< Torati 17 >

1 Haupaswi kumtolea dhabihu Yahwe Mungu wako ng'ombe au kondoo aliye na kasoro au kitu chochote kibaya, kwa kuwa hiyo itakuwa chukizo kwa Yahwe Mungu wako.
Thou shalt not sacrifice unto the LORD thy God an ox, or a sheep, wherein is a blemish, even any evil thing; for that is an abomination unto the LORD thy God.
2 Kama kunapatikana miongoni mwenu, ndani ya malango ya mji wowote ambao Yahwe Mungu wenu anawapatia, mwanaume yoyote au mwanamke ambaye anafanya uovu mbele ya Yahwe Mungu wenu kuiharibu agano lake -
If there be found in the midst of thee, within any of thy gates which the LORD thy God giveth thee, man or woman, that doeth that which is evil in the sight of the LORD thy God, in transgressing His covenant,
3 yoyote ambaye ameenda na kuabudu miungu mingine na kuisujudia, wala jua, mwezi, au kati ya jeshi la mbinguni- hakuna chochote nimekuamuru,
and hath gone and served other gods, and worshipped them, or the sun, or the moon, or any of the host of heaven, which I have commanded not;
4 na kama ungeambiwa kuhusu hiki, au kama una mifugo- basi unapaswa kufanya uchunguzi wa makini. Kama ni kweli na hakika kwamba chukizo kama hilo limefanyika Israeli-
and it be told thee, and thou hear it, then shalt thou inquire diligently, and, behold, if it be true, and the thing certain, that such abomination is wrought in Israel;
5 -basi utamleta huyo mwanaume au mwanamke, aliyefanya uovu huu, katika malango ya mji, kwamba mwanaume kabisa au mwanamke, na umponde huyo mtu mpaka kufa.
then shalt thou bring forth that man or that woman, who have done this evil thing, unto thy gates, even the man or the woman; and thou shalt stone them with stones, that they die.
6 Kwa kinywa cha mashahidi wawili, au mashahidi watatu, itakuwa yeye anayepaswa kuuwawa; lakini kwa kinywa cha shahidi mmoja peke hatauwawa.
At the mouth of two witnesses, or three witnesses, shall he that is to die be put to death; at the mouth of one witness he shall not be put to death.
7 Mkono wa mashahidi unapaswa kuwa wa kwanza kumuuwa, na badae mkono wa watu wote; na mtamuondoa muovu miongoni mwenu.
The hand of the witnesses shall be first upon him to put him to death, and afterward the hand of all the people. So thou shalt put away the evil from the midst of thee.
8 Kama jambo linatokea ambalo ni gumu kwenu kufanya maamuzi- pengine swali la mauaji au kifo cha ajali, haki ya mtu mmoja na haki ya mtu mwingine, au swali moja la aina ya kuzulu kufanyika, au aina nyingine ya jambo-mambo ya utata ndani ya malango yenu, basi utapaswa kwenda kwenye eneo ambalo Yahwe Mungu wako atachagua kama patakatifu pake.
If there arise a matter too hard for thee in judgment, between blood and blood, between plea and plea, and between stroke and stroke, even matters of controversy within thy gates; then shalt thou arise, and get thee up unto the place which the LORD thy God shall choose.
9 Utapaswa kwenda kwa makuhani, wazao wa Lawi, na kwa mwamuzi atakayetumika kwa wakati huo; mtatafuta ushauri wao, na watawapa ninyi maamuzi.
And thou shall come unto the priests the Levites, and unto the judge that shall be in those days; and thou shalt inquire; and they shall declare unto thee the sentence of judgment.
10 Mnapaswa kufuata sheria mliyopewa, katika eneo Yahwe atachagua kama patakatifu pake. Mtakuwa makini kufanya kila kitu ambacho wanawaelekeza kufanya.
And thou shalt do according to the tenor of the sentence, which they shall declare unto thee from that place which the LORD shall choose; and thou shalt observe to do according to all that they shall teach thee.
11 Fuata sheria wanayowafundisha, na kufanya kulingana na maamuzi wanawapa. Msigeuke kutoka kwa kile wanawambia, kwa kulia au kushoto.
According to the law which they shall teach thee, and according to the judgment which they shall tell thee, thou shalt do; thou shalt not turn aside from the sentence which they shall declare unto thee, to the right hand, nor to the left.
12 Yeyote anayefanya kwa kiburi, kwa kutomsikiliza kuhani anayesimama kutumika mbele ya Yahwe Mungu wako, au kwa kutomsikiliza mwamuzi- huyu mtu atakufa; mtaweka mbali uovu kutoka Israeli.
And the man that doeth presumptuously, in not hearkening unto the priest that standeth to minister there before the LORD thy God, or unto the judge, even that man shall die; and thou shalt exterminate the evil from Israel.
13 Watu wote wanapaswa kusikia na kuogopa, na kutofanya kwa kiburi tena.
And all the people shall hear, and fear, and do no more presumptuously.
14 Wakati mlipokuja kwenye nchi ambayo Yahwe Mungu anawapa, na wakati mnamiliki na kuanza kuishi ndani yake, na halafu unasema, 'Nitajiwekea mfalme juu yangu, kama mataifa yote yanayonizunguka mimi,'
When thou art come unto the land which the LORD thy God giveth thee, and shalt possess it, and shalt dwell therein; and shalt say: 'I will set a king over me, like all the nations that are round about me';
15 basi unapaswa kwa hakika kujiwekea mfalme juu yako mtu yeyote ambaye Yahwe atachagua. Unapaswa kujiweka kama mfalme juu yako mtu yeyote kutoka miongoni mwa ndugu zenu. Haupaswi kuweka mgeni, ambaye si ndugu yenu, juu yenu.
thou shalt in any wise set him king over thee, whom the LORD thy God shall choose; one from among thy brethren shalt thou set king over thee; thou mayest not put a foreigner over thee, who is not thy brother.
16 Lakini hapaswi kuzidisha farasi kwa ajili yake, wala kusababisha watu kurudi Misri ili kwamba aweze kuzidisha farasi, kwa kuwa Yahwe alikwisha sema kwako, 'Unapaswa kuanzia sasa usirudi njia hiyo tena.'
Only he shall not multiply horses to himself, nor cause the people to return to Egypt, to the end that he should multiply horses; forasmuch as the LORD hath said unto you: 'Ye shall henceforth return no more that way.'
17 Na hapaswi kuzidisha wake kwa ajili yake, ili kwamba moyo wake usigeuke kotoka kwa Yahwe; wala hapaswi sana kuzidisha kwa ajili yake fedha au dhahabu.
Neither shall he multiply wives to himself, that his heart turn not away; neither shall he greatly multiply to himself silver and gold.
18 Wakati aketipo kwenye kiti cha enzi cha ufalme wake, anapaswa kuandika kwenye kitabu kwa ajili yake nakala ya sheria hii, kutoka kwenye sheria ambayo iko mbele ya makuhani, ambao ni Walawi.
And it shall be, when he sitteth upon the throne of his kingdom, that he shall write him a copy of this law in a book, out of that which is before the priests the Levites.
19 Kitabu kinapaswa kuwa na yeye, na anapaswa kusoma ndani yake kwa siku zake zote, ili kwamba aweze kujifunza kumheshimu Yahwe Mungu wako, ili kwamba ashike maneno yote ya sheria hii na amri hizi, kuzishika.
And it shall be with him, and he shall read therein all the days of his life; that he may learn to fear the LORD his God, to keep all the words of this law and these statutes, to do them;
20 Anapaswa kufanya hivi ili kwamba moyo wake usiinuliwe zaidi ya ndugu zake, na ili kwamba asigeuke mbali na amri, kwa kulia au kwa kushoto' kwa kusudi kwamba aweze kuzidisha siku zake katika ufalme wake, yeye na watoto wake, miongoni mwa Israel.
that his heart be not lifted up above his brethren, and that he turn not aside from the commandment, to the right hand, or to the left; to the end that he may prolong his days in his kingdom, he and his children, in the midst of Israel.

< Torati 17 >