< Torati 11 >

1 Kwa hiyo mtampenda Yahwe Mungu wenu na daima mtashika maelekezo yake, maagizo yake, sheria zake, na amri zake.
And you will love Yahweh God your and you will keep command his and statutes his and judgments his and commandments his all the days.
2 Kumbuka kwamba siongei kwa watoto wako, ambao hawajajua wala kuona hukumu ya Yahwe Mungu wako, ukuu wake, mkono wake wa uweza, mkono wake ulionyoshwa,
And you will know this day that - not children your who not they have known and who not they have seen [the] training of Yahweh God your greatness his hand his mighty and arm his outstretched.
3 Ishara na matendo ambayo alifanya katikati ya Misri kwa Farao, mfalme Misri, na nchi yake yote.
And signs his and deeds his which he did in [the] midst of Egypt to Pharaoh [the] king of Egypt and to all land his.
4 Wala hawakuona kile alichofanya kwa jeshi la Misri, kwa farasi wao, au magari yao; namna alivyoyafanya maji ya bahari ya Reeds kuwaelemea kwa sababu ya kuwafuatilia, na namna Yahwe alivyowaangamiza mpaka leo,
And which he did to [the] army of Egypt to horses its and to chariotry its when he caused to flow [the] water of [the] sea of reed[s] over faces their when pursued they after you and he destroyed them Yahweh until the day this.
5 au nini alifanya kwenu kwenye jangwa mpaka mlikuja eneo hili.
And which he did to you in the wilderness until came you to the place this.
6 Hawajaona nini Yahwe alichofanya kwa Dathani na Abiramu, wana wa Eliabu mwana wa Reubeni; namna dunia ilifungua kinywa chake na kuwameza, nyumba zao, mahema yao, na kila kitu hai kilichowafuata, katikati mwa Israeli yote.
And which he did to Dathan and to Abiram [the] sons of Eliab [the] son of Reuben when it opened the earth mouth its and it swallowed them and households their and tents their and all the substance which [was] at feet their in [the] midst of all Israel.
7 Lakini macho yenu yameona kazi yote kuu ya Yahwe aliyoifanya.
For eyes your [are] the [ones which] saw all [the] work of Yahweh great which he did.
8 Kwa hiyo shikeni amri zote ambazo ninawaamuru leo, kwamba mweze kuwa imara, na kuingia na kuimiliki nchi, ambayo unaenda zaidi kuimiliki;
And you will keep all the commandment which I [am] commanding you this day so that you may be strong and you will go and you will take possession of the land where you [are] about to pass over there towards to take possession of it.
9 na kwamba uweze kuongeza siku zako katika nchi ambayo Yahwe aliapa kwa baba zako kuwapa na uzao wao, nchi itiririkayo maziwa na asali.
And so that you may prolong days on the land which he swore Yahweh to ancestors your to give to them and to offspring their a land flowing of milk and honey.
10 Kwa kuwa nchi, ambayo unaingia kumiliki, siyo kama nchi ya Misri, ambako mlitoka, ambako mlipanda mbegu na kumwagilizia kwa miguu yenu, kama bustani ya mitishamba;
For the land where you [are] about to go there towards to take possession of it not [is] like [the] land of Egypt it where you came out from there where you sowed seed your and you watered [it] with foot your like [the] garden of vegetable[s].
11 Lakini nchi, ambayo unaenda kuimiliki, ni nchi ya milima na mabonde, na kunywa maji ya mvua mbinguni,
And the land where you [are] about to pass over there towards to take possession of it [is] a land of mountains and valleys to [the] rain of the heavens it drinks water.
12 nchi ambayo Yahwe Mungu wenu awajali; macho ya Yahwe Mungu wenu daima yako juu yake, kuanzia mwanzo wa mwaka mpaka mwisho wa mwaka.
A land which Yahweh God your [is] caring for it continually [the] eyes of Yahweh God your [are] on it from [the] beginning of the year and until [the] end of a year.
13 Itatokea, kama mtazisikiliza kwa bidii amri zangu ambazo ninawaamuru leo kumpenda Yahwe Mungu wenu, na kumtumikia kwa moyo wenu wote na roho zenu zote,
And it will be certainly [if] you will obey commandments my which I [am] commanding you this day to love Yahweh God your and to serve him with all heart your and with all being your.
14 kwamba nitawapa mvua nchi yenu kwa majira yake, mvua za awali na mvua za badaye, ili kwamba mweze kukusanya nafaka zenu, mvinyo wenu mpya, na mafuta yenu.
And I will give [the] rain of land your at appropriate time its autumn rain and spring rain and you will gather grain your and new wine your and fresh oil your.
15 Nitawapa nyasi kwenye mashamba yenu kwa ajili ya mifugo yenu, na mtakula na kushiba.
And I will give grass in field[s] your for cattle your and you will eat and you will be satisfied.
16 Uwe makini mwenyewe, ili kwamba moyo wako usidanganyike, na kugeuka na kuabudu miungu mingine, na kuisujudia;
Take heed to yourselves lest it should be deceived heart your and you will turn aside and you will serve gods other and you will bow down to them.
17 ili kwamba hasira ya Yahwe isiwashiwe dhidi yenu, na ili kwamba asifunge mbingu, kwamba pasiwe na mvua, na nchi haitavuna matunda, na ili kwamba mpotee kwa haraka kutoka nchi nzuri ambayo Yahwe anawapa.
And it will burn [the] anger of Yahweh on you and he will shut up the heavens and not it will come rain and the ground not it will yield produce its and you will perish quickly from on the land good which Yahweh [is] about to give to you.
18 Kwa hiyo yaweke haya maneno ndani ya moyo wako na roho; yafunge kama ishara kwenye mkono wako, na yawe utepe katikati ya macho yako.
And you will put words my these on heart your and on being your and you will tie them for a sign on hand your and they will be for marks between eyes your.
19 Utayafundisha kwa watoto na kuongea juu yake wakati uketipo ndani ya nyumba yako, wakati utembeapo barabarani, wakati ulalapo, na wakati uinukapo.
And you will teach them children your by speaking in them when sitting you in house your and when walking you on the road and when lying down you and when rising up you.
20 Utayaandika kwenye miimo ya milango ya nyumba zenu na kwenye malango yenu,
And you will write them on [the] doorposts of house your and on gates your.
21 kwamba siku zenu na siku za watoto wenu ziweze kuongezeka katika nchi ambayo Yahwe aliapa kwa mababu zenu kuwapa, maadamu mbingu ziko juu ya ardhi.
So that they may increase days your and [the] days of children your on the land which he swore Yahweh to ancestors your to give to them like [the] days of the heavens above the earth.
22 Kama mtayashika kwa bidii maagizo haya yote ambayo ninawaamuru nyinyi, ili kwamba myafanye, mpende Yahwe Mungu wenu, tembea katika njia zake zote, na kushikamana naye,
That except certainly you will keep! all the commandment this which I [am] commanding you to do it to love Yahweh God your to walk in all ways his and to cleave to him.
23 basi Yahwe atawaondosha mataifa haya yote kutoka mbele yenu, na mtayafukuza mataifa makubwa na yenye nguvu kuliko nyie.
And he will dispossess Yahweh all the nations these from to before you and you will dispossess nations great and mighty more than you.
24 Kila eneo ambalo unyao wa miguu utatembea litakuwa lenu; kutoka jangwani hadi Lebanoni, toka mto wa Euphratesi, hadi magharibi mwa bahari itakuwa mpaka wenu.
Every place which it will tread [the] sole of foot your on it to you it will belong from the wilderness and Lebanon from the River [the] river of Euphrates and to the sea western it will be territory your.
25 Hakuna mtu ataweza kusimama mbele yenu; Yahwe Mungu wenu ataweka hofu yenu na ugaidi wenu juu ya nchi yote mnayotembea juu yake kama alivyosema na ninyi.
Not he will stand anyone in faces your dread your and fear your he will put - Yahweh God your over [the] face of all the land which you will tread on it just as he spoke to you.
26 Tazama, naweka mbele yenu baraka na laana;
See I [am] setting before you this day a blessing and a curse.
27 baraka, kama mtasikiliza amri za Yahwe ambazo ninakuamuru leo,
The blessing that you will obey [the] commandments of Yahweh God your which I [am] commanding you this day.
28 na laana, kama hamtasikiliza amri za Yahwe Mungu wenu, lakini mkaicha njia ninayokuamuru leo, kuendea miungu mingine ambayo hamjaijua.
And the curse if not you will obey [the] commandments of Yahweh God your and you will turn aside from the way which I [am] commanding you this day to walk after gods other which not you have known.
29 Itakuwa wakati Yahwe Mungu wenu anawaleta ninyi katika nchi ambayo mnaenda kumiliki, kwamba mtaweka baraka juu ya mlima Gerizimu na laana juu ya mlima Ebali.
And it will be that he will bring you Yahweh God your into the land where you [are] about to go there towards to take possession of it and you will set the blessing on [the] mountain of Gerizim and the curse on [the] mountain of Ebal.
30 Hawako ng'ambo ya pili zaidi ya Yordani, magharibi mwa barabara la magharibi, katika nchi ya Wakanani wanaoishi Arabah, juu dhidi ya Gilgali, kando ya mialo ya Moreh?
¿ Not [are] they on [the] other side of the Jordan behind [the] direction of [the] setting of the sun in [the] land of the Canaanite[s] who is dwelling in the Arabah opposite to Gilgal beside [the] great trees of Moreh.
31 Kwa maana mtavuka ng'ambo ya pili ya Yordani kuingia kumiliki nchi ambayo Yahwe Mungu wenu anawapa, na mtamiliki na kuishi ndani yake.
For you [are] about to pass over the Jordan to go to take possession of the land which Yahweh God your [is] about to give to you and you will take possession of it and you will dwell in it.
32 Mtashika sheria zote na amri ninazoweka mbele yenu leo.
And you will take care to observe all the statutes and the judgments which I [am] setting before you this day.

< Torati 11 >