< Torati 12 >

1 Hizi ni amri na sheria ambazo mtazishika katika nchi ambayo, Yahwe Mungu wa baba zenu, amewapa kumiliki, siku zote mnazoishi kwenye ardhi.
These are the statutes and the judgments which you shall observe to do in the land which Adonai, the God of your fathers, has given you to possess it, all the days that you live on the earth.
2 Hakika mtaharibu maeneo yote ambapo mataifa mtakayofukuza miungu yao walioabudu, kwenye milima mirefu, kwenye vilima, na chini ya kila mti wa kijani.
You shall surely destroy all the places in which the nations that you shall dispossess abad ·served· their deities, on the high mountains, and on the hills, and under every green tree.
3 Na mtazivunja madhabahu zao chini, mtaharibu kwa vipandepande nguzo zao za mawe, na kuchoma ncha za Asherahi, mtazikata sanaa za kuchongwa za miungu yao na kuangamiza jina lao nje ya eneo hilo.
You shall break down their altars, and dash their pillars in pieces, and burn their Asherah poles with fire. You shall cut down the engraved images of their deities. You shall destroy their name out of that place.
4 Hamtamwabudu Yahwe Mungu wenu kama hivyo.
You shall not do so to Adonai your God.
5 Lakini kwa eneo ambalo Yahwe Mungu wenu atachagua kutoka makabila yenu kuweka jina lake, hapo patakuwa ni eneo analoishi na huko ndiyo mtaenda.
But to the place which Adonai your God shall choose out of all your tribes, to put his name there, you shall seek his habitation, and there you shall come.
6 Ni huko ndiko mtaleta sadaka ya kutekeketezwa, dhabihu zenu, zaka zenu, na sadaka zinazotolewa kwa mkono wenu, sadaka zenu za viapo, sadaka za utayari na mzao wa kwanza wa mifugo na wanyama.
There you shall bring your burnt offerings, your sacrifices, your tithes, the wave offering of your hand, your vows, your free will offerings, and the firstborn of your herd and of your flock.
7 Ni huko mtakula mbele za Yahwe Mungu wenu na kufurahi kuhusu kila kitu ambacho mmeweka mkono, nyie na jamaa zenu, ambapo Yahwe Mungu wenu amewabariki.
There you shall eat before Adonai your God, and you shall rejoice in all that you put your hand to, you and your households, in which Adonai your God has blessed you.
8 Hamtafanya mambo yote ambayo tunafanya hapa leo; sasa kila moja anafanya chochote kile kizuri machoni pake,
You shall not do after all the things that we do here today, every man whatever is right in his own eyes;
9 kwa kuwa bado hamjapumzika, kwa urithi ambao Yahwe Mungu wenu anawapa.
for you haven’t yet come to the rest and to the inheritance, which Adonai your God gives you.
10 Lakini pindi mnaenda ng'ambo ya pili ya Yordani na kuishi ndani ya nchi ambayo Yahwe Mungu wenu anasababisha ninyi kurithi, na wakati awapa pumziko kutoka kwa maadui zenu wanaowazunga karibu, ili kusudi muishi kwa usalama,
But when you go over the Jordan [Descender], and dwell in the land which Adonai your God causes you to inherit, and he gives you rest from all your enemies around you, so that you dwell in safety;
11 kisha itakuwa eneo ambalo Yahwe Mungu wenu atachagua kusababisha jina lake kuishi, huko mtaleta yote ninayowaamuru; sadaka za kuteketezwa, dhabihu zenu, zaka zenu, sadaka zilizotolewa kwa mkono wenu, na sadaka za chaguo lenu kwa ajili ya nadhiri mtakazotoa kwa Yahwe.
then it shall happen that to the place which Adonai your God shall choose, to cause his name to dwell there, there you shall bring all that I enjoin you: your burnt offerings, your sacrifices, your tithes, the wave offering of your hand, and all your choice vows which you vow to Adonai.
12 Mtafurahi mbele za Yahwe Mungu wenu-nyie, watoto wenu, binti zenu, wajakazi wa kiume, wajakazi wa kike, na Walawi walio ndani ya lango lenu, kwa sababu hana sehemu au urithi miongoni mwenu.
You shall rejoice before Adonai your God, you, and your sons, your daughters, your male servants, your female servants, and the Levite [Descendant of United with] who is within your gates, because he has no portion nor inheritance with you.
13 Uwe makini mwenyewe kwamba usitoe sadaka zako za kuteketezwa kila eneo unaloona;
Be careful that you don’t offer your burnt offerings in every place that you see;
14 lakini ni katika eneo hilo ambalo Yahwe atawachagua miongoni moja kati ya makabila yenu ambalo litatoa sadaka ya kuteketezwa, na huko mtafanya kila kitu ninachokuamuru.
but in the place which Adonai chooses in one of your tribes, there you shall offer your burnt offerings, and there you shall do all that I enjoin you.
15 Hata hivyo, mtaweza kuua na kula wanyama ndani ya malango yenu, kama mnavyotaka, kupokea baraka ya Yahwe Mungu wenu kwa ajili ya yote amewapa; na watu wasio safi na safi wote wanaweza kula, wanyama kama vile paa na kulungu.
Notwithstanding, you may kill and eat meat within all your gates, after all the desire of your soul, according to Adonai your God’s blessing which he has given you. The unclean and the clean may eat of it, as of the gazelle, and as of the deer.
16 Lakini hamtakula damu, mtaimwaga kwenye ardhi kama maji.
Only you shall not eat the blood. You shall pour it out on the earth like water.
17 Mnaweza msile ndani ya malango kutoka kwenye zaka ya nafaka zenu, mvinyo wenu mpya, mafuta yenu au mzao wa kwanza wa mifugo au wanyama; na mnaweza msile nyama yoyote mnayoitoa dhabihu pamoja na viapo vyovyote vyenu mnafanya, wala sadaka yenu ya utayari, wala sadaka mnayotoa kwa mkono wenu.
You may not eat within your gates the tithe of your grain, or of your new wine, or of your oil, or the firstborn of your herd or of your flock, nor any of your vows which you vow, nor your free will offerings, nor the wave offering of your hand;
18 Badala yake, mtakula mbele ya Yahwe Mugu wenu katika eneo ambalo Yahwe Mungu atachagua- nyie, mtoto wenu, binti yenu, mjakazi wa kiume, mjakazi wa kike, na Mlawi aliye malangoni mwenu; mtafurahi mbele ya Yahwe Mungu wenu kuhusu kila kitu ambacho mnaweka mkono wenu.
but you shall eat them before Adonai your God in the place which Adonai your God shall choose, you, your son, your daughter, your male servant, your female servant, and the Levite [Descendant of United with] who is within your gates. You shall rejoice before Adonai your God in all that you put your hand to.
19 Muwe makini wenyewe ili kwamba msimwache Mlawi maadamu mnaishi kwenye nchi yenu.
Be careful that you don’t forsake the Levite as long as you live in your land.
20 Wakati Yahwe Mungu wenu apanua mipaka yenu, kama alivyowaahidi, na kusema, “Nitakula nyama,” kwa sababu ya tamaa zenu mnakula nyama, mnaweza kula nyama, kama tanmaa za roho zenu.
When Adonai your God enlarges your border, as he has promised you, and you shall say, “I want to eat meat,” because your soul desires to eat meat; you may eat meat, after all the desire of your soul.
21 Kama eneo ambalo Yahwe Mungu wenu achagua kuliweka jina lake ni mbali kutoka kwenu, basi mtaua baadhi ya mifugo yenu na wanyama wenu ambao Yahwe amewapa, kama nilivyowaamuru: hivyo mnaweza kula ndani ya malango yenu, kama tamaa za roho zenu.
If the place which Adonai your God shall choose, to put his name there, is too far from you, then you shall kill of your herd and of your flock, which Adonai has given you, as I have enjoined you; and you may eat within your gates, after all the desire of your soul.
22 Kama paa na Kulungu wanaliwa, hivyo mtakula watu wasio safi na wasafi wanaweze kula kadhalika.
Even as the gazelle and as the deer is eaten, so you shall eat of it. The unclean and the clean may eat of it alike.
23 Lakini muwe na uhakika kwamba hamtumii damu, kwa kuwa damu ni uhai, hamtakula uhai pamoja na nyama.
Only be sure that you don’t eat the blood; for the blood is the life. You shall not eat the life with the meat.
24 Hamtakula, mtaimwaga nje kwenye ardhi kama maji.
You shall not eat it. You shall pour it out on the earth like water.
25 Hamtakula, ili kwamba iweze kuwa vizur kwenu, na watoto wenu baada yenu, wakati mtafanya kile kilicho sahihi machoni pa Yahwe.
You shall not eat it; that it may go well with you, and with your children after you, when you shall do that which is right in Adonai’s eyes.
26 Lakini mambo ambayo ni ya Yahwe ambayo mnayo na sadaka za viapo vyenu-mtachukua hizi na kwenda eneo ambalo Yahwe achagua.
Only your holy things which you have, and your vows, you shall take, and go to the place which Adonai shall choose.
27 Hapo mtatoa sadaka ya kuteketekezwa, nyama na damu, kwenye madhabahu ya Yahwe Mungu wenu, damu ya dhabihu zenu itamwangwa nje kwenye madhabahu ya Yahwe Mungu wenu, na mtakula nyama.
You shall offer your burnt offerings, the meat and the blood, on Adonai your God’s altar; and the blood of your sacrifices shall be poured out on Adonai your God’s altar; and you shall eat the meat.
28 Mchunguze na msikilize haya maneno yote ambayo - ninawaamuru, ili iwe uzuri kwenu na watoto wenu baada yenu milele, wakati mnafanya kile kilicho kizuri na sawa machoni pa Yahwe Mungu wenu.
Observe and sh'ma ·hear obey· all these words which I enjoin you, that it may go well with you, and with your children after you forever, when you do that which is good and right in Adonai your God’s eyes.
29 Wakati Yahwe Mungu wenu anapunguza mataifa kutoka kwenu, wakati mnaingia kuwafukuza, na mnawafukuza na kuishi katika nchi yao,
When Adonai your God cuts off the nations from before you, where you go in to dispossess them, and you dispossess them, and dwell in their land;
30 muwe makini wenyewe ili kwamba msinaswe kwa kuwafuata, baada ya kuangamizwa kutoka kwenu kunaswa katika kuchunguza miungu yao, katika kuuliza, “Kwa namna gani haya mataifa yanaabudu muingu yao? Nitafanya hivyo hivyo.
be careful that you are not ensnared to follow them, after that they are destroyed from before you; and that you not inquire after their deities, saying, “How do these nations abad ·serve· their deities? I will do likewise.”
31 Hautafanya hivyo katika kumheshimu Yahwe Mungu wako, kwa kuwa kila kitu ambacho ni chukizo kwa Yahwe, mambo ambayo anayachukia- wamefanya haya na miungu yao, hata mnateketeza vijana wao na binti zao kwenye moto kwa ajili ya miungu yao.
You shall not do so to Adonai your God; for every abomination to Adonai, which he hates, have they done to their deities; for they even burn their sons and their daughters in the fire to their deities.
32 Chochote ninakuamuru, chunguza. Usiongeze juu yake au kupunguza.
Whatever thing I enjoin you, that you shall observe to do. You shall not add to it, nor take away from it.

< Torati 12 >