< Danieli 3 >

1 Mfalme Nebukadneza alitengeneza sanamu ya dhahabu ambayo ilikuwa na urefu wa dhiraa sitini na upana dhiraa sita. Aliiweka katika uwanda wa Dura katika jimbo la Babeli.
Nebuchadnezzar the king hath made an image of gold, its height sixty cubits, its breadth six cubits; he hath raised it up in the valley of Dura, in the province of Babylon;
2 Kisha Nebukadneza alituma ujumbe wa kuwaita pamoja magavana wote wa majimbo, magavana wa mikoa, na magavana wa vijiji, pamoja na na washauiri, wahazini, waamuzi, mahakimu, na maafisa wengine wakuu wa majimbo ili waje kwa ajili ya uzinduzi wa sanamu aliyokuwa ameiweka.
and Nebuchadnezzar the king hath sent to gather the satraps, the prefects, and the governors, the honourable judges, the treasurers, the counsellors, the sheriffs, and all the rulers of the province, to come to the dedication of the image that Nebuchadnezzar the king hath raised up.
3 Ndipo magavana wa majimbo, magavana wa mikoa, na magavana wa vijiji, pamoja na washauri, wahasibu, waamuzi, mahakimu, na maafisa wa juu wa majimbo walikusanyika kwa pamoja katika uzinduzi wa sanamu ambayo Nebukadneza aliyokuwa ameiweka. Walisimama mbele yake.
Then are gathered the satraps, the prefects, and the governors, the honourable judges, the treasurers, the counsellors, the sheriffs, and all the rulers of the province, to the dedication of the image that Nebuchadnezzar the king hath raised up: and they are standing before the image that Nebuchadnezzar hath raised up.
4 Kisha mtangazaji alipiga kelele, “Enyi watu, mataifa, na lugha mmeamriwa
And a crier is calling mightily: 'To you they are saying: O peoples, nations, and languages!
5 kwamba mtakaposikia sauti za pembe, filimbi, ala za muziki, zeze, vinubi na zumari na aina zote za muziki, ni sharti kuanguka na kuisujudia ninyi wenyewe sanamu ya dhahabu ambayo Mfalme Nebukadneza alikuwa ameiweka.
at the time that ye hear the voice of the cornet, the flute, the harp, the sackbut, the psaltery, the symphony, and all kinds of music, ye fall down and do obeisance to the golden image that Nebuchadnezzar the king hath raised up:
6 Na yeyote asiyeanguka na kuiabuda, kwa wakati huo huo atatupwa katika tanuru la moto.”
and whoso doth not fall down and do obeisance, in that hour he is cast into the midst of a burning fiery furnace.'
7 Basi watu walilposikia sauti za pembe, filimbi, ala za muziki, zeze, vinubi na zumari na aina zote za muziki, watu wote, mataifa na lugha walianguka na kuisujudia wao wenyewe sanamu ya dhahabu ambayo Nebukadneza mfalme alikuwa ameiweka.
Therefore at that time, when all the peoples are hearing the voice of the cornet, the flute, the harp, the sackbut, the psaltery, and all kinds of music, falling down are all the peoples, nations and languages, doing obeisance to the golden image that Nebuchadnezzar the king hath raised up.
8 Wakati huu baadhi ya Walkadayo walikuja na kuleta mashitaka kinyume na Wayahudi.
Therefore at that time drawn near have certain Chaldeans, and accused the Jews;
9 Walimwambia mfalme Nebukadneza, “mfalme aishi milele!
they have answered, yea, they are saying to Nebuchadnezzar the king, 'O king, to the ages live!
10 Ewe mfalme, umeweka amri kwamba kila mtu aisikiye sauti ya pembe, filimbi, ala za muziki, zeze, vinubi na zumari, na aina zote za muziki, lazima kuanguka na kuisujudia sanamu ya dhahabu.
Thou, O king, hast made a decree that every man who doth hear the voice of the cornet, the flute, the harp, the sackbut, the psaltery, and the symphony, and all kinds of music, doth fall down and do obeisance to the golden image;
11 Mtu yeyote asiyeanguka na kuiabudu sharti atupwe katika tanuru linalowaka moto.
and whoso doth not fall down and do obeisance, is cast into the midst of a burning fiery furnace.
12 Sasa kuna baadhi ya Wayahudi ambao umewaweka juu masuala ya jimbo la Babeli; majina yao ni Shadraka, Meshaki, na Abednego. Mfalme, hawa watu hawakutii wewe. Hawataiabudu, kuitumikia wala kuisujudia wenyewe sanamu ya dhahabu ambayo umeiweka.”
There are certain Jews whom thou hast appointed over the work of the province of Babylon — Shadrach, Meshach, and Abed-Nego, these men have not made of thee, O king, [any] regard; thy gods they are not serving, and to the golden image thou hast raised up — are not making obeisance.'
13 Ndipo Nebukadneza alijawa na hasira na ghadhabu, aliagiza kwamba Shadraka, Meshaki na Abednego waletwe kwake. Hivyo, waliwalete hawa watu mbele ya mfalme.
Then Nebuchadnezzar, in anger and fury, hath said to bring in Shadrach, Meshach, and Abed-Nego. Then these men have been brought in before the king.
14 Nebukadneza aliwaambia, “Je mmejipanga katika akili zenu, enyi Shadraka, Meshaki na Abedinego, kwamba hamtaiabudu miungu yangu wala kuisujudia wenyewe sanamu ile ya dhahabu ambayo nimeiweka?
Nebuchadnezzar hath answered and said to them, 'Is [it] a laid plan, O Shadrach, Meshach, and Abed-Nego — my gods ye are not serving, and to the golden image that I have raised up ye are not doing obeisance?
15 Basi sasa kama mko tayari - mtakaposikia sauti pembe, filimbi, ala za muziki, zeze, vinumbi na zumari, aina zote za muziki - kuanguka chini na kuisujudia wenyewe sanamu ile ambayo nimeitengeneza, mambo yote yatakuwa mazuri. Lakini kama hamtaiabudu, mtatupwa mara katika tanuru la moto. Ni mungu gani atakayeweza kuwaokoa katika mikono yangu?”
Now, lo, ye are ready, so that at the time that ye hear the voice of the cornet, the flute, the harp, the sackbut, the psaltery, and the symphony, and all kinds of music, ye fall down and do obeisance to the image that I have made! — and lo, ye do no obeisance — in that hour ye are cast into the midst of a burning fiery furnace; who is that God who doth deliver you out of my hands?'
16 Shadraka, Meshaki, na Abednego wakamjibu mfalme, “Nebukadneza, hatuhitaji kukujibu wewe katika jambo hili.
Shadrach, Meshach, and Abed-Nego have answered, yea, they are saying to the king Nebuchadnezzar, 'We have no need concerning this matter to answer thee.
17 Kama kuna jibu, ni kwamba Mungu wetu ambaye tunamtumikia anaweza kutuhifadhi sisi salama katika katika tanuru la moto, na atatuokoa sisi katika mkono wako, mfalme.
Lo, it is; our God whom we are serving, is able to deliver us from a burning fiery furnace; and from thy hand, O king, He doth deliver.
18 Kama sivyo, na ijulikane kwako, wewe mfalme, kwamba hatutaiabudu miungu yako, na wala hatutaisujudia wenyewe sanamu ya dhahabu uliyoiweka.
And lo — not! be it known to thee, O king, that thy gods we are not serving, and to the golden image thou hast raised up we do no obeisance.'
19 Ndipo Nebukadneza alijawa na ghadhabu; mwonekano wa uso wake ulibadilika kinyume na Shadraka, Meshaki na Abedinego. Aliagiza kuwa tanuru lichochewe ukali mara saba zaidi kuliko lilivyokuwa kawaida.
Then Nebuchadnezzar hath been full of fury, and the expression of his face hath been changed concerning Shadrach, Meshach, and Abed-Nego; he answered and said to heat the furnace seven times above that which it is seen to be heated;
20 Kisha aliwaamuru baadhi ya watu wenye nguvu katika jeshi lake kuwafunga Shadraka, Meshaki na Abednego na kuwatupa katika tanuru liwakalo moto.
and to certain mighty men who [are] in his force he hath said to bind Shadrach, Meshach, and Abed-Nego, to cast into the burning fiery furnace.
21 Walifungwa akali wakiwa wamevaa nguo zao, kanzu, kilemba, na mavazi mengine, na walitupa katika tanuru liwakalo moto.
Then these men have been bound in their coats, their tunics, and their turbans, and their clothing, and have been cast into the midst of the burning fiery furnace.
22 Kwasababu ya agizo la mfalme lilifuatwa na tanuru lilikuwa na joto sana, miali ya moto iliwaua watu waliowatupa Shadraka, Meshaki, na Abedinego.
Therefore, because that the word of the king is urgent, and the furnace heated exceedingly, those men who have taken up Shadrach, Meshach, and Abed-Nego — killed them hath the spark of the fire.
23 Hawa wanaume watatu, Shadraka, Meshaki, na Abednego, waliangukia katika tanuru liwakalo moto wakali wamefungwa.
And these three men, Shadrach, Meshach, and Abed-Nego, have fallen down in the midst of the burning fiery furnace — bound.
24 Kisha Nebukadneza mfalme alishangazwa na alisimam haraka. Aliwauliza washauri wake, “Je hatukutupa watu watatu wakiwa wamefungwa katika moto?” Nao walimjibu mfalme, “Hakika mfalme.”
Then Nebuchadnezzar the king hath been astonished, and hath risen in haste; he hath answered and said to his counsellors, 'Have we not cast three men into the midst of the fire — bound?' They have answered and are saying to the king, 'Certainly, O king.'
25 Alisema, “Lakini ninaona watu wanne ambao hawajafungwa wakizunguka katika moto, na hawajaumizwa. Mng'ao wa mtu wa nne ni kama mwana wa miungu.”
He answered and hath said, 'Lo, I am seeing four men loose, walking in the midst of the fire, and they have no hurt; and the appearance of the fourth [is] like to a son of the gods.'
26 Ndipo Nebukadneza aliposogea karibu na mlango wa tanuru liwakalo moto na akaaita, “Shadraka, Meshaki na Abednego, watumishi wa Mungu Aliye Juu, tokeni nje! Njooni hapa! Ndipo Shadraka, Meshaki na Abednego walitoka nje ya moto.
Then Nebuchadnezzar hath drawn near to the gate of the burning fiery furnace; he hath answered and said, 'Shadrach, Meshach, and Abed-Nego, servants of God Most High come forth, yea, come;' then come forth do Shadrach, Meshach, and Abed-Nego, from the midst of the fire;
27 Magavana wa majimbo, magavana wengine, na washauri wa mfalme waliokuwa wamekusanyika kwa pamoja waliwaona watu hawa. Moto haukuunguza miili yao; nywele katika vichwa vyao hazikuungua; mavazi yao yalikuwa hayajaharibiwa; na hawakuwa na harufu ya moto.
and gathered together, the satraps, the prefects, and the governors, and the counsellors of the king, are seeing these men, that the fire hath no power over their bodies, and the hair of their head hath not been singed, and their coats have not changed, and the smell of fire hath not passed on them.
28 Nebukadneza alisema, “Na tumsifu Mungu wa Shadraka, Meshaki na Abedinego, ambaye amemtuma mjumbe wake na amewapa ujumbe watumishi wake. Walimtumaini yeye wakati walipoikana amri yangu, na waliitoa miili yao badala ya kuabudu au kusujudia mungu mwingine isipokuwa Mungu wao.
Nebuchadnezzar hath answered and hath said, 'Blessed [is] the God of Shadrach, Meshach, and Abed-Nego, who hath sent His messenger, and hath delivered His servants who trusted on Him, and the word of the king changed, and gave up their bodies that they might not serve nor do obeisance to any god except to their own God.
29 Hivyo basi ninaagiza kwamba watu wote, taifa au lugha ambayo itazungumza kitu chochote kinyume na Mungu wa Shadraka, Meshaki na Abedinego lazima wakatwe vipande, na ya kwamba nyumba zao lazima zifanywe kuwa vichuguu vya uchafu kwasababu hakuna mungu mwingine anayeweza kuokoa kama hivi.”
And by me a decree is made, that any people, nation, and language, that doth speak erroneously concerning the God of Shadrach, Meshach, and Abed-Nego, pieces he is made, and its house is made a dunghill, because that there is no other god who is able thus to deliver.'
30 Ndipo mfalme aliwapandisha cheo Shadraka, Meshaki na Abednego katika jimbo la Babeli.
Then the king hath caused Shadrach, Meshach, and Abed-Nego, to prosper in the province of Babylon.

< Danieli 3 >