< Danieli 5 >

1 Mfalme Belshaza alifanya sherehe kubwa kwa kwa ajili ya wakuu wake wa kuheshimiwa wapatao elfu moja, na alikunywa divai mbele yao wote watu elfu moja.
Цар Валтасар направи голям пир на хиляда от големците си, и пиеше вино пред хилядата.
2 Wakati Belshaza alipokuwa akionja divai, alitoa agizo la kuleta vyombo vilivyotengenezwa kwa dhahabu au kwa fedha ambavyo Nebukadneza baba yake alikuwa amevichukua kutoka katika hekalu huko Yerusalemu, ambavyo yeye, na wakuu wake, na wake zake, na masuria waliweza kuvinywea.
Когато пиеше виното, Валтасар заповяда да донесат златните и сребърните съдове, които дядо му Навуходоносор беше задигнал от храма, който бе в Ерусалим, за да пият с тях царят и големците му, жените му и наложниците му.
3 Watumishi walivileta vyombo ya dhahabu vilivyokuwa vimechukulia katika hekalu, nyumba ya Mungu huko Yerusalemu. Mfalme na wakuu wake, na wake zake na masuria walivinywea.
Тогава донесоха златните съдове, които бяха задигнати от храма на Божия дом, който бе в Ерусалим; и с тях пиеха царят и големците му, жените му и наложниците му.
4 Walikunywa divai na kuzisifu sanamu zao zilizotengenezwa kwa dhahabu na fedha, shaba, chuma, mbao na mawe.
Пиеха вино, и хвалеха златните, сребърните, медните, железните, дървените и каменните богове.
5 Kwa wakati huo huo vidole vya mkono wa mtu vilionekana mbele ya kinara cha taa na kuandika katika ukuta uliopigwa lipu katika ikulu ya mfalme. Mfalme aliweza kuona sehemu ya mkono ulipokuwa unaandika.
В същия час се появиха пръсти на човешка ръка, които пишеха, срещу светилника, по мазилката на стената на царския палат; и царят видя тая част от ръката, която пишеше.
6 Ndipo uso wa mfalme ulibadilika na mawazo yake yalimwogopesha; miguu yake haikuweza kumfanya asimame, na magoti yake yalikuwa yakigongana kwa pamoja.
Тогава изгледът на лицето на царя се измени и мислите му го смущаваха, така щото ставите на кръста му се разхлабиха, и колената му се удряха едно о друго.
7 Mfalme alitoa agizo kwa kupiga kelele, waletwe ndani wale ambao hudai wanaweza kuzungumza na wafu, watu wenye hekima, na wataalamu wa nyota. Mfalme akawaambia wale waliojulikana kwa hekima katika Babeli, “Yeyote atakayeyaeleza maandishi haya na maana yake atavikwa nguo za zambarau na atavikwa na mkufu wa dhahabu shingoni mwake. Naye atakuwa mtawala wa tatu wa juu kwa mamlaka katika ufalme.”
Царят извика с голям глас да въведат вражарите, халдейците, и астролозите, на които вавилонски мъдреци царят проговаряйки, рече: Който прочете това писание и ми яви значението му ще бъде облечен в багреница, златна огърлица ще се окачи около шията му, и ще бъде един от тримата, които ще владеят царството.
8 Ndipo watu wote wa mfalme walikuwa wakijulikana kwa hekima yao waliingia ndani, lakini hawakuweza kuyasoma maandishi wala kueleza maana yake kwa mfalme.
Влязоха прочее всичките царски мъдреци; но не можаха да прочетат написаното, нито да явят на царя значението му.
9 Kisha mfalme Belshaza alishitushwa sana na mwonekano wa uso wake ulibadilika. Wakuu wake nao walishangazwa sana.
Тогава цар Валтасар се смути много, изгледът на лицето му се измени, и големците му се смаяха.
10 Ndipo sasa malkia alikuja katika nyumba ya sherehe kwasababu ya kile ambacho mfalme na wakuu wake walikuwa wamekisema. Malkia akasema, “Mfalme na aishi milele! Usiache mawazo yako yakakusumbua. Usiruhusu mwonekano wa uso wako ubadilike.
От думите на царя и на големците му овдовялата царица влезе в къщата на пируването; и царицата проговаряйки, рече: Царю, да си жив до века! Да те не смущават мислите ти, нито да се изменява лицето ти.
11 Kuna mtu katika ufalme wako ambaye ana roho ya miungu watakatifu dani yake. Katika siku za baba yako, mwanga na weledi na hekima ya miungu ilipatikana ndani yake. Mfalme Nebukadneza, baba yako mfalme, alimfanya kuwa mkuu wa waganga, pamoja na mkuu wa wale wanazungumza na wafu, na wa wenye hekima, na wa wataalamu wa nyota.
Има човек в царството ти, в когото е духът на светите богове; и в дните на дядо ти, в него се намериха светлина, разум, и мъдрост като мъдростта на боговете; и дядо ти Навуходоносор, -дядо ти, казвам, царю, - го постави началник на врачовете, на вражарите, на халдейците, и на астролозите,
12 Roho bora, ufahamu, weledi, kutafsiri ndoto, kufafanua mafumbo na kutatua matatizo - hizi ni sifa zilizopatikana kwa mtu huyu Danieli, ambaye mfalme alimwita Belteshaza. Sasa mwiteni Danieli naye atawaambia maana ya kile kilichoandikwa.”
защото превъзходен дух и знание, разум за тълкуване сънища, изясняване на гатанки, и разрешаване на недоумения се намираха в тоя Даниил, когото царят преименува Валтасасар. Сега нека се повика Даниил, и той ще покаже значението на написаното.
13 Ndipo Danieli alipoletwa mbele ya mfalme. Mfalme akamwambia, “Wewe ni yule Danieli, mmoja kati ya watu wa mateka wa Yuda, ambao baba yangu mfalme aliwaleta kutoka Yuda.
Тогава Даниил биде въведен пред царя. Царят проговаряйки, рече на Даниила: Ти ли си оня Даниил, който си от пленените юдейци, които дядо ми царят доведе от Юдея?
14 Nimesikia habari kukuhusu wewe, kwamba roho ya miungu iko ndani yako, na ya kwamba mwanga na ufahamu na hekima bora inapatikana ndani yako.
Чух за тебе, че духът на боговете бил в тебе, и че светлина, разум, и превъзходна мъдрост се намирали в тебе.
15 Na sasa watu wanaojulikana kwa hekima na wale wanaozungumza na wafu, wamekwisha kuletwa mbele yangu, ili kusoma maandishi haya na kunijulisha maana ya tafsiri yake, lakini hawakuweza kunijulisha tafsiri yake.
И сега бяха въведени пред мене мъдреците и вражарите, за да прочетат това писание и ми явят значението му; но не можаха да покажат значението на това нещо.
16 Nimesikia kwamba unaweza kutoa tafsiri na kutatua matatizo. Sasa kama utaweza kusoma maandishi na kuniambia maana yake, utavikwa nguo za zambarau na kuwa na kuvalishwa mkufu wa dhahabu shingoni mwako, na utakuwa mtawala wa tatu mwenye mamlaka katika ufalme.”
Но аз чух за тебе, че си могъл да тълкуваш, и да разрешаваш недоумения; прочее, ако можеш да прочетеш написаното и да ми явиш значението му, ще бъдеш облечен в багреница, златна огърлица ще се окачи около шията ти, и ти ще бъдеш един от тримата, които ще владеят царството.
17 Kisha Danieli akajibu mbele ya mfalme, “Zawadi yako na iwe kwa ajili yako mwenyewe, na thawabu yako na umpe mtu mwingine. Hata hivyo, mfalme, nitakusomea maandishi na nitakwaambia maana.
Тогава в отговор Даниил рече пред царя: Подаръците ти нека останат за тебе, и дай на другиго наградите си; все пак аз ще прочета на царя написаното, и ще му явя значението му.
18 Na juu yako, Ewe mfalme, Mungu Aliye juu sana alimpa Nebukadneza baba yako ufalme, ukuu, heshima na enzi.
Царю, Всевишният Бог даде на дядо ти Навуходоносора царство и величие, сила и чест;
19 Na kwasababu ya ukuu huo, Mungu alimpa watu wote, mataifa, na lugha walimtetemekea na kumwogopa. Aliwauwa wale aliotaka wafe na aliwaacha hai wale aliotaka waishi. Aliwainua wale aliowataka, na aliwashusha wale aliowataka.
и поради величието, което му даде, всичките племена, народи, и езици трепереха и се бояха пред него; когото искаше убиваше, и когото искаше опазваше жив, когото искаше възвишаваше, и когото искаше унижаваше.
20 Lakini wakati moyo ulipokuwa na kiburi na roho yake ilifanywa kuwa mgumu na kwasababu hiyo alitenda kwa kiburi, alishushwa kutoka kiti chake cha enzi cha kifalme, na waliiondoa enzi yake.
Но когато се надигна сърцето му, и духът му закоравя та да постъпва гордо, той биде свален от царския си престол, славата му се отне от него,
21 Aliondolewa katika ubinadamu, alikuwa na akili za mnyama, na aliishi na punda wa mwituni. Alikula majani kama ng'ombe. Mwili wake ulilowanishwa kwa umande wa kutoka mbinguni mpaka pale alipojifunza kwamba Mungu Aliye Juu anatawala juu ya falme za watu na ya kwamba humweka mtu yeyote amtakaye juu yake.
и биде изгонен измежду човеците; сърцето му стана като на животните, и жилището му бе между живите осли; хранеха го с трева като говедата, и тялото му се мокреше от небесната роса, додето призна, че Всевишният Бог владее над царството на човеците, и когото иска поставя над него.
22 Wewe mwana wake, Belshaza, haujaunyenyekeza moyo wako, ingawa aliyajua haya yote.
А ти, негов внук, Валтасаре, не си смирил сърцето си, ако и да знаеше всичко това,
23 Umejiinua mwenyewe kinyume cha Bwana wa mbinguni. Katika nyumba yake walikuletea vyombo ambavyo wewe, wakuu wako, wake zako na masuria wako walivinywea, na kisha ukaisifia sana sanamu zilitengenezwa kwa fedha na dhahabu, shaba, chuma, mbao, na mawe - sanamu ambazo haziwezi kuona, kusikia wa kujua kitu chochote. Haujamheshimu Mungu ambaye anaishikilia pumzi yako katika mkono wake na ambaye anazijua njia zako zote.
но си се надигнал против небесния Господ; и донесоха пред тебе съдовете на дома му, с които пиехте вино ти и големците ти, жените ти и наложниците ти; и ти славослови сребърните, златните, медните, железните, дървените и каменните богове, които не виждат, нито чуват, нито разбират; а Бога, в Чиято ръка е дишането ти, и в Чиято власт са всичките твои пътища, не си възвеличил.
24 Ndipo Mungu aliutuma mkono kutoka katika makao yake na maandishi haya yaliandikwa.
Затова, от Него е била изпратена частта от ръката, и това писание се написа.
25 Haya ndiyo maandishi ambayo yaliandikwa: 'Mene, Mene, Tekeli na Peresin.'
И ето, писанието, което се написа: М'не, М'не, Т'кел, упарсин.
26 Maana yake ni: 'Mene,' 'Mungu ameuhesabu ufalme wako na ameukomesha.'
Ето и значението на това нещо: М'не, Бог е преброил дните на твоето царство, и го е свършил;
27 'Tekeli' 'umepimwa katika mizani na umeonekana umepungua.'
Т'кел, Претеглен си на везните, и си бил намерен недостатъчен;
28 'Peresi' 'ufalme wako umegawanyika na wamepewa Wamedi na Waajemi.'”
П'рес, Раздели се царството ти, и се даде на мидяните и персите.
29 Ndipo Belshaza alitoa agizo, na walimvalisha Danieli mavazi ya zambarau. Mkufu wa dhahabu walimvisha shingoni, na mfalme alitoa tamko juu ya Danieli kuwa atakuwa mtawala mwenye mamlaka ya nafasi ya tatu katika ufalme.
Тогава Валтасар заповяда, та облякоха Даниила в багреницата, окачиха златната огърлица около шията му, и прогласиха за него да бъде един от тримата, които да владеят царството.
30 Usiku ule Belshaza, mfalme wa Babeli aliuawa,
В същата нощ царят на халдейците Валтасар биде убит.
31 na Dario Mwajemi aliuchukua ufalme alipokuwa na miaka ipatayo sitini na miwili.
И мидянинът Дарий, който бе около на шестдесет и две години, взе царството.

< Danieli 5 >