< Danieli 2 >

1 Katika mwaka wa pili wa utawala wa Nebukadneza, alikuwa na ndoto. Akili yake ilisumbuka, na hakuweza kulala.
And in year two of [the] reign of Nebuchadnezzar he dreamed Nebuchadnezzar dreams and it was troubled spirit his and sleep his it happened on him.
2 Ndipo mfalme alipowaita waganga na wale wenye kuongea na wafu. Lakini pia aliwaita wachawi na watu wenye hekima. Aliwataka wamwambie juu ya ndoto zake. Basi walikuja na kusimama mbele za mfalme.
And he said the king to summon the soothsayer-priests and the conjurers and the sorcerers and the Chaldeans to tell to the king dreams his and they came and they stood before the king.
3 Mfalme akawambia, “Nilikuwa na ndoto, na akili yangu ina mashaka nataka kujua ndoto hiyo nini maana yake.”
And he said to them the king a dream I have dreamed and it was troubled spirit my to know the dream.
4 Kisha watu wenye hekima wakamwambia mfalme katika Kiaramaiki, “Mfalme, aishi milele! Twambie sisi ndoto, watumishi wako, nasi tutaifunua maana yake.”
And they spoke the Chaldeans to the king Aramaic king O for ever live! tell! dream the (to servant your *QK) and interpretation the we will declare.
5 Mfalme akawajibu watu wenye hekima, “Jambo hili limeshamalizika. Kama hamtaweza kuiweka wazi ndoto kwangu na kuitafsiri, miili yenu itakatwa vipande vipande na nyumba zenu zitafanywa kuwa vichuguu vya uchafu.
[was] replying King the and [was] saying (to Chaldeans the *QK) word the from me [is] assured if not you will make known to me dream the and interpretation its members you will be made and houses your a refuse-heap they will be made.
6 Lakini kama mtaniambia ndoto na maana yake, mtapokea zawadi kutoka kwangu, thawabu, na heshima kubwa. Basi niambie ndoto na maana yake.”
And if dream the and interpretation its you will declare gifts and a reward and honor great you will receive from before me therefore dream the and interpretation its declare to me.
7 Wakamjibu tena na kusema, “Mfalme na atuambie, watumishi wake, ndoto nasi tukwambia maana yake.”
They replied a second [time] and [they were] saying king O dream the let him tell to servants his and interpretation the we will declare.
8 Mfalme akawajibu, “Ninajua kwa hakika mnahitaji muda zaidi kwasababu mmeona maamuzi yangu ni magumu kuhusu jambo hili.
[was] replying King the and [was] saying according to certain [am] knowing I that time you [are] gaining as to because that you have seen that [is] assured from me word the.
9 Lakini kama hamtaweza kuniambia ndoto, kuna sentensi moja tu kwa ajili yenu. Mmeamua kuandaa uongo na maneno ya kudanganya ambayo mmekubaliana kwa pamoja kuniambia mpaka pale nitakapobadili akili zangu. Basi, niambieni ndoto, na kisha nitajua kuwa mnaweza kuitafsiri kwa ajili yangu.”
That if dream the not you will make known to me [is] one it decree your and a word a lie and corrupt (you have agreed together *QK) to say before me until that time the it will be changed therefore dream the tell! to me so I may know that interpretation its you will declare to me.
10 Watu wenye hekima wakamjibu mfalme, “Hakuna mtu katika dunia anayeweza kutimiza matakwa ya mfalme. Hakuna mfalme yoyote mkuu na mwenye nguvu ambaye alishataka jambo kama hilo kutoka kwa wachawi, wala wenye kuongea na wafu, wala mwenye hekima.
They replied (Chaldeans the *QK) before king the and [they were] saying not there [is] a person on earth the who [the] matter of king the he will be able to declare as to because that any king great and powerful a matter like this not he has asked to any magician and conjurer and Chaldean.
11 Kile anachokitaka mfalme ni kigumu, na hakuna yeyote awezaye kumwambia mfalme isipokuwa miungu, ambayo haishi miongoni mwa watu.”
And matter the which king the [is] asking [is] difficult and [is] another not there who he will declare it before king the except gods who dwelling place their [is] with flesh not there it.
12 Jambo hili lilimfanya mfalme akasirike na kughadhabika sana, na alitoa amri kuwaangamiza wale wote waliojulikana kuwa ni wenye hekima zao katika Babeli.
As to because this king the he was angry and he was furious exceedingly and he said to destroy all [the] wise men of Babylon.
13 Hivyo, amri ilitoka kwamba wale wote waliojulikana kwa hekima yao ni lazima wauawe. Na kwa sababu ya amri hii, walimtafuta Daniel na rafiki zake ili kwamba wauawe.
And decree the it went out and wise men the [were] about to be killed and they sought Daniel and companions his to be killed.
14 Ndipo Daniel alipomjibu kwa busara na umakini, Arioki, kamanda wa walinzi wa mfalme, ambaye alikuwa amekuja kuwaua wale wote waliojulikana kuwa na hekima katika Babeli.
Then Daniel he sent back counsel and discretion to Arioch [the] chief executioners the of king the who he went out to kill [the] wise men of Babylon.
15 Danieli alimwuliza kamanda wa mfalme, “Kwanini amri ya mfalme ni ya haraka hivyo?” Hivyo, Arioki akamwambia Danieli kile kilichotokea.
[he was] replying And [he was] saying to Arioch captain the of king the on what? [is] decree the harsh from before king the then matter the he made known Arioch to Daniel.
16 Ndipo Danieli aliingia ndani na akaomba ahadi ya muda wa kuonana na mfalme ili kwamba aweze kuwasilisha tafsiri kwa mfalme.
And Daniel he went in and he asked from king the that time he will give to him and interpretation the to declare to king the.
17 Kisha Danieli aliingia ndani ya nyumba na aliwaelezea Hanania, Mishaeli, na Azaria, kile kilichotokea.
Then Daniel to house his he went and to Hananiah Mishael and Azariah companions his matter the he made known.
18 Aliwasihi kutafuta rehema kutoka kwa Mungu wa mbinguni kuhusiana na siri hii ili kwamba yeye na wao wasije wakauawa pamoja na watu wengine waliosalia waliojulikana kuwa na hekima katika Babeli.
And compassion to ask from before [the] God of heavens the concerning secret the this that not they will destroy Daniel and companions his with [the] rest of [the] wise men of Babylon.
19 Usiku ule siri ilifunuliwa kwa Danieli katika maono. Kisha Danieli akamtukuza Mungu wa mbinguni
Then to Daniel in vision the of night the secret the it was revealed then Daniel he blessed [the] God of heavens the.
20 na kusema, “Litukuzwa jina la Mungu milele na milele; kwa kuwa hekima na nguvu ni zake.
[was] replying Daniel and [was] saying let it be name his of true God the [be] blessed from antiquity and to perpetuity that wisdom and power which [is] to him it.
21 Anabadili wakati na majira; anaondoa wafalme na kuweka wafalme katika viti vyao vya enzi. Anawapa hekima wenye hekima na ufahamu kwa wenye weledi.
And he [is] changing times the and appointed times the [he is] removing kings and [he is] setting up kings [he is] giving wisdom to wise men and understanding to ones knowing discernment.
22 Hufunua vitu vya chini na vilifichika kwa sababu anajua kile kilicho gizani, naye anaishi pamoja na mwanga.
He [is] revealing deep [things] and hidden [things] [he is] knowing what? [is] in darkness the (and light the *Qk) with him [is] dwelling.
23 Mungu wa baba zetu, ninakushukuru na kukutukuza wewe kwa ajili ya hekima na nguvu uliyonipa. Sasa umeyafanya yawe wazi kwetu yale tuliyokuomba; umetujulisha mambo yamhusuyo mfalme.”
You - O God of fathers my [am] praising and [am] praising I that wisdom and power you have given to me and now you have made known to me that we asked from you that [the] matter of king the you made known to us.
24 Ndipo Danieli alienda kumwona Arioki ( yule ambaye mfalme alimchagua kuua kila mtu aliyekuwa na hekima katika Babeli). Alimwendea na kumwambia, “Usiwauwe watu wenye hekima katika Babeli. Nipeleke kwa mfalme na nitamwonesha mfalme tafsiri ya ndoto yake.”
As to because this Daniel he went in to Arioch whom he had appointed king the to destroy [the] wise men of Babylon he went - and as follows he said to him [the] wise men of Babylon may not you destroy bring in me before king the and interpretation the to king the I will declare.
25 Kisha Arioki kwa haraka alimleta Danieli mbele za mfalme na kusema, “Nimempata miongoni wa watu wa mateka wa Yuda mtu ambaye atafunua maana ya ndoto ya mfalme.”
Then Arioch in haste he brought in Daniel before king the and as follows he said to him that I have found a man from [the] sons of exile the of Judah who interpretation the to king the he will make known.
26 Mfalme akamwambia Danieli (ambaye alikuwa akiitwa Beliteshaza), “Je unaweza kunimbia ndoto niliyoiona na maana yake?”
[was] replying King the and [was] saying to Daniel who name his [was] Belteshazzar (¿ [are] you *Qk) able to make known to me dream the which I saw and interpretation its.
27 Danieli alimjibu mfalme na kusema, “Siri ambayo mfalme ameiomba haiwezi kufunuliwa na watu wenye hekima, wala wale wenye kuongea na wafu, wala wachawi, na wala wataalamu wa nyota.
[was] replying Daniel before king the and [was] saying secret the which king the [is] asking not wise men conjurers magicians astrologers [are] being able to declare to king the.
28 Isipokuwa kuna Mungu ambaye anaishi mbinguni, ambaye hufunua siri, na amekwisha kukujulisha wewe, mfalme Nebukadneza, kile kitakachotokea katika siku zijazo. Hizi ndizo Ndoto na maono ya akili zako uliyoyaona wakati ulipokuwa umelala kitandani mwako.
Nevertheless there [is] a God in heavens the [who] reveals secrets and he has made known to king the Nebuchadnezzar what that it will be at [the] end of days the dream your and [the] visions of head your on bed your [is] this it.
29 Na kwako Wewe, mfalme, mawazo yako kitandani mwako yalikuwa ni juu ya mambo yajayo, na yule afichuaye siri ameifanya ijulikane kwako kuhusu kile kilicho karibu kutokea.
(You *Qk) king O thought[s] your on bed your they came up what that it will be after this and [one who] reveals secrets he has made known to you what that it will be.
30 Na kuhusu mimi, siri hii haikufunuliwa kwangu kwa sababu ya hekima yoyote niliyo nayo zaidi ya mtu yoyote anayeishi. Siri hii imefunliwa kwangu ili kwamba wewe, mfalme, uweze kufahamu maana, na ili kwamba ujuwe mawazo yaliyo ndani mwako.
And I not by wisdom which there [is] in me more than all living [people] the secret the this it has been revealed to me but on [the] cause that interpretation the to king the they will make known and [the] thoughts of heart your you will know.
31 Mfalme, uliangalia juu na ukaona sanamu kubwa. Sanamu hii ambayo ilikuwa yenye nguvu na yenye kung'aa, ilisimama mbele yako. Mng'ao wake ulikuwa unatisha.
(You *Qk) king O seeing you were and lo! an image one great image the this [was] great and splendor its extraordinary [was] standing before you and appearance its [was] terrible.
32 Kichwa cha sanamu kilikuwa kimetengenezwa kwa dhahabu safi. Matiti yake na mikono ilikuwa ya fedha. Sehemu ya katikati na mapaja yake yalikuwa yametengenezwa kwa shaba,
It image the head its of gold good breast its and arms its of silver belli its and loins its of bronze.
33 na miguu yake ilikuwa imetengenezwa kwa chuma. Miguu yake ilikuwa ilitengenezwa kwa sehemu chuma na sehemu kwa udongo.
Legs its of iron feet its (some of them *QK) of iron (and some of them *QK) of clay.
34 Ulitazama juu, na jiwe lilikuwa limechongwa, ingawa si kwa mikono ya wanadamu, na liliipiga sanamu katika miguu yake ya chuma na udongo, na ponda ponda.
Seeing you were until that it was cut out a stone which not [was] by hands and it struck image the on feet its of iron the and clay the and it shattered them.
35 Kisha chuma, udongo, fedha, na dhahabu zilivunjwa katika vipande vipande kwa wakati mmoja na yakawa kama makapi yaliyo katika sakafu za kupuria kipindi cha kiangazi. Upepo huyapeperushia mbali na hakuna alama inayoachwa. Lakini jiwe lililoipiga sanammu likawa mlima mkubwa na kuijaza dunia yote.
Then they were shattered as one iron the clay the bronze the silver the and gold the and they were like chaff from threshing floors of summer and it carried away them wind the and any place not it was found for them and stone the - which it struck image the it became a mountain great and it filled all earth the.
36 Hii ndiyo ilikuwa ndotoyako. Na sasa tutamwambia mfalme maana yake.
This [was] dream the and interpretation its we will tell before king the.
37 Wewe, mfalme, ni mfalme wa wafalme kwa wale ambao Mungu wa mbinguni amekupa ufalme, nguvu, uweza na heshima.
(You *Qk) king O [are] [the] king of kings the whom [the] God of heavens the kingdom the power the and strength the and honor the he has given to you.
38 Amevitia mkononi mwako sehemu ambazo binadamu huishi. Amekupa wanyama wa mwituni na ndege wa angani katika mkono wako, na amekufanya wewe utawale juu yao wote. Wewe u kichwa cha dhahabu cha sanamu.
And over all that ([are] dwelling *Qk) [the] sons of humankind [the] animal[s] of field the and [the] bird[s] of heavens the he has given in hand your and he has made ruler you over all of them (you *QK) [are] it head the of gold.
39 Baada yako, ufalme mwingine utainuka ambao ni mdogo kwako, na hata ufalme wa tatu wa shaba utatawala juu ya dunia yote.
And after you it will arise a kingdom another earthward more than you and a kingdom (third *Qk) another of bronze the which it will rule over all earth the.
40 Kutakuwa na ufalme wa tatu, wenye nguvu kama chuma, kwa kuwa chuma huvunja vipande vipande vitu vingine na kuponda ponda kila kitu. Itaviharibu vitu hivi vyote na kuvisaga.
And a kingdom (fourth *Qk) it will be strong like iron as to because that iron the [is] shattering and [is] crushing everything and like iron which [is] crushing all these it will shatter so it may crush.
41 Kama vile ulivyoona, miguu na vidole vilikuwa kwa sehemu vimetengenezwa kwa udongo na kwa sehemu vimefanywa kwa chuma, hivyo utakuwa ni ufalme uliogawanyika; baadhi ya nguvu za chuma zitakuwa ndani yake, kama tu ulivyoona kuwa chuma kimechanganyikana na udongo laini.
And that you saw feet the and toes the (some of them *QK) clay of a potter (and some of them *QK) iron a kingdom divided it will be and some of firmness the of iron the it will be in it as to because that you saw iron the mixed with [the] clay of clay the.
42 Kama vile vidole vya miguuni vilivyokuwa kwa sehemu vimetengenezwa kwa chuma na kwa sehemu vimetengenezwa kwa udongo, ndivyo ufalme utakuwa kwa sehemu una nguvu na kwa sehemu utakuwa dhaifu.
And [the] toes of feet the (some of them *QK) iron (and some of them *QK) clay from [the] part of kingdom the it will be strong and from it it will be breakable.
43 Kama ulivyoona chuma kimechanganywa na udongo laini, na hivyo na watu watakuwa wamechanganyikana; hawakaa kwa pamoja, kama vile chuma kisivyoweza kushikamana na udongo
(And that *QK) you saw iron the mixed with [the] clay of clay the mixing they will be with [the] offspring of humankind and not they will be clinging this with this here! like that iron not [is] mixing with clay.
44 Katika siku za wafalme hao, Mungu wa mbinguni ataanzisha ufalme ambao hautaweza kuangushwa, wala kushindwa na watu wengine. Utazivunja falme zingine vipande vipande na kuzikomesha zote, nao utadumu milele.
And in days their of kings the those he will set up [the] God of heavens the a kingdom which for ever not it will be destroyed and kingdom the to a people another not it will be left it will shatter so it may put an end to all these kingdoms the and it it will endure for ever.
45 Kama tu ulivyoona, jiwe lilichongwa kutoka katika mlima, lakini si kwa mikono ya wanadamu. Lilivunja vunja chuma, shaba, udongo, fedha, na dhahabu katika vipande vipande. Mungu mkuu amekujulisha wewe, mfalme, kile kitakachotokea baada ya haya. Ndoto ni ya kweli na tafsiri yake ni ya kuaminika.
As to because that you saw that from mountain it was cut out a stone which not [was] by hands and it shattered iron the bronze the clay the silver the and gold the God great he has made known to king the what that it will be after this and [is] certain dream the and [is] trustworthy interpretation its.
46 Mfalme Nebukadneza alianguka kifudifudi mbele ya Daniel na alimweshimu; aliamuru kwamba sadaka zitolewe na manukato yatolewe kwake.
Then king the Nebuchadnezzar he fell on face his and to Daniel he paid homage and offering and soothing offerings he said to offer in sacrifice to him.
47 Mfalme alimwambia Danieli, “Hakika Mungu wako ni Mungu wa miungu, Bwana wa wafalme, na ambaye hufunua mafumbo, kwa kuwa umekuwa ukiweza kufumbua mafumbo haya.”
[was] replying King the to Daniel and [was] saying from truth that God your he [is the] God of gods and [the] lord of kings and [one who] reveals secrets that you have been able to reveal secret the this.
48 Ndipo mfalme alimfanya Danieli kuwa wa kuheshiwa sana na alimpa zawadi nyingi nzuri. Alimfanya kuwa mtawala juu ya jimbo lote la Babeli. Danieli akawa liwali mkuu juu watu wenye hekima wa Babeli.
Then king the Daniel he made great and gifts great many he gave to him and he made ruler him over all [the] province of Babylon and chief of prefects over all [the] wise men of Babylon.
49 Danieli alipeleka ombi kwa mfalme, na mfalme aliwateua Shadraka, Meshaki na Abedinego kuwa watawala juu ya jimbo la Babeli. Lakini Danieli alisalia katika ikulu ya mfalme.
And Daniel he asked from king the and he appointed over administration the of [the] province of Babylon Shadrach Meshach and Abed-nego and Daniel [was] in [the] gate king the.

< Danieli 2 >