< Torati 15 >

1 Kila mwisho wa kila miaka saba, mnapaswa kufuta madeni.
Every seven years you shall make a release.
2 Hii ni tabia ya ukombozi. Kila mkopeshaji atafuta kile alichompa jirani yake, hata dai kutoka kwa jirani yake au ndugu yake kwa sababu ufutaji wa madeni wa Yahwe umetangazwa.
And this [is] the ordinance of the release: you shall remit every private debt which your neighbour owes you, and you shall not ask payment of it from your brother; for it has been called a release to the Lord your God.
3 Kutoka kwa mgeni mnaweza kudai; lakini kwa chochote chenu kilicho na ndugu yenu mnapaswa mkitoe.
Of a stranger you shall ask again whatever he has of your, but to your brother you shall remit his debt to you.
4 Hata hivyo, pasiwepo maskini miongoni mwenu (kwa kuwa Yahwe kwa hakika atawabariki kwenye nchi ambayo anawapa kama urithi kumiliki)
For [thus] there shall not be a poor person in the midst of you, for the Lord your God will surely bless you in the land which the Lord your God gives you by inheritance, that you should inherit it.
5 kama peke yenu mnasikiliza kwa bidii sauti ya Yahwe Mungu wenu, kuzishika amri zote ambazo anawaamuru leo.
And if you shall indeed listen to the voice of the Lord your God, to keep and do all these commandments, as many as I charge you this day,
6 Kwa kuwa Yahwe Mungu wenu atawabariki, kama alivyowaahidia; mtakopesha mataifa mengi, lakini hamtaazima; mtaongoza juu ya mataifa mengi, lakini hayatawaongoza ninyi.
(for the Lord your God has blessed you in the way of which he spoke to you, ) then you shall lend to many nations, but you shall not borrow; and you shall rule over many nations, but they shall not rule over you.
7 Kama kuna mtu maskini miongoni mwenu, moja wa ndugu zenu, ndani ya malango yenu yoyote kwenye nchi yenu ambayo Yahwe Mungu wenu anawapa, msifanye migumu mioyo yenu wala kufunga mkono wenu toka kwa ndugu yenu,
And if there shall be in the midst of you a poor [man] of your brethren in one of your cities in the land, which the Lord your God gives you, you shall not harden your heart, neither shall you by any means close up your hand from your brother who is in lack.
8 Lakini mnapaswa hakika kufungua mkono wenu kwake na hakika mkopeshe yeye vya kutosha hitaji lake.
You shall surely open your hands to him, and shall lend to him as much as he wants according to his need.
9 Muwe makini kutokuwa na wazo ovu au potovu katika moyo wenu, kusema, “Mwaka wa saba, mwaka wa ukombozi u karibu; ili kwamba msiwe wachoyo kuhusiana na ndugu zenu maskini na haumpi chochote; anaweza kumlilia Yahwe kuhusu nyie, na itakuwa dhambi yenu.
Take heed to yourself that there be not a secret thing in your heart, an iniquity, saying, The seventh year, the year of release, draws near; and your eye shall be evil to your brother that is in lack, and you shall not give to him, and he shall cry against you to the Lord, and there shall be great sin in you.
10 Mnapaswa kwa hakika mmpe, na moyo wenu hampaswi kuhuzunika wakati mnampa, kwa sababu kurudishiwa kwa Yahwe huyu Mungu wenu atawabariki katika kazi zenu zote na katika chochote mnaweka mkono wenu.
You shall surely give to him, and you shall lend him as much as he wants, according as he is in need; and you shall not grudge in your heart as you give to him, because on this account the Lord your God will bless you in all your works, and in all things on which you shall lay your hand.
11 Kwa kuwa maskini kamwe hatakoma kuishi katika nchi, kwa hiyo nakuamuru wewe na kusema, “Unapaswa kwa hakika ufungue mkono wako kwa ndugu yako, kwa mhitaji wako, na kwa maskini wako katika nchi yako.
For the poor shall not fail off your land, therefore I charge you to do this thing, saying, You shall surely open your hands to your poor brother, and to him that is distressed upon your land.
12 Kama ndugu yako, ni mwebrania wa kiume au mwebrania wa kike, ameuzwa kwako na anakutumikia kwa miaka saba, basi katika mwaka wa saba unapaswa umwache aende zake huru.
And if your brother [or sister], a Hebrew man or a Hebrew woman, be sold to you, he shall serve you six years, and in the seventh year you shall send him out free from you.
13 Unapomwacha aende zake huru, usimwache aende mkono mtupu.
And when you shall send him out free from you, you shall not send him out empty.
14 Unapaswa kwa ukarimu hutoe kwake kutoka mifugo yako, kutoka pura iliyo chini, na kinu chako cha mvinyo. Kama Yahwe Mungu wako alivyokubariki, unapaswa umpe yeye.
You shall give him provision for the way from your flock, and from your corn, and from your wine; as the Lord your God has blessed you, you shall give to him.
15 Unapaswa kukumbuka kwamba ulikuwa mtumwa kwenye nchi ya Misri, na kwamba Yahwe Mungu wako alikukomboa; kwa hiyo ninakuamuru leo kufanya hivi.
And you shall remember that you were a servant in the land of Egypt, and the Lord your God redeemed you from thence; therefore I charge you to do this thing.
16 Itakuwa kwamba kama atasema kwako, “Sitaenda mbali yako; kwa sababu anakupenda na nyumba yako, na kwa sababu ni mzuri kwako,
And if he should say to you, I will not go out from you, because he continues to love you and your house, because he is well with you;
17 basi unapaswa kuchukua uma na msukumo kupitia sikio lake kwenye mlango, na atakuwa mtumwa wako milele. Na pia kwa mtumwa wako wa kike utafanya vilevile.
then you shall take an awl, and bore his ear through to the door, and he shall be your servant for ever; and in like manner shall you do to your maidservant.
18 Isionekane kuwa vigumu kwako kumwachia aende zake huru, kwa sababu amekutumikia kwa miaka sita na amekupa mara mbili udhamani wa mtu aliyeajiriwa. Yahwe Mungu wako atakubariki katika yote unayofanya.
It shall not seem hard to you when they are sent out free from you, because [your servant] has served you six years according to the annual hire of a hireling; so the Lord your God shall bless you in all things whatever you may do.
19 Wazao wote wa kwanza wa kiume katika wanyama na mifugo wako unapaswa uwatenge kwa Yahwe Mungu wako. Hautafanya kazi na mzao wa kwanza wa wanyama wako wala kumnyoa mzao wa kwanza wa mfugo wako.
Every firstborn that shall be born amongst your kine and your sheep, you shall sanctify the males to the Lord your God; you shall not work with your firstborn calf, and you shall not shear the firstborn of your sheep.
20 Unapaswa umle mzaliwa wa kwanza mbele ya Yahwe Mungu wako kila mwaka katika eneo ambalo Yahwe atachagua, wewe na nyumba yako.
You shall eat it before the Lord year by year in the place which the Lord your God shall choose, you and your house.
21 Kama ina kasoro yoyote- kwa mfano, kama ni kilema au kipofu, au ana kasoro yoyote- haupaswi kumtoa dhabihu kwa Yahwe Mungu wako.
And if there be in it a blemish, if it be lame or blind, an evil blemish, you shall not sacrifice it to the Lord your God.
22 Utamla ndani ya malango yako; mtu asiye najisi na aliye najisi ni sawa unapaswa kula, kama ungekula paa au kulungu.
You shall eat it in your cities; the unclean in you and the clean shall eat it in like manner, as the doe or the stag.
23 Pekee haupaswi kunywa damu yake; unapaswa kuimwanga damu yake juu ya ardhi kama maji.
Only you shall not eat the blood; you shall pour it out on the earth as water.

< Torati 15 >