< Danieli 5 >

1 Mfalme Belshaza alifanya sherehe kubwa kwa kwa ajili ya wakuu wake wa kuheshimiwa wapatao elfu moja, na alikunywa divai mbele yao wote watu elfu moja.
Belshazzar king [the] to make feast great to/for noble his thousand and to/for before thousand [the] wine [the] to drink
2 Wakati Belshaza alipokuwa akionja divai, alitoa agizo la kuleta vyombo vilivyotengenezwa kwa dhahabu au kwa fedha ambavyo Nebukadneza baba yake alikuwa amevichukua kutoka katika hekalu huko Yerusalemu, ambavyo yeye, na wakuu wake, na wake zake, na masuria waliweza kuvinywea.
Belshazzar to say in/on/with command wine [the] to/for to come to/for utensil gold [the] and silver [the] that to go out Nebuchadnezzar father my from temple [the] that in/on/with Jerusalem and to drink in/on/with them king [the] and noble his consort his and concubine his
3 Watumishi walivileta vyombo ya dhahabu vilivyokuwa vimechukulia katika hekalu, nyumba ya Mungu huko Yerusalemu. Mfalme na wakuu wake, na wake zake na masuria walivinywea.
in/on/with then to come utensil gold [the] that to go out from temple [the] that house god [the] that in/on/with Jerusalem and to drink in/on/with them king [the] and noble his consort his and concubine his
4 Walikunywa divai na kuzisifu sanamu zao zilizotengenezwa kwa dhahabu na fedha, shaba, chuma, mbao na mawe.
to drink wine [the] and to praise to/for god gold [the] and silver [the] bronze [the] iron [the] wood [the] and stone [the]
5 Kwa wakati huo huo vidole vya mkono wa mtu vilionekana mbele ya kinara cha taa na kuandika katika ukuta uliopigwa lipu katika ikulu ya mfalme. Mfalme aliweza kuona sehemu ya mkono ulipokuwa unaandika.
in/on/with her moment [the] (to go out *Qk) digit that hand man and to write to/for before lampstand [the] since plaster [the] that wall temple: palace [the] that king [the] and king [the] to see palm hand [the] that to write
6 Ndipo uso wa mfalme ulibadilika na mawazo yake yalimwogopesha; miguu yake haikuweza kumfanya asimame, na magoti yake yalikuwa yakigongana kwa pamoja.
then king [the] splendor his to change him and thought his to dismay him and joint loin his to loose and knee his this to/for this to knock
7 Mfalme alitoa agizo kwa kupiga kelele, waletwe ndani wale ambao hudai wanaweza kuzungumza na wafu, watu wenye hekima, na wataalamu wa nyota. Mfalme akawaambia wale waliojulikana kwa hekima katika Babeli, “Yeyote atakayeyaeleza maandishi haya na maana yake atavikwa nguo za zambarau na atavikwa na mkufu wa dhahabu shingoni mwake. Naye atakuwa mtawala wa tatu wa juu kwa mamlaka katika ufalme.”
to read king [the] in/on/with strength to/for to come to/for enchanter [the] (Chaldean my *QK) and to determine [the] to answer king [the] and to say to/for wise Babylon that all man that to read inscription [the] this and interpretation his to show me purple [the] to clothe (and chain [the] *Qk) that gold [the] since neck his and third in/on/with kingdom [the] to rule
8 Ndipo watu wote wa mfalme walikuwa wakijulikana kwa hekima yao waliingia ndani, lakini hawakuweza kuyasoma maandishi wala kueleza maana yake kwa mfalme.
then (to come *Qk) all wise king [the] and not be able inscription [the] to/for to read (and interpretation his *QK) to/for to know to/for king [the]
9 Kisha mfalme Belshaza alishitushwa sana na mwonekano wa uso wake ulibadilika. Wakuu wake nao walishangazwa sana.
then king [the] Belshazzar greatly to dismay and splendor his to change since him and noble his be perplexed
10 Ndipo sasa malkia alikuja katika nyumba ya sherehe kwasababu ya kile ambacho mfalme na wakuu wake walikuwa wamekisema. Malkia akasema, “Mfalme na aishi milele! Usiache mawazo yako yakakusumbua. Usiruhusu mwonekano wa uso wako ubadilike.
queen [the] to/for before word king [the] and noble his to/for house feast [the] (to come *Qk) to answer queen [the] and to say king [the] to/for perpetuity to live not to dismay you thought your and splendor your not to change
11 Kuna mtu katika ufalme wako ambaye ana roho ya miungu watakatifu dani yake. Katika siku za baba yako, mwanga na weledi na hekima ya miungu ilipatikana ndani yake. Mfalme Nebukadneza, baba yako mfalme, alimfanya kuwa mkuu wa waganga, pamoja na mkuu wa wale wanazungumza na wafu, na wa wenye hekima, na wa wataalamu wa nyota.
there is man in/on/with kingdom your that spirit god holy in/on/with him and in/on/with day father your illumination and insight and wisdom like/as wisdom god to find in/on/with him and king [the] Nebuchadnezzar father your great magician enchanter Chaldean to determine to stand: establish him father your king [the]
12 Roho bora, ufahamu, weledi, kutafsiri ndoto, kufafanua mafumbo na kutatua matatizo - hizi ni sifa zilizopatikana kwa mtu huyu Danieli, ambaye mfalme alimwita Belteshaza. Sasa mwiteni Danieli naye atawaambia maana ya kile kilichoandikwa.”
like/as to/for before: because that spirit preeminent and knowledge and insight to interpret dream and explanation riddle and to loose joint to find in/on/with him in/on/with Daniel that king [the] to set: make name his Belteshazzar now Daniel to read and interpretation [the] to show
13 Ndipo Danieli alipoletwa mbele ya mfalme. Mfalme akamwambia, “Wewe ni yule Danieli, mmoja kati ya watu wa mateka wa Yuda, ambao baba yangu mfalme aliwaleta kutoka Yuda.
in/on/with then Daniel to come before king [the] to answer king [the] and to say to/for Daniel (you *Qk) he/she/it Daniel that from son: type of captivity [the] that Judah that to come king [the] father my from Judah
14 Nimesikia habari kukuhusu wewe, kwamba roho ya miungu iko ndani yako, na ya kwamba mwanga na ufahamu na hekima bora inapatikana ndani yako.
and to hear (since you *Qk) that spirit god in/on/with you and illumination and insight and wisdom preeminent to find in/on/with you
15 Na sasa watu wanaojulikana kwa hekima na wale wanaozungumza na wafu, wamekwisha kuletwa mbele yangu, ili kusoma maandishi haya na kunijulisha maana ya tafsiri yake, lakini hawakuweza kunijulisha tafsiri yake.
and now to come before me wise [the] enchanter [the] that inscription [the] this to read and interpretation his to/for to know me and not be able interpretation word [the] to/for to show
16 Nimesikia kwamba unaweza kutoa tafsiri na kutatua matatizo. Sasa kama utaweza kusoma maandishi na kuniambia maana yake, utavikwa nguo za zambarau na kuwa na kuvalishwa mkufu wa dhahabu shingoni mwako, na utakuwa mtawala wa tatu mwenye mamlaka katika ufalme.”
and me to hear (since you *Qk) that (be able *Qk) interpretation to/for to interpret and joint to/for to loose now if (be able *Qk) inscription [the] to/for to read and interpretation his to/for to know me purple [the] to clothe (and chain [the] *Qk) that gold [the] since neck your and third [the] in/on/with kingdom [the] to rule
17 Kisha Danieli akajibu mbele ya mfalme, “Zawadi yako na iwe kwa ajili yako mwenyewe, na thawabu yako na umpe mtu mwingine. Hata hivyo, mfalme, nitakusomea maandishi na nitakwaambia maana.
in/on/with then to answer Daniel and to say before king [the] gift your to/for you to be and reward your to/for another to give nevertheless inscription [the] to read to/for king [the] and interpretation [the] to know him
18 Na juu yako, Ewe mfalme, Mungu Aliye juu sana alimpa Nebukadneza baba yako ufalme, ukuu, heshima na enzi.
(you *Qk) king [the] god [the] (Most High [the] *Qk) kingdom [the] and greatness [the] and honor [the] and honor [the] to give to/for Nebuchadnezzar father your
19 Na kwasababu ya ukuu huo, Mungu alimpa watu wote, mataifa, na lugha walimtetemekea na kumwogopa. Aliwauwa wale aliotaka wafe na aliwaacha hai wale aliotaka waishi. Aliwainua wale aliowataka, na aliwashusha wale aliowataka.
and from greatness [the] that to give to/for him all people [the] people [the] and tongue [the] to be (to tremble *Qk) and to fear from before him that to be to will to be to slay and that to be to will to be to live and that to be to will to be to rise and that to be to will to be be low
20 Lakini wakati moyo ulipokuwa na kiburi na roho yake ilifanywa kuwa mgumu na kwasababu hiyo alitenda kwa kiburi, alishushwa kutoka kiti chake cha enzi cha kifalme, na waliiondoa enzi yake.
and like/as that to rise heart his and spirit his to grow strong to/for be proud to descend from throne kingdom his and honor [the] to pass on/over/away from him
21 Aliondolewa katika ubinadamu, alikuwa na akili za mnyama, na aliishi na punda wa mwituni. Alikula majani kama ng'ombe. Mwili wake ulilowanishwa kwa umande wa kutoka mbinguni mpaka pale alipojifunza kwamba Mungu Aliye Juu anatawala juu ya falme za watu na ya kwamba humweka mtu yeyote amtakaye juu yake.
and from son: type of man [the] to chase away and heart his with beast [the] (be like *QK) and with wild donkey [the] dwelling his grass [the] like/as bullock to feed him and from dew heaven [the] body his to drench till that to know that ruling god [the] (Most High [the] *Qk) in/on/with kingdom man [the] and to/for who? that to will to stand: establish (since her *Qk)
22 Wewe mwana wake, Belshaza, haujaunyenyekeza moyo wako, ingawa aliyajua haya yote.
(and you *Qk) son: child his Belshazzar not be low heart your like/as to/for before: because that all this to know
23 Umejiinua mwenyewe kinyume cha Bwana wa mbinguni. Katika nyumba yake walikuletea vyombo ambavyo wewe, wakuu wako, wake zako na masuria wako walivinywea, na kisha ukaisifia sana sanamu zilitengenezwa kwa fedha na dhahabu, shaba, chuma, mbao, na mawe - sanamu ambazo haziwezi kuona, kusikia wa kujua kitu chochote. Haujamheshimu Mungu ambaye anaishikilia pumzi yako katika mkono wake na ambaye anazijua njia zako zote.
and since lord heaven [the] to rise and to/for utensil [the] that house his to come (before you and you and noble your *Qk) consort your and concubine your wine [the] to drink in/on/with them and to/for god silver [the] and gold [the] bronze [the] iron [the] wood [the] and stone [the] that not to see and not to hear and not to know to praise and to/for god [the] that breath your in/on/with hand his and all way your to/for him not to honor
24 Ndipo Mungu aliutuma mkono kutoka katika makao yake na maandishi haya yaliandikwa.
in/on/with then from before him to send palm [the] that hand [the] and inscription [the] this to sign
25 Haya ndiyo maandishi ambayo yaliandikwa: 'Mene, Mene, Tekeli na Peresin.'
and this inscription [the] that to sign mina mina shekel and half
26 Maana yake ni: 'Mene,' 'Mungu ameuhesabu ufalme wako na ameukomesha.'
this interpretation word [the] mina to reckon/appoint god [the] kingdom your and be complete her
27 'Tekeli' 'umepimwa katika mizani na umeonekana umepungua.'
shekel to weigh in/on/with scale [the] and to find lacking
28 'Peresi' 'ufalme wako umegawanyika na wamepewa Wamedi na Waajemi.'”
half to divide kingdom your and to give to/for Mede and Persia
29 Ndipo Belshaza alitoa agizo, na walimvalisha Danieli mavazi ya zambarau. Mkufu wa dhahabu walimvisha shingoni, na mfalme alitoa tamko juu ya Danieli kuwa atakuwa mtawala mwenye mamlaka ya nafasi ya tatu katika ufalme.
in/on/with then to say Belshazzar and to clothe to/for Daniel purple [the] (and chain [the] *Qk) that gold [the] since neck his and to proclaim since him that to be ruling third [the] in/on/with kingdom [the]
30 Usiku ule Belshaza, mfalme wa Babeli aliuawa,
in/on/with him in/on/with night [the] to slay Belshazzar king [the] (Chaldean [the] *Qk)
31 na Dario Mwajemi aliuchukua ufalme alipokuwa na miaka ipatayo sitini na miwili.
and Darius (Mede [the] *QK) to receive kingdom [the] like/as son year sixty and two

< Danieli 5 >