< Danieli 8 >

1 Katika mwaka wa tatu wa utawala wa mfalme Belshaza, mimi Danieli niliona maono (baada ya maono ya awali yaliyonipata).
In the third year of the reign of King Belshazzar, I, Daniel, had a vision appear to me (after the one that appeared to me at first).
2 Nilipokuwa nikiangalia katika ndoto, niliona kwamba nilikuwa katika mji wa Shushani wenye ngome katika jimbo la Elamu. Niliona katika ndoto kuwa nilikuwa karibu na mfereji wa Ulai.
I saw in the vision, as I was looking, that I was in the fortress of Susa in the province of Elam. I saw in the vision that I was beside the Ulai Canal.
3 Nilitazama juu na nikaona mbele yangu kondoo dume lenye mapembe mawili, limesimama pembeni mwa mfereji. Pembe moja lilikuwa refu kuliko jingine, lakini pembe ndefu ilikuwa inakua pole pole kuliko ile fupi na pembe fupi ilirefuka na kuizidi nyingine.
I looked up and saw before me a ram with two horns, standing beside the canal. One horn was longer than the other, but the longer one grew more slowly than the shorter and was passed up in length by it.
4 Niliona kondoo mme akiishambulia magharibi, kisha kaskazini, na baadaye kusini; hakuna mnyama mwingine aliyeweza kusimama mbele yake. Hakuna yeyote aliyeweza kumwokoa yeyote katika mkono wake. Alifanya chochote kile alichokitaka, na alikuwa mtu mkubwa sana.
I saw the ram charging west, then north, and then south; no other animal could stand before him. None of them was able to rescue anyone out of his hand. He did whatever he wanted, and he became great.
5 Na nilipokuwa natafakari juu ya haya, niliona beberu akitoka magharibi, na kuvuka katika uso wa dunia yote, akikimbia kwa kasi kana kwamba hakuonekana kama aligusa ardhini. Mbuzi huyo alikuwa na pembe kubwa katikati ya macho yake.
As I was thinking about this, I saw a male goat come from the west, who went across the surface of the whole earth, running fast, not seeming to touch the ground. The goat had a large horn between his eyes.
6 Alienda mpaka kwa kondoo aliyekuwa na pembe mbili, nilikuwa nimemwona kondoo dume amesimama katika ukingo wa mfereji na mbuzi alikimbia kumwelekea kondoo dume kwa hasira kali.
He came to the ram who had two horns—I had seen the ram standing on the bank of the canal—and the goat ran toward the ram in a powerful rage.
7 Niliiona mbuzi ikija karibu na kondoo. Mbuzi alikuwa na hasira na kondoo, alimpiga kondoo na alizivunja pembe zake mbili. Kondoo hakuwa na nguvu za kusimama mbele zake. Mbuzi alimgonga kondoo akaanguka chini na akamkanyaga. Hapakuwa na yeyote wa kumwokoa kutoka katika nguvu zake.
I saw the goat come close to the ram. He was very angry at the ram, and he hit the ram and broke off its two horns. The ram was powerless to stand before him. The goat knocked him down to the ground and trampled on him. There was no one who could rescue the ram from his power.
8 Ndipo mbuzi alikua akawa mkubwa, lakini alipokuwa na nguvu, pembe kubwa ilivunjwa, na katika sehemu yake zilichipuka na kukua pembe nne kubwa zilizochomoza kuelekea pepo nne za mbingu.
Then the goat became very large. But when he became strong, the large horn was broken, and in its place four other large horns grew up that pointed toward the four winds of the heavens.
9 Kutoka katika pembe moja ilichipuka pembe nyingine, ilikuwa ndogo hapo awali, lakini baadaye ilikuwa pembe kubwa upande wa kusini, na mashariki, na katika nchi ya uzuri.
Out of one of them grew another horn, little at first, but which became very large in the south, in the east, and in the land of beauty.
10 Pembe ilikuwa kubwa na matokeo yake iliinua vita dhidi ya jeshi la mbinguni. Baadhi ya jeshi na nyota kadhaa zilitupwa chini duniani, na zilikanyagwa.
It became so large as to engage in war with the army of heaven. Some of that army and some of the stars were thrown down to the earth, and it trampled on them.
11 Alizidi kuwa mkubwa, mkubwa kama kamanda wa jeshi la kimungu. Sadaka za kuteketezwa za kila siku ziliondolewa mbali na yeye, na sehemu yake takatifu zilitiwa unajisi.
It made itself to be as great as the commander of the army. It took away from him the regular burnt offering, and the place of his sanctuary was polluted.
12 Kwasababu ya uasi, pembe ya mbuzi ilipewa jeshi, na sadaka za kuteketezwa zitasitishwa. Pembe itautupa ukweli chini ardhini, na itafanikiwa katika kila jambo ilifanyalo.
Because of rebellion, the army will be given over to the goat's horn, and the burnt offering will be stopped. The horn will throw truth down to the ground, and it will succeed in what it does.
13 Kisha nilimsikia mtakatifu mmoja akiongea na mtakatifu mwingine akamjibu, “Mambo haya yatadumu kwa muda gani, maono haya ya sadaka ya kuteketezwa, dhambi ile iletayo uharibifu, ukabidhiajia wa sehemu takatifu, na jeshi la mbinguni kukanyagwa?
Then I heard a holy one speaking and another holy one answering him, “How long will these things last, this vision about the burnt offering, the sin that brings destruction, the handing over of the sanctuary, and heaven's army being trampled on?”
14 Aliniambia, “Itadumu kwa jioni na asubuhi zipatazo 2, 300. Baada ya hapo, mahali patakatifu patawekwa sawa.”
He said to me, “It will last for 2,300 evenings and mornings. After that the sanctuary will be put right.”
15 Wakati mimi Danieli, nilipoona maono, nilijaribu kuyaelewa. na hapo mbele yangu alisimama yule aliyeoneakana kama mtu.
When I, Daniel, had seen the vision, I tried to understand it. Then there stood before me one who looked like a man.
16 Niliisikia sauti ya mtu ikiita katikati ya kingo za mfereji wa Ulai. Alisema, “Gabrieli, msaidie mtu huyu kuelewa maono.”
I heard a man's voice calling between the banks of the Ulai Canal. He said, “Gabriel, help this man understand the vision.”
17 Basi alikuja karibu na mahali niliposimama. Na alipokuja, niliogopa na nilisujudia hadi chini. Aliniambia,”Fahamu, mwana wa mtu, kwamba maono ni kwa ajili ya wakati wa mwisho.”
So he came near where I stood. When he came, I was frightened and prostrated myself on the ground. He said to me, “Understand, son of man, that the vision is for the time of the end.”
18 Alipokuwa anaongea na mimi, nilipata usiingizi mzito nikiwa nimelala kifudifudi. Kisha alinishika na kunisimamisha.
When he spoke to me, I fell into a deep sleep with my face to the ground. Then he touched me and made me stand up.
19 Akaniambia, “Tazama, nitakuonyesha kile kitachotokea baadaye katika kipindi cha ghadhabu, kwasababu maono haya yanahusu wakati wa mwisho uliopangwa.
He said, “See, I will show you what will happen later in the time of wrath, because the vision concerns the appointed time for the end.
20 Na kuhusu kondoo mme uliyemwona, yule mwenye pembe mbili - ni wafalme wawili wa Umedi na Uajemi.
As for the ram you saw, the one that had two horns—they are the kings of Media and Persia.
21 Mbuzi dume ni mfalme wa Ugiriki. Pembe kubwa katikati ya macho yake ni mfalme wa kwanza.
The male goat is the king of Greece. The large horn between his eyes is the first king.
22 Na kuhusu pembe iliyovunjika, ambayo katika nafasi yake pembe zingine nne zilichipuka - hizi ni falme nne zitakazoinuka kutoka katika taifa lake, lakini hazitakuwa na nguvu kubwa.
As for the horn that was broken, in the place of which four others arose—four kingdoms will arise from his nation, but not with his great power.
23 Katika siku zijazo za falme hizo, wakati ambapo wahalifu watakuwa wamefikia kikomo chao, mfalme mwenye uso katili, na yeye mwenye akili sana, atainuka.
At the latter time of those kingdoms, when the transgressors shall have reached their limit, a grim-faced king, one who is very intelligent, will arise.
24 Nguvu zake zitakuwa kubwa, lakini si kwa nguvu zake mwenyewe. Atakuwa wa kustaajabisha kwa kile atakachokuwa anakiharibu; atafanya na kufanikiwa. Atawaangamiza watu wenye nguvu, watu miongoni wa watakatifu.
His power will be great—but not by his own power. He will be amazing in what he destroys; he will act and succeed. He will destroy powerful people, people among the holy ones.
25 Ataufanya udanganyifu usitawi chini ya mkono wake kwasababu ya ujanja wake. Atawaangamiza watu wengi bila kutegemea. Atainuka pia hata kinyume cha Mfalme wa wafalme, na atavunjwa, lakini si kwa mkono wowote wa binadamu.
By his craftiness he will make deceit prosper under his hand. He will become great in his own mind. He will unexpectedly destroy many people. He will even rise up against the King of kings, and he will be broken, but not by any human hand.
26 Maono kuhusu jioni na asubuhi ulizoambiwa ni ya kweli. Lakini uyafunge maono haya, kwa kuwa yanahusu siku nyingi za wakati ujao.
The vision about the evenings and mornings that has been told is true. But seal up the vision, for it refers to many days in the future.”
27 Ndipo mimi, Danieli nilichoka sana na nikalala nikiwa dhaifu kwa siku kadhaa. Kisha nikainuka na nikaenda kufanya kazi za mfalme. Lakini nilikuwa nimetishwa sana na maono, na hapakuwa na mtu yeyote aliyeweza kuyaelewa.
Then I, Daniel, was overcome and lay weak for several days. Then I got up, and went about the king's business. But I was appalled by the vision, and there was no one who understood it.

< Danieli 8 >