.
19 Itakuwa kama yeyote hatasikia maneno yangu ambayo anazungumza kwa jina langu, nitalitaka kwake.
And it will be the person who not he will listen to words my which he will speak in name my I I will require from with him.
20 Lakini nabii ambaye anazungumza neno kwa kiburi kwa jina langu, neno ambalo sijamuamuru kusema, au ambaye anayezungumza kwa jina la miungu mingine, huyo nabii atakufa.
Nevertheless the prophet who he will act presumptuously by speaking a word in name my [that] which not I commanded him to speak and who he will speak in [the] name of gods other and he will die the prophet him.
21 Hivyo ndivyo unapaswa kusema katika mioyo yenu: “Tutagunduaje kuwa ujumbe ambao Yahwe hajazungumza?
And if you will say in heart your how? will we know the word which not he has spoken it Yahweh.
22 Mtagundua ujumbe ambao Yahwe amezungumza pindi nabii azungumzapo kwa jina la Yahwe. Kama hiyo haitokei wala kufanyika, basi hicho ni kile ambacho Yahwe hajazungumza na nabii amezungumza kwa kiburi, na hampaswi kumuogopa.
That he will speak the prophet in [the] name of Yahweh and not it will happen the thing and not it will come that [is] the word which not he has spoken it Yahweh with presumption he has spoken it the prophet not you will be afraid from him.

< Torati 18 >