< Danieli 1 >

1 Katika mwaka wa tatu wa utawala wa Yehoyakimu mfalme wa Yuda, Nebukadneza mfalme wa Babeli alikuja Yerusalemu na kuuzunguka mji ili kuzuia mahitaji yake yote.
В третата година от царуването на Юдовия цар Иоаким дойде вавилонския цар Навуходоносор в Eрусалим и го обсади.
2 Bwana alimpa Nebukadneza ushindi dhidi ya Yehoyakimu mfalme wa Yuda, na alimpatia vitu vitakatifu kutoka nyumba ya Mungu. Alivipeleka vitu hivyo mpaka katika nchi ya Babeli, kwa nyumba ya mungu wake, na aliviweka vitu vitakatifu katika hazina ya mungu wake.
И Господ предаде в ръката му Юдовия цар Иоаким и част от съдовете в Божия дом; и той ги занесе в земята Сенаар, в капището на своя бог, и съдовете внесе в съкровищницата на своя бог.
3 Mfalme akamwambia Ashipenazi, afisa wake mkuu, awalete baadhi ya watu wa Israeli, wa familia ya kifalme na za kiungwana -
И царят заповяда на началника на скопците си Асфеназ да доведе някой от израиляните, сиреч, от царския род и от благородните,
4 vijana wasio na hila, wenye mwonekano wa kuvutia, wenye ujuzi katika hekima yote, wenye kujawa na ufahamu na weledi, na wenye sifa za kutumika katika ikulu ya mfalme. Alitakiwa kuwafundisha maandiko na lugha ya Babeli.
юноши без никакъв недостатък, красиви на глед, които проумяваха всякаква мъдрост, вещи във всякакво знание, такива, които владееха науките и бяха достойни да стоят в царския палат, та да ги учението и езика на халдейците.
5 Mfalme aliwatengea kwa ajili yao fungu kutoka katika chakula chake kizuri kwa kila siku na katika divai aliyokunywa. Vijana hawa walitakiwa kufunzwa kwa miaka mitatu, na baada ya hapo, wangeweza kumtumikia mfalme.
И царят им определи за всеки ден дял от царските изрядни ястия и от виното, което той пиеше, с които да ги хранят три години, за да стоят пред царя след изтичането на това време.
6 Miongoni mwao walikuwa ni Danieli, Hanania, Mishaeli, na Azaria, baadhi ya watu wa Yuda.
А между тях бяха, от юдейците, Даниил, Анания, Мисаил, и Азария,
7 Afisa mkuu aliwapa majina: Danieli alimwita Belteshaza, Hanania alimwita Shadraka, Mishaeli alimwita Meshaki, na Azaria alimwita Abedinego.
които началникът на скопците преименува, като нарече Даниила Валтасасар, и Анания Седрах, Мисаила Мисах, и Азария, Авденаго.
8 Lakini Danieli alinuia katika akili yake kuwa asingejitia ujanisi mwenyewe kwa chakula kizuri cha mfalme wala kwa divai ambayo alikunywa.
Но Даниил реши в сърцето си да се не оскверни от изрядните ястия на царя, нито от виното, което той пиеше; затова, помоли началника на скопците да се не оскверни.
9 Basi, aliomba ruhusa kutoka kwa afisa mkuu ili kwamba asije akajitia uchafu yeye mwenyewe. Hivyo, Mungu alimpa Danieli kibali na huruma kupitia katika heshima ambayo afisa mkuu alikuwa nayo kwake.
А Бог направи щото Даниил да придобие благоволение и милост пред началника на скопците.
10 Afisa mkuu alimwambia Danieli, “Ninamwogopa bwana wangu mfalme. Ameagiza aina ya chakula na vinywaji mnavyotakiwa kutumia. Kwa nini awaone ninyi mkiwa mnaonekana vibaya kuliko vijana wengine wa umri wenu? Mfalme aweza kukitwaa kichwa changu kwa sababu yenu.
И началникът на скопците рече на Даниила: Аз се боя от господаря си царя, който определи ястието ви и питието ви, да не би да види, че лицата ви са по-малко поправени от лицата на юношите вашите връстници, и така да турите главата ми в опасност пред царя.
11 Kisha Daniel akamwambia msimamizi ambaye afisa mkuu alikuwa amemweka juu ya Danieli, Hanania, Mishaeli, na Azaria.
Тогава Даниил рече на надзирателя, когото началникът на скопците беше поставил над Даниила, Анания, Мисаила, и Азария.
12 Alisema, “Tafadhari tujaribuni, sisi watumishi wako kwa siku kumi. Tupatieni tu mboga mboga za kula na maji ya kunywa.
Опитай, моля, слугите си десет дни, през което време да ни се даде зеленчук да ядем и вода да пием;
13 Kisha ulinganishe mwonekano wetu na mwonekano wa vijana wanaokula vyakula vya mfalme, na mtutendee, sisi watu wako kulingana na kile unachokiona.”'
после нека се прегледат пред тебе нашите лица и лицата на юношите, които ядат от изрядните ястия на царя; и според каквото видиш постъпи със слугите си.
14 Hivyo msimamizi alikubaliana naye kufanya hivi, na aliwajaribu kwa siku kumi.
И той ги послуша в това нещо, и ги опита десет дена.
15 Katika mwisho wa siku kumi mwonekano wao ulikuwa ni wenye afya nzuri kuliko wa wale vijana waliokula vyakula vya kifalme.
И на края на десетте дена техните лица изглеждаха по-красиви и по-пълни, отколкото лицата на всичките юноши, които ядяха от изрядните ястия на царя.
16 Basi, msimamizi aliliondoa fungu lao la chakula na vivywaji vyao na walipewa mboga mboga tu.
И тъй, надзирателят отнемаше от тях изрядното ястие и виното, което трябваше да пият, и им даваше зеленчук.
17 Na kuhusu vijana hawa nne Mungu aliwapa uelewa na ufahamu katika maandiko yote na hekima, na Danieli aliweza kupambanua aina zote za maono na ndoto.
А на тия четири юноша Бог даде знание и разум във всяко учение и мъдрост; и Даниил можеше да проумява всички видения и сънувания.
18 Katika mwisho wa muda uliokuwa umepangwa na mfalme kuwaleta ndani, afisa mkuu aliwaleta mbele ya Nebukadneza.
И на края на дните, когато царят бе заповядал да ги въведат, началникът на скопците ги въведе пред Навуходоносора.
19 Mfalme aliongea nao, na miongoni mwa kundi lote hapo hapakuwa na wa kuwalinganisha na akina Danieli, Hanania, Mishaeli, na Azaria. Walisimama mbele ya mfalme, wakiwa tayari kumtumikia.
И като разговаря с тях царят, между всички тях не се намери подобен на Даниила, Анания, Мисаила, и Азария; за това, те стояха пред царя.
20 Katika kila swali la hekima na ufahamu ambalo mfalme aliwauliza, aliwakuta wakiwa na uwezo mara kumi kuliko waganga wote na wale waliojidai kusema na wafu, waliokuwa katika ufalme wake wote.
И във всяко дело, което изискваше мъдрост и проумяване, за което царят ги попита, намери ги десет пъти по-добри от всичките врачове и вражари, които бяха в цялото му царство.
21 Danieli alikuwa hapo mpaka mwaka wa kwanza wa Mfalme Koreshi.
И Даниил остана до първата година на цар Кира.

< Danieli 1 >